|
Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?
Haleluyah ni siku/wiki nyingine tena Mungu wetu ametuchagua na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....
Tumshukuru Mungu wetu katika yote...
Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!
Kijana atatunzaje maisha yake kuwa safi? Kwa kuyaongoza kadiri ya neno lako. Najitahidi kukutii kwa moyo wote; usiniache nikiuke amri zako. Nimeshika neno lako moyoni mwangu, nisije nikakukosea.
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea Jehovah usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona....
Utukuzwe, ee Mwenyezi-Mungu! Unifundishe masharti yako. Nitayarudia kwa sauti maagizo yako yote uliyotoa.
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe
Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...
Nafurahi kufuata maamuzi yako, kuliko kuwa na utajiri mwingi. Nazitafakari kanuni zako, na kuzizingatia njia zako. Nayafurahia masharti yako; sitalisahau neno lako.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu kila mmoja na mahitaji yake Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako wakasimamie Neno lako nalo likawaweke huru Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele Amina...!!
Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea kama inavyompendeza yeye.... Nawapenda.
|
Mika anawashutumu viongozi wa Israeli
1Sasa sikilizeni enyi wakuu wa wazawa wa Yakobo,
sikilizeni, enyi watawala wa wazawa wa Israeli!
Nyinyi ndio mnaopaswa kujua mambo ya haki.
2Lakini nyinyi mnachukia mema na kupenda maovu.
Mnawachuna ngozi watu wangu,
na kubambua nyama mifupani mwao.
3Mnajilisha kwa nyama ya watu wangu
mnawachuna ngozi yao,
mnaivunjavunja mifupa yao,
na kuwakatakata kama nyama ya kupika,
kama nyama ya kutia ndani ya chungu.
4Wakati unakuja ambapo mtamlilia Mwenyezi-Mungu,
lakini yeye hatawajibu.
Atauficha uso wake wakati huo,
kwa sababu mmetenda mambo maovu.
5Mwenyezi-Mungu asema hivi
kuhusu manabii wanaowapotosha watu wake;
manabii ambao hutabiri amani wakipewa kitu,
lakini huwatishia watu kwa vita wasipopewa kitu:
6“Kwenu manabii kutakuwa usiku bila maono,
kutakuwa giza kwenu bila ufunuo.
Kwenu manabii kutakuchwa,
mchana utakuwa giza kwenu.”
7Mabingwa wa maono watafedheheka,
mafundi wa kubashiri wataaibishwa;
wote watafunga midomo yao,
maana hawatapata jibu lolote kutoka kwa Mungu.
8Lakini kwa upande wangu,
nimejazwa nguvu na roho ya Mwenyezi-Mungu;
nimejaliwa kujua haki na kuwa na uwezo
niwatangazie wazawa wa Yakobo kosa lao,
niwaambie Waisraeli dhambi yao.
9Sikieni jambo hili enyi viongozi wa wazawa wa Yakobo,
sikilizeni, enyi watawala wa Waisraeli:
Nyinyi mnachukia mambo ya haki
na kupotosha mambo ya adili.
10Nyinyi mnajenga mji wa Siyoni kwa damu,
naam, mji wa Yerusalemu kwa dhuluma.
11Waamuzi hufanya kazi yao kwa rushwa,
makuhani wake hufundisha kwa malipo,
manabii hutabiri kwa fedha.
Hata hivyo hujidai kumtegemea Mwenyezi-Mungu,
wakisema, “Mwenyezi-Mungu, si yupo pamoja nasi?
Hatutapatwa na madhara yoyote!”
12Haya! Kwa sababu yenu,
Siyoni utalimwa kama shamba,
Yerusalemu utakuwa magofu,
nao mlima wa hekalu utakuwa msitu.
Mika3;1-12
Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)
"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe
No comments:
Post a Comment