Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 31 March 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 2...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru Mungu kwa  kutuchagua tena na kutupa kibali cha kuiona leo hii,si kwa ujuzi wetu, wala si kwa uwezo wetu,si kwamba sisi ni wema sana,  si kwamba ni wazuri mno zaidi ya wengine ambao Leo hii wapo hoi kitandani, wengine hawana hata kauli ya kusema au kuita Mungu wangu niokoe..na wengine wameaga Dunia..


Nini tumempa Mungu zaidi  ilituendelee kuishi na tukiwa na uwezo wa kumtukuza, kumsifu, kuomba toba,kujifunza na kumtafuta yeye?
Mungu ametupa nafasi hii ya  kuiona siku hii kwa Neema/Rehema yake..
Nimapenzi yake basi nasi tusisite wala kuchelewa kutumia nafasi hii tuliyo ipata kutoka kwa Muumba wetu,Baba yetu,Muumba Mbingu na Nchi,Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo..Yahweh...!!! Jehovah..!!
Tunakuja mbele zako na kujinyenyekeza Baba Mungu,Tunaomba utubariki katika maisha yetu, Baba ubariki Kazi zetu,Biashara,Masomo, Tuingiapo/Tutokapo,Vyombo vya usafiri, tutembeapo na hatua zetu ziwe nawe Yahweh..!!!!


Baba tunakwenda kinyume na adui, Mwovu, Nguvu za Giza,Nguvu za mapepo,Nguvu za mizimu,Nguvu za Mpinga Kristo zishindwe katika Jina lililo kuu la Yesu Kristo wa Nazareti...


1“Nimewaambieni hayo kusudi msiiache imani yenu. 2Watu watawafukuza nyinyi katika masunagogi yao. Tena, wakati unakuja ambapo kila atakayewaua nyinyi atadhani anamhudumia Mungu. 3Watawatendeeni mambo hayo kwa sababu hawamjui Baba, wala hawanijui mimi. 
4Basi, nimewaambieni mambo haya ili saa yake itakapofika mkumbuke kwamba niliwaambieni.[Yohane 16:1-4]



Tunakuja mbele zako Baba tunaomba utusamehe dhambi zetu zote

tulizowaza,tulizo nena,tulizo tenda kwakujua/kutojua Mfalme wa Amani
tunaomba utupe Neema ya kuweza kuwasamehe wale waliotukosea..
Baba ukawaponye/kuwagusa wenye Shida/Tabu, Wagonjwa,wafiwa ukawe mfariji wao..waliovifungoni Baba ukawafungue na kuwaponya kimwili na kiroho..
Roho mtakatifu akatuongoze kwenye kunena/kutenda,kutambua/kujitambua..



Basi, nimewaambieni mambo haya ili saa yake itakapofika mkumbuke kwamba niliwaambieni. “Sikuwaambieni mambo haya tangu mwanzo kwa sababu nilikuwa pamoja nanyi. Lakini sasa namwendea yule aliyenituma; na hakuna hata mmoja wenu anayeniuliza: ‘Unakwenda wapi?’ Kwa kuwa nimewaambieni mambo hayo mmejaa huzuni mioyoni mwenu. Lakini, nawaambieni ukweli: Afadhali kwenu mimi niende zangu, maana nisipokwenda Msaidizi hatakuja kwenu. Lakini nikienda, basi, nitamtuma kwenu. Naye atakapokuja atawathibitishia walimwengu kwamba wamekosea kuhusu dhambi, uadilifu na hukumu ya Mungu. Wamekosea kuhusu dhambi kwa sababu hawaniamini; kuhusu uadilifu, kwa sababu nakwenda zangu kwa Baba, nanyi hamtaniona tena; kuhusu hukumu, kwa sababu mkuu wa ulimwengu huu amekwisha hukumiwa. “Ninayo bado mengi ya kuwaambieni, ila kwa sasa hamwezi kuyastahimili. Lakini atakapokuja huyo Roho wa ukweli atawaongoza kwenye ukweli wote; maana hatasema kwa mamlaka yake mwenyewe, bali atasema atakayoyasikia na kuwajulisheni yatakayokuja. Yeye atanitukuza mimi kwa kuwa atawajulisheni yale atakayopata kutoka kwangu. Vyote alivyo navyo Baba ni vyangu; ndiyo maana nimesema kwamba huyo Roho atawajulisheni yale atakayopata kutoka kwangu.

Baba ukabariki Ridhiki zetu ziingiapo/zitokapo..
Mfalme wa Amani tunaiweke nchi hii tunayoshi mikononi mwako na ukaibariki na kuwabariki watu wake...Baba tunaiweka mikononi mwako na  Tanzania uibariki na kubariki watu wake,Bariki Afrika Baba na Dunia yote wewe ukatawale..Bariki wanaotuongoza nawo wakatuongoze katika haki na kweli..
Baba tunayaweka haya mikononi mwako, Sifa na Utukufu ni wako Daima..
Tukishukuru na kuamini wewe ni Bwana na Mwokozi wetu..
Amina..!!!!

Amani ya Bwana iwe Nanyi.



Mtoto Mose anaokotwa mtoni Nili

1Kulikuwa na mtu mmoja wa ukoo wa Walawi aliyemwoa mwanamke mmoja ambaye pia alikuwa wa ukoo wa Walawi. 2Taz Mate 7:20; Ebr 11:23 Basi, mama huyu akapata mimba, akajifungua mtoto wa kiume. Alipoona kwamba mtoto huyo mchanga alikuwa mzuri, akamficha kwa muda wa miezi mitatu. 3Lakini kwa vile hakuweza kumficha zaidi ya muda huo, alitengeneza namna ya kikapu cha mafunjo,2:3 mafunjo: Aina ya majani yaotayo mtoni au ziwani na mabua yake yalitumika hapo kale kutengenezea karatasi (papiro). akakipaka namna ya lami, akamtia huyo mtoto ndani. Kisha akakiweka kikapu kando ya mto Nili kwenye majani. 4Dada yake huyo mtoto akajificha karibu na mahali hapo ili aone yatakayompata nduguye.
5Basi, binti Farao akashuka mtoni kuoga, na watumishi wake wakawa wanatembeatembea kandokando ya mto. Binti Farao akakiona kile kikapu katika majani, akamtuma mjakazi wake akichukue. 6Alipokifungua, alimwona yule mtoto mchanga, analia. Basi, akamwonea huruma, akasema, “Huyu ni mmojawapo wa watoto wa Waebrania.”
7Papo hapo dada yake yule mtoto akajitokeza, akamwambia binti Farao, “Je, niende nikakutafutie yaya miongoni mwa wanawake wa Kiebrania akulelee mtoto huyu?” 8Binti Farao akamwambia, “Naam; nenda.” Basi, huyo msichana akaenda, akamwita mama yake huyo mtoto. 9Binti Farao akamwambia huyo mama, “Mtunze mtoto huyu, umlee kwa niaba yangu, nami nitakulipa mshahara wako.” Basi, huyo mama akamchukua mtoto, akamlea.
10Mtoto alipokuwa mkubwa kiasi, mama yake akampeleka kwa binti Farao, naye akamchukua na kumfanya mwanawe. Binti Farao akasema, “Nimemtoa majini,” kwa hiyo akampa mtoto huyo jina Mose.2:10 Mose: Jina “Mose” katika Kiebrania lafanana na neno “mashah” maana yake “kutoa” lakini jina hilo ni la Kimisri maana yake “Kupata mtoto.” (Linganisha aya hii na Mate 7:21.)

Mose anakimbilia Midiani
11Siku moja, Mose alipokuwa mtu mzima, aliwaendea Waebrania wenzake ili kujionea taabu zao. Basi, akamwona Mmisri mmoja anampiga Mwebrania, mmoja wa ndugu zake Mose. 12Mose akatazama huku na huko, na alipoona kwamba hakuna mtu karibu, alimuua yule Mmisri na kumficha mchangani. 13Kesho yake, Mose alitoka tena, akaona Waebrania wawili wanapigana. Basi, akamwuliza yule aliyekosea, “Kwa nini unampiga mwenzako?” 14Naye akamjibu, “Nani aliyekuweka wewe kuwa mkuu na mwamuzi wetu? Je, unataka kuniua kama ulivyomuua yule Mmisri?” Hivyo, Mose aliogopa na kufikiri, “Bila shaka jambo hilo limejulikana!” 15Naye Farao aliposikia juu ya tukio hilo akakusudia kumuua Mose. Lakini Mose alimkimbia Farao, akaenda kukaa katika nchi ya Midiani.2:15 Midiani: Jina la makabila ambayo yalihamahama kwenye eneo la kusini mwa nchi ya Palestina. Kulingana na Mwa 25:2, Midiani alikuwa mtoto wa Abrahamu.
Siku moja, Mose alikuwa ameketi kando ya kisima cha maji. 16Basi, binti saba wa kuhani mmoja wa huko Midiani walifika kuchota maji na kuwanywesha kondoo na mbuzi wa baba yao. 17Wachungaji wengine wakaja na kuwafukuza hao binti. Lakini Mose akawasaidia binti hao na kuwanywesha wanyama wao. 18Walipomrudia baba yao Reueli, yeye akawauliza, “Mbona leo mmerudi upesi hivyo?” 19Nao wakamjibu, “Mmisri mmoja alituokoa mikononi mwa wale wachungaji, naye mwenyewe akachota maji na kuwanywesha wanyama wetu.” 20Baba yao akawauliza binti zake, “Yuko wapi? Mbona mmemwacha huko? Mwiteni aje ale chakula.”
21Mose akakubali kukaa kwa huyo mtu. Basi, huyo mtu akampa Mose binti yake aitwaye Zipora awe mke wake. 22Zipora akamzalia mtoto wa kiume. Mose akasema, “Nimekimbilia katika nchi ya kigeni”, kwa hiyo akampa huyo mtoto jina Gershomu.2:22 Gershomu: Neno kwa neno maana yake ni “mkimbizi huko”.

Kilio cha Waisraeli utumwani

23Baada ya muda mrefu, mfalme wa Misri akafa. Waisraeli wakapiga kite na kulia kutokana na hali yao ya utumwa, na kilio chao kikamfikia Mungu juu. 24Mungu akasikia kilio chao, naye akakumbuka agano alilofanya na Abrahamu, na Isaka na Yakobo. 25Mungu aliwaangalia Waisraeli, akaona kuwa hali yao ni mbaya.
Kutoka2;1-25
Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 30 March 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Tuanze Kitabu Cha Kutoka 1...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tunamshukuru Mungu kwa Kutuwezesha kumaliza kitabu cha Mwanzo na Leo tunaanza kitabu cha "KUTOKA"
Nimatumaini yangu kuna mtu amaeguswa na amepata/amejifunza chochote katika mwendelezo wa kitabu cha Mwanzo..Mungu andelee kutuongoza na kutupa Neema ya kumtafuta yeye kwa bidii..Leo tunapoanza kitabu hiki Mungu akaonekane na kutupa shauku ya kusoma/kujifunza zaidi..Ninaimani kuna watu tutakuwa pamoja mpaka mwisho na hawatoondoka hivihivi pasipo na faida..Faida si kufanikiwa kipesa tuu..Hata kuongeza ufahamu na kujifunza zaidi,kutafakari Neno la Mungu na kumjua zaidi ni faida kubwa pia..
Karibu Mpendwa/Muungwana tuungane pamoja katika Kujifunza zaidi
yeye atutiaye nguvu nakutupa  Neema hii akatubariki na kutupa macho ya rohoni.Asanteni wote kwa kuwapamoja..
Injili na iende mbele..!!!

Tuombe..Mtakatifu Mtakatifu, Mtakatifu...!!Baba wa Mbinguni,Mungu wetu,Muumba wetu, Muumba Mbingu na Nchi na Vyote vilivyomo ni mali yako,Hata sisi Baba ni Mali yako..Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo..
Baba wa Yatima,Mume wa wajane,Mungu usiye sinzia wala kulala,Mungu unayejibu,Wewe ni mwamzo na wewe ni Mwisho..
Asante kwa kutucghagua tena Baba umetupa Kibali cha kuiona tena Leo hii..Tazama Jana imepita Baba.. Leo ni siku mpya na Kesho ni siku nyingine Jehovah...!!!Tunajinyenyekeza na kujiachilia mikononi mwako Mfalme wa Amani..Tunakuja mbele zako Baba wa Mbinguni,Tunaomba Utubariki na kubariki siku hii na siku zote Yahweh..!!
Ikawe yenye Amani,Furaha,Upendo na tukakupendeze wewe..
Tulinde Tuingiapo/Tutokapo,Vyombo vya usafiri,Tutembeapo,Hatua zetu ziwe nawe Yahweh..Ukabariki Kazi zetu,Biashara,Masomo,Vilaji/Vinywaji Mfalme wa Mbinguni..Roho Mtakatifu akatuongoze kwenye Kunena na Kutenda,Kutambua/Kujitambua..Ukatufanye Chombo chako chema na tukatumike sawasawa na Mapenzi yako..
Ukabariki Ridhiki zetu ziingiazo na zitokazo..
Baba utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe,Nasi utupe Neema ya kuweza kusamehena..
Yahweh.. ukawaguse na kuwaponya wote wanaopitia Magumu/majaribu, Wagonjwa,Wafiwa ukawe mfariji wao, Wenye shida/Tabu, waliomagerezani pasipo na hatia Baba ukawaguse na haki ikatendeke...
Waliovifungoni mwa mwovu Baba ukawaponye na kuwaokoa..
Kwakuwa Ufalme ni Wako Nguvu na Utukufu Hata Milele...
Amina...!!!!
Tuanze na Bwana..Mungu wabariki sana.

Waisraeli wanateswa nchini Misri
1Haya ndiyo majina ya watoto wa kiume wa Israeli,1:1 Israeli: Jina jingine la Yakobo (taz Mwa 32:29) jina ambalo baadaye lilikuwa jina la wazawa wa Yakobo: Waisraeli. Linganisha 1:1-4 na Mwa 46:8-27. ambao walikwenda Misri, kila mmoja na jamaa yake: 2Reubeni, Simeoni, Lawi, Yuda, 3Isakari, Zebuluni, Benyamini, 4Dani, Naftali, Gadi na Asheri. 5Wazawa wote wa Yakobo walikuwa watu 70.1:5 sabini: Tafsiri ya Kigiriki: Sabini na watano; kadhalika na hati moja ya Kiebrania iliyopatikana kule Kumrani. Idadi hiyo pia yatajwa katika Mate 7:14 (taz pia Mwa 46:27). Wakati huo Yosefu alikuwa amekwisha tangulia kukaa huko Misri.
6Baadaye, Yosefu alifariki, hali kadhalika ndugu zake na kizazi kile chote. 7Taz Mate 7:14 Lakini wazawa wa Israeli waliongezeka sana, wakawa wengi na wenye nguvu mno, wakaenea kila mahali nchini Misri.
8Basi, akatokea mfalme mwingine1:8 mfalme mwingine: Huenda huyo alikuwa Farao Ramesesi II (1304-1238 Kabla ya Kristo). huko Misri ambaye hakumjua Yosefu. 9Naye akawaambia watu wake, “Tazameni jinsi Waisraeli walivyo wengi na wenye nguvu kuliko sisi. 10Ni lazima tutafute hila ya kuwapunguza na kuzuia wasiongezeke; la sivyo, kama vita vikitokea watajiunga na adui zetu na kuitoroka1:10 kuitoroka: Au Kuitawala. nchi.”
11Basi, Wamisri wakawateua wanyapara wawasimamie Waisraeli na kuwatesa kwa kazi ngumu. Waisraeli wakafanya kazi ya kumjengea Farao miji ya kuwekea akiba, Pithomu na Ramesesi. 12Lakini kadiri walivyoteswa ndivyo Waisraeli walivyozidi kuongezeka na kuenea nchini. Hivyo Wamisri wakawaogopa sana watu wa Israeli. 13Basi, Wamisri wakawatumikisha Waisraeli kikatili, 14wakayafanya maisha yao kuwa magumu kwa kazi ngumu ya kutengeneza chokaa na kufyatua matofali, na kazi zote za shambani. Katika kazi hizo zote, Waisraeli walitumikishwa kwa ukatili.
15Kisha, mfalme wa Misri akawaambia wakunga wa Misri, Shifra na Pua, ambao waliwahudumia wanawake wa Kiebrania, 16“Mnapowahudumia wanawake wa Kiebrania wanapojifungua, ikiwa mtoto anayezaliwa ni wa kiume, muueni. Lakini ikiwa ni wa kike, mwacheni aishi.” 17Lakini kwa kuwa wakunga hao walimcha Mungu, hawakufanya kama walivyoamriwa na mfalme wa Misri, bali waliwaacha watoto wa kiume wa Waisraeli waishi. 18Basi, mfalme wa Misri akawaita wakunga hao, akawauliza, “Kwa nini mmefanya hivyo? Mbona mmewaacha watoto wa kiume waishi?” 19Wao wakamjibu Farao, “Wanawake wa Kiebrania si sawa na wanawake wa Misri. Wao ni hodari; kabla mkunga hajafika, wao huwa wamekwisha jifungua.”
20Basi, Mungu akawajalia mema wakunga hao, nao Waisraeli wakazidi kuongezeka na kuwa na nguvu sana. 21Na kwa vile wakunga hao walimcha Mungu, Mungu akawajalia kupata jamaa zao wenyewe. 22Taz Mate 7:20; Ebr 11:23 Kisha Farao akawaamuru watu wake wote hivi, “Kila mtoto wa kiume atakayezaliwa kwa Waebrania mtupeni mtoni Nili. Lakini kila mtoto wa kike, mwacheni aishi
Kutoka1;1-22


Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Wednesday 29 March 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Mwanzo50...Mwisho wa Kitabu cha Mwanzo..Mungu wetu yu Mwema Sana..!!

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru Mungu kwa mema mengi aliyotutendea/anayotutendea..
Sifa na Utukufu ni kwake Daima..



Mbingu zatangaza utukufu wa Mungu; anga ladhihirisha kazi ya mikono yake. Mchana waupasha habari mchana ufuatao, usiku waufahamisha usiku ufuatao. Hamna msemo au maneno yanayotumika; wala hakuna sauti inayosikika; hata hivyo, sauti yao yaenea duniani kote, na maneno yao yafika kingo za ulimwengu. Mungu ameliwekea jua makao yake angani; nalo hutoka kama bwana arusi chumbani mwake, lafurahi kama shujaa aliye tayari kushindana. Lachomoza toka upande mmoja, na kuzunguka hadi upande mwingine; hakuna kiwezacho kuliepa joto lake. Sheria ya Mwenyezi-Mungu ni kamilifu, humpa mtu uhai mpya; masharti ya Mwenyezi-Mungu ni thabiti, huwapa hekima wasio na makuu. Kanuni za Mwenyezi-Mungu ni sawa, huufurahisha moyo; amri ya Mwenyezi-Mungu ni safi, humwelimisha mtu. Kumcha Mwenyezi-Mungu ni jambo jema, na la kudumu milele; maagizo ya Mwenyezi-Mungu ni sawa, yote ni ya haki kabisa. Yatamanika kuliko dhahabu; kuliko dhahabu safi kabisa. Ni matamu kuliko asali; kuliko asali safi kabisa. Yanifunza mimi mtumishi wako; kuyafuata kwaniletea tuzo kubwa. Lakini nani aonaye makosa yake mwenyewe? Ee Mungu, niepushe na makosa nisiyoyajua. Unikinge mimi mtumishi wako na makosa ya makusudi, usikubali hayo yanitawale. Hapo nitakuwa mkamilifu, wala sitakuwa na hatia ya kosa kubwa. Maneno ya kinywa changu, na mawazo ya moyo wangu, yakubalike mbele yako, ee Mwenyezi-Mungu, mwamba wangu na mkombozi wangu!

Yeye aliyetupa Kibali cha kuiona Leo hii..
Yeye ni Mungu wetu ,Muumba wetu,Muumba Mbingu na Nchi,Yeye atosha,Yeye Mwanzo na Yeye ni Mwisho..Yeye asiyesinzia wala kulala.. Mchana yupamoja nasi Usiku yupamoja nasi Jana,Leo, Kesho na hata Milele yeye atabaki kuwa Mungu, Ije mvua lije jua Mungu yu mwema sana...!!!!Hakuna wa kufanana naye,Hakuna na hatakuwepo kama yeye..
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...Jehovah..!! Yahweh..!! wewe ni Mkuu wa Yote..
Tunajinyeyekeza mbele zako Baba  na kujiachilia mikononi mwaka Leo na siku zote..Utubariki Baba wa Mbinguni,Tuingiapao/Tutokapo, Tutembeapao,Hatua zetu ziwe nawe Yahweh..
Ubariki Vinywaji/Vilaji,Vyombo vya usafari na vyote tunavyoenda kugusa/kutumia Baba ukavitakase na Damu ya Mwanao, Bwana wetu Na Mwokozi wetu..Yesu Kristo wa Nazareti....!!!!
Ututakase Miili yetu na Akili zetu Baba..
Roho mtakatifu akatuongoze kwenye kunena/kutenda..Kutambua/kujitambua..
Baba ukabariki Kazi zetu,Biashara,Masomo na Ridhiki zetu Baba ziingiapo na zitokapo Mfalme wa Amani..!!!!
Utusamehe dhambi zetu Baba tulizozitenda kwa kujua/kutojua..
Baba utupe Neema ya kuweza nasi kuwasamehe waliotukosea...
Baba ukawawaponye na kuwaokoa wenye Shida/Tabu, wanaopitia Majaribu/Magumu,wagonjwa,wafiwa ukawe mfariji wao,Waliomagerezani pasipokuwa na hatia,waliofungwa na mwovu, Baba nyoosha mkono wako ukawaguse na kuwaokoa wawe huru kimwili na kiroho..
Mfalme wa Amani Ukatawale na kuibariki Nchi hii tunayoishi, Ukabariki Tanzania Baba, Afrika yote na Dunia nzima..
Ukawaongoze wanaotuongoza nao wakatuongoze katika haki na kweli..
Tunakwenda kinyume na Mwovu Baba..
Tunakuja mbele zako Yahweh..! Sifa na Utukufu ni wako Jehovah..!!tunashukuru na kuaminia kwamba  wewe ni Bwana wetu

na Mwokozi wetu..Yote tunaweka mikononi mwako..
Amina..!!

Muwe na wakati mwema.

1Hapo Yosefu akamkumbatia baba yake akilia na kumbusu. 2Kisha, akawaagiza waganga wake wampake Israeli, baba yake, dawa ili asioze, nao wakafanya hivyo. 3Kama kawaida, siku arubaini zilihitajika kwa kazi hiyo. Wamisri nao wakaomboleza kifo cha Yakobo kwa muda wa siku sabini.
4Baada ya matanga kumalizika, Yosefu akawaambia watu wa jamaa ya Farao, “Ikiwa nimekubalika mbele yenu, tafadhali zungumzeni na Farao kwa niaba yangu kwamba baba yangu aliniapisha, akisema, 5‘Mimi karibu nitafariki. Yakupasa kunizika katika kaburi nililojichongea katika nchi ya Kanaani.’ Kwa hiyo namwomba aniruhusu niende kumzika baba yangu, kisha nitarudi.” 6Farao akajibu, “Nenda ukamzike baba yako kama alivyokuapisha.” 7Basi, Yosefu akaondoka kwenda kumzika baba yake akifuatana na watumishi wote wa Farao, wazee wa nyumba ya Farao, pamoja na wazee wa nchi nzima ya Misri. 8Hali kadhalika, Yosefu alifuatana na jamaa yake yote, ndugu zake na jamaa yote ya baba yake Yakobo. Katika eneo la Gosheni walibaki watoto wao tu pamoja na kondoo, mbuzi na ng'ombe wao. 9Pia waliandamana naye wapandafarasi na magari; lilikuwa kundi kubwa sana.
10Walipofika katika uwanja wa kupuria nafaka wa Atadi, ngambo ya mto Yordani, waliomboleza kwa huzuni kubwa, naye Yosefu akamfanyia baba yake marehemu matanga ya siku saba. 11Wakanaani wenyeji wa nchi hiyo, walipoyaona maombolezo yaliyofanywa kwenye uwanja wa kupuria nafaka wa Atadi, wakasema, “Maombolezo haya ya Wamisri, kweli ni makubwa!” Kwa hiyo, mahali pale pakaitwa Abel-misri, napo pako ngambo ya mto Yordani.
12Wana wa Yakobo walimfanyia baba yao kama alivyowaagiza: 13Walimchukua mpaka nchi ya Kanaani, wakamzika katika pango lililokuwa katika shamba kule Makpela, mashariki ya Mamre. Pango pamoja na shamba hilo Abrahamu alikuwa amelinunua kwa Efroni Mhiti, ili pawe mahali pake pa kuzikia. 14Baada ya kumzika baba yake, Yosefu alirudi Misri pamoja na ndugu zake na watu wote waliokuwa wameandamana naye kwenda kumzika baba yake.

Yosefu awaondolea shaka ndugu zake

15Baada ya kifo cha baba yao, ndugu zake Yosefu walisemezana, “Huenda Yosefu atatuchukia na kutulipiza mabaya yote tuliyomtendea.” 16Kwa hiyo wakampelekea Yosefu ujumbe, wakisema, “Baba yako, kabla hajafariki, aliagiza hivi, 17‘Mwambieni Yosefu kwa niaba yangu: Tafadhali uwasamehe ndugu zako makosa yao mabaya na maovu yote waliyokutendea.’ Sasa basi, tafadhali usamehe uovu tuliokutendea sisi watumishi wa Mungu wa baba yako.” Yosefu alipopata ujumbe huu, alilia. 18Kisha ndugu zake wakamjia, wakainama mpaka chini mbele yake, wakasema, “Tazama, sisi tu watumishi wako.” 19Lakini Yosefu akawaambia, “Msiogope, je, mimi ni badala ya Mungu? 20Nyinyi mlitaka kunitendea vibaya, lakini Mungu alikusudia mema ili watu wengi wapate kuwa hai kama mwonavyo leo. 21Haya, msiogope. Mimi nitawapeni chakula pamoja na watoto wenu.” Basi akawafariji na kusema nao vizuri.

Kifo cha Yosefu
22Yosefu akaendelea kukaa katika nchi ya Misri pamoja na jamaa yote ya baba yake. Aliishi kwa muda wa miaka 110. 23Yosefu alijaliwa kuwaona watoto na wajukuu wa mwanawe Efraimu, na pia kuwapokea kama wanawe watoto wa Makiri mwana wa Manase.
24Baadaye Yosefu aliwaambia ndugu zake, “Mimi sasa ninakaribia kufa. Lakini Mungu hakika atawajia kuwasaidia. Atawatoa katika nchi hii na kuwapelekeni katika nchi aliyowaapia Abrahamu, Isaka na Yakobo.” 25Kisha Yosefu akawaapiza wana wa Israeli, akisema, “Mungu atakapowajia kuwasaidia, hakikisheni kwamba mmeichukua mifupa yangu kutoka huku.”
26Basi, Yosefu akafariki kule Misri, akiwa na umri wa miaka 110. Nao wakaupaka mwili wake dawa usioze, wakauweka katika jeneza kule Misri.
Mwanzo50;1-26
Bible Society of Tanzania

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Tuesday 28 March 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Mwanzo49...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Asante Mungu wetu Baba Yetu,Muumba wetu,Muumba Mbingu na Nchi,Mfalme wa Amani,Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...

Tunashukuru na kukusifu daima,Hakuna wa kufanana nawe,Wewe ni mwanzo na wewe ni mwisho...Tazama jana imepita Baba wa Mbinguni Leo ni siku mpya na Kesho ni sikunyingine Jehovah..!!!Asante kwa ktuchagua kuiona tena Leo hii Baba Mungu, Umetupa Neema/Rehema hii Mfalme wa Amani, si kwamba sisi ni watenda mema sana, kwamba ni wazuri sana,si kwamba wajuaji na wenye nguvu hapana si kwa nguvu/utashi wetu Baba..Bali ni kwa mapenzi yako..
Tunaomba ukaibariki siku hii Baba ..ikawe yenye kukupendeza wewe, Amani na Upendo..Baba Tubariki Tuingiapo/Tutokapo,vyombo vya usafiri,tutembeapo hatua zetu ziwe nawe Yahweh..!! 
Vilaji/vinywaji na vyote tunavyoenda kugusa/kutumia Baba wa Mbinguni ukavitakase na Damu ya Mwanao, Bwana wetu na Mwokozi wetu Yesu Kristo..Ukatutakase Miili na Akili zetu, Roho Mtakatifu akatuongoze kwenye kunena/kutenda..
Utusamehe pale tulikwenda kinyume nawe Baba wa Mbinguni..Nasi utupe Neema ya kuweza kuwasamehe wengine..
Baba ukwaguse/kuwaponya wote wanaopitia Magumu/Majaribu, Wagonjwa, Wenye Shida/Tabu,Waliovifungoni Baba ukawafungue na ukaweke huru kimwili na kiroho.. 

1Wanaomtegemea Mwenyezi-Mungu, wako kama mlima Siyoni,
ambao hautikisiki bali wabaki imara daima.
2Kama Yerusalemu inavyozungukwa na milima,
ndivyo Mwenyezi-Mungu awazungukavyo watu wake,
tangu sasa na hata milele.[Zaburi 125:1-2]

Baba ukawabariki na kuwapa Neema ya kukujua zaidi na Kutembea nawe watoto wetu, familia na wote wakutafutao

10Wanaokujua wewe, ee Mungu hukutegemea,
wewe Mwenyezi-Mungu huwatupi wakutafutao.
11Mwimbieni sifa Mwenyezi-Mungu akaaye Siyoni.

Yatangazieni mataifa mambo aliyotenda![Zaburi 9:1o-11]

Sifa na Utukufu ni kwako Daima..
Tunajinyenyekeza na kujiachilia mikononi mwako Muumba wetu.. Tukiamini wewe ni Bwana na Mwokozi wetu..
Amina..!!
Mungu awabariki.

Yakobo anawabariki wanawe

1Yakobo akawaita wanawe, akasema, “Kusanyikeni pamoja niwaambieni mambo yatakayowapata siku zijazo.
2“Kusanyikeni msikie, enyi wana wa Yakobo,
nisikilizeni mimi Israeli, baba yenu.
3“Wewe Reubeni ni mzaliwa wangu wa kwanza,
nguvu yangu na tunda la ujana wangu.
Wewe wawapita ndugu zako kwa ukuu na nguvu.
4“Wewe ni kama maji ya mafuriko.
Lakini hutakuwa wa kwanza tena,
maana ulipanda kitandani mwangu mimi baba yako,
wewe ulikitia najisi;
naam wewe ulikipanda!
5“Simeoni na Lawi ni ndugu:
Silaha zao wanatumia kufanya ukatili,
6lakini mimi sitashiriki njama zao;
ee roho yangu, usishiriki mikutano yao,
maana, katika hasira yao, walimuua mtu,
kwa utundu wao walikata mshipa wa ng'ombe.
7“Nalaani hasira yao maana ni kali mno,
na ghadhabu yao isiyo na huruma.
Nitawatawanya katika nchi ya Yakobo,
nitawasambaza katika nchi ya Israeli.
8“Wewe Yuda, ndugu zako watakusifu.
Adui zako utawakaba shingo;
na ndugu zako watainama mbele yako.
9“Wewe Yuda, mwanangu, ni kama mwanasimba
ambaye amepata mawindo yake akapanda juu.
Kama simba hujinyosha na kulala chini;
simba mwenye nguvu, nani athubutuye kumwamsha?
10“Fimbo ya kifalme haitatoka kwa Yuda,
wala bakora ya utawala miguuni pake,
mpaka atakapofika yule ambaye ni yake;49:10 yule ambaye ni yake: Maana katika Kiebrania si dhahiri.
ambaye mataifa yatamtii.
11“Atafunga punda wake katika mzabibu
na mwanapunda wake kwenye mzabibu bora.
Hufua nguo zake katika divai,
na mavazi yake katika divai nyekundu.
12“Macho yake ni mekundu kwa divai,
meno yake ni meupe kwa maziwa.
13“Zebuluni ataishi sehemu za pwani,
pwani yake itakuwa mahali pa kuegesha meli.
Nchi yake itapakana na Sidoni.
14“Isakari ni kama punda mwenye nguvu,
ajilazaye kati ya mizigo yake.
15“Aliona kuwa mahali pa kupumzikia ni pema,
na kwamba nchi ni ya kupendeza,
akauinamisha mgongo wake kubeba mzigo,
akawa mtumwa kufanya kazi za shuruti.
16“Dani atakuwa mwamuzi wa watu wake,
kama mojawapo ya makabila ya Israeli.
17“Atakuwa kama nyoka njiani,
nyoka mwenye sumu kando ya njia,
aumaye visigino vya farasi,
naye mpandafarasi huanguka chali.
18“Ee Mwenyezi-Mungu, nangojea uniokoe!
19“Gadi atashambuliwa na wanyanganyi,
lakini yeye atawafuata nyuma na kuwashambulia.
20“Ardhi ya Asheri itatoa mavuno kwa wingi,
naye atatoa chakula kimfaacho mfalme.
21“Naftali ni kama paa aliye huru,
azaaye watoto walio wazuri.49:21 azaaye … wazuri: Au naye huimba nyimbo nzuri.
22“Yosefu ni kama mti uzaao,
mti uzaao kando ya chemchemi,
matawi yake hutanda ukutani.
23“Wapiga mishale walimshambulia vikali,
wakamtupia mishale na kumsumbua sana.
24“Lakini upinde wake bado imara,
na mikono yake imepewa nguvu,
kwa uwezo wa Mwenye Nguvu wa Yakobo,
kwa jina la Mchungaji, Mwamba wa Israeli;
25“kwa Mungu wa baba yako atakayekusaidia,
kwa Mungu mwenye nguvu atakayekubariki;
upate baraka za mvua toka juu mbinguni,
baraka za maji ya vilindi vilivyo chini,
baraka za uzazi wa akina mama na mifugo.
26Baraka za baba yako zishinde baraka za milima ya milele,
ziwe bora kuliko vilima vya kale.
Baraka hizo na ziwe juu ya kichwa cha Yosefu,
juu ya paji lake yeye aliyekuwa ametengwa na ndugu zake.
27“Benyamini ni mbwamwitu mkali;
asubuhi hula mawindo yake,
na jioni hugawa nyara.”
28Hayo ndiyo makabila kumi na mawili ya Israeli, na hayo ndiyo maneno aliyowaambia baba yao alipowabariki, kila mmoja wao kama alivyostahili.

Kifo cha Yakobo

29Kisha Israeli akawaagiza wanawe hivi, “Mimi karibu nife na kujiunga na watu wangu. Nizikeni pamoja na wazee wangu katika pango lililoko shambani mwa Efroni Mhiti, 30kule Makpela, mashariki ya Mamre, nchini Kanaani. Abrahamu alinunua pango na shamba hilo kwa Efroni, Mhiti, liwe lake la kuzikia. 31Huko ndiko walikozikwa Abrahamu na mkewe Sara; huko ndiko walikozikwa Isaka na mkewe Rebeka; na huko ndiko nilikomzika Lea. 32Shamba hilo na pango lake lilinunuliwa kwa Wahiti.”
33Yakobo alipomaliza kuwausia wanawe, aliirudisha miguu yake kitandani, akatoa roho akajiunga na wazee wake.
Mwanzo49;1-33

Bible Society of Tanzania

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 27 March 2017

Mahojiano na Dj D - Ommy ndani ya Kilimanjaro Studios U.S.A



Machi 16 2017, Mubelwa Bandio na Viola walipata nafasi ya kufanya mazungumzo na Dj D-Ommy katika studio za Kilimanjaro Studios.

Dj D-Ommy ambaye alikuwa katika ziara ya kikazi nchini Marekani amezungumza mengi kuhusu maisha, kazi na tasnia nzima ya muziki.

Pia akapata fursa kuzindua rasmi kifaa kipya cha kazi kwa studio yetu, Pioneer DDJ SZ2

Karibu usikilize

Kikombe Cha Asubuhi;Mwanzo48...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru Mungu kwa mema mengi aliyotutendea/anayoendelea kututenda..

Heri wote wamchao Mwenyezi-Mungu, wanaoishi kufuatana na amri zake. Utapata matunda ya jasho lako, utafurahi na kupata fanaka. Mkeo atakuwa kama mzabibu wa matunda mengi nyumbani mwako; watoto wako kama chipukizi za mzeituni kuzunguka meza yako. Naam, ndivyo atakavyobarikiwa mtu amchaye Mwenyezi-Mungu. Mwenyezi-Mungu akubariki kutoka Siyoni! Uione fanaka ya Yerusalemu, siku zote za maisha yako. Uishi na hata uwaone wajukuu zako! Amani iwe na Israeli!
Mtakatifu Mtakatifu Mtakati.. Baba Wa Mbinguni,Muumba wetu,Mungu wetu,Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo..!!! Wewe ni Mwanzo wewe ni Mwisho Hakuna wa kufanana nawe..
Asante kwa kutuchagua  na kutupa tena Kibali cha kuiona Leo hii Baba wa Mbinguni..Tunaanza siku/wiki hii nawe Mungu wetu, Ukaibariki katika Kazi zetu,Biashara,Masomo, Vilaji/Vinywaji,Tuingiapo/Tutokapo, Hatua zetu ziwe nawe Mfalme wa Amani..
Roho Mtakatifu akatuongoze kwenye kunena/kutenda..Ukatufanye chombo chombo chema na ukatutumie sawasawa na Mapenzi yako Yahweh..!!

Usiache Mguu wetu ukasogezwa Baba wa Mbingu, Utupe Afya njema,Akili ya kujitambua/kutambua Baba..Ukabariki ridhiki zetu Baba ziingiapo/zitokapo Mfalme wa Amani..
Utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe Mfalme wa Amani
Nasi tupe Neema ya kuweza kusameheana Baba..
Baba wa Mbinguni Ukawaguse/Kuwaponya wote wanaopitia Magumu/Majaribu,Vifungo vyovyote vya mwovu na uonevu Baba,Wagonjwa,Wenye Shida/Tabu, Wafiwa wakawe mfariji wao Baba..
Tunajinyenyekeza na kujiachilia mikononi mwako Jehovah..!
Sifa na utukufu ni wako, wema na fadhili ni zako..
Upendo na Furaha vipo kwako..Uponyaji na Amani vipo nawe Yahweh..!!

Tunashukuru na Kuamini wewe ni Bwana na Mwokozi wetu..
Amina...!!
Mungu awabariki Sana.




Yakobo anawabariki Efraimu na Manase

1Baada ya hayo, Yosefu alipewa habari kwamba baba yake ni mgonjwa. Hivyo, akawachukua wanawe wawili, Manase na Efraimu, akaenda nao kwa baba yake. 2Yakobo alipofahamishwa kwamba mwanawe Yosefu amefika kumwona, akajitahidi kuinuka, akaketi kitandani. 3Yakobo akamwambia Yosefu, “Mungu mwenye nguvu alinitokea nilipokuwa kule Luzu katika nchi ya Kanaani, akanibariki. 4Aliniambia, ‘Tazama, nitakufanya uwe na wazawa na uongezeke; nitakufanya uwe babu wa jamii kubwa za watu. Ardhi hii nitawapa wazawa wako, waimiliki milele.’” 5Yakobo akaendelea kusema, “Wanao wawili uliowapata hapa Misri kabla sijafika, ni wanangu; Efraimu na Manase watakuwa wangu kama walivyo Reubeni na Simeoni. 6Lakini, watoto utakaopata baadaye watakuwa wako; kwa jina la ndugu zao wataitwa katika urithi wao. 7Taz Mwa 35:16-19 Naamua hivyo kwa sababu ya mama yako, Raheli. Nilipokuwa narudi kutoka Padani yeye alifariki katika nchi ya Kanaani, tukiwa karibu kufika Efratha, akaniachia huzuni. Basi, nikamzika papo hapo, kando ya njia iendayo Efratha, yaani Bethlehemu.”
8Israeli alipowaona wana wa Yosefu, akamwuliza, “Ni akina nani hawa?” 9Yosefu akamjibu baba yake, “Hawa ni wanangu alionijalia Mungu nikiwa huku.” Israeli akasema, “Tafadhali, walete karibu nipate kuwabariki.” 10Macho ya Israeli yalikuwa hayaoni vizuri kwa sababu ya uzee. Basi, Yosefu akawasogeza wanawe karibu na baba yake, naye akawabusu na kuwakumbatia. 11Kisha Israeli akamwambia Yosefu, “Sikutazamia kuuona uso wako tena; lakini, kumbe, Mungu amenijalia hata kuwaona watoto wako!” 12Hapo Yosefu akawaondoa wanawe kwenye magoti ya baba yake, kisha akainama kwa heshima. 13Yosefu akawainua wanawe wawili, Efraimu katika mkono wake wa kulia, akimwelekeza kwenye mkono wa kushoto wa baba yake, na Manase katika mkono wake wa kushoto, akimwelekeza kwenye mkono wa kulia wa baba yake, akawasogeza kwa babu yao. 14Lakini Israeli akaipishanisha mikono yake: Mkono wake wa kulia akauweka juu ya kichwa cha Efraimu, ingawa alikuwa mdogo, na mkono wake wa kushoto akauweka juu ya kichwa cha Manase, aliyekuwa mzaliwa wa kwanza. 15Kisha Israeli akambariki Yosefu, akisema,
“Mungu ambaye babu zangu
Abrahamu na Isaka walimtii maishani mwao,
Mungu ambaye ameniongoza maishani mwangu hadi leo,
16na malaika ambaye aliniokoa katika mabaya yote,
na awabariki vijana hawa!
Jina langu na majina ya wazee wangu, Abrahamu na Isaka,
yadumishwe katika vijana hawa;
nao waongezeke kwa wingi duniani.”
17Yosefu alipoona kwamba baba yake ameuweka mkono wake wa kulia juu ya kichwa cha Efraimu hakupendezwa. Basi, akaushika mkono wa baba yake, akitaka kuuondoa juu ya kichwa cha Efraimu auweke juu ya kichwa cha Manase. 18Akamwambia baba yake, “Sivyo, baba! Huyu hapa ndiye mzaliwa wa kwanza. Tafadhali, uweke mkono wako wa kulia juu ya kichwa chake.” 19Lakini baba yake akakataa, akisema, “Najua, mwanangu, najua. Wana wa Manase pia watakuwa taifa kubwa na mashuhuri. Hata hivyo, ndugu yake mdogo atakuwa mkuu kuliko yeye, na wazawa wake watakuwa mataifa mengi.” 20Taz Ebr 11:21 Basi, Israeli akawabariki siku hiyo, akisema,
“Waisraeli watayatumia majina yenu kubarikia,
watasema, ‘Mungu akutendee mema kama Efraimu na Manase!’”
Ndivyo Israeli alivyomweka Efraimu mbele ya Manase.
21Kisha Israeli akamwambia Yosefu, “Kama uonavyo, mimi niko karibu kufa. Hata hivyo, Mungu atakuwa pamoja nanyi, na kuwarudisheni katika nchi ya babu zenu. 22Zaidi ya hayo, nimekupa wewe, wala si ndugu zako, eneo moja milimani,48:22 eneo moja milimani: Kiebrania: Shekemu. nililowanyanganya Waamori kwa upanga na upinde wangu.”
Mwanzo48;1-22

