Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 30 June 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Mika 4...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Unitendee mimi mtumishi wako kwa ukarimu, nipate kuishi na kushika neno lako. Uyafumbue macho yangu, niyaone maajabu ya sheria yako. Mimi ni mkimbizi tu hapa duniani; usinifiche amri zako.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako,
Tukijinyenyekeza,tukijiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunamomba utusamehe dhambi zetu
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
 ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea

Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Roho yangu yaugua kwa hamu kubwa ya kutaka kujua daima maagizo yako. Wewe wawakemea wenye kiburi, walaanifu, ambao wanakiuka amri zako.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Uniepushe na matusi na madharau yao, maana nimeyazingatia maamuzi yako. Hata kama wakuu wanakula njama dhidi yangu; mimi mtumishi wako nitayatafakari maamuzi yako. Masharti yako ni furaha yangu; hayo ni washauri wangu.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...

Nawapenda.

Mungu atatawala watu wote kwa amani
(Isa 2:1-4)
1Utakuja wakati ambapo
mlima wa nyumba ya Mwenyezi-Mungu
utakuwa mkubwa kuliko milima yote.
Naam, utakwezwa juu ya vilima vyote.
Watu wengi watamiminika huko,
2mataifa mengi yataujia na kusema:
“Twendeni juu kwenye mlima wa Mwenyezi-Mungu,
twende katika nyumba ya Mungu wa Yakobo,
ili atufundishe njia zake,
nasi tufuate nyayo zake.
Maana mwongozo utatoka huko Siyoni;
neno la Mwenyezi-Mungu huko Yerusalemu.”
3Mungu atasuluhisha mizozo ya mataifa mengi,
atakata mashauri ya mataifa makubwa ya mbali.
Nayo yatafua mapanga yao kuwa majembe,
na mikuki yao kuwa miundu ya kupogolea.
Taifa halitapigana na taifa lingine,
wala hayatafanya tena mazoezi ya vita.
4Kila mtu atakaa kwa amani
chini ya mitini na mizabibu yake,
bila kutishwa na mtu yeyote.
Mwenyezi-Mungu wa majeshi, ametamka yeye mwenyewe.
5Mataifa mengine hufuata njia zao,
kwa kuitegemea miungu yao,
lakini sisi twafuata njia zetu kwa kumtegemea Mwenyezi-Mungu,
Mungu wetu, milele na milele.
Waisraeli watarudi kutoka utumwani
6Mwenyezi-Mungu asema,
“Siku ile nitawakusanya walemavu,
naam, nitawakusanya waliochukuliwa uhamishoni,
watu wale ambao niliwaadhibu.
7Hao walemavu ndio watakaobaki hai;
hao waliochukuliwa uhamishoni watakuwa taifa lenye nguvu.
Nami Mwenyezi-Mungu nitawatawala mlimani Siyoni,
tangu wakati huo na hata milele.”
8Nawe kilima cha Yerusalemu,
wewe ngome ya Siyoni,
ambamo Mungu anafanya ulinzi juu ya watu wake,
kama mchungaji juu ya kondoo wake;
wewe utakuwa tena mji maarufu kama hapo awali,
Yerusalemu utakuwa tena mji mkuu wa mfalme.
9Sasa kwa nini mnalia kwa sauti?
Je, hamna mfalme tena?
Mshauri wenu ametoweka?
Mnapaza sauti ya uchungu,
kama mama anayejifungua!
10Enyi watu wa Siyoni,
lieni na kugaagaa kama mama anayejifungua!
Maana sasa mtaondoka katika mji huu
mwende kukaa nyikani,
mtakwenda mpaka Babuloni.
Lakini huko, mtaokolewa.
Huko Mwenyezi-Mungu atawakomboa makuchani mwa adui zenu.
11Mataifa mengi yamekusanyika kuwashambulia.
Yanasema: “Acheni mji wao utiwe najisi,
nasi tuyaone magofu ya Siyoni!”
12Lakini wao
hawafahamu mawazo ya Mwenyezi-Mungu
wala hawaelewi mpango wake:
Kwamba amewakusanya pamoja,
kama miganda mahali pa kupuria.
13Mwenyezi-Mungu asema,
“Enyi watu wa Siyoni,
inukeni mkawaadhibu adui zenu!
Nitawapeni nguvu kama fahali
mwenye pembe za chuma na kwato za shaba.
Mtawasaga watu wa mataifa mengi;
mapato yao mtaniwekea wakfu mimi,
mali zao mtanitolea mimi Bwana wa dunia yote.”


Mika4;1-13

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

Monday 29 June 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Mika 3...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki nyingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...
Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!

Kijana atatunzaje maisha yake kuwa safi? Kwa kuyaongoza kadiri ya neno lako. Najitahidi kukutii kwa moyo wote; usiniache nikiuke amri zako. Nimeshika neno lako moyoni mwangu, nisije nikakukosea.
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona

Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona....

Utukuzwe, ee Mwenyezi-Mungu! Unifundishe masharti yako. Nitayarudia kwa sauti maagizo yako yote uliyotoa.
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu

Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Nafurahi kufuata maamuzi yako, kuliko kuwa na utajiri mwingi. Nazitafakari kanuni zako, na kuzizingatia njia zako. Nayafurahia masharti yako; sitalisahau neno lako.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimamie Neno lako nalo likawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.

Mika anawashutumu viongozi wa Israeli
1Sasa sikilizeni enyi wakuu wa wazawa wa Yakobo,
sikilizeni, enyi watawala wa wazawa wa Israeli!
Nyinyi ndio mnaopaswa kujua mambo ya haki.
2Lakini nyinyi mnachukia mema na kupenda maovu.
Mnawachuna ngozi watu wangu,
na kubambua nyama mifupani mwao.
3Mnajilisha kwa nyama ya watu wangu
mnawachuna ngozi yao,
mnaivunjavunja mifupa yao,
na kuwakatakata kama nyama ya kupika,
kama nyama ya kutia ndani ya chungu.
4Wakati unakuja ambapo mtamlilia Mwenyezi-Mungu,
lakini yeye hatawajibu.
Atauficha uso wake wakati huo,
kwa sababu mmetenda mambo maovu.
5Mwenyezi-Mungu asema hivi
kuhusu manabii wanaowapotosha watu wake;
manabii ambao hutabiri amani wakipewa kitu,
lakini huwatishia watu kwa vita wasipopewa kitu:
6“Kwenu manabii kutakuwa usiku bila maono,
kutakuwa giza kwenu bila ufunuo.
Kwenu manabii kutakuchwa,
mchana utakuwa giza kwenu.”
7Mabingwa wa maono watafedheheka,
mafundi wa kubashiri wataaibishwa;
wote watafunga midomo yao,
maana hawatapata jibu lolote kutoka kwa Mungu.
8Lakini kwa upande wangu,
nimejazwa nguvu na roho ya Mwenyezi-Mungu;
nimejaliwa kujua haki na kuwa na uwezo
niwatangazie wazawa wa Yakobo kosa lao,
niwaambie Waisraeli dhambi yao.
9Sikieni jambo hili enyi viongozi wa wazawa wa Yakobo,
sikilizeni, enyi watawala wa Waisraeli:
Nyinyi mnachukia mambo ya haki
na kupotosha mambo ya adili.
10Nyinyi mnajenga mji wa Siyoni kwa damu,
naam, mji wa Yerusalemu kwa dhuluma.
11Waamuzi hufanya kazi yao kwa rushwa,
makuhani wake hufundisha kwa malipo,
manabii hutabiri kwa fedha.
Hata hivyo hujidai kumtegemea Mwenyezi-Mungu,
wakisema, “Mwenyezi-Mungu, si yupo pamoja nasi?
Hatutapatwa na madhara yoyote!”
12Haya! Kwa sababu yenu,
Siyoni utalimwa kama shamba,
Yerusalemu utakuwa magofu,
nao mlima wa hekalu utakuwa msitu.

Mika3;1-12

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

Friday 26 June 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Mika 2...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!



Heri watu wanaoishi bila kosa, wanaozingatia sheria ya Mwenyezi-Mungu. Heri wanaozingatia matakwa yake, wanaomtafuta kwa moyo wao wote,

Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....



watu wasiotenda uovu kamwe, bali daima hufuata njia zake. Ee Mungu, umetupatia kanuni zako ili tuzishike kwa uaminifu.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...



