Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 31 March 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Ezekieli 30...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Filipo akamwambia, “Bwana, tuoneshe Baba, nasi tutatosheka.” Yesu akamwambia, “Nimekaa nanyi muda wote huu, nawe Filipo hujanijua? Aliyekwisha niona mimi amemwona Baba. Unawezaje basi, kusema: ‘Tuoneshe Baba?’
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....



Je, huamini kwamba mimi niko ndani ya Baba, naye Baba yuko ndani yangu? Maneno ninayowaambieni siyasemi kwa mamlaka yangu; Baba aliye ndani yangu anafanya kazi yake. Mnapaswa kuniamini ninaposema kwamba mimi niko ndani ya Baba naye Baba yuko ndani yangu. Ama sivyo, aminini kwa sababu ya mambo ninayofanya.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...



Kweli nawaambieni, anayeniamini atafanya mambo ninayofanya mimi; naam, atafanya hata makuu zaidi, kwani ninakwenda kwa Baba. Na chochote mtakachoomba kwa jina langu nitafanya, ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Mkiniomba chochote kwa jina langu, nitawafanyieni.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Mwenyezi-Mungu ataiadhibu Misri
1Neno la Mwenyezi-Mungu lilinijia: 2“Wewe mtu! Toa unabii useme kuwa mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema hivi:
Ombolezeni na kusema: ‘Ole wetu siku ile!’
3Kwa maana, siku hiyo imekaribia;
siku ile ya Mwenyezi-Mungu iko karibu.
Hiyo itakuwa siku ya mawingu,
siku ya maangamizi kwa mataifa.
4Vita vitazuka dhidi ya Misri,
na wasiwasi mkuu utaikumba nchi ya Kushi,
wakati Wamisri wengi wataanguka wameuawa,
mali zao zitakapochukuliwa,
na misingi ya miji yao kubomolewa.
5“Watu wote waliofungamana na Wamisri, yaani watu wa Kushi, Puti, Ludi, Arabia yote na Libia wataangamia pamoja nao.
6“Mimi Mwenyezi-Mungu nasema hivi:
Wote wanaoiunga mkono Misri wataangamia,
mashujaa wake wenye fahari wataangamizwa,
tangu Migdoli mpaka Syene watu watauawa vitani.
Mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nimesema.
7Misri itakuwa jangwa kama nchi zilizo jangwa
na miji yake itakuwa magofu kama miji iliyoteketezwa.
8Nitakapoiteketeza Misri kwa moto
na kuwavunjilia mbali wasaidizi wake wote
ndipo watakapotambua kuwa mimi ni Mwenyezi-Mungu.
9Siku hiyo, nitapeleka wajumbe kwenda kuwatisha
Waethiopia wanaojidhani kuwa salama.
Watatetemeka siku Misri itakapoangamia.
Naam! Kweli siku hiyo yaja!
10“Mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema hivi:
Nitamtumia Nebukadneza, mfalme wa Babuloni,
kukomesha utajiri wa nchi ya Misri.
11Nebukadneza mwenyewe pamoja na watu wake,
taifa katili kuliko mataifa yote,
watatumwa kuiangamiza nchi ya Misri.
Watachomoa panga zao dhidi ya Misri
na kuijaza nchi hiyo watu waliouawa.
12Nitaukausha mto Nili na vijito vyake,
na kuwauzia watu waovu nchi ya Misri.
Nitasababisha uharibifu nchini kote
kwa mkono wa watu wageni.
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
13“Mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema hivi:
Nitaharibu vinyago vya miungu,
na kukomesha sanamu mjini Memfisi.
Hakutakuwa na mkuu tena huko Misri.
Nitasababisha hofu itawale nchini Misri.
14Mji wa Pathrosi nitaufanya kuwa mtupu,
mji wa Soani nitauwasha moto,
mji wa Thebesi nitauadhibu.
15Nitamwaga ghadhabu yangu juu ya Pelusiumu,
ile ngome inayotegemewa na Misri;
na kuangamiza makundi ya Thebesi.
16Nitaiwasha moto nchi ya Misri.
Pelusiumu utashikwa na dhiki kubwa,
ukuta wa Thebesi utabomolewa,30:16 ukuta … utabomolewa: Makala ya Kiebrania si dhahiri.
nao Memfisi utakabiliwa na adui mchana wazi.
17Vijana wanaume wa Oni na Pi-besethi watauawa kwa upanga,
na wakazi wengine watachukuliwa uhamishoni.
18Huko Tahpanesi mchana utakuwa giza
wakati nitavunja mamlaka ya Misri
na kiburi chake kikuu kukomeshwa.
Wingu litaifunika nchi ya Misri
na watu wake watachukuliwa mateka.
19Ndivyo nitakavyoiadhibu Misri.
Na watu watatambua kuwa mimi ni Mwenyezi-Mungu.”
Kuvunjwa kwa nguvu za Misri
20Siku ya saba ya mwezi wa kwanza, mwaka wa kumi na moja tangu uhamisho wetu, neno la Mwenyezi-Mungu lilinijia: 21“Wewe mtu! Nimeuvunja mkono wa Farao mfalme wa Misri, nao haukufungwa ili uweze kupona na kuweza kushika upanga. 22Kwa hiyo, mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema hivi: Nitapambana na Farao mfalme wa Misri. Nitaivunja mikono yake yote miwili, ule mzima na hata uliovunjika. Na upanga ulio mkononi mwake utaanguka chini. 23Nitawatawanya Wamisri kati ya mataifa na kuwasambaza katika nchi nyingine. 24Mikono ya mfalme wa Babuloni nitaitia nguvu na kutia upanga wangu mkononi mwake. Lakini nitaivunja mikono ya Farao, naye atapiga kite mbele ya mfalme wa Babuloni kama mtu aliyejeruhiwa vibaya sana. 25Mikono ya mfalme wa Babuloni nitaiimarisha, lakini mikono ya Farao italegea. Hapo watu watatambua kuwa mimi ni Mwenyezi-Mungu. Nitakapotia upanga wangu mkononi mwa mfalme wa Babuloni, ataunyosha dhidi ya nchi ya Misri, 26nami nitawatawanya Wamisri kati ya mataifa mengine na kuwasambaza katika nchi nyingine. Ndipo watakapotambua kuwa mimi ni Mwenyezi-Mungu.”


Ezekieli30;1-26

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 30 March 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Ezekieli 29...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki/nyingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...


Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu

Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!


Yesu aliwaambia, “Msifadhaike mioyoni mwenu. Mwaminini Mungu, niaminini na mimi pia. Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; kama isingekuwa hivyo, ningalikwisha waambieni. Sasa nakwenda kuwatayarishieni nafasi.

Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona

Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona....
Na nikienda na kuwatayarishieni nafasi, nitarudi na kuwachukueni kwangu, ili nanyi muwe pale nilipo mimi. Mnajua njia ya kwenda huko ninakokwenda.”

Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu

Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...
Thoma akamwuliza, “Bwana, hatujui unakokwenda, tutawezaje basi, kuijua hiyo njia?” Yesu akamjibu, “Mimi ni njia, na ukweli na uhai. Hakuna awezaye kwenda kwa Baba ila kwa kupitia kwangu. Ikiwa mnanijua mimi, mnamjua na Baba yangu pia. Na tangu sasa, mnamjua, tena mmekwisha mwona.”
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimamie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.




Unabii dhidi ya Misri
1Siku ya kumi na mbili ya mwezi wa kumi, mwaka wa kumi tangu uhamisho wetu, neno la Mwenyezi-Mungu lilinijia: 2“Wewe mtu! Mgeukie Farao mfalme wa Misri, utoe unabii juu yake na nchi yote ya Misri. 3Mwambie kuwa mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema hivi:
Mimi nitapambana na wewe mfalme wa Misri,
wewe mamba ulalaye mtoni Nili!
Wewe unafikiri kwamba Nili ni wako,
kwamba wewe ndiwe uliyeufanya!
4Basi, nitakutia ndoana tayani mwako,
na kufanya samaki wakwame magambani mwako.
Nitakuvua kutoka huko mtoni.
5Nitakutupa jangwani,
wewe na samaki hao wote.
Mwili wako utaanguka mbugani;
wala hakuna atakayekuokota akuzike.
Nimeutoa mwili wako
uwe chakula cha wanyama wakali na ndege.
6 29:6 Taz Isa 36:6 Hapo ndipo wakazi wote wa Misri watatambua kuwa mimi ni Mwenyezi-Mungu.
“Waisraeli walikutegemea wewe ee Misri, lakini umekuwa dhaifu kama utete. 7Walipokushika kwa mkono, ulivunjika na kutegua mabega yao. Walipokuegemea ulivunjika na kutetemesha viungo vyao. 8Kwa hiyo, mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema hivi: Nitazusha upanga dhidi yako na kuwaua watu na wanyama wako wote. 9Kwa sababu umesema kuwa mto Nili ni wako, kwamba ndiwe uliyeufanya, basi, nchi yako, Misri, itakuwa tupu na jangwa. Ndipo watu watatambua kuwa mimi ni Mwenyezi-Mungu. 10Hakika nitakuadhibu wewe na mito yako; kwa hiyo nitaifanya nchi ya Misri kuwa jangwa na tupu toka Migdoli mpaka Syene hadi mipakani mwa Kushi. 11Hakuna mtu wala mnyama atakayepita huko. Haitakaliwa kwa muda wa miaka arubaini. 12Kati ya miji yote iliyoharibiwa, miji ya Misri itakuwa mitupu kwa miaka arubaini. Nitawatawanya Wamisri kati ya watu wa mataifa mengine na kuwasambaza katika nchi nyingine.
