Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Saturday 31 March 2012

Chaguo la Mswahili Leo,mambo ya Taarab-Utalijua Jiji!

Haya Waungwana mambo hayo, hahaaaa Mambo ya Taarab... Swahili na Waswahili twende Sote sasa!!

Thursday 29 March 2012

MAZISHI YA MAREHEMU DENIS OSWALD KAPINGA


Ndg. Joseph Oswald Kapinga

Ndugu Joseph Kapinga pichani hapo juu anapenda kuwajulisha ndugu, jamaa na marafiki kuwa Ratiba ya mazishi ya mpendwa mdogo wetu Denis O. Kapinga yatafanyika leo Tarehe 29/03/2012 katika makaburi ya Sinza karibu na ukumbi wa mwika.

Ratiba itakuwa kama ifuatavyo:

Mwili wa marehemu utafika Nyumbani maeneo ya Sinza karibu na New White Inn Bar bara bara ya Sinza uzuri mnamo saa 6.00 Mchana kutoka Hospitali ya Mwananyamala.

Mwili utaagwa nyumbani saa 7.00 Mchana na baadae utapelekwa kanisa la Roman Catholic Sinza kwa Ibada.

Baada ya hapo Saa 8.30 Mchana mwili wa marehemu utapelekwa Makaburi ya Sinza kwenye nyumba yake ya milele.

"BWANA ALITOA NA BWANA 

Poleni sana Familia ya Kapinga.
Swahili na Waswahili tunaungana nanyi katika wakati huu mgumu kwenu.

Mungu awatie Nguvu.
Ulale kwa Amani kaka Denis.O.Kapinga.

Tuesday 27 March 2012

Jikoni Leo-Ni kwa Mama Mwakitalu!!!Pata na Burudani ya Ngoma!!!!![Mwanamke jiko au Mwaume Jiko?]



Da'Masika/mama Mwakitalu
Mboga za Majani Mchanganyiko,Majani ya Kunde na Majani ya Maboga
Mchuzi wa Samaki Umeungwa/wekwa Nazi na nyanyachungu

Maandaziiiiii na hapo chini ni Mahindi ya Kuchemsha.

Haya Waungwa,vipi wewe unapenda kupika?au Unapika kwasababu ni lazima upike na ule?Kwenye kazi za Nyumbani kila mmoja kuna kazi anapenda kuifanya, Na kuna baadhi ya Kazi hatuzipendi,Lakini tunafanya kwa sababu ni lazima zifanywe,Na utasikia duuh yule kaka/dada au Mama/Baba anajua Kupika sana,Hivi kujua kupika ni Chakula kiive au?
Kwani Utamu/Radha ya chakula wewe unaweza kupendezwa nacho na mwingine asipendezwe nacho.
Jee Kazi/Ujuzi wa Kupika ni kwa Wanawake tuu?Kwani mara nyingi utasikia Mwanamke jiko na si Mwanaume Jiko,Hasa kwa Maisha ya Leo,
 kwa Maisha ya Zamani wengi wao Mama/Dada kazi yao kubwa ni Upishi na Baba wengi ndiyo walikuwa wanafanya Kazi hasa Mijini, Kwa Vijijini Woote BABA na MAMA Wanaenda shambani lakini Kupika ni MAMA.Jee Leo Tunaweza Thubutu kusema MWANAUME JIKO? AU TUTAKUA TUMEWADHALILISHA?Kwani wapo Wanakarangiza haswaaaa kutushinda au Hamjakutana nao?.


Karibuni Waumgwana kwa Mawazo na Kuelimisha na Kwa upendo.

MWAKILISHI WA UNOPS NCHINI SIERA LEONE NDUGU OMARY MJENGA AKISALIMIANA NA RAIS KIKWETE WAKATI WA MAZISHI YA MKUU WA WILAYA YA LIWALE MAREHEMU VICTOR P. CHIWILE JANA KIBAHA.


Mmoja wa waombolezaji akimsalimia Rais Kikwete kwa kuibusi Pete yake, kulia ni Ndugu Omary Mjenga akishuhudia tukio hilo.
Rais akisalimiana na Ndugu Omary Mjenga jana walipokutana kwenye mazishi ya Mkuu wa Wilaya ya Liwale.
Ndugu Mjenga alikuwa Personal Secretary wa Rais Kikwete wakati alipokuwa Waziri wa Mambo ya Nje kabla hajawa Rais.

Habari hii nimetumiwa na KapingaZ Blog. http://kapingaz.blogspot.co.uk/
Ahsante Sana.

Sunday 25 March 2012

Nawatakia J'Pili Njema Woote!!Burudani-AIC Chang'ombe Vijana Choir - Hakuna

Nawatakiaeni J'pili njema yenye kheri,Baraka,Upendo na Utu wema.
Neno la Leo;Zaburi ya 121:1-8.Nitayainua Macho yangu niitazame Milima,Msaada wangu Utatoka Wapi?Endelea.
Nijambo Gani linalomshinda MUNGU BABA?.

Saturday 24 March 2012

Chaguo la Mswahili Leo-Twanga Pepeta - Mtu Pesa na nyingine nyingi!!!

Papaa Sunday, Yeye ndiyo aliyenianzishia wana Twangwa leo, Ahsante kaka yangu, Duhh Pia nimekumbuka Mengi sana Ndugu yangu. Papaa Huyu tumecheza nae sana Mpira wa Makaratasi,Makonzi , Hahahahhaaha Enzi za Masonge muuza Mihogo,Mzee wasiwasi ooohhiiii. Tumetoka mbali sanaaaaa!!Hili nitalikumbushia siku nyingine, Pata Burudani na Nawatakia J'mosi Njeeeeeemaaa!!!Mimi nawapenda Wooote Waungwana. Twende Sote sasa.Twanga pepeta Inapendaga Watu Woteeee ehhhh ohhhhh Ehhhheee!!!!!!!

Wednesday 21 March 2012

Waswahili na Maisha Yao - Zanzibar na Mwaka Kogwa Festiva-Burudani Marashi ya Pemba!!


Waungwana Waswahili wa Zenji wanamambo yao,Unajua kuhusu Mwaka Kogwa?Sijui ni Matambiko,Michezo,Sherehe au?Jee mpenzi msomaji Umeshawahi kukutana,Kuona,Kushiriki Mwaka Kogwa?Hivi wanavyotandikana, Kama kunamtu unasababu nae si ndiyo Utamtandika Kwa hasira?Jee Mwaka Kogwa wanaruhusu kushiriki mtu yeyote au mpaka uwe Mzaliwa wa huko?
Karibuni sana Waungwa!!

Waswahili na Maisha yao!!!!!!!

Hakuna linaloshindikana au?Asante mwanangu Amina kwa kazi nzuri,Joto sasa basi.Kumbe inawezekana!!!!

Sunday 18 March 2012

J'Pili ya leo ni Maombi kwa Wajane,Yatima , Wenye shida na Tabu; Kabula anasema Dhihirisha na Upendo anasema Hapa Nilipo!!!!!!!


Leo ni siku ya Mama,Tuwaweke kwenye Maombi,Sala,Dua, Wajane,Yatima, Wenye Shida na Tabu.Mungu awasimamie katika Maisha yao Wajane na Yatima,Mungu uwaguse wenye Shida na Tabu, Wengine wanahitaji Watoto,Wanahitaji kuwa MAMA/BABA,Kuna wanohitaji Wenza/Ndoa,Elimu,Chakula,Malazi,Upendo,Faraja.Wagonjwa walio Hospitalini na Majumbani.Waliokata Tamaa.Waliopoteza Wapendwa wao katika Majanga mbalimbali.Walio vitani.Na mengine Meengi. Mungu uwaguse kwa Mkono wako wenye Nguvu.

Neno la leo;Matendo ya Mitume:9;36-43.Na Mwanafunzi mmoja alikuwa Yafa Jina lake Tabitha,Tafsiri yake ni Dorkasi[yaani Paa];Mwanamke huyu  alikuwa amejaa matendo mema na sadaka alizozitoa.Endelea na Uwe na wakati mwema.

Saturday 17 March 2012

Chaguo la Mswahili Leo-Congo - Pepe Kalle!!!!!!!

Nawatakieni J'mosi njema!Kumbuka Enzi zako, hahah wapi dada Mwasu KLM, my Wifi Neema Nyanyile, Mama Kisa na da' Nana Msilie wapendwa wangu,Enzi hairudi ikipita imepita, kumbukumbu ipo lakini..Waungwana nini Mnakumbuka kukisiliza nyimbo hizi?.Twende sote sasa Anakala Manzeeeeee!!!!!!!!.Pamoja sana.

Thursday 15 March 2012

Mswahili Wetu Leo; DR. SHABANI KACHUA MTANZANIA ANAEIPEPERUSHA VEMA BENDERA YA TANZANIA NCHINI CANADA



Dr. Engineer Shabani G Kachua akijiandaa kuingia kwenye Professional Engineer Induction Ceremony nchini Canada
Hapa Dr. Kachua akionyesha moja ya Nishani aliyotunukiwa siku hiyo
Dr Kachua akiwa amesimama kwa nyuma na Mainjinia wenzake
Akipiga picha ya pamoja kwa kumbukumbu na mainjinia wenzake.
Kwa niaba ya Watanzania ninapenda kukupongeza kwa kuipeperusha vema Bendera ya Tanzania.

Habari hii nimetumiwa na KapingaZ Blog.http://kapingaz.blogspot.com/

Ahsante sana.

Wednesday 14 March 2012

Watoto na Urembo,Wanapaka Shedoooooo!!!!!!

Wazazi/Walezi hapo vipi?Kuna msemo sikuhizi; Aku babu najiremba mie napishana na Uzee!Nao Watoto sasa;Aku bibi nakufuata hukohuko!!Mambo ya kileo hayo, Zamani ulikuwa huruhusiwi kupaka,Wanja,Poda na vipodozi vingine, mpaka siku ya KUOLEWA!!Eti ukipaka  kabla,Siku ya Arusi hautapendeza!!Na walikuwa Wakisuka Nywele Ufunge kilemba mpaka MUMEO kwanza Aone!!''Hizi hadithi mie nazisikia''.Hahahahahha Ohiiii Leo hii nani umfungishe Kilemba?Tena ukienda salon ndiyo unafunga kilemba kama nywele zimeharibika, ukimaliza tuu kilemba kuleeee,Wataanza kuona kina baba/mama John,Juma,Neema,Pili na mnaopishana Njiani, hee dada wewe Umependeza, Umetoka Chicha na..Nani kakusuka dada mmoja anaitwa YASINTA NGONYANI!!!Muwe na Wakati Mwema Waungwa, Karibu Sana sana.

Tuesday 13 March 2012

Wanawake na Mitindo ya Nywele,Pata na kideo Jinsi ya kuweka Nywele Bandia!!!!!!

Haya Waungwana Mitindo ya Nywele kwa Wanawake, Mmmh lakini kwa sasa hakuna cha Wanaume wala cha Wanawake, kila mmoja  anajaribu kuingilia Mitindo ya Jinsia nyingine,Au labda mimi ndiyo sielewi, kwamba hakuna Mitindo ya Wanawake na Wanaume Wote ni Sawa!!!!Wewe uliyepita hapa unaonaje?
Swali ;Wanaume wengi Wanaofanya Kazi  SALON zA Wanawake Wengi wao/Baadhi yao ni MASHOGA?

Sunday 11 March 2012

Nawatakia j'Pili Njema Wapendwa,Burudani,Rose Muhando-Tamalaki''Na nyingine Mpya!!



Mzee,kwa Gayo mpenzi,nimpendaye katika kweli.2Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako kama vile roho yako ifanikiwavyo.Neno linapatikana;WARAKA WA TATU WA  YOHANA:soma 1-13.15;Amani kwako,Rafiki zetu wakusalimu.Wasalimu hao rafiki zetu,kila mtu kwa jina lake.Mbarikiwe sana!!!mimi nabarikiwa sana na nyimbo nyingi kupitia hapa kwa Kaka yangu Matondo.http://nyimbozadini.blogspot.com/

Saturday 10 March 2012

Wanawake na Mitindo-da'Levina na Rafiki zake!! Chaguo la Mswahili-Yvonne Chaka - Mamaland na Umgombothi


                                         Da'Levina[Aliye shika kiuno] na Rafiki katika poziii
                                         Dadazzz mmependeza mnoo,Asanteni sana  kwa kutuwakilisha.Siku ya Wanawake ,Wao walijumuika na wenzao kwa Shamim.Duuhh kivazi cha kanga kikitengenezwa, kinapendeza haswaaa.Wanawatakia Wanawake Woote Duniani ,Baraka, Amani,Upendo na Umoja.WANAWAKE JUU!!!

Thursday 8 March 2012

Nawatakia kheri na Baraka, Wanawake wote!!Burudani,Vicky Kamata - Wanawake Maendeleo


Namshukuru Mungu kwa kuniumba  Mwanamke,Najivunia kuwa Mwanamke!Nawatakia Wanawake wenzangu woote Kheri,Baraka,Upendo,Utuwema,Fadhili na Yootee yanayostahili.Wanawake Tujiheshimu na Kuheshimu Wengine,Tupendane na Tujipende,Tushirikianae na Kuelimishana,Tusamehe nasi Tusamehewe.Wanawake wa Zamani hata akiwa mama wa Nyumbani lakini alikuwa anakitu kidogo cha kufanya,kama, Kusuka ukili,Kufuma vitambaa,Biashara ndogo ndogo,Kushona na mambo meengi ili kuongezea kipato.Hata Wanawake wa sasa hatuja chelewa, kama hakuna Ajira basi Tunaweza Kusjishughulisha,hakuna asiyeweza kufanya lolote na hakuna aliye zaliwa anaweza.Japo masoko yamekuwa magumu,lakini Tusikate Tamaa.Pale tunapokwama tusisite kutafuta Ushauri na maelekezo, Kwani kuuliza si Ujinga.Mungu awabariki sana,WANAWAKE JUUU!!!!!

Tuesday 6 March 2012

Kaka Farid atimiza miaka 14-Ona mambo yake!!!

                                               Poziii
                                     Mpirani
                          Shughulika baba!!!!
                                             Vituko
                                           Mapenzi kwa mama.
Hongera sana kaka Faridi kwa kutimiza miaka 14,Mungu akubariki na kukulinda wakati wote.
Uwe baraka kwa wazazi na watu wote.
Hongera pia Wazazi na Mungu awape Maarifa, Usimamizi na Mema  Yote kwenye Malezi.


Waungwana; Eti watoto Wengi  wa  Kiume ni rafiki/wapo karibu  sana na MAMA kuliko BABA?
Pamoja Wapendwa!!

Monday 5 March 2012

Wanawake na Mitindo Leo-Da'SUBIRA WAHURE DESIGNS!!!!!!



Waungwana Wanawake wa leo wapo mbio sana kutafuta/Kusaidiana katika Maisha.
Da'Subira anaomba  wenye mapenzi mema,wamsaidie kufikisha Ujumbe huu.
Hizo ndizo kazi afanyazo.
Ukitaka kumfahamu zaidi ingia.http://www.subirawahure.blogspot
  Hongera sana da'Subira,Kazi nzuri na Mungu akubariki kwa kazi zaMikono yako!!
                         























Sunday 4 March 2012

Nawatakia J'Pili Njema!!Burudani- Sauti Ikatoka na Mimi Yesu!!!!!!


Mzee kwa mama mteule na watoto wake niwapendao katika kweli;Wala si mimi peke yangu,Bali na wote waijuao ile kweli.2Kwa ajili ya hiyo kweli ikaayo ndani yetu,Nayo itakuwa pamoja nasi hata milele.Neno la Leo:WARAKA WA PILI WA YOHANA..Nawatakia J'Pili yenye Upendo na Amani!!!!

Saturday 3 March 2012

Chaguo la Mswahili Leo-Ngoma & Kidumbak na Ahmada Umelewaaaa!!

Haya Waungwana  pata Burudani Muruwaaaaa!!!!!Mambo ya Zenji au?? Ngoma ya Kidumbaku,, na Kingine ni Ahmada Umelewaa, sijui hii ni chakacha au Taarabu, Jibu utalipa ukisikiliza, na unaweza kutujuza nasie!!!Karibuni sana. Waungwana kila J'Mosi kuna chaguo la Mswahili,si mimi Pekeyangu nawe kama unataka Kuchagua Mziki,Ngoma na......Ruksa nitumie Email, rasca@hotmail.co.uk  Swahili na Waswahili Waungwana  au Vipi?Twende Sote sasa!!!!!