Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 7 June 2012

"Sing" for HM Queen Elizabeth II (Diamond Jubilee)!!!!!!!

Mmmmhhh Umoja ni Nguvu na Penye Wengi Pana Mengi!!!"Sauti tamuuu Twende Sote Waungwana,Lalalalalaaaaaaaaaaa.....Swahili na Waswahili" Pamoja sana!!!!

Wednesday 6 June 2012

Jikoni Leo; ni da'Maidana wa Tmark!!!!!!!!!

Mwenyewe da'Maidana,mamake na Taqqiyyah
Samaki na Mazagazaga na ameungwa/tiwa Nazi
Kitu Samaki kimepakuliwa
Samaki wa Kubanikwa
Visheti,Kashata,Keki, hivyo vyenye kidoti mie naviitaga vibata, sijui vyaitwaje?Hapa bado Ufuta jamani duuhh
Mikate,sijui wewe utaitaje kwani hapa kwangu kila mtu anajina lake!
                                           Ipo kwa umbo tofauti

Waungwana karibuni tena  "JIKONI LEO".Leo Mpishi wetu si Mwingine ni da'Maidana,Ni blogger Mwenza,Pia ni MjasiriaMali,Ukitaka kujua zaidi. Anapatikana.http://tmark-turn.blogspot.co.uk

Nimegundua Waswahili Wengi Wanapenda kupika na kujifunza Mapishi Mbalimbali.
Vipi wewe mwenzangu unapenda kupika?jee mbali na kupika Unapenda/Unaweza Kufanya  nini kwa Mikono yako?



Karibuni sana Waungwana katika yoote!!!!!!
"Swahili na Waswahili" pamoja sana!!!!

Tuesday 5 June 2012

SHUKRANI KUTOKA KWA MCHUNGAJI JOHN KUPAZA WA KANISA LA BAPTIST TANGA.


Marehemu Mama Mchungaji John Kupaza
Familia ya Mchungaji John Kupaza wa Kanisa la Baptist Kisosora Tanga anapenda kutoa shukrani zake za dhati kwa wale wote waliojaribu kuokoa maisha ya Mke wake Mpendwa Marehemu Mama Mchungaji Kupaza na wale walioshiriki kwa dhati katika shughuli za mazishi.
Mchungaji J. Kupaza anapenda shukrani zake za dhati ziwafikie Baptist Convention of Tanzania, Mwenyekiti wa Jumuiya Kuu ya Wanawake wa Baptist Tanzania, Dr. Lugano Mtafya, Umoja wa Makanisa ya Baptist Dar es salaam, Baptist Kanda ya Kaskazini, Umoja wa Makanisa Tanga, Manesi na Wauguzi wa Hospitali ya Muhimbili, Hospitali ya Cancer ya Ocean Road, Hospitali ya Bombo Tanga, Madaktari na wauguzi wa Magomeni Baptist Center, Majirani wote wa Mchungaji Kupaza na watoto wa Marehemu Sarah, Samwel, Rosemary, Dr. Lawi, Potinna, David na Tumaini wote kwa pamoja wanawashukuru wote mlioshirikiana nao katika kipindi hiki kigumu. Mungu awabariki wote.
Marehemu Mama Mchungaji Kupaza alifariki Tar. 18/05/2012 Jijini Dar es slaam na kuzikwa Tarehe 21/05/2012 Jijini Tanga katika makaburi ya Bombo.
BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE
AMEN.

Monday 4 June 2012

Mambo ya Igatanzania!!Ungana nami kujua zaidi!!!!!!

Haya Waungwana mambo ya Igatanzania hayo!!!
Niwauzaji wa T-shirt,Jezi,Kanga,Vitenge,Viatu vya shanga,Bangili,Makembe na vitu vyooote vya urembo kutoka nyumbani Tanzania.

 Pia ni Wapishi wa vitafunwa/Vitafunio,Vyakula vyooote ujuavyo vya kiswahili.
Pata kitu Roho inapenda na waswahili wa "Igatanzania"

Wapo Coventry u.k.

kwa mawasiliano zaidi piga namba hii.07730008921.

KARIBUNI SANA WAUNGWANA.

Orijino Komedi na -OK Msuruhishi wa Muungano-Msudani.avi

Hahahhhaahahhahah haya,Waungwana Mambo ya Tanganyika na Zanzibar!!!!!!
[Watoto wa mujini wanasema Kimenuka huko].


Sina la zaidi Mengi Mtasema Wenyewe!!PaMoja sana "Swahili na

 Waswahili"
Mungu ibariki Tanzania.

Sunday 3 June 2012

Nawatakia J'Pili Njema,Burudani- Upendo Nkone,Abihudi Misholi!!!!!!


6.Lakini nasema neno hili,Apandaye haba atavuna haba;Apandae kwa Ukarimu Atavuna kwa Ukarimu.
7.Kila mtu na Atende kama alivyokusudia Moyoni mwake,si kwa Huzuni,wala si kwa Lazima;Maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa Moyo wa Ukunjufu.
Neno la Leo:Wakorintho9:6-15.

Mungu atubariki Sote!!!!

Saturday 2 June 2012

Chaguo la Mswahili Leo-Tupo Burundi;Ndugu zangu wa Buyenzi Mpo?!!!!!

 Bibi na Bwana Billy.Hongereni sana Kwa kupata mtoto wa kiume.Mungu amlinde na kumkuza vyema.Nanyi awape hekima katika malezi yenu.Ngoja leo niwasogeze nyumbani.
 

Waungwana "CHAGUO LA MSWAHLI LEO" Nimewapeleka BURUNDI.
Haya umeona waRundi waishio CANADA wanavyofunza watoto wao Utamaduni wao?Jee wewe unaonaje kuhusu hili la kuwafundisha watoto mambo yakwenu?

Jee unao wakati wa kuwafundisha watoto hata Kibuzi,Kinyunyu,Ukuti,Rede,Nyimbo hata zile za Mchakamchaka?Au Muda hautoshi?

Nakumbuka kama wikimbili 2 tulikutana Waswahili kwenye Mnuso Mmoja hivi, Baada ya Kushiba Tukaanza kuimba hii Nyimbo.

Alisemaaa  Alisemaaa,Alisema Nyerere Alisema,Vijana wangu wote Mmeleegea, Sharti Tuanze Mchaka Mchaka.................Hahahahaa

 Swahili na Waswahili Waungwana.

 Kama unalolote utahitaji kuwajuza wenzio. Tutumie Kupitia Email.rasca@hotmail.co.uk.Pamoja sana!!!!!!