Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 2 June 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Tunamshukuru Mungu kwa kumaliza Kitabu cha Hosea,Leo Tunaanza Kitabu cha Yoeli..1


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tunamshukuru Mungu kwa kutupa kibali cha
 kupitia kitabu cha "HOSEA
"
Ni matumaini yangu kuna mengi tumejifunza/kufaidika
na kutupa mwanga/kuelewa kwenye kitabu hiki...

Leo tunapokwenda anza kupitia Kitabu cha"YOELI"tunamuomba Mungu wetu akatupe kibali,macho ya rohoni
 na akili ya kuelewa katika kujifunza NENO lake...
Ee Mungu  tunaomba ukatuongoze...!!
Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...


Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Neno la Mwenyezi-Mungu likanijia: “Nenda ukawatangazie waziwazi wakazi wote wa Yerusalemu kuwa mimi Mwenyezi-Mungu nasema hivi: Naukumbuka uaminifu wako ulipokuwa kijana, jinsi ulivyonipenda kama mchumba wako, ulivyonifuata jangwani kwenye nchi ambayo haikupandwa kitu.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Israeli, wewe ulikuwa mtakatifu kwangu, ulikuwa matunda ya kwanza ya mavuno yangu. Wote waliokudhuru walikuwa na hatia, wakapatwa na maafa. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....


Sikilizeni neno la Mwenyezi-Mungu, enyi wazawa wa Yakobo. Sikilizeni enyi jamaa zote za wazawa wa Israeli. Mwenyezi-Mungu asema hivi: “Wazee wenu waliona kosa gani kwangu hata wakanigeuka na kuniacha, wakakimbilia miungu duni, hata nao wakawa watu duni?
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

1Neno la Mwenyezi-Mungu lililomjia Yoeli, mwana wa Pethueli:
Watu waombolezea mimea
2Sikilizeni kitu hiki enyi wazee;
tegeni sikio wakazi wote wa Yuda!
Je, jambo kama hili limewahi kutokea maishani mwenu,
au nyakati za wazee wenu?
3Wasimulieni watoto wenu jambo hili,
nao wawasimulie watoto wao,
na watoto wao wakisimulie kizazi kifuatacho.
4Nzige, makundi kwa makundi, wameivamia mimea;
kilichoachwa na nzige kimeliwa na tunutu,
kilichoachwa na tunutu kimeliwa na parare,
kilichoachwa na parare kimeliwa na matumatu.
5Enyi walevi, levukeni na kulia;
pigeni yowe, enyi walevi wa divai;
zabibu zote za kutengeneza divai mpya zimeharibiwa.
6 Taz Ufu 9:8 Jeshi la nzige limeivamia nchi yetu;
lina nguvu na ni kubwa ajabu;
meno yake ni kama ya simba,
na magego yake ni kama ya simba jike.
7Limeiharibu mizabibu yetu,
na kuitafuna mitini yetu.
Limeyabambua magamba yake na kuyatupa chini,
na matawi yake yameachwa meupe.
8Lieni kama msichana aliyevaa vazi la gunia
akiombolezea kifo cha mchumba wake.
9Sadaka za nafaka na kinywaji zimetoweka nyumbani kwa Mwenyezi-Mungu.
Makuhani, wahudumu wa Mwenyezi-Mungu, wanaomboleza.
10Mashamba yamebaki matupu;
nchi inaomboleza,
maana nafaka imeharibiwa,
divai imetoweka,
mafuta yamekosekana.
11Ombolezeni enyi wakulima;
pigeni yowe enyi watunza mizabibu.
Ngano na shayiri zimeharibika,
mavuno yote shambani yameangamia.
12Mizabibu imenyauka;
mitini imedhoofika;
mikomamanga, mitende na mitofaa imekauka,
naam miti yote shambani imekauka.
Furaha imetoweka miongoni mwa watu.
13Enyi makuhani, jivikeni magunia kuomboleza,
lieni enyi wahudumu wa madhabahu.
Ingieni hekaluni mkaomboleze usiku kucha!
Sadaka za nafaka na kinywaji zimetoweka nyumbani kwa Mungu.
14Toeni amri watu wafunge;
itisheni mkutano wa kidini.
Kusanyeni wazee na wakazi wote wa nchi,
nyumbani kwa Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu,
na humo mkamlilie Mwenyezi-Mungu.
15Ole wetu kwa ile siku ya Mwenyezi-Mungu,
siku hiyo ya Mwenyezi-Mungu inakaribia;
inakuja pamoja na maangamizi,
kutoka kwa Mungu Mkuu.
16Mazao yetu yameharibiwa huku tunatazama.
Furaha na kicheko vimetoweka nyumbani kwa Mungu wetu.
17Mbegu zinaoza udongoni;
ghala za nafaka ni ukiwa mtupu,
ghala zimeharibika,
kwa kukosa nafaka ya kuhifadhi.
18Tazama wanyama wanavyolia kwa huzuni!
Makundi ya ng'ombe yanahangaika,
kwa sababu yamekosa malisho;
hata makundi ya kondoo yanateseka.
19Ninakulilia wewe, ee Mwenyezi-Mungu,
moto umemaliza malisho nyikani,
miali ya moto imeteketeza miti mashambani.
20Hata wanyama wa porini wanakulilia wewe,
maana, vijito vya maji vimekauka,
moto umemaliza malisho nyikani.

Yoeli1;1-20

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

No comments: