Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 29 November 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 66....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Mnamo mwaka wa nne wa utawala wake, mfalme Sedekia alikwenda Babuloni pamoja na ofisa wa askari wake aitwaye Seraya mwana wa Neria na mjukuu wa Maseya. Kutokana na fursa hiyo mimi Yeremia nilimpa Seraya ujumbe.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....


Nilikuwa nimeandika kitabuni maafa yote niliyotangaza juu ya Babuloni na pia maneno mengine kuhusu Babuloni. Nilimwambia Seraya: “Utakapofika Babuloni ni lazima uwasomee wote ujumbe huu. Kisha umalizie na maneno haya: ‘Ee Mwenyezi-Mungu, wewe umesema kwamba utapaharibu mahali hapa hata pasikaliwe na kiumbe chochote, mwanadamu au mnyama, na kwamba nchi hii itakuwa jangwa milele.’
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Utakapomaliza kusoma kitabu hiki, kifungie jiwe, kisha ukitumbukize katikati ya mto Eufrate, ukisema: ‘Hivi ndivyo mji wa Babuloni utakavyozama, wala hautainuka tena, kwa sababu ya maafa ambayo Mwenyezi-Mungu anauletea.’” Mwisho wa maneno ya Yeremia.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Ibada ya uongo na ya kweli
1Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Mbingu ni kiti changu cha enzi,
dunia ni kiti cha kuwekea miguu yangu.
Mtanijengea nyumba ya namna gani basi,
Mahali nitakapoweza kupumzika?
2Mimi mwenyewe nilivifanya vitu hivi vyote,
na hivi vyote ni mali yangu.
Lakini ninachojali mimi
ni mtu mnyenyekevu na mwenye majuto,
mtu anayetetemeka asikiapo neno langu.
3“Lakini watu hawa wanafanya wanavyotaka:
Wananitolea tambiko ya ng'ombe
na mara wanaua watu kutambikia.
Wananitolea sadaka ya mwanakondoo
na pia wanamvunja mbwa shingo.
Wananitolea tambiko ya nafaka
na pia kupeleka damu ya nguruwe.
Wanachoma ubani mbele yangu
na kwenda kuabudu miungu ya uongo.
Hao wamechagua kufuata njia zao wenyewe.
4Basi, nitawaletea taabu;
yatawapata yaleyale wanayoyahofia;
maana nilipoita hakuna aliyeitika,
niliponena hawakusikiliza.
Bali walifanya yaliyo maovu mbele yangu,
walichagua yale ambayo hayanipendezi.”
Adhabu na wokovu
5Sikilizeni neno la Mwenyezi-Mungu,
enyi msikiao neno lake mkatetemeka:
“Ndugu zenu ambao wanawachukia,
na kuwapiga marufuku kwa sababu yangu,
wamesema kwa dharau
‘Mungu na aoneshe utukufu wake,
nasi tuwaone nyinyi mkishinda!’
Lakini wao wenyewe ndio watakaoaibishwa!
6Sikilizeni, ghasia kutoka mjini,
sauti kutoka hekaluni!
Hiyo ni sauti ya Mwenyezi-Mungu
akiwaadhibu maadui zake!
7 66:7 Taz Ufu 12:5 “Mji wangu mtakatifu,
ni kama mama ajifunguaye bila kuona uchungu;
kabla uchungu kuanza, amekwisha zaa mtoto.
8Ni nani aliyepata kusikia jambo kama hilo?
Ni nani aliyewahi kuona jambo kama hilo?
Je, nchi nzima yaweza kuzaliwa siku moja?
Je, taifa zima laweza kuzaliwa mara moja?
Maana Siyoni, mara tu alipoanza kuona uchungu,
alijifungua watoto wake.
