Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 29 July 2014

Eid Mubarak Waungwana!!!!!

Nawatakia Eid Njema[Eid Mubarak]Ndugu,Jamaa,Marafiki na Wote .....
Muendelee/Muwe na Wakati Mwema,Amani,Upendo na Furaha.
"Swahili Na Waswahili"Pamoj Sana.

Sunday 27 July 2014

Muendelee na Jumapili Vyema;Burudani-Angela Chibalonza - Yahwe Uhimidiwe na Nyingine...Na Siku Kama Ya Leo Bibi na Bwana Isaac Walifunga Ndoa [Happy Anniversary]


Siku kama ya Leo, Bibi na Bwana Isaac,[Isaacrachel]Tuliungana na kuwa mwili mmoja[Tulifunga Ndoa].
Tuna Mshukuru sana MUNGU katika yote na   tunazidi kujiachilia mikononi mwake.Si kwa uwezo wetu  wala akili zetu.ni Mapenzi yake/Kwa Neema tuu
.


Wapendwa; Natumaini Jumapili inandelea/ilikuwa njema,MUNGU azidi kuwabariki,Kuwainua,Kuwalinda,Kuwaponya,Kuwatendea,Kuwafariji,Kuwapa amani,Kuwapa Furaha,kuwaunganisha na Kuwafunulia.......

Ndipo Samweli akatwaa jiwe,na kulisimamisha kati ya Mispa na Sheni, akaliita jina lake Eben-ezeri,akisema, Hata sasa BWANA ametusaidia.

Neno La Leo;1Swamweli:7:1-17
Hivyo wafilisti walishindwa,wasiingie tena  ndani ya mipaka ya Israeli; na mkono wa BWANA ulikuwa juu ya Wafiristi siku zote za Samweli..........








"Swahili Na Waswahili" Mbarikiwe Wote.

Sunday 20 July 2014

Natumaini JumaPili inaendelea Vyema;Burudani-Swahilli Worship Songs!!!!!

Wapendwa;Natumaini Jumapili  inaendelea vyema,Iwe Yenye Imani,Tumaini,Baraka,Furaha na Amani....

Na wale waliotumwa waliporudi nyumbani,wakamkuta yule mtumwa ni mzima.

Neno La Leo;Luka Mtakatifu:7:1-10

Alipokwisha kuyamaliza maneno yake yote masikioni mwa watu,aliingia Kapernaumu.......



"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe Wote.

Tuesday 15 July 2014

Siku Kama Ya Leo da'Sandra-Neema Alizaliwa







 Wapendwa/Waungwana;Siku kama ya Leo ,1998.
 Familia ya Isaac,MUNGU alitubariki/Kutujaalia mtoto wa kike.
Sandra-Neema.Umekuwa na Endelea kuwa Baraka kwetu.

Tunamshukuru sana MUNGU kwa baraka hii na Tunazidi kumtukuza katika yote.
Tunayaweka Maisha ya Sandra-Neema mikononi mwake Mungu.

Azidi kukua Kiroho/Kiimani,Kimaadili,Kimo,Kimaarifa.
Azidi kuwa Baraka Kwetu sisi Wazazi naWalezi,Ndugu,Jamaa,Marafiki,Majirani,Wakubwa Kwa Watoto na Jamii Nzima.
Shukrani sana Kwa wote tunaoshirikiana katika Malezi,Maombi/Sala/Dua na Katika yote yanayochangia Maisha ya binti yetu.
Mungu Baba azidi kuwabariki na Kuwaonngezea kila lililo jema.


Hongera sana da'Sandra-Neema katika siku yako hii  Muhimu.
Hongera kwa kumaliza vyema GCSE's Na tunakitakia kila la heri katika A-Levels[Sixth Form].
Ukawe kichwa na si Mkia.
Tunakupenda Sana na Tunakuunga mkono katika Safari yako njema ya Maisha.
MUNGU ndiyo kila kitu katika Maisha yako.Ubarikiwe Mno!!!!

Happy birthday Sandra[se-Ndondole].Wako;Mama,Baba,Mdogo wako-Tracey-Sarah.[Isaac Family]
MUNGU wetu ni Mwema Sana.



"Swahili Na Waswahili" Rachel siwa, ninawapenda Wote.

Monday 14 July 2014

Mahojiano na washiriki wa maonyesho ya Utamaduni wa Kenya hapa Washington DC


Kati ya Juni 25 na Julai 6, jiji la Washington DC lilikuwa mwenyeji wa maonyesho ya kila mwaka ya yanayohusu maisha a watu na jamii mbalimbali.

Mwaka huu, nchi ya Kenya ilishirikishwa, wakionyesha utamaduni wao na changamoto za kuzidumisha katika zama hizi za sayansi na teknolojia.

Kwanza Production ilipata fursa ya kutembelea maonyesho hayo na kuzungumza na baadhi ya washiriki wa maonyesho hayo ambapo walieleza mengi ya kufurahisha.

KARIBU UUNGANE NASI


Zaidi ya washiriki 100 kutoka nchini Kenya waLIkuja hapa jijini kuonyesha mambo mbalimbali kama kutengeneza vyungu kwa ufinyanzi, uchongaji vinyago, mapambo ya shanga, useremala, nakshi za majengo, ujenzi wa majahazi, mapishi , muziki na mengine yanayotunza utamaduni wa nchi hiyo


Maelezo ya ujenzi na sehemu za JAHAZI (DHOW) toka kwa Ali Skanda aliyetoka Lamu Kenya
Na mtangazaji mkongwe abdushakur Aboud mbele ya Jahazi lililoletwa kwenye makumbusho ya hapa Washington DC kutoka Lamu nchini Kenya
Mtaalamu wa mapambo yatokanayo na shanga na usimamizi wa filamu nchini Kenya Emmah Irungu
Mwandishi wa habari kutoka Kenya BMJ Mureithi

Sunday 13 July 2014

Tumalizie JumaPili hii na Pastor Donis and Nnunu Nkone- SINGING WITH THEIR CHILDREN

Wapendwa;Natumaini MUNGU anazidi kuwabariki na Mnaendelea Vyema na Jumapili hii..
Iwe Njema,Yenye Heri,Baraka,Neema,Tumaini,Utuwema,Fadhili,Shukrani na Amani.

Neno La Leo;Tumsikilize, Pastor Donis na Familia Yake ......




Shukrani Sana na MUNGU azidi kuwabariki;Donis-andNnunu Nkone

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe Wote.

Friday 11 July 2014

Jikoni Leo;How to Make Mbaazi,Viazi Vya Tamu Vya Nazi na Mswahili Sheikha Agil

Waungwana;"Jikoni Leo"  Mapishi haya yatasaidia sana wanaofunga Mwezi huu[Futari]....
Mengi sina nawatakia Mapishi mema.






Shukrani;Sheikha Agil

"Swahili Na Waswahili" Pamoja Sana.

Sunday 6 July 2014

Tuendelee Na JumaPili hii Vyema;Burudani-Furaha Choir London - Tuimbe Wimbo (Muda Tutakwenda Nyumbani)na Nyingine...!!!

Wapendwa; natumaini Jumapili hii inaendelea Vyema,Iwe yenye Amani,Baraka,Furaha,Upendo,Fadhili, Shukran,Utukufu tumrudishie MUNGU.......

Mkimshukuru Baba,aliyewastahilisha kupokea  sehemu ya Urithi wa watakatifu katika nuru.

Neno La Leo;Wakolosai:1:1-29


Nae alituokoa katika nguvu za giza,akatuhamisha na kutuingiza katika uflame wa Mwana wa pendo Lale.




"Swahili Na Waswahili"Pamoja Daima

Saturday 5 July 2014

Mahojiano ya Kwanza Production na Diamond Platnumz baada ya tuzo za BET‏


Diamond Platnumz na DMK kwenye utoaji tuzo za BET Los Angeles
Photo Credits: DMK Global Promotions' facebook page
Karibu katika mahojiano ya Kwanza Production na Damond Platnumz. Msanii mwenye mafanikio makubwa kutoka nchini Tanzania
Amejiunga nasi kwa njia ya simu punde baada ya kuhudhuria utoaji tuzo za BET ambako yeye alikuwa mmoja wa waliokuwa wakiwania tuzo hizo.
Kazungumza mengi kuhusu TUZO HIZO.
Alipopokea na alivyopokea uteuzi wake, aliloliona kwenye tuzo hizo, ulinganishaji wake katika utoaji tuzo hizi na za Tanzania / Afika, alichojifunza, faida ya kuja kushiriki hili na hata mikakati yake ijayo kuhakikisha kuwa muziki wa Tanzania unafika mbali zaidi.
SWALI jingine alilojibu ni kuwa....ni kweli kuwa ili muziki wa Tanzania ushinde tuzo ni lazima uwe na mahadhi ya Afrika Magharibi (kama muziki wake wa Number One) ama Afrika Kusini 
Amejiunga nasi kwa msaada wa promota Dickson Mkama almaarufu DMK ambaye pia ndiye meneja wa msanii huyo hapa nchini.
KARIBU





Thursday 3 July 2014

Chaguo La Mswahili Leo;Michelle Williams - Say Yes ft. Beyoncé, Kelly Rowland.!!!!!

Waungwana Chaguo La Mswahili Leo.Say Yes.....
Mmmhhh Maneno mengi sina..Twende sote sasaaaaa.....
.



Mimi umenishikaaa..wewe je?

"Swahili Na Waswahili" Pamoja Sana
.

Wednesday 2 July 2014

Mahojiano na Kwanza Production na NURU THE LIGHT‏


Photo Credits: Bongo Celebrity 
Karibu katika mahojiano kamini kati ya Kwanza Production na NURU THE LIGHT.
Msanii, Mjasiriamali, Mtangazaji, Blogger na Mwanaharakati ambaye amekuwa mkarimu sana kujiunga nasi moja kwa moja kutoka Stockholm Sweden
Kazungumza mengi ikiwa ni pamoja na alivyoanza muziki
Kisha akagusia kuhusu onyesho lake la kwanza kabisa jukwaani.
Na kama nilivyokuja kumtambua, ni mtu mwenye misimamo na anayejitambua, utamsikia msimamo wake awapo studio
Nikataka kujua pia, nini anaona kama tatizo kubwa kwenye muziki wetu?
Haya ni machache kati ya mengi aliyozungumza nami
JIUNGE NASI