Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 29 March 2019

Kikombe Cha Asubuhi ;Zaburi 92...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Katika nchi ya Misri ulifanya maajabu, ukatenda miujiza, na unaendelea kufanya hivyo mpaka leo miongoni mwa Waisraeli na katika mataifa mengine pia, jambo ambalo limekufanya ujulikane kila mahali.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Kwa maajabu na miujiza uliyowatisha nayo Wamisri, uliwatoa watu wako Misri kwa nguvu zako nyingi na uwezo wako mkuu. Uliwapa nchi hii ambayo uliahidi kuwapa wazee wao, nchi inayotiririka maziwa na asali.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Nao walifika, wakaitwa na kuimiliki. Lakini wao hawakukusikiliza, wala hawakufuata sheria zako. Hawakutenda mambo uliyoamuru. Ndiyo maana utawafanya wapatwe na balaa hii.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....
Nawapenda.

Wimbo wa kumsifu Mungu
(Zaburi. Wimbo wa siku ya Sabato)
1Ni vema kukushukuru, ee Mwenyezi-Mungu,
kuliimbia sifa jina lako, ee Mungu Mkuu.
2Ni vema kutangaza fadhili zako asubuhi,
na uaminifu wako nyakati za usiku,
3kwa muziki wa zeze na kinubi,
kwa sauti tamu ya zeze.
4Ee Mwenyezi-Mungu, matendo yako yanifurahisha;
nitashangilia kwa sababu ya mambo yote uliyotenda.
5Matendo yako, ee Mwenyezi-Mungu, ni makuu mno!
Mawazo yako ni mazito mno!
6Mtu mpumbavu hawezi kufahamu,
wala mjinga hajui jambo hili:
7Kwamba waovu waweza kustawi kama nyasi,
watenda maovu wote waweza kufanikiwa,
lakini mwisho wao ni kuangamia milele,
8bali wewe, ee Mwenyezi-Mungu, u mkuu milele.
9Hao maadui zako, ee Mwenyezi-Mungu,
naam, hao maadui zako, hakika wataangamia;
wote watendao maovu, watatawanyika!
10Wewe umenipa nguvu kama nyati;
umenimiminia mafuta ya kuburudisha.
11Kwa macho nimeona maadui zangu wameshindwa;
nimesikia kilio chao watendao maovu.
12Waadilifu hustawi kama mitende;
hukua kama mierezi ya Lebanoni!
13Kama miti iliyopandwa nyumbani mwa Mwenyezi-Mungu,
hustawi katika nyua za Mungu wetu;
14huendelea kuzaa matunda hata uzeeni;
daima wamejaa utomvu na wabichi;
15wapate kutangaza kwamba Mwenyezi-Mungu ni mnyofu,
Mwamba wangu, kwake hamna upotovu.


Zaburi92;1-15

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 28 March 2019

Kikombe Cha Asubuhi ;Zaburi 91...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Mwenyezi-Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi: “Chukua hati hizi zote mbili, hati hii ya kumiliki shamba iliyotiwa sahihi, na hii nyingine iliyo wazi, uziweke katika chungu ili zipate kuhifadhiwa kwa muda mrefu.” Maana Mwenyezi-Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi: “Nyumba na mashamba, pamoja na mashamba ya mizabibu katika nchi hii yatanunuliwa tena.”
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Baada ya kumkabidhi Baruku mwana wa Neria, hati ya kumiliki shamba nilimwomba Mwenyezi-Mungu nikisema: Ee Mwenyezi-Mungu, ni wewe ambaye kwa nguvu zako nyingi na uwezo wako mkuu, umeziumba mbingu na dunia; hakuna kisichowezekana kwako. Wewe unaonesha fadhili zako kwa maelfu ya watu; lakini pia unawaadhibu watu kwa sababu ya dhambi za wazee wao. Wewe ni Mungu mkuu, mwenye nguvu, Mwenyezi-Mungu wa Majeshi ndilo jina lako.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Wewe unapanga kwa hekima na unafanya maajabu; njia za watu wote ziko wazi mbele yako, unamlipa kila mmoja kadiri ya njia zake na matendo yake.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....
Nawapenda.

