Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 30 April 2012

Wimbo Mpya "Uhuru wa Habari" kutoka Ngoma Africa band aka FFU





                  FFU wa Ngoma Africa Band wameachia Jipya "Uhuru wa Habari"
                  Unasikika at www.ngoma-africa.com


Kwa kawaida wanahabari na vyombo vyao ndio wanarusha hewani habari za
matukio mbali mbali pamoja wasanii na burudani zao kwa jamii,
Lakini bendi maarufu Ngoma Africa aka FFU imewageuzia kibao !!
Kuliweka hewani song jipya "Uhuru wa habari" wimbo huo mpya
utunzi wake kamanda Ras Makunja akiimba kwa kushirikiana na
kijana Christian Bakotessa aka Chris-B,ambaye pia ni mpiga
gitaa la solo(mtutu) wa kikosi kazi iko.
Bendi hiyo maarufu Ngoma Africa yenye makao yake kule ujerumani,
miezi michache tu iliachia hewani CD ya "Miaka 50 ya Uhuru" na sasa
wanarusha hewani "Uhuru wa habari" ,
Taarifa za kuhaminika zinaeleza kuwa Remix ya wimbo huo pia itakua
hewani siku za usoni,katika Remix hiyo kutakua na majina mengi ya wa
dau wa habari ambao wanachangia kuijulisha jamii habari mbali mbali.
Sikiliza na pata burudani ya bure katika ffu camp at www.ngoma-africa.com
au http://www.ngoma-africa.com


















Sunday 29 April 2012

Nawatakia J'Pili Njema;Burudani-liko lango moja wazi,Bwana Usehemu Yangu,Si Mbali



Nawatakia J'Pili Yenye Furaha,Upendo,Uvumilivu,Fadhili,Busara,Kiasi na Shukrani.
Utamlinda yeye ambaye moyo wake  Umekutegemea katika Amani Kamilifu,Kwa kuwa Anakutumaini
Neno la Leo;Isaya 26:3-4.
Mbarikiwe Woooote.

Friday 27 April 2012

Chaguo la Mswahili Leo-Sweet Mother ,Wagadu Gu,Colombia,!!!!!!!!



Wakaka na Karikiti!!!!
Haya Waungwa, yakale ni Dhahabu Waswahili wanasema au?
Kuna lolote unakumbuka hapa?


Inavuka soxxxx kinabakia kiatuuuu.
Muwe na wakati mwema!!!!!!!!

Wednesday 25 April 2012

Swali kutoka kwa Mwanamke wa Shoka[da'Mija] na Blogger wa Kwanza Mwanamke Mswahili!!!

Kwangu mimi ni Mwanamke wa Shoka huyu dada,Kichwa,mama Vipaji.
Ni Mwanamke wa Kwanza Blogger Mswahili mimi kumfahamu.blog yake http://damija.blogspot.co.uk
Da'Mija na Wanawake wa Shoka.
Swali;wewe Unafikiri Wanawake wa Shoka Wakoje?.

Haya tukiachana na hayo, Shuka Chini uone Swali lake analotaka KuJibiwa,Linatokana na  Mada ya Jikoni leo ni Kakazz.
Mama MM[Jina lake linaanzia na M,Mume wake M, watoto wao M.M]
Kidada zaidi au vipi!!Una mbwembwe wewe dadake.
Nanukuu..
"Swali;Eti Wanaume wengi wanaopenda Kupika na Kujifanyia kazi za ndani wenyewe Huchagua sana Wanawake wa Ku OA,Huchelewa KUOA au Kuto OA Kabisa?."


Nami ngoja niulize kulingana na swali.."Kwani nafasi ya mwanamke ni ipi katika ndoa..Je ni kupika na kufanya kazi za ndani? au kwa maana nyingine ni kwa nini hasa mwanaume huamua kuoa?


Wanaume tungependa majibu yenu zaidi hapa...

        

Monday 23 April 2012

Siku kama ya leo kaka Twahil Alizaliwa na Siku kama ya Leo Tulimpoteza baba yetu Kipenzi!!!!!!

Siku kama ya leo,Bibi na Bwana M.S.Kiwinga wa Ilala Sharifu Shamba,Dar-es-salaam.Walipata mtoto wa kiume na wakamwita Twahil.Mtoto huyu Siku alipofikisha umri wa miaka 9.Ndiyo Siku ambayo baba yetu, Kipenzi chetu,Muhimili Wetu,Faraja yetu,Rafiki yetu, yaani ni kila kitu Maishani mwetu,Marehemu M.S.KIWINGA.Aliga DUNIA!!! Ohhhhh Siku ambayo Familia hii hatuwezi kuisahau kamweee.