13“Lakini mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema hivi: Baada ya miaka arubaini nitawakusanya Wamisri kutoka kwa mataifa walimotawanywa. 14Nitawafanikisha tena Wamisri. Nitawarudisha katika nchi ya Pathrosi, nchi yao ya asili. Huko watakuwa na ufalme usio na nguvu, 15ufalme dhaifu kuliko falme zote; wala hawataweza kujikuza juu ya mataifa mengine. Nitawafanya Wamisri wawe watu dhaifu hata wasiweze kuyatawala mataifa mengine tena. 16Misri haitakuwa tena na nguvu za kuweza kutegemewa na watu wa Israeli. Waisraeli watakumbuka jinsi walivyokosa kwa kutegemea nchi ya Misri. Waisraeli watatambua kuwa mimi ni Bwana Mwenyezi-Mungu.”
Mfalme Nebukadneza ataishinda Misri
17Siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, mwaka wa ishirini na saba tangu uhamisho wetu, neno la Mwenyezi-Mungu lilinijia: 18“Wewe mtu! Nebukadneza,29:18 Nebukadneza: Au Nebukadreza. mfalme wa Babuloni, alilipa jeshi lake jukumu gumu la kuishambulia Tiro. Vichwa vyote vya wanajeshi wake vilipata upara na mabega yote yalichubuka. Lakini yeye, wala jeshi lake, hawakuambulia chochote kutokana na uvamizi huo alioufanya dhidi ya Tiro. 19Kwa hiyo, mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema hivi: Nitampa Nebukadneza mfalme wa Babuloni, nchi ya Misri. Ataipora mali yake yote, na kuchukua utajiri wa Misri kuwa ujira wa jeshi lake. 20Nimempa nchi ya Misri kuwa ujira wa jasho lake kwa kuwa majeshi yake yalifanya kazi kwa ajili yangu. Mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nimesema. 21Siku hiyo, nitawafanya Waisraeli wawe na nguvu na kukuwezesha wewe Ezekieli uongee miongoni mwao. Nao watapata kujua kuwa mimi ni Mwenyezi-Mungu.”



Ezekieli29;1-21

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Friday 27 March 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Ezekieli 28...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Adhabu yao itakuwa kuangamizwa milele na kutengwa mbali na utukufu wake mkuu, wakati atakapokuja siku ile kupokea utukufu kutoka kwa watu wake na heshima kutoka kwa wote wanaoamini. Nyinyi pia mtakuwa miongoni mwao, kwani mmeuamini ule ujumbe tuliowaletea.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Ndiyo maana tunawaombeeni daima. Tunamwomba Mungu wetu awawezesheni kustahili maisha aliyowaitia muyaishi. Tunamwomba, kwa uwezo wake, atimize nia yenu ya kutenda mema na kukamilisha kazi yenu ya imani.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Kwa namna hiyo, jina la Bwana wetu Yesu litapata utukufu kutoka kwenu, nanyi mtapata utukufu kutoka kwake kwa neema ya Mungu wetu na ya Bwana Yesu Kristo.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...

Nawapenda.


Unabii juu ya mfalme wa Tiro
1Neno la Mwenyezi-Mungu lilinijia: 2“Wewe mtu! Mwambie mfalme wa Tiro kuwa mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema hivi:
Wewe una kiburi cha moyo,
na umesema kwamba wewe ni mungu,
kwamba umekalia kiti cha enzi cha miungu,
umekaa mbali huko baharini.
Lakini, wewe ni binadamu tu wala si Mungu,
ingawa wajiona kuwa una hekima kama Mungu.
3Haya! Wewe wajiona mwenye hekima kuliko Danieli,
wadhani hakuna siri yoyote usiyoijua.
4Kwa hekima na akili yako
umejipatia utajiri,
umejikusanyia dhahabu na fedha
ukaziweka katika hazina zako.
5Kwa busara yako kubwa katika biashara
umejiongezea utajiri wako,
ukawa na kiburi kwa mali zako!
6Kwa hiyo mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema hivi:
Kwa vile unajiona mwenye hekima kama Mungu,
7basi nitakuletea watu wageni,
mataifa katili kuliko yote.
Wataharibu fahari ya hekima yako
na kuchafua uzuri wako.
8Watakutumbukiza chini shimoni,
nawe utakufa kifo cha kikatili kilindini mwa bahari.
9Je, utajiona bado kuwa mungu
mbele ya hao watakaokuua?
Mikononi mwa hao watakaokuangamiza,
utatambua kuwa wewe ni mtu tu, wala si Mungu!
10Utakufa kifo cha aibu kubwa
mikononi mwa watu wa mataifa.
Ni mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nimesema.”
Kuanguka kwa mfalme wa Tiro:
11Tena neno la Mwenyezi-Mungu lilinijia: 12“Wewe mtu! Imba wimbo wa maombolezo juu ya mfalme wa Tiro. Mwambie kuwa mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema hivi:
Wewe mfalme wa Tiro ulikuwa upeo wa ukamilifu;28:12 makala ya Kiebrania si dhahiri.
ulijaa hekima na uzuri kamili.
13Ulikaa Edeni, bustani ya Mungu.
Ulipambwa kwa kila namna ya johari,
akiki, topazi, yaspi, zabarajadi, berili,
sardoniki, johari ya rangi ya samawati, almasi na zumaridi.
Ulikuwa na mapambo ya dhahabu.
Yote uliwekewa tayari siku ulipoumbwa.28:13 siku ulipoumbwa: Makala ya Kiebrania si dhahiri.
14Nilimteua malaika kukulinda,28:14 Nilimteua … kukulinda: Makala ya Kiebrania si dhahiri.
uliishi katika mlima wangu mtakatifu
na kutembea juu ya vito vinavyometameta.
15Uliishi maisha yasiyo na lawama,
tangu siku ile ulipoumbwa,
hadi ulipoanza kufanya uovu.
16Ufanisi wa biashara yako
ulikujaza dhuluma, ukatenda dhambi.
Kwa hiyo nilikufukuza kama kinyaa,
mbali na mlima wangu mtakatifu.
Na yule malaika aliyekulinda
akakufukuzia mbali na vito vinavyometameta.
17Ulikuwa na kiburi
kwa sababu ya uzuri wako.
Uliharibu hekima yako kwa sababu ya fahari yako.
Nilikubwaga chini udongoni,
nikakufanya kuwa kioja kwa wafalme.
18Kwa wingi wa uhalifu wako
na udanganyifu katika biashara yako
ulipachafua mahali pako pa ibada;
kwa hiyo nilizusha moto kwako, nao ukakuteketeza,
nami nikakufanya majivu juu ya nchi,
mbele ya wote waliokutazama.
19Wote wanaokufahamu kati ya mataifa
wameshikwa na mshangao juu yako.
Umeufikia mwisho wa kutisha,
na hutakuwapo tena milele.”
Unabii juu ya Sidoni
20 28:20-26 Taz Yoe 3:4-8; Zek 9:1-2; Mat 11:21-22; Luka 10:13-14 Neno la Mwenyezi-Mungu lilinijia: 21“Wewe mtu! Ugeukie mji wa Sidoni, 22utoe unabii juu yake kwamba mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema hivi:
Mimi nitapambana nawe Sidoni,
na kuudhihirisha utukufu wangu kati yako.
Nitakapotekeleza hukumu zangu juu yako
na kukudhihirishia utakatifu wangu,
ndipo utakapotambua kuwa mimi ni Mwenyezi-Mungu.
23Nitakupelekea maradhi mabaya
na umwagaji damu utafanyika katika barabara zako.
Utashambuliwa kwa upanga toka pande zote
na watu wako watakaouawa, watakuwa wengi.
Ndipo watakapotambua kuwa mimi ni Mwenyezi-Mungu.”
Waisraeli watapata baraka
24Mungu asema, “Mataifa jirani na Waisraeli ambayo yalikuwa yanawaudhi hayataweza tena kuwaumiza Waisraeli kama vile kwa miiba na michongoma. Ndipo watakapojua ya kuwa mimi ni Bwana Mwenyezi-Mungu.
25“Mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema hivi: Nitawakusanya na kuwaleta Waisraeli kutoka katika mataifa yote ambamo walitawanywa. Hivyo nitawafanya watu wa mataifa waone kuwa mimi ni mtakatifu. Watu wa Israeli wataishi katika nchi yao ambayo mimi nilimpa mtumishi wangu Yakobo. 26Watakaa humo salama salimini; watajenga nyumba na kupanda mizabibu. Wataishi bila hofu maana mataifa jirani zao ambayo yaliwaudhi, mimi nitayaadhibu. Hapo watatambua kuwa mimi ni Mwenyezi-Mungu, Mungu wao.”