Mungu mlinzi wetu
1Anayekaa chini ya ulinzi wa Mungu Mkuu,
anayeishi chini ya kivuli cha Mungu Mwenye Nguvu,
2ataweza kumwambia Mwenyezi-Mungu:
“Wewe ni kimbilio langu na ngome yangu;
Mungu wangu, ninayekutumainia!”
3Hakika Mungu atakuokoa katika mtego;
atakukinga na maradhi mabaya.
4Atakufunika kwa mabawa yake,
utapata usalama kwake;
mkono wake91:4 mkono: Au uaminifu. utakulinda na kukukinga.
5Huna haja ya kuogopa vitisho vya usiku,
wala shambulio la ghafla mchana;
6huna haja ya kuogopa baa lizukalo usiku,
wala maafa yanayotokea mchana.
7Hata watu elfu wakianguka karibu nawe,
naam, elfu kumi kuliani mwako,
lakini wewe baa halitakukaribia.
8Kwa macho yako mwenyewe utaangalia,
na kuona jinsi watu waovu wanavyoadhibiwa.
9Wewe umemfanya Mwenyezi-Mungu kuwa kimbilio lako;
naam, Mungu aliye juu kuwa kinga yako.
10Kwa hiyo, hutapatwa na maafa yoyote;
nyumba yako haitakaribiwa na baa lolote.
11 Taz Mat 4:6; Luka 4:10 Maana Mungu atawaamuru malaika zake,
wakulinde popote uendapo.
12 Taz Mat 4:6; Luka 4:11 Watakuchukua mikononi mwao,
usije ukajikwaa kwenye jiwe.
13 Taz Luka 10:19 Utakanyaga simba na nyoka,
utawaponda wana simba na majoka.
14Mungu asema: “Nitamwokoa yule anipendaye;
nitamlinda anayenitambua!
15Akiniita, mimi nitamwitikia;
akiwa taabuni nitakuwa naye;
nitamwokoa na kumpa heshima.
16Nitamridhisha kwa maisha marefu,
nitamjalia wokovu wangu.”


Zaburi91;1-16

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Wednesday 27 March 2019

Kikombe Cha Asubuhi ;Zaburi 90...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Yeremia akasema, Mwenyezi-Mungu alinena nami akasema: “Hanameli, mwana wa baba yako mdogo Shalumu, atakujia na kusema: ‘Nunua shamba langu lililoko Anathothi, maana wewe ni ndugu yangu kabisa, na unayo haki ya kulikomboa.’” Kisha binamu yangu Hanameli alinijia katika ukumbi wa walinzi kama alivyonifahamisha Mwenyezi-Mungu, akaniambia, “Nunua shamba langu lililoko Anathothi katika nchi ya Benyamini maana wewe una haki ya kulikomboa. Linunue kwa faida yako.” Ndipo nilipotambua kwamba lilikuwa kweli neno la Mwenyezi-Mungu.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizo zifanya
Kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....


Basi, nililinunua shamba hilo lililoko Anathothi, kutoka kwa binamu yangu Hanameli, nikamlipa bei yake shekeli kumi na saba za fedha. Nikaitia sahihi hati ya kumiliki, nikaipiga mhuri, nikawaita mashahidi na kuipima ile fedha katika mizani. Kisha, nilichukua ile hati ya kumiliki niliyoipiga mhuri, ambayo ilikuwa na masharti na kanuni, pamoja na nakala nyingine iliyokuwa wazi.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe....
Yahweh  tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni

Yahweh ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetuBaba wa Mbinguni tukanene yaliyo yako
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe

Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Nilimpa hiyo hati ya ununuzi Baruku mwana wa Neria mwana wa Maaseya, mbele ya binamu yangu Hanameli na mashahidi waliokuwa wametia sahihi hati ya ununuzi, na mbele ya Wayahudi wote waliokuwa wameketi katika ukumbi wa walinzi. Mbele ya watu wote hao, nilimpa Baruku maagizo yafuatayo:
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,
wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Jehovah ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu kila mmoja na mahitaji yake...
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao....
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako,
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele....
Amina..!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,
Mungu Baba aendelee kuwatendea sawasawa na mapezni yake...

Nawapenda.

KITABU CHA NNE
(Zaburi 90–106)
Mungu wa milele na binadamu kiumbe
(Sala ya Mose, mtu wa Mungu)
1Ee Bwana, tangu vizazi vyote,
wewe umekuwa usalama90:1 neno kwa neno: Makao; hati nyingine: Kimbilio. wetu.
2Kabla ya kuwapo milima,
kabla hujauumba ulimwengu;
wewe ndiwe Mungu, milele na milele.
3Wamwambia binadamu, “Rudi mavumbini!”
Naye binadamu hurudi mavumbini alimotoka!
4 Taz 2Pet 3:8 Kwako miaka elfu ni kama siku moja tu,
ni kama jana ambayo imekwisha pita;
kwako ni kama mkesha mmoja wa usiku!
5Wawafutilia mbali watu kama ndoto!
Binadamu ni kama nyasi zinazochipua asubuhi:
6Asubuhi huchipua na kuchanua,
jioni zimekwisha nyauka na kukauka.
7Hasira yako inatuangamiza;
tunatishwa na ghadhabu yako.
8Maovu yetu umeyaweka mbele yako;
dhambi zetu za siri ziko wazi mbele yako.
9Kwa hasira yako maisha yetu yatoweka,
yanaisha kama pumzi.
10Miaka ya kuishi ni sabini,
au tukiwa wenye afya, themanini;
lakini yote ni shida na taabu!
Siku zapita mbio, nasi twatoweka mara!
11Nani anayetambua uzito wa hasira yako?
Nani anayejali matokeo ya ghadhabu yako?
12Utufundishe ufupi wa maisha yetu
ili tuweze kuwa na hekima.
13Urudi, ee Mwenyezi-Mungu!
Utakasirika hata lini?
Utuonee huruma sisi watumishi wako.
14Utushibishe fadhili zako asubuhi,
tushangilie na kufurahi maisha yetu yote.
15Utujalie sasa miaka mingi ya furaha,
kama ulivyotupa miaka mingi ya shida na taabu.
16Utuoneshe matendo yako sisi watumishi wako;
uwaoneshe wazawa wetu uwezo wako mtukufu.
17Utufadhili ee Bwana, Mungu wetu;
uzitegemeze kazi zetu,
uzifanikishe shughuli zetu.



Zaburi90;1-17

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Tuesday 26 March 2019

Kikombe Cha Asubuhi ;Zaburi 89...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Neno la Mwenyezi-Mungu lililomjia Yeremia mnamo mwaka wa kumi wa utawala wa Sedekia, mfalme wa Yuda, ambao ulikuwa mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Nebukadneza. Wakati huo, majeshi ya mfalme wa Babuloni yalikuwa yakiuzingira mji wa Yerusalemu, naye nabii Yeremia alikuwa amezuiliwa katika ukumbi wa walinzi uliokuwa ndani ya ikulu ya mfalme wa Yuda.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizo zifanya
Kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Maana Sedekia, mfalme wa Yuda, alikuwa amemfunga Yeremia akisema, “Kwa nini unatabiri na kusema: ‘Mwenyezi-Mungu asema hivi: Tazama, mimi nautia mji huu mikononi mwa mfalme wa Babuloni, naye atauteka. Sedekia, mfalme wa Yuda, hataepa kutiwa mikononi mwa Wakaldayo; hakika atatekwa na mfalme wa Babuloni, ataonana naye uso kwa uso na kuongea naye ana kwa ana.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji

Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu Baba wa Mbinguni
tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe....


Yahweh  tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni

Yahweh ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe

Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Sedekia atachukuliwa hadi Babuloni, naye atakaa huko mpaka nitakapomchukulia hatua. Hata kama Sedekia atapigana na Wakaldayo, hatashinda.’”
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,
wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake

Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe Yahweh tunaomba ukawape neema ya kujiombea
Kufuata njia zako nazo zikawaweke huru
Ukawaokoe na kuwalinda,ukawaponye kimwili na kiroho
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao,Amani ikatawale katika maisha yao,Upendo ukadumu kati yao Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako,kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina..!



Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,
Mungu Baba aendelee kuwatendea sawasawa na mapezni yake...

Nawapenda.

Wakati wa taabu ya kitaifa

(Utenzi wa Ethani Mwezrahi)
1Ee Mwenyezi-Mungu, nitaimba fadhili zako milele;
nitavitangazia vizazi vyote uaminifu wako.
2Natamka kuwa fadhili zako zadumu milele;
uaminifu wako ni thabiti kama mbingu.
3Umesema: “Nimefanya agano na mteule wangu,
nimemwapia mtumishi wangu Daudi:
4 Taz Zab 132:11; Mate 2:30 ‘Daima nitamweka mzawa wako kuwa mfalme,
tena nitaudumisha ufalme wako milele.’”
5Mbingu na zisifu maajabu yako, ee Mwenyezi-Mungu;
uaminifu wako usifiwe katika kusanyiko la watakatifu.
6Nani mbinguni awezaye kulinganishwa nawe ee Mwenyezi-Mungu?
Nani aliye sawa nawe kati ya viumbe vya mbinguni?
7Wewe waogopwa katika baraza la watakatifu;
wote wanaokuzunguka wanatiwa hofu kuu.
8Ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wa majeshi,
ni nani mwenye nguvu kama wewe, ee Mwenyezi-Mungu?
Uaminifu umekuzunguka pande zote.
9Wewe watawala machafuko ya bahari;
mawimbi yake yakiinuka, wayatuliza.
10Uliliponda joka Rahabu na kuliua;
uliwatawanya adui zako kwa nguvu yako.
11Mbingu ni zako na dunia ni yako pia;
ulimwengu na vitu vyote vilivyomo wewe uliviumba.
12Wewe uliumba kaskazini na kusini;
milima Tabori na Hermoni inakusifu kwa furaha.
13Mkono wako una nguvu,
mkono wako una nguvu na umeshinda!
14Uadilifu na haki ni msingi wa utawala wako;
fadhili na uaminifu vyakutangulia!
15Heri watu wanaojua kukushangilia,
wanaoishi katika mwanga wa wema wako, ee Mwenyezi-Mungu.
16Wanafurahi mchana kutwa kwa sababu yako,
na kukusifu kwa ajili ya uadilifu wako.
17Wewe ndiwe fahari na nguvu yao;
kwa wema wako twapata ushindi.
18Ee Mwenyezi-Mungu, mlinzi wetu ni wako,
mfalme wetu ametoka kwako ewe Mtakatifu wa Israeli.
Ahadi ya Mungu kwa Daudi
19Zamani ulinena katika maono,
ukawaambia watumishi wako waaminifu:
“Nimempa nguvu shujaa mmoja,
nimemkuza huyo niliyemteua kati ya watu.
20 Taz Mate 13:22 Nimempata Daudi, mtumishi wangu;
nimemweka wakfu kwa mafuta yangu matakatifu.
21Mkono wangu wa nguvu utakuwa naye daima;
mkono wangu mimi mwenyewe utamwimarisha.
22Maadui hawataweza kumshinda,
wala waovu hawatamnyanyasa.
23Mimi nitawaponda wapinzani wake;
nitawaangamiza wote wanaomchukia.
24Nitakuwa mwaminifu kwake na kumfadhili,
kwa jina langu atapata ushindi mkubwa.
25Nitaimarisha nguvu na utawala wake,
toka bahari hata mito.
26Yeye ataniita: ‘Wewe ni Baba yangu,
Mungu wangu, mwamba wa wokovu wangu.’
27 Taz Ufu 1:5 Nami nitamfanya kuwa mzaliwa wangu wa kwanza,
mkuu kuliko wafalme wote duniani.
28Fadhili zangu nitamwekea milele,
na agano langu kwake litadumu daima.
29Nitaudumisha daima ukoo wake wa kifalme,
na ufalme wake kama mbingu.
30“Lakini wazawa wake wakiiacha sheria yangu,
wasipoishi kadiri ya maagizo yangu,
31kama wakizivunja kanuni zangu,
na kuacha kutii amri zangu,
32hapo nitawaadhibu makosa yao;
nitawapiga kwa sababu ya uovu wao.
33Lakini sitaacha kumfadhili Daudi,
wala kuwa mwongo kuhusu uaminifu wangu.
34Sitavunja agano langu naye,
wala kubatili neno nililotamka kwa mdomo wangu.
35“Nimeapa mara moja tu kwa utakatifu wangu;
nami sitamwambia Daudi uongo.
36Ukoo wake utadumu milele;
na ufalme wake kama jua.
37Utadumu milele
kama mwezi utokezavyo angani.”
Majonzi ya sasa
38Lakini sasa ee Mungu, umemtupa na kumkataa,
umejaa ghadhabu dhidi ya huyo uliyemweka wakfu.
39Umefuta agano ulilofanya na mtumishi wako;
umeitupa taji yake mavumbini.
40Kuta zote za mji wake umezibomoa;
ngome zake umezivunjavunja.
41Wote wapitao wanampokonya mali zake;
amekuwa dharau kwa jirani zake.
42Maadui zake umewapa ushindi;
umewafurahisha maadui zake wote.
43Silaha zake umezifanya butu;
ukamwacha ashindwe vitani.
44Umemvua madaraka yake ya kifalme89:44 Umemvua … kifalme: Kiebrania: Umemvua usafi wake wa kifalme.
ukauangusha chini utawala wake.
45Umezipunguza siku za ujana wake,
ukamfunika fedheha tele.
Kuomba usalama
46Ee Mwenyezi-Mungu, utajificha hata milele?
Hata lini hasira yako itawaka kama moto?
47Ukumbuke, ee Bwana, ufupi wa maisha yangu;
kwamba binadamu uliyemuumba anaishi muda mfupi!
48Ni mtu gani aishiye asipate kufa?
Nani awezaye kujiepusha na kifo?
49Ee Bwana, ziko wapi basi fadhili zako,
ulizomwapia Daudi kwa uaminifu wako?
50Ee Bwana, ukumbuke anavyotukanwa mtumishi wako,
jinsi nivumiliavyo matusi ya wasiokujua.
51Ona wanavyomzomea, ee Mwenyezi-Mungu;
jinsi wanavyomdhihaki mteule wako kila aendako.
52Asifiwe Mwenyezi-Mungu milele!
Amina! Amina!


Zaburi89;1-52

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 25 March 2019

Kikombe Cha Asubuhi ;Zaburi 88...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?
Haleluyah ni siku/wiki  nyingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!


Wakati tulipowafundisheni juu ya ukuu wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo, hatukutegemea hadithi tupu zisizo na msingi. Sisi tuliuona utukufu wake kwa macho yetu wenyewe. Sisi tulikuwapo wakati alipopewa heshima na utukufu kutoka kwa Mungu Baba, wakati sauti ilipomjia kutoka kwake yeye aliye Utukufu Mkuu, ikisema: “Huyu ni Mwanangu mpenzi ambaye nimependezwa naye.” Tena, sisi wenyewe tulisikia sauti hiyo kutoka mbinguni wakati tulipokuwa pamoja naye juu ya ule mlima mtakatifu.
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona...

Tena, ujumbe wa manabii watuthibitishia jambo hilo; nanyi mwafanya vema kama mkiuzingatia, maana ni kama taa inayoangaza mahali penye giza mpaka siku ile itakapopambazuka na mwanga wa nyota ya asubuhi utakapong'ara mioyoni mwenu.
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Zaidi ya hayo, lakini, kumbukeni kwamba hakuna mtu yeyote awezaye kufafanua mwenyewe unabii ulio katika Maandiko Matakatifu. Maana hakuna ujumbe wa kinabii unaotokana na matakwa ya binadamu, bali watu walitoa unabii wakiongozwa na Roho Mtakatifu.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopotia magumu/majaribu mbalimbali
watoto wako wanaokuomba kwa bidii na imani
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Yahweh tunaomba ukaonekane katika maisha yao
Jehovah tunaomba ukawaokoe,ukawavushe salama na  kuwalinda
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimaie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Baba wa Mbinguni ukapokee sala/maombi yetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.

Kilio cha msaada
(Wimbo. Zaburi ya Wakorahi. Kwa Mwimbishaji: Mtindo wa Mahalathi Nealothi. Utenzi wa Hemani Mwezrahi)
1Ee Mwenyezi-Mungu, mwokozi wangu,
ninalia mchana kutwa,
na usiku nakulalamikia.
2Sala yangu ikufikie,
usikilize kilio changu.
3Maafa mengi yamenipata,
nami niko karibu kufa.
4Ninaonekana kama mtu anayekufa,
nguvu zangu zote zimeniishia.
5Nimesahauliwa kati ya wafu,
kama waliouawa, walioko kaburini;
kama wale ambao huwakumbuki tena,
ambao wametengwa na ulinzi wako.
6Umenitupa katika kina cha kaburi;
katika sehemu za giza na kina kikuu.
7Hasira yako imenilemea;
umenisonga kwa mawimbi yako yote.
8Umewafanya rafiki zangu waniepe,
umenifanya kuwa chukizo kwao.
Nimefungwa ndani, wala siwezi kutoroka;
9macho yangu yamefifia kwa huzuni.
Kila siku nakulilia, ee Mwenyezi-Mungu;
ninakunyoshea mikono yangu.
10Je, wewe huwatendea wafu maajabu yako?
Je, mizimu hufufuka na kukusifu?
11Je, fadhili zako zinatajwa kaburini,
au uaminifu wako kwenye makao ya maangamizi?
12Je, maajabu yako yanajulikana humo gizani,
au wema wako katika nchi ya waliosahauliwa?
13Lakini mimi nakulilia, ee Mwenyezi-Mungu;
kila asubuhi nakuletea ombi langu.
14Mbona ee Mwenyezi-Mungu wanitupilia mbali?
Kwa nini unanificha uso wako?
15Nimeteseka na kukaribia kifo tangu ujana wangu;
nateseka kwa mapigo yako, niko hoi kabisa.
16Ghadhabu yako imeniwakia;
mashambulio yako ya kutisha yananiangamiza.
17Yananizunguka kama mafuriko mchana kutwa;
yananizingira yote kwa pamoja.
18Umewafanya rafiki na wenzangu wote waniepe;
giza ndilo limekuwa mwenzangu.

Zaburi88;1-17

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.