9Je, nitawatunza watu wangu mpaka karibu wazaliwe,
halafu niwazuie wasizaliwe?
Au mimi mwenye kuwajalia watoto,
nitafunga kizazi chao?
Mimi Mungu wenu nimesema.”
10Shangilieni na kufurahi pamoja na Yerusalemu enyi mnaoupenda!
Shangilieni pamoja nao enyi nyote mlioulilia!
11Kama mama, Yerusalemu utawanyonyesha,
nanyi mtashiba kwa riziki zake;
mtakunywa shibe yenu na kufurahi,
kutokana na wingi wa fahari yake.
12Maana Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Nitakuletea fanaka nyingi kama mto,
utajiri wa mataifa kama mto uliofurika.
Nanyi mtanyonya na kubebwa kama mtoto mchanga,
mtabembelezwa kama mtoto magotini mwa mama yake.
13Kama mama amtulizavyo mwanawe,
kadhalika nami nitawatuliza;
mtatulizwa mjini Yerusalemu.
14Mtayaona hayo na mioyo yenu itafurahi;
mifupa yenu itapata nguvu kama majani mabichi.
Hapo itajulikana kuwa mimi Mwenyezi-Mungu huwalinda watumishi wangu,
lakini nikikasirika huwaadhibu maadui zangu.”
15Mwenyezi-Mungu atakuja kama moto,
na magari yake ya vita ni kimbunga.
Ataiacha hasira yake ifanye kazi yake kwa ukali,
na onyo lake litekelezwe kwa miali ya moto.
16Mwenyezi-Mungu atatoa hukumu kwa moto,
atawaadhibu watu wote kwa upanga;
nao atakaowaangamiza watakuwa wengi.
17Mwenyezi-Mungu asema hivi: “Wapo watu wanaojitakasa na kutawadha wapate kuingia kwenye bustani za ibada za sanamu; wanafanya maandamano na kuhani akiwa kati yao. Watu hao hula nguruwe, panya na vyakula vingine haramu. Watu hao hakika watakufa wote pamoja. 18Nayajua matendo yao na mawazo yao. Naja kuwakusanya watu wa mataifa yote na lugha zote, wajumuike pamoja na kuuona utukufu wangu. 19Nitaweka kati yao alama ya uwezo wangu. Watakaosalimika kati yao nitawapeleka kwa watu wa mataifa huko Tarshishi, Puti,66:19 Puti: Kiebrania: Puli. Ludi, nchi zenye wapiga upinde stadi; watakwenda pia Tubali na Yowani na nchi ambapo watu hawajapata kusikia umaarufu wangu wala kuuona utukufu wangu. Hao wajumbe wangu watautangaza utukufu wangu katika mataifa hayo. 20Watawarejesha ndugu zenu wote kutoka katika mataifa yote kama matoleo yangu mimi Mwenyezi-Mungu. Watawaleta wamepanda farasi, nyumbu, ngamia na magari ya farasi mpaka Yerusalemu, kwenye mlima wangu mtakatifu. Watawaleta kama Waisraeli waletavyo sadaka ya nafaka katika chombo safi hadi nyumbani kwangu mimi Mwenyezi-Mungu. 21Pia nitawachagua baadhi yao kuwa makuhani na baadhi yao kuwa Walawi. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
22“Kama vile mbingu mpya na dunia mpya nitakazoumba
zitakavyodumu milele kwa uwezo wangu,
ndivyo wazawa wako na jina lako litakavyodumu.
23Katika kila sikukuu ya mwezi mpya,
na katika kila siku ya Sabato,
binadamu wote watakuja kuniabudu.
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
24“Kisha watakwenda kuziona maiti za wale walioniasi. Wadudu watakaowala hawatakufa, na moto utakaowachoma hautazimika kamwe. Watakuwa chukizo kwa watu wote.”


Isaya66;1-24

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 28 November 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 65....



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

“Sikiliza! Kilio kinasikika kutoka Babuloni! Kishindo cha maangamizi makubwa kutoka nchi ya Wakaldayo! Maana mimi Mwenyezi-Mungu naiangamiza Babuloni, na kuikomesha kelele yake kubwa. Adui ananguruma kama mawimbi ya maji mengi, sauti ya kishindo chao inaongezeka.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Naam, mwangamizi anaijia Babuloni; askari wake wametekwa, pinde zao zimevunjwavunjwa. Mimi Mwenyezi-Mungu ni Mungu mwenye kuadhibu, hakika mimi nitalipiza kisasi kamili.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....


Nitawalewesha wakuu na wenye hekima wake, watawala wake, madiwani na askari wake; watalala usingizi wa milele wasiinuke tena. Nasema mimi mfalme ambaye jina langu ni Mwenyezi-Mungu wa Majeshi. “Mimi Mwenyezi-Mungu wa Majeshi nasema: Ukuta mpana wa Babuloni utabomolewa mpaka chini, na malango yake marefu yatateketezwa kwa moto. Watu wanafanya juhudi za bure, mataifa yanajichosha maana mwisho wao ni motoni!”
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.


Mungu huwaadhibu waasi
1Mwenyezi-Mungu asema;
“Nilikuwa tayari kujionesha
kwao wasiouliza habari zangu.
Nilikuwa tayari kuwapokea
wale wasionitafuta.
Nililiambia taifa ambalo halikuomba kwa jina langu:
‘Nipo hapa! Nipo hapa!’
2 65:2 Taz Rom 10:21 Mchana kutwa niliwanyoshea mikono watu waasi,
watu ambao hufuata njia zisizo sawa,
watu ambao hufuata fikira zao wenyewe.
3Ni watu ambao daima hunichokoza waziwazi;
hutambikia miungu yao katika bustani,
na kuifukizia ubani juu ya matofali.
4Huketi makaburini na kukaa mafichoni usiku.
Hula nyama ya nguruwe na mchuzi wa wanyama haramu.
5Huwaambia wale wanaokutana nao:
‘Kaeni mbali nami;
msinikaribie kwani mimi ni mtakatifu!’
Watu hao wananikasirisha mno,
hasira yangu ni kama moto usiozimika.
6“Jueni kuwa nimelitia jambo hilo moyoni,
sitanyamaza bali nitawafanya walipe;
nitawafanya walipe kwa wingi.
7Mimi Mwenyezi-Mungu, nitawalipiza maovu yao
wayalipie na maovu ya wazee wao.
Wao waliifukizia ubani miungu yao milimani,
wakanitukana mimi huko vilimani.
Nitawafanya walipe kwa wingi,
watayalipia matendo yao ya awali.”
8Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Mtu akikuta kishada cha zabibu nzuri,
watu husema: ‘Tusikiharibu; kina baraka.’
Ndivyo nitakavyofanya kwa ajili ya watumishi wangu;
sitawaangamiza wote.
9Nitawajalia watu wa Yakobo,
na Yuda nitamjalia warithi wa milima yangu;
watumishi wangu watakaa huko.
10Nchi tambarare ya Sharoni itakuwa malisho,
bonde la Akori65:10 Akori: Maana yake Taabu. litakuwa mapumziko ya mifugo
kwa ajili ya watu wangu walionitafuta.
11“Lakini nitafanya nini na nyinyi
mnaoniacha mimi Mwenyezi-Mungu,
msioujali Siyoni, mlima wangu mtakatifu,
nyinyi mnaoabudu mungu ‘Gadi’,
na kumtolea tambiko ya divai mungu ‘Meni’?65:11 Gadi, yaani bahati na Meni, yaani ajali ni majina ya miungu.
12Nimewapangia kifo kwa upanga,
nyote mtaangukia machinjoni!
Maana, nilipowaita, hamkuniitikia;
niliponena, hamkunisikiliza.
Mlitenda yaliyo maovu mbele yangu,
mkachagua yale nisiyoyapenda.
13Basi, mimi Mwenyezi-Mungu nasema,
watumishi wangu watakula,
lakini nyinyi mtaona njaa;
watumishi wangu watakunywa,
lakini nyinyi mtaona kiu;
watumishi wangu watafurahi,
lakini nyinyi mtafedheheka.
14Watumishi wangu wataimba kwa furaha moyoni,
lakini nyinyi mtalia kwa uchungu moyoni
na kupiga kelele kwa uchungu mkubwa rohoni.
15Wale niliowachagua nitawapa jina jipya.
Lakini nyinyi jina lenu watalitumia kulaania;
‘Watasema: Bwana Mungu awaue kama hao.’
16Basi, mwenye kujitakia baraka nchini,
atajitakia baraka kwa Mungu wa kweli.
Mwenye kuapa katika nchi hii,
ataapa kwa Mungu wa kweli.
Maana taabu za zamani zimepita
zimetoweka kabisa mbele yangu.
Ulimwengu mpya
17“Sasa, naumba mbingu mpya na dunia mpya.
mambo ya zamani hayatakumbukwa tena.
18Furahini, mkashangilie milele,
kwa ajili ya vitu hivi ninavyoumba.
Yerusalemu nitaufanya mji wa shangwe,
na watu wake watu wenye furaha.
19 65:19 Taz Ufu 21:4 Nami nitaufurahia mji wa Yerusalemu,
nitawafurahia watu wangu.
Sauti ya kilio haitasikika tena,
kilio cha taabu hakitakuwako.
20Hakutakuwa tena na vifo vya watoto wachanga,
wazee nao hawatakufa kabla ya wakati wao.
Akifa mtu wa miaka 100 amekufa akiwa kijana;
na akifa kabla ya miaka 100 ni balaa.
21Watu watajenga nyumba na kuishi humo;
watalima mizabibu na kula matunda yake.
22Hawatajenga nyumba zikaliwe na watu wengine,
wala kulima chakula kiliwe na watu wengine.
Maana watu wangu niliowachagua
wataishi maisha marefu kama miti;
wateule wangu watafurahia matunda ya jasho lao.
23Kazi zao hazitakuwa bure,
wala hawatazaa watoto wa kupata maafa;
maana watakuwa waliobarikiwa na Mwenyezi-Mungu,
wamebarikiwa wao pamoja na wazawa wao.
24Hata kabla hawajaniita, mimi nitawaitikia;
kabla hawajamaliza kusema, nitakuwa nimewajibu.
25Mbwamwitu na kondoo watakula pamoja,
simba watakula nyasi kama ng'ombe,
nao nyoka chakula chao kitakuwa vumbi.
Katika mlima wangu wote mtakatifu,
hakuna atakayeumiza au kuharibu kitu.
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”


Isaya65;1-25

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Wednesday 27 November 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 64....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu



Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Msife moyo wala msiwe na hofu, kwa sababu ya uvumi mnaosikia nchini. Mwaka huu kuna uvumi huu, mwaka mwingine uvumi mwingine; uvumi wa ukatili katika nchi, mtawala mmoja dhidi ya mtawala mwingine. Kweli siku zaja, nitakapoadhibu sanamu za Babuloni; nchi yake yote itatiwa aibu, watu wake wote watauawa humohumo.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....


Kisha mbingu, dunia na vyote vilivyomo vitaimba kwa furaha kuhusu kuanguka kwa Babuloni, waangamizi watakapofika kutoka kaskazini kuushambulia. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.” Babuloni umesababisha vifo duniani kote; sasa wenyewe utaangamizwa kwa mauaji ya Israeli. “Nyinyi mlinusurika kifo, ondokeni sasa, wala msisitesite! Ingawa mko nchi ya mbali mkumbukeni Mwenyezi-Mungu, ukumbukeni pia mji wa Yerusalemu.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Mnasema: ‘Tumeaibishwa na kufadhaishwa; aibu imezifunika nyuso zetu, kwa sababu wageni wameingia katika sehemu takatifu za nyumba ya Mwenyezi-Mungu.’ “Kwa hiyo, wakati unakuja, nasema mimi Mwenyezi-Mungu, ambapo nitaviadhibu vinyago vya Babuloni, na majeruhi watapiga kite katika nchi yake yote. Ingawa Babuloni atapanda mpaka mbinguni, na kuziimarisha ngome zake ndefu, waangamizi watakuja kutoka kwangu kumvamia. 2Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.



1Laiti ungalizipasua mbingu ukashuka chini,
milima ikakuona na kutetemeka kwa hofu! 64:1 Katika Kiebrania ni 64:11.
2Ingeteketea kama moto uchomavyo kichaka,
kama vile moto uchemshavyo maji.
Njoo upate kuwajulisha maadui zako jina lako
nayo mataifa yatetemeke kwa kuwako kwako!
3Wakati ulipotenda maajabu ambayo hatukutazamia,
ulishuka chini nayo milima ikatetemeka ilipokuona.
4 64:4 Taz 1Kor 2:9 Tangu kale hakuna aliyepata kuona
wala kusikia kwa masikio yake;
hakuna aliyepata kumwona Mungu aliye kama wewe
atendaye mambo kwa ajili ya wale wanaomtegemea!
5Wewe waja kuwasaidia watendao haki kwa furaha,
wanaokukumbuka na kuzingatia njia zako.
Ulitukasirikia tulipokuwa wenye dhambi;
sisi tumeasi kwa muda mrefu.64:5 aya ya 5 Kiebrania si dhahiri. Tafsiri ya hapa kufuatana na tafsiri ya Kigiriki.
6Sote tumekuwa kama watu walio najisi;
matendo yetu yote mema ni kama nguo chafu.
Sote tunanyauka kama majani,
uovu wetu watupeperusha kama upepo.
7Hakuna hata mmoja anayekuja kukuomba;
hakuna anayejishughulisha kukutafuta.
Wewe unauficha uso wako mbali nasi,
umetuacha tukumbwe na maovu yetu.
8Hata hivyo, ee Mwenyezi-Mungu, wewe ni Baba yetu.
Sisi ni kama udongo, wewe ni mfinyanzi.
Sisi sote ni kazi ya mikono yako.
9Usitukasirikie mno, ee Mwenyezi-Mungu,
usiukumbuke uovu wetu daima!
Ukumbuke kwamba sisi sote ni watu wako!
10Miji yako mitakatifu imekuwa nyika;
Siyoni umekuwa mahame,
Yerusalemu umekuwa uharibifu.
11Nyumba yetu takatifu na nzuri,
ambamo wazee wetu walikusifu,
imeteketezwa kwa moto.
Mahali petu pote pazuri pamekuwa magofu.
12Je, kwa hayo yote utajizuia usifanye kitu?
Je, utaendelea kunyamaza tu, ee Mwenyezi-Mungu,
na kututesa kupita kiasi?

Isaya64;1-12

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Tuesday 26 November 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 63....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Nitawashusha chini kama kondoo wa kuchinjwa, kama vile kondoo dume na beberu. Ajabu kutekwa kwa Babuloni; mji uliosifika duniani kote umechukuliwa! Babuloni umekuwa kinyaa kati ya mataifa!
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....


Bahari imefurika juu ya Babuloni, Babuloni imefunikwa mawimbi yaliyochafuka. Miji yake imekuwa kinyaa, nchi ya ukavu na jangwa, nchi isiyokaliwa na mtu yeyote, wala kupitika na binadamu yeyote.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Nitamwadhibu mungu Beli huko Babuloni, nitamfanya akitoe alichokimeza. Mataifa hayatamiminika tena kumwendea. Ukuta wa Babuloni umebomoka. “Tokeni humo enyi watu wangu! Kila mtu na ayasalimishe maisha yake, kutoka hasira kali ya Mwenyezi-Mungu.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

Mungu awaadhibu maadui za watu wake
1Ni nani huyu ajaye kutoka Edomu,
anayefika kutoka Bosra na mavazi ya madoa mekundu?
Ni nani huyo aliyevaa mavazi ya fahari,
anatembea kwa nguvu zake kubwa?
Ni mimi Mwenyezi-Mungu
ninayetangaza ushindi wangu;
nami ni mwenye nguvu ya kuokoa.
2Lakini mbona nguo yako ni nyekundu,
nyekundu kama ya mtu anayekamua zabibu?
3Naam, nimekamua zabibu peke yangu,
wala hakuna mtu aliyekuja kunisaidia.
Nimeyakanyaga mataifa kwa hasira yangu,
niliyapondaponda kwa ghadhabu yangu.
Nguo zangu zimejaa madoa ya damu yao,
imeyachafua kabisa mavazi yangu.
4Niliamua kuwa siku ya kulipiza kisasi imefika;
wakati wa kuwakomboa watu wangu umefika.
5Nilitazama na hapakuwa na wa kunisaidia;
nilishangaa hapakuwa na wa kuniunga mkono.
Lakini nilijipatia ushindi kwa mkono wangu,
ghadhabu yangu ilinihimiza.
6Kwa hasira yangu niliwaponda watu,
niliwalewesha kwa ghadhabu yangu;
damu yao niliimwaga chini ardhini.”
Wema wa Mungu kwa Israeli
7Nitasimulia fadhili za Mwenyezi-Mungu;
nitataja matendo yake yote yastahiliyo sifa,
kwa sababu ya yote aliyotutendea,
wema wake mkuu aliowapa Waisraeli kwa huruma yake,
kadiri ya wingi wa fadhili zake.
8Maana alisema juu yao:
“Hakika, hawa ni watu wangu;
watoto wangu ambao hawatanidanganya.”
Basi yeye akawa Mwokozi wao.
9Katika taabu zao zote,
hakumtuma mjumbe63:9 … hakumtuma mjumbe … au Malaika; Yeye aliwaokoa. Yeye Mwenyewe alitaabika walipotaabika, akamtuma malaika wake awaokoe. mwingine kuwasaidia,
ila yeye mwenyewe alikuja kuwaokoa.
kwa upendo na huruma yake aliwakomboa.
Aliwabeba na kuwachukua tangu zamani.
10Lakini wao walikuwa wakaidi,
wakaihuzunisha roho yake takatifu.
Basi, Mungu akageuka, akawa adui yao;
yeye mwenyewe akapigana nao.
11Ndipo walipokumbuka63:11 walipokumbuka: Kiebrania: Alipozikumbuka. siku za zamani,
wakati wa Mose mtumishi wa Mwenyezi-Mungu.
Wakauliza, “Yuko wapi sasa Mwenyezi-Mungu,
aliyewaokoa wachungaji wa kundi lake baharini?
Yuko wapi yule aliyeiweka roho yake takatifu kati yao,
12ambaye kwa mkono wake wenye nguvu
alifanya maajabu kwa njia ya Mose,
akapasua bahari na kuwaongoza watu wake,
na kujipatia jina la milele?
13Aliwaongoza katikati ya vilindi vya bahari,
wakapita humo kama farasi bila kujikwaa.
14Kama ng'ombe wapelekwavyo malishoni bondeni,
ndivyo roho ya Mungu ilivyowapumzisha watu wake.
Ndivyo ee Mungu ulivyowaongoza watu wako,
nawe ukajipatia jina tukufu.”
Sala ya kuomba msaada
15Ututazame kutoka mbinguni ee Mungu, uone,
utuangalie kutoka makao yako matakatifu na matukufu.
Iko wapi bidii yako kwa ajili yetu na nguvu yako?
Usiache kutuonesha upendo wako.63:15 Usiache … upendo wako: Tafsiri ya neno kwa neno: Upendo na huruma yako vimezuiwa visionekane kwetu.
16Maana wewe ndiwe Baba yetu;
Abrahamu, mzee wetu, hatujali,
naye Israeli hatutambui;
lakini wewe, ee Mwenyezi-Mungu, ni Baba yetu.
Wewe umeitwa tangu kale: “Mkombozi wetu.”
17Ee Mwenyezi-Mungu, mbona unatukosesha njia zako?
Mbona unatufanya kuwa wakaidi hata tusikuogope?
Rudi ee Mungu kwa ajili ya watumishi wako,
makabila ambayo daima yalikuwa mali yako.
18Kwa kitambo tu sisi watakatifu wako tulimiliki nchi,
lakini maadui zetu wakaja wakaharibu maskani yako.63:18 aya 18 makala ya Kiebrania si dhahiri.
19Tumekuwa kama watu ambao hujawatawala kamwe,
kama watu ambao hawakujulikana kwa jina lako.

Isaya63;1-19

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.