Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 30 May 2012

Jikoni Leo; ni Wasomali na Darasa la Mapishi na Utamaduni wao;Wazazi wa Marekani.na Da'Mariam!!!!!!

Waungwana "Jikoni Leo" ni Wasomali;
Wazazi/Walezi wa Marekani Wakiwafundisha Watoto wao Jinsi ya Kupika na Tamaduni za Kwao.


Pia da'Mariam naye Hayuko Nyuma kuonyesha/Kuwafunza watu wengine Jinsi "East Africa" wapikavyo.
 

Hapa nimeona Wasomali wanajitahidi kuwafundisha kupika watoto wa kike tuu,Sijui watoto wa kiume kwao Hawapiki?au bado wanamambo yaleee mtoto wakike "LAKE JIKO".

Waungwana Mmejifunza nini kwa haya ya Wenzetu Wasomali?

Karibuni sana kwa Maoni,Ushauri na Kuelimishana kwa Upendo.

Pamoja sana."Swahili na Waswahili."

Tuesday 29 May 2012

Wa Afrika na Sherehe zao;Leo ni Wadigo wedding , Kenya!!!!!!

Hahhahahhah Kadala,Mwanamke wa shoka, Mwanakwetu,Kadoda,Ndugu wa mimi na Waungwana Woooote,
Mambo hayo ya kupetipeti!!
Sina lazaidi Mengi Mnayo Wenyewe Yakheeeeee!!!!


Karibuni sana. "Swahili na Waswahili".Pamoja sana tuu.

Monday 28 May 2012

Da'Tracey-Sarah,Atimiza Miaka 11!!!!!!!

Da'Tracey-Sarah
Da'Sandra akiandaa Keki
Tumtangulize Mungu kwanza katika Yote!!!

Leo umezima 11,mungu akulinde uzime 100!!!
Anaitwa Mkama; kwakuzima Mishumaa hayuko nyuma,Kama mtoto wako anasuasua kuzima,Tuwasiliane!!
da'Tracey akikata keki na da'Mija akihakikisha mambo yako sawa!!!

da'Elizabeth na da'Mija wakiandaa keki,watu tule!!kweli watoto wa Shoka,Mungu awabariki sana!!
Mama akimlisha Mwana!!
Da'Mija akilishwa na Rafiki yake kipenzi,Mungu azidi kuwaunganisha daima!!
Da'Tracey akilishwa na dada yake!!
Da'Sandra akilishwa na Mdogo wake, duuh kuna haja ya kuongeza sijui!!
Da'Anita akilishwa,Chezea yeye!!!
Da'Asiimwe akilishwa,huwa hana haraka wala maneno mengi,jicho tuu linaongea!!
Da'Manjula aliamua kupanda juu ya kiti,Ale kwa raha,nani anapenda Ufupi?
Kamanda Mkama a.k.a.Mzee wa Next,Akipata kipande chake!!!
Dada Mkubwa,Eliza naye akijipatia keki!!
Pamoja daima!!!!
Katuni/Vibonzo lazima tuangalie!!!
Mapoziiiiiii
Unahitaji wanamitindo? Tuwasiliane.....hahahahaha
Na muziki tulisakata, sikunyingine nitaweka Video!!!Lakini Zilipendwa waligomaaa!!!
Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi,da'Mija[Mia] akipozi baada ya kazi kubwa!!
Da'Tracey[Sarah]Akipozi  na Kuwashukuru Wazazi,Ndugu,Jamaa na Marafiki kwa yooote!!!



Familia ya Isaac,Tunamshukuru sana Mungu kwa Mema Mengi aliyotutendea,Asante kwa kumtunza na kumlinda Mtoto wetu Tracey-Sarah na Familia pia.
Asante kwa Kumaliza SAT'S,Salama,wewe ulimlinda akiwa Shule ya Msingi pia Tunamuweka Mikononi mwako Aendapo Secondary.

Shukrani Nyingi Ziwaendee,Familia ya Nyotu[Kamau].Familia ya Manju[Da'Mija Mwanamke wa Shoka].Kaka Don,baba Eliza na Familia yako. Da'Maggie[dadake]Asante sana.

Mungu awabariki sana kwa Moyo wenu wa Upendo na Kutumia Muda wenu kuwa nasi.

Pamoja sana Wapendwa,MUNGU NI PENDO APENDA WATU.Nasi TUNAWAPENDA WOOOOOTE.

Friday 25 May 2012

Waswahili wetu Leo;WaTanzania na Madawa ya Kulevya!!!!!!!

Haya Waungwana;Hawa ni Ndugu zetu,Jamaa zetu,Rafiki zetu,
Jee nani Alaumiwe? Muuzaji au Mtumiaji?
"Swahili na Waswahili" Pamoja sana.

Tuesday 22 May 2012

Wa Afrika na Sherehe Zao;Nigerian Bride (Traditional Wedding) and Gele Styles!!!!

Swali; Jee WaTanzania tunaweza kuvaa nini kwenye Ndoa,Siku ya Posa,Siku ya kuagwa, K/party au Sherehe yoyote inayotakiwa Kuonyesha Utanzania Wetu?

Nimeshaona wengi wakivaa kimasi, Jee Vazi hili linaweza kututambulisha?

Waungwana karibuni sana katika Kuelimishana,Kushauriana  na Mapenzi yako katika Vazi la Nyumbani.
Pamoja sana .Swahili na Waswahli!!!!!

Monday 21 May 2012

Jikoni Leo. Mswahili; da'Sophi na Tupike Pamoja!!! Angalia Video!!!!




Karibuni "tupikepamoja.com"


Habari utakazo zipata katika tovuti hii ni picha za video na maelezo ya kina kuhusu namna ya kupika mapishi na vyakula vizuri vya kimataifa muhimu zaidi ni rahisi kupika.
Tovuti hii ni kwa ajili ya watu wanaopenda kupika, kujaribu vyakula vipya na ladha mpya ili kuwashangaza rafiki na familia zao kwa ladha hizo. Maelekezo ya mapishi utakayopata hapa ni kwa ajili ya meza kuu ingawa wakati mwingine tunashirikiana nawe katika vinywaji na viburudisho (deserts & sweets).
kwa kuanzia ni matumaini yetu utafurahia kupika kama sisi.
Pia usisahau kututumia maoni yako, maswali na ujumbe tuweze kuboresha na kutimiza mahitaji yako, Asante kwa ushirikiano wako
Furahia chakula chako!

Kujua zaidi Mtembelee.www.tupikepamoja.com
Haya Waungwana Mambo hayo kazi kwenu na "Tupike Pamoja"

Hongera da'Sophi kazi nzuri.

Sunday 20 May 2012

Nawatakia J'Pili Njema;Burudani;Sarah K - Liseme.The Christ Ambassadors-Moyoni Mwangu na Kazi Tufanye!!!!!!



Watoto wa KKkT Kijito Nyama
Nawatakia J'Pili yenye Baraka, Upendo,Amani, Umoja na Furaha.
1;Haleluya.Msifuni Mungu katika Patakatifu pake;
Msifuni katika anga la uweza wake.
Neno la Leo:Zaburi ya 150:1-6. 

6;Kila mwenye Pumzi na Amsifu BWANA.
Haleluya!!!!!!!!!.

Saturday 19 May 2012

Chaguo la Mswahili Leo;Celine&R.kelly- I'm Your Angel, The Step in the Name of Love. Na nyingineee!!!



 Waungwana Nawatakia j'Mosi yenye Amani na Furaha daima!!.
Leo ngoja Tuangalie/twende Pande hii.
 Sina Mengi Zaidi Nakusikiliza wewe tuu.Baada ya Burudani, Umekumbuka nini,Umeguswa,Umefurahi,Umenuna au? "Swahili na Waswahili" Pamoja sana

Friday 18 May 2012

MTANZANIA DR ENGINEER SHABAN KACHUA ATUNUKIWA RASMI SHAHADA YAKE YA UDAKTARI WA FALSAFA NCHINI CANADA.


Dr Engineer Shaban Kachua mwenye joho lenye rangi nyekundu na Bluu akiwa na waafrika wenzake wakati wa alipotunukiwa Shahada yake ya Udaktari wa falsafa Nchini Canada.
Hapa Dr Kachua akiwa amekaa mstari wa mbele kabisa na wahitimu wenzake.
Mama Mzazi wa Dr Kachua (mwenye blauzi nyeusi), akiwa na Mama mkwe wake, wote kwa pamoja walishiriki katika tukio la kihistoria la kutunukiwa Shahada ya PHD kwa mtoto wao nchini Canada.
Mrs Dr Shaban Kachua (Jemima) akiwa na furaha pamoja na watoto wao walishiriki katika shughuli ya kutunukiwa Mume wake shahada ya udaktari wa Falsafa (PHD).

Kwa sasa Dr Shaban Kachua anaishi Nchini Canada pamoja na familia yake. Sisi kama watanzania wenzake tunapenda kumpongeza sana kwa kuweza kuipeperusha vema Bendera yetu, tunapenda kumshauri pia, elimu yake hiyo aweze kuitumia pia kulisaidia Taifa lake la Tanzania hasa katika nyanja hiyo ya Sayansi, kwa kutambua zaidi tuna upungufu mkubwa wa wanasayansi katika Taifa letu.