Ezekieli28;1-26

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 26 March 2020

Watoto na Malezi;Shule ya Nyumbani-Jikoni Leo;Ratiba Ya Chakula Na Rachel-siwa...







Ratiba ya chakula ya watoto Waswahili wakati huu Wa Shule Ya Nyumbani

 :8:30-Uji;wa-Mchele,wa-Dona,wa-urezi,wa-Muhogo n.k.

 :10:30-CHai/juisi; na-Mihogo,Viazi,Chapati,maandazi,                             Vitumbua n.k.

 :1:00-Ugali/wali,Ndizi/viazi,Makande n.k
         Mboga;Nyama/kuku/samaki,Maharage/kunde/mbaazi,
        Mboga za majani,bamia/mrenda n.k

 :4:00-Chai/juisi/maji;na kachori,visheti,katlesi,                                        Keki,Bagia/badia/bajia 🤷🏽‍♀️za dengu/kunde n.k

 :6:00-Wali,Tambi,chipsi(zege)n.k

       : Chakula cha mchana kama kimebaki kinaweza kuliwa ..
       :Matunda wakati wowote 🍎(Desert)upendavyo 🍮🍧
    :Jumamosi/jumapili,wajiachie tuu wanavyopenda -🍔🌭🌮
    :Kutupa chakula ni mwiko ..

   :Ratiba ya chakula kipindi hiki watoto wapo nyumbani 
   :Tujaribu kuwalisha kama waswahili 🤣kama itawezekana 🤔
     :
     :
  :Nimatumaini yangu wakirudi shule watakuwa wenye nguvu na        Afya Njema 💪🏽💃🏾...

  :Mzazi/Mlezi;unaweza kuongeza/kupunguza na kusahihisha                              nilipokosea.
 :Pia unaweza kuandaa ya kwako ili tupate kujifunza zaidi
 :Unaweza kunitumia kwa :E-mail;rasca@hotmail.co.uk

  :
  :
 : Angalizo;mimi si mtaalamu wa Chakula na Lishe..
                 Unaweza kufanya utafiti zaidi
                Kulingana na afya ya mtoto wako 🙏🏽


Imeandikwa na Rachel siwa 🙏🏽❤️
Asanteni.





"Swahili Na Waswahili"Pamoja Sana.

Kikombe Cha Asubuhi; Ezekieli 27...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Mimi Paulo, Silwano na Timotheo, kwa jumuiya ya kanisa la Thesalonike, ambayo ni watu wake Mungu Baba yetu na wa Bwana Yesu Kristo. Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....


Ndugu, tunapaswa kumshukuru Mungu daima kwa ajili yenu. Inafaa kwetu kufanya hivyo kwani imani yenu inakua sana na kupendana kwenu kunaongezeka sana. Ndio maana sisi tunajivunia nyinyi katika makanisa ya Mungu. Tunaona fahari juu ya jinsi mnavyoendelea kuamini na kustahimili katika udhalimu wote na mateso mnayopata.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Hayo yote yanathibitisha kwamba hukumu ya Mungu ni ya haki, na matokeo yake, nyinyi mtastahili ufalme wake ambao kwa ajili yake mnateseka. Mungu atafanya jambo la haki: Atawalipa mateso wale wanaowatesa nyinyi na kuwapeni nafuu nyinyi mnaoteseka, na sisi pia. Atafanya jambo hilo wakati Bwana atakapotokea kutoka mbinguni pamoja na malaika wake wenye nguvu na miali ya moto, kuwaadhibu wale wanaomkataa Mungu na wale wasiotii Habari Njema ya Bwana wetu Yesu.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Maombolezo juu ya Tiro
1Neno la Mwenyezi-Mungu lilinijia: 2“Sasa ewe mtu, imba utenzi huu wa maombolezo juu ya mji wa Tiro, 3mji ule kando ya bahari, unaofanya biashara na mataifa ya pwani. Uambie: Bwana Mwenyezi-Mungu asema hivi:
Ewe Tiro, wewe umejigamba
u mzuri kwelikweli!
4Mipaka yako imeenea kwelikweli!
Umejengwa kama meli nzuri.
5Wajenzi wako walitumia misonobari kutoka Seniri
kupasua mbao zako zote;
walichukua mierezi kutoka Lebanoni
kukutengenezea mlingoti.
6Walichukua mialoni toka Bashani
wakakuchongea makasia yako;
walikitengenezea silaha
kwa misonobari ya kisiwa cha Kupro,
na kuipamba kwa pembe.
7Kitani kilichotariziwa kutoka Misri
kilikuwa kwa kupamba tanga lako
na kwa ajili ya bendera yako.
Chandarua chako kilitengenezwa
kwa rangi ya samawati na urujuani
kutoka visiwa vya Elisha.
8Watu wa Sidoni na Arvadi
walikuwa wapiga makasia wako.
Wenye hekima wako walikuwa ndani
wakifanya kazi kama wanamaji.
9Wazee wa Gebali na mafundi wao
walikuwa kwako kuziba nyufa zako.
Mabaharia waliokuwa wakipitia kwako
walifanya biashara nawe.
10Watu kutoka Persia, Ludi na Puti
walijiunga katika jeshi lako;
walirundika kwenye kambi zao za jeshi
ngao zao na kofia zao.
Wanajeshi hao walikupatia fahari.
11Watu wa Arvadi na wa Hele na jeshi lao walilinda kuta zako pande zote, nao watu wa Gamadi walilinda minara yako. Walitundika ngao zao kwenye kuta zako pande zote, na hivyo wakaukamilisha uzuri wako. 12Watu wa Tarshishi walifanya biashara nawe kwa sababu ya utajiri wako mwingi na wa kila namna. Walitoa fedha, chuma, bati, na risasi kupata bidhaa zako. 13Watu wa Yavani, Tubali na Mesheki, walifanya biashara nawe, wakakupatia watumwa na vifaa vya shaba wapate bidhaa zako. 14Bidhaa zako uliziuza huko Beth-togarma ili kujipatia farasi wa mizigo na wa vita, ngamia na nyumbu. 15Watu wa Dedani27:15 Dedani: Tafsiri ya Kigiriki ni Rode. walifanya biashara nawe. Nchi nyingi za pwani zilikuwa masoko yako maalumu. Watu wake walikuletea pembe za ndovu na mipingo kulipia bidhaa zako. 16Watu wa Edomu27:16 Edomu: Hati nyingine: Aramu. walifanya biashara nawe kwa sababu ya wingi wa bidhaa zako. Kwa kupata bidhaa zako walikupa akiki, vitambaa vya urujuani, vitambaa vilivyonakshiwa, kitani safi, matumbawe na yakuti. 17Hata watu wa Yuda na Israeli walifanya biashara nawe; walikupa ngano,27:17 makala ya Kiebrania ina maneno mawili yasiyoeleweka. zeituni, tini za mwanzoni, asali, mafuta na marhamu kulipia bidhaa zako. 18Watu wa Damasko walifanya biashara nawe kwa sababu ya wingi wa bidhaa zako; walikupa divai kutoka Helboni na sufu nyeupe. 19Vedani na Yavani walisafirisha bidhaa zako toka Uzali; hata chuma kilichofuliwa, mdalasini na mchaichai ili kupata bidhaa zako. 20Watu wa Dedani walifanya biashara nawe kwa kukupatia matandiko ya farasi. 21Waarabu na wakuu wote wa nchi ya Kedari walikuwa wachuuzi wako wakuu katika biashara ya wanakondoo, kondoo madume na mbuzi. 22Wachuuzi wa Sheba na wa Rama walifanya biashara nawe; walikuletea viungo vya chakula, vito vya thamani na dhahabu kujipatia bidhaa zako safi. 23Wakazi wa miji ya Harani, Kane na Edeni na wachuuzi wa Ashuru na Kilmadi walifanya biashara nawe. 24Hao walifanya nawe biashara ya mavazi ya fahari, nguo za buluu zilizotariziwa, mazulia ya rangi angavu vifundo na kamba zilizosokotwa imara. 2527:25-36 Taz Ufu 18:11-19 Merikebu za Tarshishi ndizo zilikusafirishia bidhaa zako.
Basi kama meli katikati ya bahari
wewe ulikuwa umejaa shehena.
26Wapiga makasia wako walikupeleka mbali baharini.
Upepo wa mashariki umekuvunjavunja
ukiwa mbali katikati ya bahari.
27Utajiri wako wa bidhaa na mali,
wanamaji wako wote chomboni,
mafundi wako wa meli na wachuuzi wako,
askari wako wote walioko kwako,
pamoja na wasafiri walioko kwako,
wote wataangamia baharini,
siku ile ya kuangamizwa kwako.
28Mlio wa mabaharia wako utakaposikika,
nchi za pwani zitatetemeka.
29Hapo wapiga makasia wote
wataziacha meli zao.
Wanamaji na manahodha watakaa pwani.
30Wataomboleza kwa uchungu wa moyo juu yako,
na kulia kwa uchungu mkubwa;
watajitupia mavumbi vichwani mwao
na kugaagaa kwenye majivu.
31Wamejinyoa vichwa kwa ajili yako
na kuvaa mavazi ya gunia.
Watalia kwa uchungu wa moyo juu yako.
32Wataimba wimbo wa ombolezo juu yako;
‘Nani aliyepata kuangamizwa kama Tiro
katikati ya bahari?’
33Bidhaa zako zilipowasili nchi za ngambo,
ulitosheleza mahitaji ya watu wengi!
Kwa wingi wa utajiri wa bidhaa zako
uliwatajirisha wafalme wa dunia.
34Lakini sasa umevunjikia baharini;
umeangamia katika vilindi vya maji.
Shehena yako na jamii ya mabaharia
vimezama pamoja nawe.
35Wakazi wote wa visiwani
wamepigwa na bumbuazi juu yako;
wafalme wao wameogopa kupindukia,
nyuso zimekunjamana kwa huzuni.
36Wachuuzi wa mataifa watakufyonya!
Umeufikia mwisho wa kutisha,
na hutakuwapo tena milele!”



Ezekieli27;1-36

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.