Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 17 June 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Amosi 9...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Basi, upepo mzuri wa kusi ulianza kuvuma, nao wakadhani wamefanikiwa lengo lao; hivyo wakangoa nanga, wakaiendesha meli karibu sana na pwani ya Krete. Lakini haukupita muda, upepo mkali uitwao “Upepo wa Kaskazi” ulianza kuvuma kutoka kisiwani.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako,
Tukijinyenyekeza,tukijiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunamomba utusamehe dhambi zetu
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
 ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea

Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Upepo uliipiga ile meli, na kwa kuwa hatukuweza kuukabili, tukaiacha ikokotwe na huo upepo. Kisiwa kimoja kiitwacho Kauda kilitukinga kidogo na ule upepo; na tulipopita kusini mwake tulifaulu, ingawa kwa shida, kuusalimisha ule mtumbwi wa meli.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Wale wanamaji waliuvuta mtumbwi ndani, kisha wakaizungushia meli kamba na kuifunga kwa nguvu. Waliogopa kwamba wangeweza kukwama kwenye ufuko wa bahari, pwani ya Libia. Kwa hiyo walishusha matanga na kuiacha meli ikokotwe na upepo.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...

Nawapenda.

Adhabu ya Mungu
1Nilimwona Mwenyezi-Mungu amesimama kando ya madhabahu, naye akaniamuru:
“Zipige hizo nguzo za hekalu
mpaka misingi yake itikisike.
Zivunje hizo nguzo ziwaangukie watu vichwani.
Wale watakaosalia nitawaua kwa upanga;
hakuna hata mmoja wao atakayenusurika,
naam, hakuna atakayetoroka.
2Wajapojichimbia njia ya kwenda kuzimu,
huko nitawachukua kwa mkono wangu;
wajapopanda mbinguni,
nitawaporomosha chini.
3Wajapojificha juu ya mlima Karmeli,
huko nitawasaka na kuwachukua;
wajapojificha mbali nami vilindini mwa bahari,
humo nitaliamuru joka la baharini liwaume.
4Wajapochukuliwa mateka na adui zao,
huko nitatoa amri wauawe kwa upanga.
Nitawachunga kwa makini sana
niwatendee mabaya na si mema.”
5Bwana Mwenyezi-Mungu wa majeshi,
anaigusa ardhi nayo inatetemeka
na wakazi wake wanaomboleza;
dunia nzima inapanda na kushuka
kama kujaa na kupwa kwa mto Nili wa Misri.
6Mwenyezi-Mungu amejenga makao yake mbinguni,
nayo dunia akaifunika kwa anga;
huyaita maji ya bahari,
na kuyamwaga juu ya nchi kavu.
Mwenyezi-Mungu, ndilo jina lake!
Marekebisho baada ya uharibifu
7Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Kwangu mimi, nyinyi Waisraeli,
hamna tofauti yoyote na watu wa Kushi!9:7 Kushi: Eneo ambalo sasa ni Ethiopia na sehemu ya Sudani.
Niliwatoa Wafilisti kutoka Krete,
na Waashuru kutoka Kiri,
kama nilivyowatoa nyinyi kutoka Misri.
8Mimi, Bwana Mwenyezi-Mungu nautazama ufalme wenye dhambi,
na nitauangamiza kabisa kutoka duniani.
Lakini sitawaangamiza wazawa wote wa Yakobo.
9“Tazama, nitatoa amri,
na kuwapepeta Waisraeli kati ya mataifa
kama mtu achekechavyo nafaka
niwakamate wote wasiofaa.
10Wenye dhambi miongoni mwa watu wangu,
watafia vitani kwa upanga;
hao ndio wasemao:
‘Maafa hayatatukumba wala kutupata!’
11“Siku yaja nitakapoisimika nyumba ya Daudi iliyoanguka;
nitazitengeneza kuta zake,
na kusimika upya magofu yake.
Nitaijenga upya kama ilivyokuwa hapo zamani.
12Nao Waisraeli watamiliki mabaki ya Edomu
na mataifa yote yaliyokuwa yangu.
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema,
na nitafanya hivyo.
13“Wakati waja kwa hakika,
ambapo mara baada ya kulima
mavuno yatakuwa tayari kuvunwa;
mara baada ya kupanda mizabibu
utafuata wakati wa kuvuna zabibu.
Milima itabubujika divai mpya,
navyo vilima vitatiririka divai.
14Nitarekebisha hali ya watu wangu Waisraeli.
Watajenga miji yao iliyoharibiwa na kuishi humo;
watapanda mizabibu na kunywa divai yake;
watalima mashamba na kula mazao yake.
15Nitawasimika katika nchi yao,
wala hawatang'olewa tena
kutoka katika nchi niliyowapa.
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”


Amosi9;1-15

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

No comments: