Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 31 January 2017

Kikombe Cha Asubuhi Mwanzo 9..

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru Mungu kwa kutuamsha tena siku hii iliyompendeza Mungu..
Ikawe yenye Baraka,Amani,Upendo na Furaha..
Abariki Kutoka/Kuingia kwetu,Katika Kazi zetu,Masomo,Biashara na yote..
Akatuongoze kwenye Kunena,Kusikia na Kutenda..
Akawaponye na kuwagusa wote wanaopitia katika Magumu/majaribu Shida/Tabu.
Sifa na Utukufu ni kwakwe Daima!!!!
Mbarikiwe sana.


Mungu anafanya agano na Noa

1Mungu akambariki Noa na wanawe, akiwaambia, “Zaeni, muongezeke, mkaijaze nchi. 2Wanyama wote, ndege wote wa angani, viumbe wote watambaao juu ya nchi na samaki wote wa baharini watakuwa na hofu na kuwaogopa nyinyi. Wote wamewekwa chini ya mamlaka yenu. 3Wanyama wote hai watakuwa chakula chenu kama vile nilivyowapa mimea kuwa chakula chenu. 4Lakini msile nyama yenye damu, kwani uhai uko katika damu. 5Damu ya uhai wenu nitaidai; nitaidai kutoka kwa kila mnyama na binadamu. Atakayemuua binadamu mwenzake, nitamdai uhai wake.
6Amwagaye damu ya binadamu,
damu yake itamwagwa na binadamu;
maana binadamu aliumbwa kwa mfano wa Mungu.
7Nanyi zaeni, mkaongezeke;
zaeni kwa wingi, mkaongezeke nchini.”

Upinde wa mvua

8Kisha Mungu akamwambia Noa na wanawe, 9“Ninaweka agano langu nanyi na wazawa wenu 10na viumbe vyote hai: Ndege, wanyama wa kufugwa na wanyama wa porini, wote waliotoka katika safina pamoja nanyi. 11Nathibitisha agano langu nanyi, kwamba, kamwe viumbe vyote hai havitaangamizwa kwa gharika, wala haitatokea tena gharika kuiharibu nchi.” 12Tena Mungu akasema, “Hii ndiyo alama ya agano ninalofanya kati yangu nanyi na kila kiumbe hai kilicho pamoja nanyi kwa vizazi vyote vijavyo. 13Naweka upinde wangu mawinguni, nao utakuwa ishara ya agano kati yangu na dunia. 14Kila nitakapoifunika dunia kwa mawingu, na huo upinde wa mvua utakapoonekana katika mawingu, 15nitalikumbuka agano langu nanyi na viumbe vyote hai. Kamwe maji hayatageuka kuwa gharika ya kuviangamiza viumbe vyote hai. 16Huo upinde utakapotokea mawinguni, nitauona na kulikumbuka agano hilo la milele kati yangu na viumbe vyote hai duniani.” 17Mungu akamwambia Noa, “Hii ndiyo ishara ya agano ambalo nimefanya na viumbe vyote hai duniani.”

Noa na wanawe

18Watoto wa Noa waliotoka katika safina walikuwa Shemu, Hamu na Yafethi. Hamu alikuwa baba yake Kanaani. 19Hao ndio watoto watatu wa Noa, na kutokana nao watu walienea duniani kote.
20Noa alikuwa mkulima wa kwanza. Alilima shamba la mizabibu, 21akanywa divai, akalewa, kisha akalala uchi hemani mwake. 22Hamu, baba yake Kanaani, aliuona uchi wa baba yake, akatoka nje na kuwaambia ndugu zake wawili. 23Lakini Shemu na Yafethi wakatwaa nguo, wakaitanda mabegani mwao, wakaenda kinyumenyume na kuufunika uchi wa baba yao. Waliangalia pembeni, wala hawakuuona uchi wa baba yao. 24Noa alipolevuka na kujua alivyotendewa na mwanawe mdogo, 25akasema,
“Kanaani na alaaniwe!
Atakuwa mtumwa wa watumwa kwa ndugu zake.”
26Tena akasema,
“Shemu na abarikiwe na Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu!
Kanaani na awe mtumwa wake.
27Mungu na amkuze Yafethi,
aishi katika hema za Shemu;
Kanaani na awe mtumwa wake.”
28Baada ya gharika, Noa aliishi miaka 350, 29kisha akafariki akiwa na umri wa miaka 950.
Mwanzo 9;1-28
Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (BHN):
Jifunze zaidi

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 30 January 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Mwanzo 8....

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Ni wiki nyingine tena kwa uwezo,Neema/Rehema za Mungu ametujaalia kuiona tena Siku hii..
Tumrudishie Sifa/Utukufu kwa Muumba wa Yote,Yeye akisema atakubariki na hufanyika hivyo,
Yeye akisema ndiyo hakuna wa kupinga,
Tuanze wiki/siku hii na Mungu wetu akawe Mwanzo wa yote na mwisho wa yote.
Akabariki Kazi,Biashara,Masomo,Familia,Ndugu,Jamaa na Marafiki...
Wenye Shida/Tabu Mungu baba akawaguse,Yatima/Wajane baba ukawe nao..
Akatupe sawasawa na mapenzi yake.
Mungu wetu yu Mwema sana...!!!!
Tuanzena Mungu.


Mwisho wa gharika

1Kisha Mungu akamkumbuka Noa na wanyama wote wa porini na wa kufugwa waliokuwa pamoja naye ndani ya safina. Basi, Mungu akavumisha upepo juu ya nchi, maji yakaanza kupungua. 2Chemchemi za maji ya vilindi na madirisha ya mbinguni yakafungwa. Mvua ikazuiwa, 3maji yakaendelea kupungua polepole katika nchi. Baada ya siku 150, maji yakawa yamepungua sana. 4Mnamo siku ya kumi na saba ya mwezi wa saba, safina ikatua juu ya milima ya Ararati. 5Maji yakaendelea kupungua polepole, na siku ya kwanza ya mwezi wa kumi, vilele vya milima vikaonekana.
6Baada ya siku arubaini, Noa alifungua dirisha alilokuwa ametengeneza katika hiyo safina, 7akamtoa kunguru nje, naye hakurudi bali aliruka huko na huko mpaka maji yalipokauka nchini. 8Kisha Noa akamtoa njiwa apate kuona kama maji yalikuwa yamepungua juu ya nchi. 9Lakini, kwa vile maji yalikuwa bado yameifunika nchi yote, huyo njiwa hakupata mahali pa kutua, akamrudia Noa katika safina. Noa akanyosha mkono, akamtwaa na kumrudisha ndani ya safina. 10Noa akangoja siku nyingine saba, kisha akamtoa tena huyo njiwa. 11Njiwa huyo akamrudia Noa saa za jioni akiwa na tawi bichi la mzeituni mdomoni mwake. Kwa hiyo Noa akajua kwamba maji yalikuwa yamepungua katika nchi. 12Kisha akangoja siku nyingine saba, akamtoa tena yule njiwa; safari hii njiwa hakurudi kabisa.
13Noa alipokuwa na umri wa miaka 601, siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, maji yalikuwa yamekauka katika nchi. Noa akafunua kifuniko cha safina na alipotazama, akaona kwamba nchi ilikuwa imekauka. 14Siku ya 27 ya mwezi wa pili, nchi ilikuwa imekauka kabisa.
15Hapo, Mungu akamwambia Noa, 16“Toka katika safina, wewe pamoja na mkeo, wanao na wake zao. 17Toa pia viumbe wote hai wa kila aina waliokuwa pamoja nawe, ndege na wanyama na kila kiumbe kitambaacho, wapate kuzaa kwa wingi duniani, waongezeke na kuenea kila mahali duniani.” 18Basi, Noa akatoka katika safina pamoja na wanawe na mkewe pamoja na wake za wanawe. 19Wakatoka kufuatana na jamii zao, wanyama wote wa porini, viumbe wote watambaao, ndege wote na wanyama wote hai duniani.

Noa anamtolea Mungu tambiko

20Noa akamjengea Mwenyezi-Mungu madhabahu, akatwaa mmoja katika kila aina ya wanyama walio safi na ndege walio safi, akamtolea Mungu sadaka za kuteketezwa. 21Harufu nzuri ya tambiko hiyo ikampendeza Mwenyezi-Mungu, naye akasema moyoni mwake, “Kamwe sitailaani tena nchi kwa sababu ya binadamu; najua kwamba mawazo yake ni maovu tangu utoto wake. Wala sitaangamiza tena viumbe wote kama nilivyofanya. 22Kadiri itakavyodumu nchi majira ya kupanda na kuvuna, ya baridi na joto, ya masika na kiangazi, usiku na mchana, hayatakoma.”
Mwanzo 8;1-22

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (BHN):
Jifunze zaidi


"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Sunday 29 January 2017

Natumaini Mlikuwa/Mnaendelea na Jumapili hii Vjema

Natumaini Jumapili Ilikuwa njema/Inaendela vyema,
Mungu yu mwema na andelee kuwabariki katika yote..
hapa kwetu ni baridi inataka moyo kuamka Asubuhi na kwenda kwenye Ibada,
Basi tujitahidi kama tuwezavyo kwenda kutafuta mkate wetu..Mungu atusaidi na tushinde
Jaribu hili....
Tukumbushane kwa Amani na Upendo..




““Mimi ni mzabibu wa kweli, na Baba yangu ndiye mkulima. Kila tawi ndani yangu lisilozaa matunda yeye huliondoa, na kila tawi lizaalo hulisafisha lipate kuzaa zaidi. Nyinyi mmekwisha kuwa safi kwa sababu ya ule ujumbe niliowaambieni. Kaeni ndani yangu, nami nikae ndani yenu. Kama vile tawi haliwezi peke yake kuzaa matunda lisipobaki katika mzabibu, hali kadhalika nanyi hamwezi kuzaa matunda msipokaa ndani yangu. “Mimi ni mzabibu, nanyi ni matawi. Akaaye ndani yangu, nami nikiwa ndani yake, huyo huzaa matunda mengi, maana bila mimi hamwezi kufanya chochote. Mtu yeyote asipokaa ndani yangu hutupwa nje kama tawi litupwalo nje hata likakauka. Watu huliokota tawi la namna hiyo na kulitupa motoni liungue. Mkikaa ndani yangu na maneno yangu yakikaa ndani yenu, basi, ombeni chochote mtakacho nanyi mtapewa. Baba yangu hutukuzwa kama mkizaa matunda mengi na kuwa wanafunzi wangu. Mimi nimewapenda nyinyi kama vile Baba alivyonipenda mimi. Kaeni katika pendo langu. Mkizishika amri zangu mtakaa katika pendo langu, kama vile nami nilivyozishika amri za Baba yangu na kukaa katika pendo lake. Nimewaambieni mambo haya ili furaha yangu ikae ndani yenu, na furaha yenu ikamilike. Hii ndiyo amri yangu: Pendaneni; pendaneni kama nilivyowapenda nyinyi. Hakuna upendo mkuu zaidi kuliko upendo wa mtu atoaye uhai wake kwa ajili ya rafiki zake. Nyinyi ni rafiki zangu mkifanya ninayowaamuru. Nyinyi siwaiti tena watumishi, maana mtumishi hajui anachofanya bwana wake. Lakini mimi nimewaita nyinyi rafiki, kwa sababu nimewajulisha yote ambayo nimeyasikia kutoka kwa Baba yangu. Nyinyi hamkunichagua mimi; mimi niliwachagueni na kuwatuma mwende mkazae matunda, matunda yadumuyo, naye Baba apate kuwapeni chochote mnachomwomba kwa jina langu. Basi, amri yangu kwenu ndiyo hii: Pendaneni.”
‭‭Yohane‬ ‭15:1-17‬ ‭BHND‬‬
http://bible.com/393/jhn.15.1-17.bhnd














"Swahili Na Waswahili"Muwe na wakati mwema.

Friday 27 January 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Mwanzo 7....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Nimatumaini yangu wengi mmeamka salama na wenye afya..
walio Wagonjwa,Wenye Shida/Tabu,Kufiwa na wanopitia kwenye Magumu/Majaribu Mungu kamwe hajawaacha.
Tuzidi kumuomba Baba wa yote,Mfalme wa Amani,Mwenye-enzi,Muumba wa Vyote,Mume wa Wajane,Baba wa Yatima,Yeye asiyechoka,Yeye asiye lala,Mwingi wa Rehema/Neema,Kimbilio letu,Baba wa Uzima,Yeye husamehe,
Sifa na Utukufu ni kwake daima...!!!!!
Akatubariki Tuingiapo/Tutokapo,Vilaji/Vinywaji,Masomoni,Biashara,Kazi
na tumtangulize kwa kila jambo.
Muwe na wakati mwema.

Gharika kuu

1Mwenyezi-Mungu akamwambia Noa, “Ingia ndani ya safina wewe pamoja na jamaa yako yote, kwa maana, kati ya watu wote wanaoishi nyakati hizi zako, nimekuona wewe peke yako kuwa mwadilifu mbele yangu. 2Chukua pamoja nawe wanyama wote walio safi, dume na jike, saba saba; lakini wanyama walio najisi, chukua dume na jike, wawiliwawili. 3Vilevile chukua ndege wa angani dume na jike, saba saba, ili kuzihifadhi hai aina zao duniani. 4Baada ya siku saba, nitanyesha mvua nchini siku arubaini mchana na usiku, na kila kiumbe hai nilichokiumba duniani nitakiangamiza.” 5Noa akafanya yote kama Mwenyezi-Mungu alivyomwamuru.
6Noa alikuwa na umri wa miaka 600 wakati gharika ilipotokea nchini. 7Noa, mkewe, wanawe na wake zao wakaingia ndani ya safina ili kuiepa gharika. 8Wanyama walio safi, wanyama walio najisi, ndege na viumbe vyote vitambaavyo, 9wawiliwawili, dume na jike, wakaingia ndani ya safina pamoja na Noa kama Mungu alivyomwamuru. 10Baada ya siku saba, maji ya gharika yakaanza kuifunika nchi.
11Noa alipokuwa na umri wa miaka 600, mnamo siku ya kumi na saba ya mwezi wa pili, siku hiyo chemchemi zote za vilindi vya nchi zikabubujika maji, na madirisha ya mbinguni yakafunguka. 12Mvua ikanyesha nchini siku arubaini mchana na usiku. 13Siku hiyohiyo mvua ilipoanza kunyesha, Noa, mkewe na wanawe, Shemu, Hamu na Yafethi, pamoja na wake zao, waliingia ndani ya safina. 14Waliingia wao wenyewe pamoja na aina zote za wanyama wa porini, wanyama wafugwao, wanyama watambaao na ndege wa kila aina. 15Waliingia ndani ya safina pamoja na Noa wiliwawili wa kila aina ya viumbe hai. 16Kila aina yao waliingia, dume na jike, kama Mungu alivyomwamuru Noa. Kisha, Mwenyezi-Mungu akaufunga mlango wa safina nyuma yake Noa.
17Gharika ilidumu nchini kwa muda wa siku arubaini. Maji yakaongezeka na kuiinua safina, ikaelea juu ya ardhi. 18Maji yakaendelea kuongezeka zaidi nchini na safina ikaelea juu yake. 19Maji hayo yakawa mengi sana juu ya nchi, yakaifunika milima yote mirefu katika nchi. 20Yaliongezeka hata kuifunika milima kiasi cha mita saba na nusu. 21Viumbe wote hai katika nchi wakafa. Ndege, wanyama wa kufugwa, wanyama wa porini, makundi ya viumbe wote katika nchi kavu na wanadamu wote; 22naam, kila kiumbe hai katika nchi kavu kilikufa. 23Mungu akaangamiza kila kiumbe kilichokuwa hai duniani: Binadamu, wanyama, viumbe vitambaavyo na ndege wa angani. Vyote viliangamizwa duniani. Noa tu ndiye aliyesalimika na wale waliokuwa pamoja naye ndani ya safina. 24Maji hayo yalidumu katika nchi siku 150.
Mwanzo 7;1-24
Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN):
Jifunze zaidi


"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 26 January 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Mwanzo 6....

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Ni kwa Neema  ya Mungu tuu wala si kwa uwezo wetu kuiona tena siku hii...
sisi tumempa nini Mungu kwa Neema hii?Kipi hata kidogo umemfanyia,Unamfanyia Mungu
kwa kukupatia Neema hii ukiwa Hai, mwenye Afya njema,Nguvu,Akili timamu?
Wangapi wametamani kuendelea kuwepo na kupata hayo niliyoyasema na zaidi au hata kimoja wapo
lakini wameshindwa Asubuhi/siku ya leo?
Basi Wapendwa/Waungwana tutumie nafasi hii ya Neema ya Mungu vyema..
Popote tulipo Mungu wetu yupo..
Mungu akawabariki katika yote... Na akatuepushe na kila Ovu...
Awe nasi katika kazi zetu,Masomo, biashara, Vyombo vya usafiri,tutembee naye,Tuingiapo na Tutokapo,
Akawaguse wanaopitia Magumu,Wenye Shida/Tabu, Yatima na Wajane, Wagonjwa mahospitalini,Majumbani,Walio Magerezani pasipo na Hatia Mungu wetu akaonekane.
Tuendelee kukumbushana vyema..!!!!!!
Muwe na wakati mzuri.




Uovu wa binadamu

1Binadamu walipozidi kuongezeka duniani na kuzaa wasichana, 2watoto wa kiume wa Mungu waliwaona hao wasichana wa watu kuwa ni wazuri, wakawachukua wale waliowapenda kuwa wake zao. 3Hapo Mwenyezi-Mungu akasema, “Roho yangu haitakaa ndani ya binadamu milele, maana yeye ni wa kufa tu. Basi, hataishi zaidi ya miaka 120.” 4Nyakati hizo na hata baadaye, kulikuwa na majitu duniani ambao walikuwa wazawa wa watoto wa kiume wa Mungu na wasichana wa watu. Hao ndio watu waliokuwa mashujaa na wenye sifa enzi hizo, nao waliitwa Wanefili.
5Mwenyezi-Mungu alipoona wingi wa uovu wa binadamu duniani, na kwamba kila analokusudia binadamu moyoni mwake ni ovu daima, 6Mwenyezi-Mungu alisikitika sana kwa kumuumba binadamu duniani. Mwenyezi-Mungu alihuzunika sana moyoni mwake, 7hivyo akasema, “Nitamfuta kabisa duniani binadamu niliyemuumba; nitafutilia mbali pia wanyama wa porini, viumbe vitambaavyo na ndege wa angani. Ninasikitika kwamba niliwaumba duniani.” 8Lakini Noa alipata fadhili mbele ya Mwenyezi-Mungu.

Noa

9Ifuatayo ni habari juu ya Noa ambaye alikuwa ndiye mwadilifu pekee na ambaye hakuwa na lawama nyakati zake. Alikuwa mcha Mungu. 10Noa alikuwa na watoto watatu wa kiume: Shemu, Hamu na Yafethi. 11Mungu aliiona dunia kuwa imeharibika na kujaa ukatili. 12Naam, Mungu aliiangalia dunia, akaona kuwa imeharibika kabisa, kwa maana kila mtu alifuata njia yake mbovu.
13Mungu akamwambia Noa, “Nimeamua kuwaangamiza binadamu wote kwa sababu wameijaza dunia ukatili. Naam, nitawaangamiza kabisa pamoja na dunia! 14Kwa hiyo, jitengenezee safina kwa mbao za mpingo. Gawa vyumba ndani yake na ipake lami ndani na nje. 15Utaitengeneza hivi: Urefu wake mita 139, upana wake mita 25 na kimo chake mita 15. 16Safina hiyo iwe ya ghorofa tatu na yenye mlango pembeni. Itengenezee paa, kisha acha nafasi ipatayo nusu mita kati ya paa na dari. 17Nitaleta gharika ili kuangamiza viumbe vyote hai duniani. Kila kiumbe hai duniani kitakufa. 18Lakini nitafanya agano nawe. Utaingia katika safina, wewe pamoja na mkeo, wanao na wake zao. 19Nawe utaingiza katika safina jozi ya kila aina ya viumbe, wa kiume na wa kike, ili kuwahifadhi hai pamoja nawe.
20“Utaingiza kila aina ya ndege wa angani, kila aina ya mnyama, kila aina ya kiumbe kitambaacho, wawiliwawili, ili kuwahifadhi hai. 21Pia chukua aina zote za vyakula vinavyolika, uvihifadhi kwa ajili ya chakula chenu na viumbe hao.” 22Noa akafanya yote kama Mungu alivyomwamuru.

Mwanzo6;1-22


Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (BHN): 
Jifunze zaidi

Wednesday 25 January 2017

Kikombe Cha Asubuhi Mwanzo.5...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru Mungu kwa kutuamsha salama na kuiona tena Leo hii..
Walio Wagonjwa,wenye Shida/Tabu,Majaribu na kukata Tamaa Mungu akawaguse na kuwaponya katika yote.
 Mungu yu mwema sana na anawapenda,
Tumaini la kweli,Uponyaji na Faraja vyote vinapatikana kwakwe.
Yeye ni mwanzo na yeye ni mwisho,
Mungu wetu si kiziwi,Si kipofu,si Bubu,Ukimuomba,Ukiabudu,Ukiamini
kamwe hawezi kukuacha yeye anatosha..
Mungu aendelee kutubariki katika Kazi zetu,Shule,Biashara , Tuingiapo na Tutokapo,Vilaji na Vinyaji na katika yote sawasawa na Mapenzi Yake...
Yeye ni Mkuu katika yote..!!!
Muwe na wakati Mwema.


Wazawa wa Adamu

(1Nya 1:1-4)

1Ifuatayo ni orodha ya wazawa wa Adamu. Wakati Mungu alipomuumba binadamu, alimuumba kwa mfano wake. 2Aliwaumba mwanamume na mwanamke, kisha akawabariki na kuwapa jina “Binadamu.”
3Adamu alipokuwa na umri wa miaka 130, alipata mtoto aliyefanana naye, na mwenye sura kama yake; akamwita Sethi. 4Baada ya kumzaa Sethi, Adamu aliishi miaka 800, na kupata watoto wengine wa kiume na wa kike. 5Adamu alifariki akiwa na umri wa miaka 930.
6Sethi alipokuwa na umri wa miaka 105, alimzaa Enoshi. 7Baada ya kumzaa Enoshi, Sethi aliishi miaka 807, na kupata watoto wengine wa kiume na wa kike. 8Sethi alifariki akiwa na umri wa miaka 912.
9Enoshi alipokuwa na umri wa miaka 90, alimzaa Kenani. 10Baada ya kumzaa Kenani, Enoshi aliishi miaka 815 na kupata watoto wengine wa kiume na wa kike. 11Enoshi alifariki akiwa na umri wa miaka 905.
12Kenani alipokuwa na umri wa miaka 70, alimzaa Mahalaleli. 13Baada ya kumzaa Mahalaleli, Kenani aliishi miaka 840 na kupata watoto wengine wa kiume na wa kike. 14Kenani alifariki akiwa na umri wa miaka 910.
15Mahalaleli alipokuwa na umri wa miaka 65, alimzaa Yaredi. 16Baada ya kumzaa Yaredi, Mahalaleli aliishi miaka 830 na kupata watoto wengine wa kiume na wa kike. 17Mahalaleli alifariki akiwa na umri wa miaka 895.
18Yaredi alipokuwa na umri wa miaka 162, alimzaa Henoki. 19Baada ya kumzaa Henoki, Yaredi aliishi miaka 800 na kupata watoto wengine wa kiume na wa kike. 20Yaredi alifariki akiwa na umri wa miaka 962.
21Henoki alipokuwa na umri wa miaka 65, alimzaa Methusela. 22Henoki alikuwa mcha Mungu. Baada ya kumzaa Methusela, Henoki aliishi miaka 300 na kupata watoto wengine wa kiume na wa kike. 23Henoki aliishi miaka 365. 24Alikuwa mcha Mungu, akatoweka, kwa maana Mungu alimchukua.
25Wakati Methusela alipokuwa na umri wa miaka 187, alimzaa Lameki. 26Baada ya kumzaa Lameki, Methusela aliishi miaka 782, na kupata watoto wengine wa kiume na wa kike. 27Methusela alifariki akiwa na umri wa miaka 969.
28Wakati Lameki alipokuwa na umri wa miaka 182, alimzaa mtoto wa kiume. 29Alimwita mtoto huyo Noa, akisema, “Mtoto huyu ndiye atakayetufariji kutokana na kazi yetu ngumu tunayofanya kwa mikono yetu katika ardhi aliyoilaani Mwenyezi-Mungu.” 30Baada ya kumzaa Noa, Lameki aliishi miaka 595 na kupata watoto wengine wa kiume na wa kike. 31Lameki alifariki akiwa na umri wa miaka 777.
32Noa alipokuwa na umri wa miaka 500, alimzaa Shemu na Hamu na Yafethi.
Mwanzo5;1-32

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN): 
Jifunze zaidi

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Tuesday 24 January 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Mwanzo 4....



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana..?
Nimatumaini yangu mmeamka salama,Tunamshukuru Mungu  ametupa Neema ya Kuiona siku nyingine..
Tunaomba Mungu aendelee Kuwabariki,Kuwalinda,Kuwaongoza kwenye Vyombo vya usafiri na watembeao,
Akabriki kazi zetu ,Wanafunzi shuleni akawape ufahamu,Kukumbuka na kuelewa katika masomo yao..
Akabariki Vilaji/Vinywaji,Tuingiapo/Tutokapo...Akawe nasi katika yote na akatupe sawasawa na Mapenzi yake.
Akawabariki Yatima,Wajane,Wenye Shida/Tabu.
Wajawazito na Watafutao watoto Mfalme wa Amani akawaguse..
Sifa na Utukufu ni kwa Mungu muumba wetu...!!!!
Mkawe na wakati mwema.


Kaini na Abeli
1Adamu akalala na Hawa mkewe, naye akapata mimba, akamzaa Kaini. Hawa akasema, “Nimepata mtoto wa kiume kwa msaada wa Mwenyezi-Mungu!” 2Halafu akamzaa Abeli nduguye. Abeli alikuwa mfugaji kondoo na Kaini alikuwa mkulima. 3Baada ya muda fulani, Kaini alimtolea Mwenyezi-Mungu sadaka kutokana na mazao ya shambani, 4naye Abeli akamtolea Mungu sadaka ya wazawa wa kwanza wa kondoo wake na nyama nono. Mwenyezi-Mungu akapendezwa na Abeli na tambiko yake, 5lakini hakupendezwa na Kaini wala na tambiko yake. Basi, Kaini akakasirika sana na uso wake ukakunjamana. 6Mwenyezi-Mungu akamwambia Kaini, “Kwa nini umekasirika, na kwa nini uso wako umekunjamana? 7Je, ukitenda vyema hutakubaliwa? Na usipotenda vyema, basi, dhambi inakuvizia mlangoni; inakutamani, lakini unapaswa kuishinda.”
8Baadaye, Kaini akamwambia Abeli nduguye, “Twende nje shambani” Basi, walipokuwa shambani, Kaini akamvamia Abeli nduguye, akamuua. 9Mwenyezi-Mungu akamwuliza Kaini, “Ndugu yako Abeli yuko wapi?” Kaini akamjibu, “Mimi sijui! Je, mimi ni mlinzi wa ndugu yangu?” 10Mwenyezi-Mungu akasema, “Umefanya nini? Damu ya ndugu yako yanililia kutoka udongoni. 11Sasa wewe umelaaniwa! Hutailima tena ardhi yenye rutuba ambayo kama kinywa imeipokea damu ya nduguyo uliyemuua. 12Ukiilima ardhi haitakupatia tena mazao yake. Utakuwa mtu wa kutangatanga, asiye na makao maalumu duniani.”
13Kaini akamwambia Mwenyezi-Mungu, “Adhabu yangu ni kubwa mno; siwezi kuistahimili. 14Leo umenifukuza kutoka ardhi yenye rutuba na mbali nawe. Basi, nitakuwa mtu wa kutangatanga, asiye na makao maalumu duniani, na yeyote atakayeniona ataniua.” 15Lakini Mwenyezi-Mungu akamjibu, “Sivyo! Atakayekuua wewe Kaini atalipizwa mara saba.” Basi, Mwenyezi-Mungu akamtia Kaini alama ya tahadhari, ili yeyote atakayemwona asimuue. 16Kisha Kaini akaondoka mbele ya Mwenyezi-Mungu, akawa anaishi katika nchi ya Nodi, upande wa mashariki wa Edeni.
Wazawa wa Kaini
17Kaini akalala na mkewe, naye akapata mimba, akamzaa Henoki. Kaini akajenga mji akauita kwa jina la Henoki mwanawe. 18Henoki akamzaa Iradi, naye Iradi akamzaa Mehuyaeli; Mehuyaeli akamzaa Methushaeli, naye Methushaeli akamzaa Lameki. 19Lameki alioa wanawake wawili, mmoja aliitwa Ada na mwingine Sila. 20Ada alimzaa Yabali ambaye alikuwa baba yao wafugaji waishio mahemani. 21Ndugu yake alikuwa Yubali; huyo alikuwa baba yao wanamuziki wote wapigao zeze na filimbi. 22Sila naye alimzaa Tubal-kaini, ambaye alikuwa mhunzi wa vyombo vyote vya shaba na chuma. Dada yake Tubal-kaini alikuwa Naama.
23Lameki akawaambia wake zake,
“Ada na Sila sikieni sauti yangu!
Sikilizeni nisemayo enyi wake za Lameki.
Mimi niliua mtu kwa kunijeruhi,
naam, nilimuua kijana kwa kuniumiza.
24Ikiwa Kaini atalipizwa mara saba,
kweli Lameki atalipizwa mara sabini na saba.”

 Sethi na Enoshi
25Adamu akalala tena na Hawa mkewe, naye akazaa mtoto wa kiume, akamwita Sethi akisema, “Mungu amenijalia mtoto mahali pa Abeli aliyeuawa na Kaini.” 26Sethi naye alipata mtoto wa kiume, akamwita Enoshi. Hapo ndipo watu walipoanza kumwomba Mwenyezi-Mungu kwa jina lake.
Mwanzo 4;1-26

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN): 
Jifunze zaidi

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 23 January 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Mwanzo 3...


Shalom,Habari za Asubuhi/Leo,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Nimatumaini yangu mnandelea vyema na Mungu anaendelea kuwatendea sawasawa na Mapenzi yake.
Ni wiki nyingine tena Mungu ametupa kibali cha kuiona tena,Tuanze wiki hii vyema na Mungu azidi
kuonekana katika maisha yetu,
Tuzidi kumsifu/Kumuabudu,Kumshukuru,Kumuomba na kumtafuta kwa bidii...
Akawe kiongozi wetu katika Kazi zetu,Shuleni,Nyumbani,Njiani na popote tulipo naye awepo...
Akatubariki tuingiapo na Tutokapo..
Akawe mfariji wa wote waliopatwa na misiba,Akawaguse wenye Shida/Tabu.
Alipo MUNGU yote yanawezekana..!!!
Muwe na siku njema.



Uasi wa binadamu
1Nyoka alikuwa mwerevu kuliko wanyama wote wa porini walioumbwa na Mwenyezi-Mungu. Basi, nyoka akamwambia huyo mwanamke, “Ati Mungu alisema msile matunda ya mti wowote bustanini?” 2Mwanamke akamjibu huyo nyoka, “Twaweza kula matunda ya mti wowote bustanini; 3lakini Mungu alisema, ‘Msile matunda ya mti ulio katikati ya bustani, wala msiuguse, msije mkafa.’” 4Nyoka akamwambia mwanamke, “Hamtakufa! 5Mungu alisema hivyo kwa sababu anajua kwamba mkila matunda ya mti huo mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya.”
6Basi, mwanamke alipoona kuwa mti huo ni mzuri kwa chakula, wavutia macho, na kwamba wafaa kwa kupata hekima, akachuma tunda lake, akala, akampa na mumewe, naye pia akala. 7Mara macho yao yakafumbuliwa, wakatambua kwamba wako uchi; hivyo wakajishonea majani ya mtini, wakajifanyia mavazi ya kiunoni.
8Jioni, wakati wa kupunga upepo, huyo mwanamume na mkewe wakasikia hatua za Mwenyezi-Mungu akitembea bustanini, nao wakajificha kati ya miti ya bustani, Mwenyezi-Mungu asipate kuwaona. 9Lakini Mwenyezi-Mungu akamwita huyo mwanamume, “Uko wapi?” 10Naye akamjibu, “Nimesikia hatua zako bustanini, nikaogopa na kujificha, maana nilikuwa uchi.” 11Mwenyezi-Mungu akamwuliza, “Nani aliyekuambia kwamba uko uchi? Je, umekula tunda la mti nililokuamuru usile?” 12Huyo mwanamume akajibu, “Mwanamke uliyenipa akae pamoja nami ndiye aliyenipa tunda la mti huo, nami nikala.”
13Hapo Mwenyezi-Mungu akamwuliza huyo mwanamke, “Umefanya nini wewe?” Mwanamke akamjibu, “Nyoka alinidanganya, nami nikala.”

Adhabu
14Kisha Mwenyezi-Mungu akamwambia nyoka,
“Kwa kuwa umefanya hivyo,
umelaaniwa kuliko wanyama wote wa kufugwa,
na kuliko wanyama wote wa porini.
Kwa tumbo lako utatambaa,
na kula vumbi siku zote za maisha yako.
15Nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke,
kati ya uzawa wako na uzawa wake;
yeye atakiponda kichwa chako,
nawe utamwuma kisigino chake.”
16Kisha akamwambia mwanamke,
“Nitakuzidishia uchungu wa kuzaa,
kwa uchungu utazaa watoto.
Hata hivyo utakuwa na hamu na mumeo,
naye atakutawala.”
17Kisha akamwambia huyo mwanamume,
“Kwa kuwa wewe umemsikiliza mkeo,
ukala matunda ya mti ambayo nilikuamuru usile;
kwa hiyo, kwa kosa lako ardhi imelaaniwa.
Kwa jasho utajipatia humo riziki yako,
siku zote za maisha yako.
18Ardhi itakuzalia michongoma na magugu,
nawe itakubidi kula majani ya shambani.
19Kwa jasho lako utajipatia chakula
mpaka utakaporudi udongoni ulimotwaliwa;
maana wewe ni mavumbi, na mavumbini utarudi.”
20Adamu akampa mkewe jina “Hawa”, kwani alikuwa mama wa binadamu wote. 21Mwenyezi-Mungu akawatengenezea Adamu na mkewe mavazi ya ngozi, akawavika.

Adamu na Hawa wanafukuzwa bustanini
22Kisha Mwenyezi-Mungu akasema, “Sasa, binadamu amekuwa kama mmoja wetu, anajua mema na mabaya. Lazima kumzuia kula lile tunda la mti wa uhai, kwani akilila ataishi milele!” 23Basi, Mwenyezi-Mungu akamfukuza Adamu nje ya bustani ya Edeni, ili akailime ardhi ambamo alitwaliwa. 24Alimfukuza nje, na kuweka mlinzi upande wa mashariki wa bustani ya Edeni na upanga wa moto uliogeuka huko na huko, kuilinda njia iendayo kwenye mti wa uhai.
Mwanzo 3;1-24

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (BHN): 
Jifunze zaidi

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Friday 20 January 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Mwanzo 2..


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamajambo Wapendwa/Waungwana?
Natumaini wote mmeamka salama na Mungu yu pamoja nanyi kwa kila jambo,
Yeye ni mwanzo kwetu na yeye ni mwisho kwetu hakuna wa kufanana naye.
Aendelee kuwabariki kuingia kwenu na kutoka kwenu,Akamguse kila mmoja
anayepitia magumu..Mungu akaonekane kwenye mapito,Shida/Tabu.
Akabariki kazi zetu na kuwaongoza wanafunzi katika masomo yao wakumbuke yote wanayofundishwa na kuelewa.
Mungu atosha..!!!!
Muwe na Wakati mwema.

     Mwanzo 2:1-25
1Hivyo ndivyo mbingu na dunia zilivyokamilika pamoja na vitu vyote vilivyomo. 2Siku ya saba Mungu alimaliza kazi yake yote aliyofanya; siku hiyo ya saba Mungu akapumzika baada ya kazi yake yote aliyofanya. 3Mungu akaibariki siku ya saba na kuitakasa, kwa kuwa siku hiyo Mungu alipumzika baada ya kazi yake yote ya kuumba. 4Hivyo ndivyo mbingu na dunia zilivyoumbwa.
Bustani ya Edeni
Siku ile Mwenyezi-Mungu alipoziumba mbingu na dunia, 5Hapakuwa na mimea juu ya nchi wala miti haikuwa imechipua kwani Mwenyezi-Mungu hakuwa ameinyeshea nchi mvua, wala hapakuwa na mtu wa kuilima. 6Hata hivyo, maji yalitoka ardhini yakainywesha ardhi yote. 7Basi, Mwenyezi-Mungu akamfanya mwanamume kwa mavumbi ya udongo, akampulizia puani pumzi ya uhai, na huyo mwanamume akawa kiumbe hai.
8Kisha Mwenyezi-Mungu akapanda bustani huko Edeni, upande wa mashariki, na humo akamweka huyo mwanamume aliyemuumba. 9Mwenyezi-Mungu akaotesha kutoka ardhini kila aina ya miti mizuri izaayo matunda yafaayo kwa chakula. Katikati ya bustani hiyo kulikuwa na mti wa uhai na mti wa ujuzi wa mema na mabaya.
10Kulikuwa na mto huko Edeni uliotiririka maji na kuinywesha hiyo bustani; kutoka huko mto huo uligawanyika kuwa mito minne. 11Jina la mto wa kwanza ni Pishoni; huo waizunguka nchi yote ya Hawila ambako kuna dhahabu. 12Dhahabu ya nchi hiyo ni safi kabisa. Huko pia kuna marashi yaitwayo bedola na vito viitwavyo shohamu. 13Jina la mto wa pili ni Gihoni; huo waizunguka nchi yote ya Kushi. 14Jina la mto wa tatu ni Tigri, nao watiririkia upande wa mashariki wa nchi ya Ashuru; na jina la mto wa nne ni Eufrate.
15Basi, Mwenyezi-Mungu akamtwaa huyo mwanamume, akamweka katika bustani ya Edeni, ailime na kuitunza. 16Mwenyezi-Mungu alimwamuru huyo mwanamume, “Waweza kula matunda ya mti wowote katika bustani; 17lakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya, usile, maana siku utakapokula matunda ya mti huo, hakika utakufa.”
18Kisha Mwenyezi-Mungu akasema, “Si vizuri huyu mwanamume kuwa peke yake. Nitamfanyia msaidizi wa kumfaa.” 19Basi, kutoka katika udongo, Mwenyezi-Mungu akaumba kila mnyama wa porini na kila ndege wa angani, halafu akamletea huyo mwanamume aone atawapa majina gani; na majina aliyowapa viumbe hao, yakawa ndio majina yao. 20Basi, huyo mwanamume akawapa majina wanyama wote wa kufugwa, wanyama wa porini na ndege wote wa angani. Lakini hakupatikana msaidizi yeyote wa kumfaa.
21Basi, Mwenyezi-Mungu akamletea huyo mwanamume usingizi mzito, na alipokuwa usingizini, akatwaa ubavu wake mmoja na kupafunika mahali pale kwa nyama. 22Na huo ubavu Mwenyezi-Mungu alioutoa kwa yule mwanamume akaufanya kuwa mwanamke, akamleta kwa huyo mwanamume. 23Ndipo huyo mwanamume akasema,
“Naam! Huyu ni mfupa kutoka mifupa yangu,
na nyama kutoka nyama yangu.
Huyu ataitwa ‘Mwanamke’,
kwa sababu ametolewa katika mwanamume.”
24Ndiyo maana mwanamume humwacha baba yake na mama yake, akaambatana na mkewe, nao wawili huwa mwili mmoja.
25Huyo mwanamume na mkewe wote walikuwa uchi, lakini hawakuona haya.
Mwanzo 2:1-25
Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (BHN): 
Jifunze zaidi

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 19 January 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Tuanze na Mwanzo

Shalom,Hamjambo Wapendwa/Waungwana?
Nimatumaini yangu mmeamka salama..
Sifa na Utukufu ni kwake Mungu Baba.
Wagonjwa,wenyeshida/Tabu Mungu akawaguse,
Tukaanze siku  na Mungu ,Atubariki,Atulinde,Atuongoze katika yote.
Muwe na wakati mwema.

               
Kuumbwa Ulimwengu


“Hapo mwanzo, Mungu aliumba mbingu na dunia. Dunia ilikuwa bila umbo na tupu. Giza lilikuwa limefunika vilindi vya maji na roho ya Mungu ilikuwa ikitanda juu ya maji. Mungu akasema, “Mwanga uwe.” Mwanga ukawa. Mungu akauona mwanga kuwa ni mwema. Kisha Mungu akautenganisha mwanga na giza, mwanga akauita “Mchana” na giza akaliita “Usiku.” Ikawa jioni, ikawa asubuhi; siku ya kwanza. Mungu akasema, “Anga liwe katikati ya maji, liyatenge maji sehemu mbili.” Mungu akalifanya anga, akayatenga maji yaliyo juu ya anga na yale yaliyo chini ya anga hilo. Ikawa hivyo. Mungu akaliita anga “Mbingu.” Ikawa jioni, ikawa asubuhi; siku ya pili. Mungu akasema, “Maji yaliyo chini ya mbingu na yakusanyike mahali pamoja, nchi kavu itokee.” Ikawa hivyo. Mungu akapaita mahali pakavu “Nchi” na kusanyiko la maji akaliita “Bahari.” Mungu akaona kuwa ni vyema. Kisha Mungu akasema, “Nchi na ioteshe mimea. Mimea izaayo mbegu, na miti izaayo matunda yenye mbegu.” Ikawa hivyo. Basi, nchi ikaotesha mimea izaayo mbegu kwa jinsi yake, na miti izaayo matunda yenye mbegu kwa jinsi yake. Mungu akaona kuwa ni vyema. Ikawa jioni, ikawa asubuhi; siku ya tatu. Mungu akasema, “Mianga na iweko angani, itenge mchana na usiku, ioneshe nyakati, majira, siku na miaka, na ingae angani na kuiangazia dunia.” Ikawa hivyo. Basi, Mungu akafanya mianga miwili mikubwa; ule mkubwa utawale mchana na ule mdogo utawale usiku; akafanya na nyota pia. Mungu akaiweka mianga hiyo angani iiangazie dunia, ipate kutawala mchana na usiku, na kuutenga mwanga na giza. Mungu akaona kuwa ni vyema. Ikawa jioni, ikawa asubuhi; siku ya nne. Mungu akasema, “Maji na yatoe makundi ya viumbe hai na ndege waruke angani.” Basi, Mungu akaumba wanyama wakubwa sana wa baharini na aina zote za viumbe vyote hai viendavyo na kujaa majini; akaumba na aina zote za ndege wote. Mungu akaona kuwa ni vyema. Mungu akavibariki, akasema, “Zaeni, muongezeke, muyajaze maji ya bahari; nao ndege waongezeke katika nchi.” Ikawa jioni, ikawa asubuhi; siku ya tano. Mungu akasema, “Nchi na itoe aina zote za viumbe hai, wanyama wa kufugwa, viumbe vitambaavyo na wanyama wa porini wa kila aina.” Ikawa hivyo. Basi, Mungu akafanya aina zote za wanyama wa porini, wanyama wa kufugwa, na viumbe vitambaavyo. Mungu akaona kuwa ni vyema. Kisha Mungu akasema, “Tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; atawale samaki wa baharini, ndege wa angani, wanyama wa kufugwa, dunia yote na viumbe vyote vitambaavyo.” Basi, Mungu akaumba mtu kwa mfano wake; naam, kwa mfano wake Mungu alimuumba. Aliwaumba mwanamume na mwanamke. Mungu akawabariki na kuwaambia, “Zaeni muongezeke, mkaijaze nchi na kuimiliki; muwatawale samaki wa baharini, ndege wa angani, na kila kiumbe hai kitembeacho duniani.” Kisha Mungu akasema, “Tazama, nawapeni kila mmea duniani uzaao mbegu, na kila mti uzaao matunda yenye mbegu; mbegu zao au matunda yao yatakuwa chakula chenu. Nao wanyama wote duniani, ndege wote wa angani, viumbe vyote vitambaavyo, naam, kila kiumbe chenye uhai, chakula chao kitakuwa majani yote ya mimea.” Ikawa hivyo. Mungu akaona kila kitu alichokifanya kuwa ni chema kabisa. Ikawa jioni, ikawa asubuhi; siku ya sita.”
Mwanzo 1:1-31 BHND
http://bible.com/393/gen.1.1-31.bhnd

"Swahili Na Waswahili"Mabarikiwe.

Wednesday 18 January 2017

Anza Nami Baba;Kikombe Cha Asubuhi....

Shalom,Habari za Asubuhi,Habari zenu,Hamjambo,Mmeamkaje,.......
wewe umezoe kutoa salam ya vipi?

Tunamshukuru Mungu kwakutuamsha salama na wenye Afya,Asante Mungu
kwa kutupa kibali cha kuiona tena siku hii, Sisi si kwamba ni wema sana,
Tunapokea kutoka kwako kwa Neema tuu..
Basi Baba ukatuongoze Kwenye Kunena na kutenda, Tuingiapo na tutokapo,Kwenye Vyombo vya Usafiri,
kwenye kula na kunywa,Baba Tunaomba Ukabariki kazi zetu na ukawaongoze watoto/wanafunzi kwenye masomo yao.
Ukawaguse wenye Shida/Tabu,Wagonjwa walio mahospitalini na Majumbani,Yatima na Wajane,
Walio magerezani pasipo na hatia,Mfalme wa Amani ukatawale kwa kila jambo.
Ameeeen.
Anza na Mungu Baba..!!!!




““Kama mkiitii sauti ya Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu na kuzingatia kwa uangalifu amri ambazo ninawaamuru leo, yeye atawaweka juu ya mataifa yote duniani. Kama mkitii sauti ya Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, mtapewa baraka zifuatazo; “Miji yenu itabarikiwa na mashamba yenu. “Mtabarikiwa mpate wazawa wengi, mavuno mengi, ng'ombe na kondoo wengi. “Vikapu vyenu vya nafaka vitabarikiwa na vyombo vyenu vya kukandia. Mtabarikiwa mnaporudi nyumbani na mnapotoka nje. Maadui zenu wakiwashambulia, Bwana atawapeni ushindi juu yao. Wakija kuwashambulia kwa njia moja watawakimbieni kwa njia saba. Baraka za Mwenyezi-Mungu zitakuwa katika ghala zenu za nafaka na katika shughuli zenu zote. Atawabariki katika nchi ambayo anawapeni. “Mwenyezi-Mungu atawafanyeni kuwa watu wake watakatifu kama alivyowaahidi, kama mkizitii amri zake yeye Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, na kufuata njia zake. Mataifa yote duniani yakiona kwamba nyinyi mnaitwa kwa jina la Mwenyezi-Mungu yatawaogopa. Mwenyezi-Mungu atawafanikisha kwa wingi: Watoto, mifugo na mavuno shambani katika nchi aliyowaapia wazee wenu kuwa atawapeni, Mwenyezi-Mungu atawafungulieni hazina yake nzuri kutoka mbinguni na kunyesha mvua katika nchi kwa wakati wake, na kubariki kazi zenu. Mtayakopesha mataifa mengi, lakini nyinyi hamtakopa. Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, atawafanya kuwa wa kwanza kwa nguvu na sio wa mwisho. Mtaendelea mbele na sio kurudi nyuma kama mkishika amri zake ambazo ninawapeni leo na kuwa waangalifu kuzitekeleza, bila kugeuka kulia au kushoto kuifuata miungu mingine na kuitumikia.”
Kumbukumbu la Sheria 28:1-14 BHND
http://bible.com/393/deu.28.1-14.bhnd

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Tuesday 17 January 2017

Saalam za Mwaka Mpya Wapendwa/Waungwana...Muwe na wiki Njema yenye Baraka..(Hata mimi nasema yu mwema Mungu)Burudani Atosha Kisaava..!!!


Habari za siku Wapendwa/Waungwana,Heri ya Mwaka Mpya.!!!
natumaini wote mmeupokea vyema na Mungu aendelee kututendea sawa sawa na mapenzi yake.
Yeye yu Mwema sana, Ije mvua lije Jua atabaki kuwa Mungu..
Ukikosa,Ukipata endelea kumuomba Na Kumtukuza yeye tuu maana yeye Atosha.
Tupo pamoja Wapendwa /Waungwana..ni mambo yanaingiliana tuu,kikubwa uzima...

AHADI YA MUNGU NI YA KWELI



              Neno La Leo;Waebrani 6:13-20

Ahadi ya Mungu ni ya kweli
13Mungu alipompa Abrahamu ahadi, aliapa kwa jina lake mwenyewe, maana hakuna aliye mkuu kuliko Mungu ambaye kwa huyo angeweza kuapa. 14Mungu alisema: “Hakika nitakubariki na nitakupa wazawa wengi.” 15Abrahamu alisubiri kwa uvumilivu na hivyo akapokea kile alichoahidiwa na Mungu. 16Watu wanapoapa, huapa kwa mmoja aliye mkuu kuliko wao, na kiapo husuluhisha ubishi wote. 17Naye Mungu aliimarisha ahadi yake kwa kiapo; na kwa namna hiyo akawaonesha wazi wale aliowaahidia kwamba hatabadili nia yake. 18Basi, kuna vitu hivi viwili: Ahadi na kiapo, ambavyo haviwezi kubadilika na wala juu ya hivyo Mungu hawezi kusema uongo. Kwa hiyo sisi tuliokimbilia usalama kwake, tunapewa moyo wa kushikilia imara tumaini lililowekwa mbele yetu.19Tunalo tumaini hilo kama nanga ya maisha yetu. Tumaini hilo lapenya mpaka mahali patakatifu mbinguni. 20 Yesu mwenyewe ametangulia kuingia humo kwa ajili yetu na amekuwa kuhani mkuu milele, kwa utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki.



"Swahili Na Waswahili"Mungu yumwema, Mbarikiwe.