HONGERA SANA
Asanteni sana KapingaZ http://kapingaz.blogspot.co.uk/

Thursday 17 May 2012

Watoto na Vituko;Pata na Burudani!!!!!!

Waungwana Mambo hayo, sina la kusema,Zaidi unayo wewe!!!!!!
Pamoja sana sana.Swahili na Waswahili!!!!!!!!

Wednesday 16 May 2012

Mswahili;SAM MACHOZI - MY ANGEL.{OFFICIAL VIDEO}

Hii ni yenu.....!! ni video yangu ya kwanza kama sam machozi nigependa sana saport zenu wa TZ ili niweze kuipeleka bendera yetu mbele kimataifa zaidi tuamini kama tunaweza na tutaweza mungu yupo na sisi milele amine... ni sam machozi`TO ALL MY BEAUTIFUL PEOPLE...!




Hayo ni Maneno yake kaka Sam Machozi.

Pamoja sana Waungwana!!! Swahili na Waswahili.

Tuesday 15 May 2012

Siku kama ya Leo da'Masika na Bw'Jamal,Waliungana na Kuwa Mke na Mume. Burudani: Nitadumu nae!!!!

                                  Nakuvisha/kuvalisha Pete[Pingu] hii..............
                                     Bwana Jamal James Umekubali..............
                                  Mke mkeo kaka J .J
                               Mama Masika katikati, Hongera mama.
                    Mwenyewe da'Masika, Raha jipe Mwenyewe!!!
                                  Mwenye Bw'J.J.Mwakitalu.
                           Shughuli Watu na Watu Walikuwepo.
BIBI na BWANA MWAKITALU.
Na Wamejaaliwa kupata Watoto Wawili
.
Tunawatakia kila lililo jema katika Maisha yenu,Mungu azidi kuwabariki na Ndoa hii Idumu!!!!

Kama una lolote unataka kushiriki nasi, tuma kupitia Email.rasca@hotmail.co.uk
                         Pamoja sana Waungwana.

Monday 14 May 2012

Wanawake na Urembo;Ya kale ni Dhahabu!!!Burudani-Rangi ya Chungwa,Pamelah!!

Mrembo wa enzi hizooooo
Nipe siri ya urembo huu


Waungwa Leo nimewaletea Mrembo wa zamani kidogo,lakini mimi kwangu bado wananibamba sana.
Angalia hajajichubua,Hana makoroooombwezo meengi,Shedo za kuwaaakaa,Jee Hajapendeza?

Na sasa naona kama vimitindo tindo vya zamani  vinarudi, Sijui kukosa ubunifu, Ya metushinda au kukumbukia Enzi?

Huyu yeye hakuweka dawa Nywele wala kusuka,Lakini wapo pia wazamani waliokuwa wakisuka,Nywele za Uzi,Rafya,Jicho la mke wenza,Kilimanjaro, walibana Mchicha, waliweka Zazuuu, wali roli , Waliweka Kan'ta, Walifunga Vilemba  na..... duuuh nimengi nao Walikuwemo sana tuu.

Jee kunachochote cha Mitindo ya Zamani wewe bado Unapenda au Kukumbuka? na nini Kimekugusa/Kuvuti,  kwa huyu Mrembo?
Unapicha za BABA/MAMA za Wakati huo wakiwa Vijana na Unapenda Tujifunze Mitindi yao?

Usiwe na Tabu Unaweza kututumia Kupitia email.rasca@hotmail.co.uk

Karibuni sana Waungwa!!!!!

Sunday 13 May 2012

Nawatakia J'Pili Njema na Hongera kina MAMA!!Burudani; mwaitege-mama ni mama.Bahati-Mapito!!!

Da'Rehema na Mwanawe Chance
Wifi'Rehema na Mwanawe Farid.


Nawatakia J'Pili na Hongera kina MAMA Woote popote Mlipo!!
 Kila lenye Kheri,Baraka,Upendo,Uvumilivu,Utuwema,Umoja,Huruma na REHEMA!!!

Wengine tulisha Sheherekea, lakini si Mbaya tukiungana Nanyi tena.

Leo da'REHEMA na wifi REHEMA ndiyo wanaotuwakilisha SWAHILI na WASWAHILI.katika Siku ya MAMA.

3;REHEMA na kweli zisifarakane nawe.6;Katika njia zako zote mkiri yeye,Naye atakuonyesha MAPITO yako.
Neno la Leo;Mithali:3;1-7

Saturday 12 May 2012

Chaguo la Mswahili Leo;Kutoka kwa Familia ya Penza.Burudani;Diamond - Moyo wangu,Mbagala,Mawazo!!!!!



Diamond na Chance
Diamond na da'Phoibe[Mwana Penza]
Waungwana Leo sipo mbaali sana,yaani si za Kale,Kijana anabamba/anafanya vyema katika Kazi yake, au vipi.
Jee wewe Muungwana Kijana Almasi anakubamba/unapenda kazi yake?Zaidi ni Sauti,Maneno,Muonekano,Uchezaji, Manjonjooo kama si Vionjooo?

Twende Sootee sasaaa, Moyo Wanguuu ooh Moyo wanguuu oooohhh.....Makuti na Mkoleeeeee duuhh mpaka Mkoleeeee!!

Pamoja sana na muwe na J'Mosi njema!!!!!!

Friday 11 May 2012

Wanawake na Shughuli;Burudani-Bembeleza,Pii pii!!!!


mwanamke akifanya vitu vyake.Picha kwa hisani ya da'Jane Siame wa http://j2wisdom.blogspot.co.uk


Waungwana  natumai wote Hamjambo.

"Wanake na Shughuli " Kumekuwa na Shughuli nyiingi sana zinazohusishwa wanawake tuu.Jee Wanaume Hampendi/Hawapendi Shughuli/kujichanganya peke yenu/Yao?


Au sisi Wanawake ndiyo haswaa tunatakiwa kujichanganya,kufurahi,kukutana wenyewe?


Na jee kwanini tunapoalikana hizo shughuli tunaambiana kuwa ni ya "WANAWAKE TUU" Sasa basi ukienda huko unakuta Dj,Mchukua matukio, Mara kaka,Mjomba kaja na mengine meeengi yanafanywa na "WANAUME".Jee kweli wanawake wa leo hakuna wakutosha kufanya hizo kazi?
Je na hawa MASHOGA  Tumeshawaweka kwenye kundi Letu?

Vipi unapoaga Nyumbani kwa baba Ngina[mume] unaenda kwenye Shughuli za Wanawake tuu, nae anakupeleka na kuishia mlangoni anarudi Nyumbani.
 Akikufuata anakutana na Wanaume kibao wanatoka humo kwa Shughuli jee hii imekaaje?


Mpenzi Msomaji wewe una Mawazo,Maoni,Ushauri Gani katika hili?


Karibuni sana Tuelimishane  Kwa Upendo!!!!

Thursday 10 May 2012

Mchague Joseph Lukaza !!!!!!!


Mchague JOSEPH LUKAZA ili aweze kuibuka mshindi katika shindano la EXCEL WITH GRAND MALT katika chuo kikuu cha Dodoma katika  Category ya Innovation Nominee
Jinsi ya kushiriki kwa njia ya kutuma ujumbe mfupi wa simu unaandika
"INV UDOM JOSEPH LUKAZA 3rd year" alafu unatuma kwenda namba 0653202000.
Na unaweza kupiga kura kwa kutumia tovuti
 
                             

Wednesday 9 May 2012

Jikoni Leo;Kitabu cha Mapishi cha da'Miriam Rose.Mapishi ya vitumbua kutoka kwa da'Cecy!!!

Cookbook Sneak Peek – Kitabu cha mapishi

Muonekano wa kitabu cha mapishi cha"A Taste of Tanzania".

Cover ame-Design Mwenyewe na Picha amepiga mwenye.Kitabu kitatoka hivi karibuni.

Utakipataje;Ataweka wazi jinsi gani unaweza kupata Kitabu.Ukiingia pale kwake kunasehemu ya mawasiliano,Unaweza kuwasiliana nae Zaidi kupitia http://www.tasteoftanzania.com

Jee da'Miriam anajua KISWAHILI?JIBU;Ndiyo,anakichapa haswa, kama ulivyoona kwenye ile post iliyopita niliandika ni Mswahili.

Nafikiri nimewajibu nijuavyo Waungwana mlionitumia Email na mlionitumia Messages kwenye sim.Na nimeweka hapa kama kuna wengine waliokuwa na maswali kama haya nao Wamepata Jibu.

Haya Waungwana pata mapishi ya UJI na FUTARI kutoka kwa da'Miriam Rose.Hapo juu.

Hapo chini;Mapishi ya "VITUMBUA"Kutoka kwa da'Cecy anapatikana http://mapishinacecy.blogspot.co.uk.

Mswahili mimi kupika vikorombwezo saaaana siweziiiiii,Najua kupika kiasi cha Kula  MUBENA yangu na Watoto yangu na Wageni kidogo tuu,Si kila mtu anaweza kila kitu jamani, Watu na VIPAJI Vyao.MIMI nitakuwa nakurushia Matukio tuu hapa.Na nikipata Muda nitaweza Kuwatembelea Wapishi Nyumbani kwao na Kuwawekea MAZUNGUMZO na MAPISHI HAPA!!AU VIPI WAUNGWANA.SWAHILI NA WASWAHILI!!!PAMOJA SANA TUU.