Laiti mwenendo wangu ungeimarika, kwa kuyafuata masharti yako! Nikizingatia amri zako zote, hapo kweli sitaaibishwa. Nitakusifu kwa moyo mnyofu, nikijifunza maagizo yako maadilifu. Nitayafuata masharti yako; usiniache hata kidogo.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Mika na wapinzani wake
1Ole wao wanaopanga kutenda maovu
wanaolala usiku wakiazimia uovu!
Mara tu kunapopambazuka,
wanayatekeleza kwani wanao uwezo.
2Hutamani mashamba na kuyatwaa;
wakitaka nyumba, wananyakua.
Huwadhulumu wenye nyumba na jamaa zao,
huwanyang'anya watu mali zao.
3Kwa hiyo, Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Ninapanga kuwaleteeni nyinyi maafa,
ambayo kamwe hamtaweza kuyakwepa.
Utakuwa wakati mbaya kwenu,
wala hamtaweza kwenda kwa maringo.
4Siku hiyo watu watawasimanga kwa wimbo,
watalia na kuomboleza kwa uchungu, wakisema:
‘Tumeangamia kabisa;
Mwenyezi-Mungu amechukua nchi yetu,
naam, ameiondoa mikononi mwetu.
Mashamba yetu amewagawia waliotuteka.’”2:4 waliotuteka: Makala ya Kiebrania: Waasi.
5Kwa hiyo hamtagawiwa sehemu yoyote ya ardhi
miongoni mwa watu wake Mwenyezi-Mungu.
Wapinzani wa nabii
6“Usituhubirie sisi.
Mambo kama hayo si ya kuhubiriwa.
Sisi hatutakumbwa na maafa!
7Je, yafaa kusema hivyo, wazawa wa Yakobo?
Je, Mwenyezi-Mungu ameacha uvumilivu wake?
Je, yeye hufanya mambo kama haya?”
Mika
Sivyo! Maneno yangu huwafaa watendao mambo mema.
8Lakini Mwenyezi-Mungu awaambia hivi:
“Nyinyi mnawavamia watu wangu kama adui.
Mnawanyang'anya mavazi yao watu watulivu;
watu wanaopita kwenda zao bila wasiwasi,
na wasio na fikira zozote za vita.
9Mnawafukuza wake za watu wangu
kutoka nyumba zao nzuri;
watoto wao mmewaondolea fahari yangu milele.
10Inukeni mwende zenu!
Hapa hamna tena pa kupumzika!
Kwa utovu wenu wa uaminifu
maangamizi makubwa yanawangojea!
11Kama mtu angetokea akatamka maneno matupu ya uongo
na kusema: ‘Nawatabirieni divai na pombe kwa wingi’,
mhubiri wa namna hiyo angependwa na watu hawa!
12“Lakini kweli nitawakusanya nyote enyi watu wa Yakobo,
naam, nitawakusanya enyi Waisraeli mliobaki,
niwalete pamoja kama kondoo katika zizi,
kama kundi kubwa la kondoo malishoni;
nanyi mtakuwa kundi la watu wengi.”
13Yule atakayetoboa njia atawatangulia,
nao watalivunja lango la mji na kutoka nje,
watapita na kutoka nje.
Mfalme wao atawatangulia;
Mwenyezi-Mungu mwenyewe atawatangulia.


Mika2;1-13

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

Thursday 25 June 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Tunamshukuru Mungu kwa kumaliza Kitabu cha Yona,Leo Tunaanza Kitabu cha Mika....1

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tunamshukuru Mungu kwa kutupa kibali cha
 kupitia kitabu cha "YONA
"
Ni matumaini yangu kuna mengi tumejifunza/kufaidika
na kutupa mwanga/kuelewa kwenye kitabu hiki...

Leo tunapokwenda anza kupitia Kitabu cha"MIKA"tunamuomba Mungu wetu akatupe kibali,macho ya rohoni
 na akili ya kuelewa katika kujifunza NENO lake...
Ee Mungu  tunaomba ukatuongoze...!!
Tumshukuru Mungu wetu katika yote...Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...


Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Kisha Elifazi, Mtemani, akajibu: “Je, mtu wa hekima hujibu kwa maneno ya upuuzi? Je, mtu huyo amejaa maneno matupu? Je, mwenye hekima hujitetea kwa maneno yasiyofaa, au kwa maneno yasiyo na maana?
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....


Lakini wewe unapuuza uchaji wa Mungu; na kuzuia kutafakari mbele ya Mungu. Uovu wako ndio unaokifundisha kinywa chako, nawe wachagua kusema kama wadanganyifu.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Maneno yako mwenyewe yanakuhukumu, sio mimi; matamshi yako yashuhudia dhidi yako. Je, wewe ni mtu wa kwanza kuzaliwa? Je, wewe ulizaliwa kabla ya kuweko vilima? Je, ulipata kuweko katika halmashauri ya Mungu? au, wewe ndiwe peke yako mwenye hekima?
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

1Neno la Mwenyezi-Mungu lilimjia Mika, mwenyeji wa Moreshethi, wakati Yothamu, Ahazi na Hezekia walipokuwa wafalme wa Yuda. Mika aliona mambo yote haya kuhusu Samaria na Yerusalemu.
Mwenyezi-Mungu aja kuhukumu
2Sikilizeni enyi watu wote;
sikiliza ewe dunia na vyote vilivyomo.
Mwenyezi-Mungu anakuja kuwashtaki,
Bwana anena kutoka hekalu lake takatifu.
3Naam! Mwenyezi-Mungu yuaja kutoka makao yake;
atashuka na kutembea juu ya vilele vya dunia.
4Milima itayeyuka chini ya nyayo zake,
kama nta karibu na moto;
mabonde yatapasuka,
kama maji yaporomokayo kwenye mteremko.
5Haya yote yatatukia
kwa sababu ya makosa ya wazawa wa Yakobo,
kwa sababu ya dhambi za wazawa wa Israeli.
Je, uhalifu wa Yakobo waonekana wapi?
Katika mji wake mkuu Samaria!
Je, uhalifu wa Yuda waonekana wapi?
Katika Yerusalemu kwenyewe!
6Kwa hiyo, Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Mji wa Samaria nitaufanya magofu nyikani,
shamba ambalo watu watapanda mizabibu.
Mawe yaliyoujenga nitayatupa bondeni,
na misingi yake nitaichimbuachimbua.
7Sanamu zake zote zitavunjwavunjwa,
kila kilichochumwa kitateketezwa kwa moto.
Vinyago vyake vyote nitaviharibu.
Vilirundikwa kutokana na ujira wa malaya,
navyo vitatumiwa tena kulipia umalaya.”
Nabii anaomboleza juu ya Yerusalemu na Yuda
8Kwa sababu hiyo, mimi nitalia na kuomboleza;
nitatembea uchi na bila viatu.
Nitaomboleza na kulia kama mbweha,
nitasikitika na kulia kama mbuni.
9Majeraha ya Samaria hayaponyeki,
nayo yameipata pia Yuda;
yamefikia lango la Yerusalemu,
mahali wanapokaa watu wangu.
10Msiitangaze habari hii huko Gathi,
wala msilie machozi!
Huko Beth-leafra mgaegae mavumbini kwa huzuni.
11Nendeni enyi wakazi wa Shafiri,
mkiwa uchi na wenye haya.
Wakazi wa Zaanani msitoke nje ya mji wenu.
Watu wa Beth-ezeli wanalia;
msaada wao kwenu umeondolewa.
12Wakazi wa Marothi wanangojea msaada kwa hamu kubwa,
lakini maangamizi yaja kutoka kwa Mwenyezi-Mungu
karibu kabisa na lango la Yerusalemu.
13Enyi wakazi wa Lakishi,
fungeni farasi wepesi na magari ya vita.
Nyinyi mlikuwa mmeiga dhambi ya watu wa Siyoni,
makosa ya Waisraeli yalikuwa kwenu.
14Hivyo, mnapaswa kuagana na kuwaacha wakazi wa Morasheth-gathi.
Nao mji wa Akzibu hautawasaidia wafalme wa Israeli,
15Enyi wakazi wa Maresha,
Mungu atawaleteeni tena adui atakayewateka.
Viongozi waheshimiwa wa Israeli
watakimbilia pangoni huko Adulamu.
16Enyi watu wa Yuda, nyoeni upara
kuwaombolezea watoto wenu wapenzi;
panueni upara wenu uwe mpana kama wa tai,
maana watoto wenu watawaacha kwenda uhamishoni.

Mika1;1-16

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe