Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 28 June 2019

Kikombe Cha Asubuhi ; Methali 7...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Mungu aliweka siku nyingine ambayo inaitwa “Leo,” akasema baadaye kwa njia ya Daudi maneno yaliyokwisha tajwa: “Kama mkisikia sauti ya Mungu leo, msiwe wakaidi.”
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Kama Yoshua angekuwa amewapa watu hao hilo pumziko, Mungu hangalisema baadaye juu ya siku nyingine. Kwa hiyo, basi, bado kuna kupumzika kwa watu wa Mungu. Maana, kila aingiaye mahali pa pumziko la Mungu atapumzika kutoka katika kazi yake kama vile pia Mungu alivyopumzika kutoka kazi yake. Basi, tujitahidi kuingia katika pumziko hilo, ili asiwepo yeyote miongoni mwetu atakayekataa kutii kama walivyofanya wao.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Neno la Mungu ni hai na lina nguvu; ni kali kuliko upanga wenye makali kuwili. Hukata kabisa mpaka mahali ambapo moyo na roho hukutana, mpaka pale vikutanapo viungo vya mwili na uboho. Neno hilo huchambua nia na fikira za mioyo ya watu. Hakuna kiumbe chochote kilichofichika mbele ya Mungu; kila kitu kimefunuliwa wazi mbele ya macho yake yeye ambaye kwake tutapaswa kutoa hoja ya matendo yetu.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....
Nawapenda.

1Mwanangu, yashike maneno yangu,
zihifadhi kwako amri zangu.
2Zifuate amri zangu nawe utaishi;
yalinde mafundisho yangu kama mboni ya jicho lako.
3Yafunge vidoleni mwako;
yaandike moyoni mwako.
4Iambie Hekima: “Wewe ni dada yangu”,
na Busara “Wewe ni rafiki yangu”.
5Vitakulinda mbali na mwanamke mbaya,
vitakuepusha na maneno matamu ya mwanamke mgeni.

Mwanamke mwasherati
6Siku moja dirishani mwa nyumba yangu,
nilichungulia nje kupitia viunzi vya dirisha,
7nikawaona vijana wengi wajinga,
na mmoja hasa aliyekuwa mpumbavu.
8Huyo alikuwa akitembea kwenye barabara ile,
karibu na kona alikoishi mwanamke fulani.
Basi akashika njia iendayo nyumbani kwa mwanamke huyo.
9Ilikuwa yapata wakati wa jioni,
giza na usiku vilikuwa vimeanza kuingia.
10Punde kijana akakutana na huyo mwanamke;
amevalia kama malaya, ana mipango yake.
11Alikuwa mwanamke wa makelele na mkaidi;
miguu yake haitulii nyumbani:
12Mara barabarani, mara sokoni,
katika kila kona ya njia hakosekani akivizia.
13Alimkumbatia kijana huyo na kumbusu,
na kwa maneno matamu, akamwambia:
14“Ilinilazimu kutoa tambiko zangu;
leo hii nimekamilisha nadhiri yangu.
15Ndio maana nimetoka ili nikulaki,
nimekutafuta kwa hamu nikakupata.
16Nimetandika kitanda changu vizuri,
kwa shuka za rangi za kitani kutoka Misri.
17Nimekitia manukato, manemane, udi na mdalasini.
18Njoo tulale pamoja mpaka asubuhi;
njoo tujifurahishe kwa mahaba.
19Mume wangu hayumo nyumbani,
amekwenda safari ya mbali.
20Amechukua bunda la fedha;
hatarejea nyumbani karibuni.”
21Alimshawishi kwa maneno mengi ya kubembeleza;
kijana akashawishika kwa maneno yake matamu.
22Hapo akamfuata huyo mwanamke moja kwa moja,
kama ng'ombe aendaye machinjioni,
kama paa arukiaye mtegoni.
23Hakutambua kwamba hiyo itamgharimu maisha yake,
mpaka alipojikuta amekuwa kama amechomwa mshale moyoni,
amekuwa kama ndege aliyenaswa wavuni.
24Sasa wanangu, nisikilizeni;
yategeeni sikio maneno ya kinywa changu.
25Msikubali kuongozwa na mwanamke kama huyo,
wala msipitepite katika mapito yake.
26Maana amewaangusha wanaume wengi;
ni wengi mno hao aliowachinja.
27Nyumba yake ni njia ya kwenda kuzimu,
ni mahali pa kuteremkia mautini.

Methali7;1-27

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 27 June 2019

Kikombe Cha Asubuhi ; Methali 6...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Basi, kwa vile ahadi ya kuingia mahali pa pumziko bado ipo, na tuogope ili yeyote kati yenu asije akashindwa kupata pumziko hilo. Maana Habari Njema imehubiriwa kwetu kama vile ilivyohubiriwa kwa hao watu wa kale. Lakini ujumbe huo haukuwafaa chochote, maana waliusikia lakini hawakuupokea kwa imani.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Basi, sisi tunaoamini tunapata pumziko hilo aliloahidi Mungu. Kama alivyosema: “Nilikasirika, nikaapa: ‘Hawataingia mahali pangu pa pumziko.’” Mungu alisema hayo ingawa kazi yake ilikuwa imekwisha malizika tangu alipoumba ulimwengu.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...

Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Maana Maandiko yasema mahali fulani kuhusu siku ya saba: “Mungu alipumzika siku ya saba, akaacha kazi zake zote.” Tena jambo hili lasemwa pia: “Hawataingia mahali pangu pa pumziko.” Basi, hiyo ahadi ya kuingia bado ipo, maana wale waliohubiriwa Habari Njema pale awali walishindwa kuingia humo kwa sababu walikosa kutii.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

Maonyo manne
1Mwanangu, kama umejitolea kumdhamini jirani yako,
ikiwa umetoa ahadi yako kwa ajili ya mtu huyo,
2umejibana kwa maneno yako mwenyewe,
umejinasa kwa ahadi uliyofanya.
3Ujue kwamba uko chini ya mamlaka ya mwenzio,
lakini mwanangu, ukitaka kujiokoa, basi fanya hivi:
Mwendee mtu huyo mara moja umsihi akupe uhuru wako.
4Jitahidi usiache macho yako yapate usingizi,
wala kope za macho yako zisinzie.
5Jiokoe kwa kujitoa katika mtego huo,
mithili ya paa ama ndege amtorokavyo mwindaji.
6Ewe mvivu! Hebu ukamchungulie sisimizi,
fikiria namna yake ya kuishi ukapate hekima.
7Sisimizi hana kiongozi, ofisa, wala mtawala;
8lakini hujiwekea chakula wakati wa kiangazi,
hujikusanyia akiba wakati wa mavuno.
9Ewe mvivu, utalala hapo mpaka lini?
Utaamka lini katika usingizi wako?
10Wasema: “Acha nilale kidogo tu,
acha nisinzie kidogo!
Niache nikunje mikono nipumzike kidogo!”
11Wakati huo umaskini utakuvamia kama mnyanganyi,
ufukara utakufuata kama jambazi.6:11 Taz pia 24:33-34
12Mtu mwovu, mtu asiyefaa kitu,
huzururazurura akisema maneno mapotovu.
13Hukonyeza jicho kuwakosesha wengine,
huparuza kwa nyayo,
na kuashiria watu kwa vidole.
14Akiwa amejaa ulaghai moyoni hutunga maovu,
huzusha ugomvi kila mahali.
15Kutokana na hayo maafa yatamvamia ghafla,
ghafla atadhurika vibaya asiweze kupona tena.
16Kuna vitu sita anavyochukia Mwenyezi-Mungu;
naam, vitu saba ambavyo ni chukizo kwake:
17Macho ya kiburi,
ulimi mdanganyifu,
mikono inayoua wasio na hatia,
18moyo unaopanga mipango miovu,
miguu iliyo mbioni kutenda maovu,
19shahidi wa uongo abubujikaye uongo,
na mtu achocheaye fitina kati ya ndugu.

Onyo dhidi ya uasherati
20Mwanangu, shika maagizo ya baba yako,
wala usisahau mafundisho ya mama yako;
21yaweke daima moyoni mwako,
yafunge shingoni mwako.
22Yatakuongoza njiani mwako,
yatakulinda wakati ulalapo,
yatakushauri uwapo macho mchana.
23Maana amri hiyo ni taa,
na sheria hiyo ni mwanga.
Maonyo hayo na nidhamu yatuweka njiani mwa uhai.
24Yatakulinda mbali na mwanamke mbaya,
yatakuepusha na maneno matamu ya mwanamke mgeni.6:24 Taz 5:5 maelezo.
25Usimtamani mwanamke huyo kwa uzuri wake,
wala usikubali kunaswa kwa kope za macho yake.
26Mtu hupoteza kipande cha mkate kwa malaya,
lakini kwa mke wa mtu mwingine utapoteza uhai wako wote.
27Je, waweza kuweka moto kifuani
na nguo zako zisiungue?
28Je, waweza kukanyaga makaa ya moto
na nyayo zako zisiungue?
29Ndivyo alivyo mwanamume alalaye na mke wa mwenzake;
yeyote anayemgusa mwanamke huyo hataacha kuadhibiwa.
30Watu hawambezi sana mtu akiiba kwa sababu ya njaa;
31lakini akipatikana lazima alipe mara saba;
tena atatoa mali yote aliyo nayo.
32Mwanamume anayezini na mke wa mtu hana akili kabisa;
huyo hujiangamiza yeye mwenyewe.
33Atapata majeraha na madharau;
fedheha atakayopata haitamtoka.
34Maana wivu wa mume humfanya kuwa mkali kabisa;
wakati atakapolipiza kisasi hana cha kuhurumia.
35Hatakubali fidia yoyote;
wala kutulizwa na zawadi zako nyingi.

Methali6;1-35

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Wednesday 26 June 2019

Kikombe Cha Asubuhi ; Methali 5...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Shauli akajibu, “Nimefanya dhambi. Hata hivyo, unistahi sasa mbele ya wazee wa watu wangu na Waisraeli. Niruhusu nirudi pamoja nawe ili nikamwabudu Mwenyezi-Mungu, Mungu wako.” Basi, Samueli akarudi pamoja naye mpaka Gilgali na Shauli akamwabudu Mwenyezi-Mungu.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Kisha Samueli akasema, “Nileteeni hapa Agagi mfalme wa Waamaleki.” Agagi akamwendea Samueli akiwa mwenye furaha kwani alifikiri, “Uchungu wa kifo umepita.” Samueli akasema, “Kwa kuwa upanga wako umewafanya akina mama wengi wasiwe na watoto, ndivyo na mama yako atakavyokuwa bila mtoto miongoni mwa akina mama.” Akamkatakata Agagi vipandevipande mbele ya Mwenyezi-Mungu huko Gilgali.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Kisha, Samueli akaenda Rama; na mfalme Shauli akarudi nyumbani kwake huko Gibea. Tangu siku hiyo, Samueli hakumwona tena Shauli, mpaka siku alipofariki. Hata hivyo Samueli alimlilia Shauli. Naye Mwenyezi-Mungu alisikitika kwamba alikuwa amemtawaza Shauli mfalme juu ya Israeli.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Onyo dhidi ya uasherati
1Mwanangu, sikia hekima yangu,
tega sikio usikilize elimu yangu.
2Ndipo utakapoweza kuhifadhi busara,
na midomo yako izingatie maarifa.
3Mdomo wa mwanamke mpotovu ni mtamu kama asali,
maneno yake ni laini kuliko mafuta;5:3-5 Kuhusu aya 3-5 Taz pia 2:16; 7:6-27; 22:14; Mhu 7:26
4lakini hatimaye ni mchungu kama pakanga,
ni mkali kama upanga wenye makali kuwili.
5Nyayo zake zaelekea chini mautini,
hatua zake zaenda kuzimu.
6Yeye haijali njia ya uhai,
njia zake ni za kutangatanga, wala hajui.
7Sasa enyi wanangu, nisikilizeni,
wala msisahau maneno ya kinywa changu.
8Iepushe njia yako mbali naye,
wala usiukaribie mlango wa nyumba yake.
9Usije ukawapa wengine heshima yako,
na wakatili miaka yako;
10wageni wasije wakajishibisha kwa mali yako,
na jasho lako likaishia nyumbani kwa mgeni.
11Mwishoni mwa maisha yako utaomboleza
wakati mwili wako utakapoangamizwa.
12Hapo utasema, “Jinsi gani nilivyochukia nidhamu,
na kudharau maonyo moyoni mwangu!
13Sikuisikiliza sauti ya waalimu wangu,
wala kuwategea sikio wakufunzi wangu.
14Sasa niko karibu kuangamia kabisa
mbali na jumuiya ya watu.”
15Mkeo ni kama kisima cha maji safi:
Kunywa maji ya kisima chako mwenyewe.
16Ya nini chemchemi zako zitawanywe mbali,
na vijito vya maji barabarani?
17Hiyo ni yako wewe mwenyewe,
wala usiwashirikishe watu wengine.
18Chemchemi yako na ibarikiwe,
umfurahie mke uliyemwoa ukiwa kijana.
19Ni mzuri kama ayala, apendeza kama paa.
Mahaba yake yakufurahishe kila wakati,
umezwe daima na pendo lake.
20Mwanangu, ya nini kutekwa na mwanamke mwasherati?
Ya nini kumkumbatia kifuani mwanamke mgeni?
21Kumbuka njia za mtu zi wazi mbele ya Mwenyezi-Mungu;
yeye anaona kila hatua anayochukua binadamu.
22Mtu mwovu hunaswa kwa uovu wake mwenyewe;
hukamatwa katika tanzi za dhambi yake mwenyewe.
23Yeye hufa kwa utovu wa nidhamu,
huangamia kwa sababu ya upuuzi wake mkuu.

Methali5;1-23

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Tuesday 25 June 2019

Kikombe Cha Asubuhi ; Methali 4..


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Shauli akamwambia Samueli, “Nimetenda dhambi. Nimeasi amri ya Mwenyezi-Mungu na amri yako, kwa sababu niliwaogopa watu, nikawatii wao. Lakini sasa nakuomba, unisamehe dhambi yangu. Niruhusu nirudi pamoja nawe ili niweze kumwabudu Mwenyezi-Mungu.”
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Samueli akamjibu: “Kamwe, siwezi kurudi pamoja nawe. Wewe umeikataa amri ya Mwenyezi-Mungu, naye amekukataa kuwa mfalme juu ya Israeli.” Samueli alipogeuka ili aende zake, Shauli akashika pindo la vazi lake, nalo likapasuka.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...

Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Ndipo Samueli alipomwambia Shauli, “Tangu leo Mwenyezi-Mungu ameurarua ufalme wa Israeli kutoka kwako na atampa mtu mwingine miongoni mwa jirani zako aliye bora kuliko wewe. Na Mungu ambaye ni utukufu wa Israeli hadanganyi, wala habadili wazo lake. Yeye si binadamu hata abadili mawazo.”
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

Manufaa ya hekima
1Wanangu, sikilizeni mwongozo wa baba yenu,
tegeni sikio mpate kuwa na akili.
2Maana ninawapa maagizo mema,
msiyakatae mafundisho yangu.
3Mimi pia nilikuwa mtoto mwenye baba,
nilikuwa mpole, kipenzi cha mama yangu.
4Baba yangu alinifundisha hiki:
“Zingatia kwa moyo maneno yangu,
shika amri zangu nawe utaishi.
5Jipatie hekima, jipatie ufahamu;
usisahau wala kupuuza maneno yangu.
6Usimwache Hekima, naye atakutunza;
umpende, naye atakulinda.
7Jambo la msingi ni kujipatia hekima;
toa vyote ulivyonavyo ujipatie akili.
8Mthamini sana4:8 Mthamini sana: Maana yake katika Kiebrania si dhahiri. Hekima, naye atakutukuza;
ukimshikilia atakupa heshima.
9Atakuvika kilemba kizuri kichwani pako,
atakupa taji maridadi.”
10Mwanangu, sikia na kuyapokea maneno yangu,
ili upate kuwa na miaka mingi ya kuishi.
11Nimekufundisha njia ya hekima,
nimekuongoza katika njia nyofu.
12Ukitembea hatua zako hazitazuiwa,
wala ukikimbia hutajikwaa.
13Zingatia mafundisho ya Hekima na usimwache aponyoke,
mshike kwa makini maana yeye ni uhai wako.
14Usijiingize katika njia ya waovu,
wala usifuate mwenendo wa watu wabaya.
15Iepe njia hiyo wala usiikaribie;
jiepushe nayo, uende zako.
16Waovu kamwe hawalali wasipotenda uovu;
hawapati usingizi wasipomkwaza mtu.
17Maana uovu ndicho chakula chao,
ukatili ndiyo divai yao.
18Njia ya watu wema ni kama nuru ya alfajiri,
ambayo hungaa zaidi na zaidi hata mchana kamili.
19Lakini njia ya waovu ni kama giza nene,
hawajui kinachowafanya wajikwae.
20Mwanangu, sikiliza kwa makini maneno yangu,
itegee sikio misemo yangu.
21Usiyaache yatoweke machoni pako,
yahifadhi ndani ya moyo wako.
22Maana hayo ni uhai kwa mtu anayeyapata,
ni dawa kwa mwili wake wote.
23Linda moyo wako kwa uangalifu wote,
maana humo zatoka chemchemi za uhai.
24Tenga mbali nawe lugha potovu;
wala midomo yako isitamke maneno madanganyifu.
25Uyaelekeze macho yako mbele kwa ujasiri,
mtazamo wako uwe mbele moja kwa moja.
26 Taz Ebr 12:13 Fikiria njia utakayochukua,
na hatua zako zote zitakuwa kamili.
27Usigeukie kulia wala kushoto;
epusha mguu wako mbali na uovu.

Methali4;1-27

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.