Tunamshuru Mungu kwa kila jambo.Kwani yeye huyu Mungu ndiye alisimamia makuzi yetu mpaka leo hii.


Hongera sana kaka Twahil, Mungu azidi kukubariki na kukulinda kila iitwapo Leo.
Tupo pamoja katika Siku yako hii muhimu japo ni siku ngumu kwetu.


Hongereni Wooote Mliozaliwa Leo na Pia Poleni sana mliopoteza Wapendwa wenu/wetu Leo.
Mungu awabariki na kuwalinda.


Wenu Rachel-siwa[Mwanapenza]hili mwanapenza ni jina la mama wa baba yangu mzazi[BIBI, Asha Penza]. Basi  baba yetu  alikuwa hupenda kutuita watoto wa kikeMAMA.
                       PAMOJA SANA,UPENDO DAIMA!!!!!!

Sunday 22 April 2012

J'Pili iwe njema kwa Wote!!Burudani-Jehovah You are the most high God na-Igwe Midnighi Crew!!!!

Muwe na J'pili njema yenye Amani na Baraka.
Akawagawanyia Lea, na Rahel, wale vijakazi wawili,wana wao.
Neno la leo;Mwanzo33:1-11.
Pamoja sana katika yote Wapendwa.

Saturday 21 April 2012

Chaguo la Mswahili Leo;Professor Jay -Anasema- hapo vipi?kama Ipo,Ndiyo Mzee!!!!!!!

Nawatakia J'Mosi Njema yenye Amani,Upendo,Uvumilivu na Umoja!!!
Burudani na Maneno muruwaaa kutoka kwake Mswahili Professor Jay-Msikilize kwa makini.NDIYO MZEE!!.
Pamoja Sana, Hapo Vipi?

Thursday 19 April 2012

MWAKILISHI MKAAZI WA UNOPS NDUGU OMARY MJENGA AKIBADILISHANA MIKATABA YA UJENZI WA HOSPITALI YA WATOTO NCHINI SIERA LEONE




Ndugu Mjenga wakijadiliana jambo na Naibu Mwakilishi wa UNICEF Bw Gopal Sharma wa nchini Siera Leone

Kutoka kulia ni Bwana Omar Mjenga, Mwakilishi Mkazi wa UNOPS Nchini Sierra Leone, akibadilisha mikataba ya ujenzi wa hospitali tatu za kisasa za watoto na Naibu Mwakilishi wa UNICEF Bw Gopal Sharma aliyemwakilisha Bw Mahimbo Mdoe ambaye ni Mwakilishi Mkazi wa UNICEF Nchini Sierra Leone na Kushoto, ni mwakilishi wa Waziri wa Afya wa Siera Leone.


Bw Mahimbo ni Mtanzania mwingine mwenye cheo cha uwakilishi. Mtanzania mwingine mwenye cheo cha uwakilishi ni Bw Gabriel Rugalema, ambaye ni Mwakilishi Mkazi wa FAO Nchini Sierra Leone. Tanzania inazidi kutamba katika nyanja za kimataifa


Habari hii nimetumiwa na KapingaZ Blog. http://kapingaz.blogspot.co.uk
Ahsanteni sana.

Wednesday 18 April 2012

Jikoni Leo ni Kakazzz,Burudani-Tmk wanaume family - Dar mpaka moro!!!!!!

Kina kaka walioandaa huu msosi.
Kachumbari

Samaki au dagaa?
vipi hapo ugali utaisha?
Mimi nafikiri mboga za leo mwenzake Nguna/Ugali,Jee mwenzangu?
Mboga ya Majani. Jee ukishiba utashushia na nini?

Waungwana Wanaume Leo ndiyo waliotuandalia Chakula,
Kumbe wakiamua wanaweza,Huko nyuma tulijadili kuhusu ''WANAUME NA JIKO'',Kaka S. [Sam mwana wa  Mbogo]Alielezea vyema sana, Hasa yeye anavyohusika Jikoni.Pia akasema Wanawake wengi wakisaidiwa huwa Wanatabia ya Kujisahau.


Kaka zangu hawa nao wanasema wao hupenda kujipikia zaidi kuliko kupikiwa.


Swali;Eti Wanaume wengi wanaopenda Kupika na Kujifanyia kazi za ndani wenyewe Huchagua sana Wanawake wa Ku OA,Huchelewa KUOA au Kuto OA Kabisa?.


Jee wewe Mwenzangu una Maoni,Ushauri Gani? Pamoja sana!!!

Sunday 15 April 2012

Nawatakia J'Pili njema,Burudani-ni wewe baba unaweza na Sifa ni kwako- living water choir!!!!!!!

Muwe na J'Pili Njema woote, Yenye Amani,Furaha, Upendo na Umoja.
Mungu akasema Iwe nuru;Ikawa nuru. Mungu akaiona Nuru,ya kuwa ni njema; Mungu akatenga nuru na giza.
Neno la Leo.Mwanzo1:1-8.
Mbarikiwe sana,Upendo Daima.

Friday 13 April 2012

Chaguo la Mswahili Leo;Swahili Taarab Bi Malika - Sitaki sitaki na Vidonge,Isaa Matona-Msumeno!!

Waungwana Mwajionaje na Khariiii?Teheheheeheh .Nimatumaini yangu woote wazima,Leo nimewaletea Taarab za Zamani kidogo,Hizi Taarab hasa hizi za Zamani zinamafumbo sana, yaani kunamaneno mengine unaweza usiyaelewe anamaanisha nini.
Jee wewe ni mpenzi wa Taarab au huwa unasikiliza/kuangalia au kucheza?
Unaona tofauti gani kati ya Taarab za Zamani na sasa na jee Unafikiri Taarab za Zamani Zinamvuto zaidi ya sasa au Za Sasa Zinamvuto kuliko za Zamani?
Karibuni sana kama hujahi kuzisikia Leo jaribu, na Wapenzi wa Taarab Jimwageni Uwanjani au...Swahili na Waswahili.Pamoja sana tuu!!!!!

Thursday 12 April 2012

Siku kama ya leo da'Victoria-Ruth Alizaliwa!!!!!!

Siku kama ya leo Bibi na Bwana Malonga wa Tanga,Walipata mtoto wa kike na wakamwita Victoria-Ruth.
Hongereni sana wazazi/Walezi na Mungu awabariki sana.


Hongera sana da'Vick-Ruth kwa kuongezeka,Mungu azidi kukubariki na kukulinda siku zote za maisha yako.
Uwe baraka kwa wazazi/walezi ndugu,jamaa ,marafiki  na watu wote wadogo kwa wakubwa.
Uwe na Wakati mzuri leo na siku zote.MUNGU NI PENDO.


Swali la Kizushi:Wapendwa eti watu wenye kutumia the,thatha badala se au sasa,Athante,ASante,walipokuwa watoto walinyonya vidole sana,walideka,walichelewa kuongea au.......


Karibuni Waungwana!!!!!!

Tuesday 10 April 2012

Maelfu ya watanzania wajitokeza kumzika Kanumba Jijini Dar !!..pata na [Video]


Safari ya Mwisho ya Mpendwa wetu Kanumba.Sisi Tulikupenda Lakini Mungu amekupenda zaidi.Ulale kwa Amani.
Picha kwa Masaada wa kaka LUKAZA wa http://josephatlukaza.blogspot.co.uk,Ubarikiwe.
Video kwa msaada wa[ Michuzi blog]http://issamichuzi.blogspot.co.uk.Ahsanteni Sana na   Tulie kwa Amani yeye Amekwenda..

Steven Kanumba (kauli yake ya mwisho) [HD]

Monday 9 April 2012

MAMA KANUMBA KAFIKA DAR NA RATIBA YA MAZISHI KAMA IFUATAVYO!!

 


WAKATI MAOMBOLEZO YA MSIBA YAKIENDELEA VIONGOZI MBALIMBALI WAKIFIKA KUTOA MKONO WAPOLE  AMBAPO LEO MHESHIMIWA PREZIDAR J.K ALIFIKA NYUMBANI KWA KANUMBA KUTOA MKONO WA POLE, NA KESHO ASUBUHU WAZIRI MKUU MHESHIMIWA PINDA ANATARAJIWA KUFIKA  KUTOA MKONO WA POLE KABLA YA KUELEKEA MKOANI DODOMA KWA AJILI YA BUNGE LINALOANZA JUMANNE
 RATIBA YA MAZISHI IMETOLEWA RASMI AMBAPO MAZISHI YAMEPANGWA KUFANYIKA SIKU YA JUMANNE KAMA ILIVYOKUWA IMEPANGWA, MAREHEMU ATAAGWA KATIKA VIWANJA VYA LEADERS CLUB AMBAPO KUANZIA SAA 4 SHUGHULI ZA MISA NA KUAGA MWILI ZITAANZA NA KISHA MAREHEMU ATAZIKWA KATIKA MAKABURI YA KINONDONI JIJINI.
R.I.P KANUMBA
Habari hii kutoka http://8020fashions.blogspot.co.uk.

Ahsanteni sana.

Saturday 7 April 2012

MAMA KANUMBA AONGEA;Mmmmmhh Pole sana Mama!!!!!!

Mama Mzazi wa Kanumba.
Mmmmhh,Pole sana Mama,Mungu akutie nguvu.
Picha na Video,kutoka ;http://bukobawadau.blogspot.co.uk   Ingia hapo kujua zaidi.Ahsanteni sana.

Ulale kwa Amani Kaka Steven Kanumba!!!!!

Steven Kanumba Enzi za Uhai Wake.
Poleni sana Ndugu,Jamaa,Marafiki,Majirani,WaTanzani na Wapenzi Woote Wa KANUMBA!!
Sisi tulimpenda sana Lakini Mungu amempenda zaidi,Tulie na Kumshukuru Mungu kwa Kila jambo,Sote ni Wapitaji katika hii Dunia,Mwenzetu Ametangulia,Inauma sana lakini hatuna Jinsi,Tukumbuke na Kuenzi Mema yote aliyoyatenda.Tuwe tayari wakati wote kwani hatujui Siku wala Muda,Tupendane na Tusameheane.Mungu awatie Nguvu Wafiwa katika Wakati huu Mgumu.
BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA JINA LAKE NA LIHIMIDIWE MILELE;
AMINA.

Thursday 5 April 2012

Watoto na Mitindo,Kutoboa/Kutoga Masikio!!!!

Haya Waungwana;Wazazi/Walezi Unaonaje watoto kutoboa/kutoga masikio wakiwa Wadogo?jee Tunawafurahisha au Tunajifurahisha?ni vyema atoboe/kutoga yeye mwenyewe akikua au bora tuwafanyie labda wakikua watatulaum?
Karibuni Sana kwa Maoni na Ushauri.Pamoja!!!!!!

Tuesday 3 April 2012

Shilingi ya ua tena Maua!!!!!!!


Waungwana sina la kuongezea hapo!!Jee Pesa ni kila kitu?Karibuni sana kwa Maoni na Kuelimishana kwa Upendo.

NDG. OMARY MJENGA MWAKILISHI WA UNOPS NCHINI SIERA LEONE AMALIZA ZIARA YAKE NCHINI.


Ndg. Omary Mjenga akipiga picha ya kumbukumbu wakati alipokwenda kumtembelea na kumuaga Rais Jakaya Kikwete jana Ikulu.
Hapa ndugu Mjenga akipiga picha na Naibu Waziri wa Jinsia, Watoto na maendeleo ya jamii, wakati alipokwenda kumtembelea.

Baada ya kutoka kuonana na Viongozi hao alishiriki Dinner Party na Wanafunzi wenzake aliosoma nao Shule ya Sekondari Songea Boys ndani ya viunga vya Rose Garden akiwemo na Naibu Waziri wa Elimu na Ufundi Mh. Philipo Mulugo.
Picha zaidi mtazipata baadae za tukio hili la kihistoria, ambalo kwa mara ya kwanza lilifanyika katika Pub ya KAPINGAZ Pub wakati huo tukimpongeza Naibu Waziri Mh. Mulugo kwa kuteuliwa.
Wana BOX 2 (Wana Luhila) walimpendekeza Ndg. Henry O. Kapinga kuwa Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo mpaka pale tutakapo itisha uchaguzi Rasmi.

Omary Mjenga anaondoka leo kurudi Siera Leone tayari kwa kuendelea na kazi zake za UNOPS.

Habari kutoka http://kapingaz.blogspot.co.uk/
Ahsante sana.

Sunday 1 April 2012

Nawatakia J'Pili Njema,Burudani-AIC Chang'ombe na Bahati Bukuku,Sikiliza mwenyewe!!


Wapendwa muwe na J'Pili yenye Amani na Baraka Tele!!!!!!Neno la Leo;zaburi:12;1-8.Bwana UokoeMaana Mcha Mungu amekoma,Maana Waaminifu wametoweka katika Wanadamu.....Endelea.