Bible Society of Tanzania

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Sunday 26 March 2017

Natumaini Juma pili Ilikuwa/Inaendelea Vyema;Happy Mothers Day..Burudani-10,000 Reasons (Bless the Lord) ,I Give You My Heart | Hillsong ,I Need You More




Wapendwa/Waunngwana Natumaini mmekuwa/Mnendelea  na wakati mzuri Jumapili ya Leo....
Mungu aendelee kuwabariki na kuwatendea katika yote yaliyo mema..Awape sawasawa na Mapenzi yake..
Hapa tulipo Leo tunasheherekea Siku Ya Mama.."Happy Mothers Day" Kwa Mama yangu Mpendwa na Nguzo yangu,
kwangu na Wamama wote..Mungu aendelee kuwabariki na kufurahia uzao wenu..!!
Mungu akawajaalie wote wanaotafuta watoto, watoto hao wakawe Baraka kwao na Jamii pia...
Mungu akabariki vizazi vyetu, watoto wetu wakamjue Mungu na wawe Baraka kwetu na Jamii pia..
Sifa na Utukufu ni kwako Mungu..

Neno La Leo;Waroma 8:18-39



Utukufu ujao
18Naona kuwa mateso ya wakati huu wa sasa si kitu kamwe kama tukiyalinganisha na ule utukufu utakaodhihirishwa kwetu. 19Viumbe vyote vinangojea kwa hamu Mungu awadhihirishe watoto wake. 20Kwa maana, viumbe viliwekwa katika hali ya kutojiweza kabisa, si kwa hiari yao, ila vilifanywa hivyo kwa mapenzi ya Mungu. Hata hivyo yapo matumaini, 21maana hivyo viumbe navyo vitaokolewa kutoka katika utumwa wa uharibifu, vishiriki uhuru mtukufu wa watoto wa Mungu. 22Kwa maana tunajua kwamba mpaka hivi sasa, viumbe vyote vinalia kwa maumivu kama ya kujifungua mtoto. 23Wala si hivyo viumbe peke yake, bali hata sisi tulio na huyo Roho, aliye wa kwanza wa zawadi za Mungu; sisi pia tunalalamika ndani yetu, tukingojea tufanywe watoto wa Mungu, nazo nafsi zenu zikombolewe. 24Maana kwa matumaini hayo sisi tumekombolewa. Lakini tumaini halina maana ikiwa tunakiona kile tunachotumainia. Maana ni nani anayetumaini kile ambacho tayari anakiona? 25Kama tunakitumaini kile ambacho hatujakiona bado, basi, tunakingojea kwa uvumilivu.
26Hali kadhalika, naye Roho anatusaidia katika udhaifu wetu. Maana hatujui inavyotupasa kuomba; lakini Roho mwenyewe anatuombea kwa Mungu kwa mlio wa huzuni usioelezeka. 27Naye Mungu aonaye mpaka ndani ya mioyo ya watu, anajua fikira ya huyo Roho; kwani huyo Roho huwaombea watu wa Mungu kufuatana na mapenzi ya Mungu.
28Tunajua kwamba, katika mambo yote, Mungu hufanya kazi na kuifanikisha pamoja na wote wampendao, yaani wale aliowaita kadiri ya kusudi lake. 29Maana hao aliowachagua tangu mwanzo, ndio aliowateua wapate kufanana na Mwanae, ili Mwana awe wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi. 30Basi, wale ambao Mungu aliwateua ndio hao aliowaita; na hao aliowaita ndio hao aliowafanya kuwa waadilifu na hao aliowafanya waadilifu ndio hao aliowashirikisha pia utukufu wake.
Upendo wa Mungu
31Kutokana na hayo, tuseme nini zaidi? Ikiwa Mungu yuko upande wetu, nani awezaye kutupinga? 32Mungu hakumhurumia hata Mwanae wa pekee, bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote. Ikiwa amefanya hivyo, je, hatatujalia pia mema yote? 33Ni nani atakayewashtaki wateule wa Mungu? Mungu mwenyewe huwaondolea hatia! 34Ni nani atakayewahukumu? Hakuna! Maana Kristo ndiye aliyekufa, tena alifufuka kutoka kwa wafu na anakaa upande wa kulia wa Mungu. Yeye anatuombea! 35Ni nani awezaye kututenga na upendo wa Kristo? Je, ni taabu, au dhiki, au mateso, au njaa, au ukosefu wa nguo, au hatari, au kifo? 36Taz Zab 44:22Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo:
“Kwa ajili yako, twakikabili kifo kutwa kucha;
tunatendewa kama kondoo wa kuchinjwa.”
37Lakini, katika mambo haya yote, tumepata ushindi mkubwa kwa msaada wake yeye aliyetupenda. 38Maana ninajua hakika kwamba hakuna kitu kiwezacho kututenganisha na upendo wake: Wala kifo, wala uhai; wala malaika au nguvu nyingine za mbinguni; wala yanayotokea sasa, wala yatakayotokea baadaye; wala mamlaka; 39wala ulimwengu wa juu, wala wa chini kabisa. Hakuna kiumbe chochote kitakachoweza kututenga na upendo wa Mungu katika Kristo Yesu Bwana wetu.
Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN):










"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Friday 24 March 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Mwanzo47...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru Mungu kwa Leo hii.Baba wa Mbinguni,Mfalme wa Amani,
Muumba wetu,Muumba Mbingu Na Nchi,Mungu usiyelala wala kunsinzia,Mungu unayejibu na Kubariki,Mungu unayesamehe,wewe ni Apha na Omega...
Tazama Baba Jana imepita Leo ni siku mpya na Kesho ni siku nyingine Mfalme wa Amani..Tunajinyenyekeza mbele zako Muumba wetu ,Tunakushukuru na kukutukuza Baba.. Tunasema asante Jehovah kwa Kibali ulichotupa Baba cha kuiona Leo hii,Tunaomba ukatuongoze na Kuibariki siku hii na Tuanze nawe Baba katika yote..Tuingiapo/Tutokapo,Vilaji/Vinywaji,Vyombo vya usafiri na tutembeapo,Hatua zetu ziwe nawe Yahweh..!!
Ukabariki kazi zetu Baba, Biashara,Masomo,Vyote tunavyoenda Kugusa/Kutumia tunaomba ukavitakase kwa Damu Ya Mwokozi wetu Bwana wetu Yesu Kristo iliyomwagika ili sisi tupate kupona..
Ukatutakase Miili yetu na Akili zetu Baba..
Ukabariki Ridhiki zetu ziingiapo na zitokapo,Ukatufanye chombo chema na tukatumike sawasawa na Mapenzi yako Baba Mungu..
Utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe Baba..
Nasi ukatupe Neema ya kusameheana..
Ukawaguse na kuwaponya wote Wanaopitia Magumu/Majaribu,Shida/Tabu..Wagonjwa,Waliokata tamaa,Waliokataliwa na Wafiwa wakawe mfariji wao..


Tena jambo hili lasemwa pia: “Hawataingia mahali pangu pa pumziko.” Basi, hiyo ahadi ya kuingia bado ipo, maana wale waliohubiriwa Habari Njema pale awali walishindwa kuingia humo kwa sababu walikosa kutii. Mungu aliweka siku nyingine ambayo inaitwa “Leo,” akasema baadaye kwa njia ya Daudi maneno yaliyokwisha tajwa: “Kama mkisikia sauti ya Mungu leo, msiwe wakaidi.” Kama Yoshua angekuwa amewapa watu hao hilo pumziko, Mungu hangalisema baadaye juu ya siku nyingine. Kwa hiyo, basi, bado kuna kupumzika kwa watu wa Mungu. Maana, kila aingiaye mahali pa pumziko la Mungu atapumzika kutoka katika kazi yake kama vile pia Mungu alivyopumzika kutoka kazi yake. Basi, tujitahidi kuingia katika pumziko hilo, ili asiwepo yeyote miongoni mwetu atakayekataa kutii kama walivyofanya wao. Neno la Mungu ni hai na lina nguvu; ni kali kuliko upanga wenye makali kuwili. Hukata kabisa mpaka mahali ambapo moyo na roho hukutana, mpaka pale vikutanapo viungo vya mwili na uboho. Neno hilo huchambua nia na fikira za mioyo ya watu. Hakuna kiumbe chochote kilichofichika mbele ya Mungu; kila kitu kimefunuliwa wazi mbele ya macho yake yeye ambaye kwake tutapaswa kutoa hoja ya matendo yetu. Basi, tuzingatie kwa makini imani tunayoiungama. Maana tunaye Kuhani Mkuu aliyeingia mpaka mbinguni; Yesu, Mwana wa Mungu. Huyu Kuhani Mkuu wetu anaelewa kabisa unyonge wetu; yeye mwenyewe alijaribiwa kama sisi kwa kila namna lakini hakutenda dhambi. Basi, na tukikaribie bila hofu kiti cha enzi cha Mungu mwenye neema, tupokee huruma na neema ya kutusaidia wakati wa shida.


Asante Mungu kwa hapa tulipo tunaomba Baba ukaibariki hii Nchi na Mfalme wa Amani ukatawale hapa tulipo...Baba ukaibariki na kutawala Tanzania,Afrika na Dunia yote..Amani yako na mkono wako ukawaguse na kuwaongoza wanaotuongoza wapate kutuongoza katika haki na kweli..Upendo,Fadhili,Umoja,Kweli, Hekima na Busara zinatoka kwako...
Utupe Neema ya kutambua/kujitambua,Roho mtakatifu akatuongoze kwenye Kunena/Kutenda...

Mwenyezi-Mungu asipoijenga nyumba, waijengao wanajisumbua bure. Mwenyezi-Mungu asipoulinda mji, waulindao wanakesha bure.[Zaburi 127:1]

Tunajiachili mikononi mwako Baba,Sifa na Utukufu ni kwako Baba..Tunashukuru na kuamini wewe ni Bwana na Mwokozi wetu ...
Amina...!!!!
Mungu awabariki.

1Basi, Yosefu akaenda kwa Farao, akamwambia, “Baba yangu na ndugu zangu pamoja na kondoo, ng'ombe na mali yao yote, wamefika kutoka nchi ya Kanaani. Sasa wako katika eneo la Gosheni.” 2Yosefu alikuwa amewachukua ndugu zake watano, akawajulisha kwa Farao. 3Farao akawauliza, “Kazi yenu ni nini?” Wakamjibu, “Bwana, sisi watumishi wako ni wachungaji, kama walivyokuwa babu zetu.” 4Kisha wakamwambia Farao, “Sisi watumishi wako tumekuja kukaa kama wageni humu nchini kwa kuwa njaa ni kali huko Kanaani na hakuna tena malisho kwa mifugo yetu. Hivyo, bwana, tunakuomba, sisi watumishi wako, uturuhusu kukaa katika eneo la Gosheni.” 5Farao akamwambia Yosefu, “Baba yako na ndugu zako wamekujia wewe. 6Nchi yote ya Misri iko chini yako; wape baba yako na ndugu zako sehemu bora ya nchi hii. Waache wakae katika eneo la Gosheni. Na iwapo unawafahamu watu stadi miongoni mwao, wateue wawe waangalizi wa mifugo yangu.”
7Kisha, Yosefu akamleta baba yake Yakobo kumwamkia Farao; naye Yakobo akampa Farao baraka zake. 8Farao akamwuliza Yakobo, “Umri wako ni miaka mingapi?” 9Yakobo akamjibu, “Umri niliojaliwa kama msafiri ni miaka 130. Miaka hiyo imekuwa michache na iliyojaa mateso, tena haijafikia idadi ya miaka waliyoishi wazee wangu kama wasafiri.” 10Kisha Yakobo akambariki Farao, akaondoka. 11Basi, Yosefu akawapa baba yake na ndugu zake eneo la Ramesesi lililo bora kabisa katika nchi ya Misri, liwe makao yao, nao wakalimiliki kama alivyoagiza Farao. 12Yosefu akawa anawapatia chakula baba yake, ndugu zake na jamaa yote ya baba yake kulingana na idadi ya watu waliowategemea.

Usimamizi wa Yosefu

13Baadaye chakula kiliadimika kabisa nchini kote. Njaa ilikuwa kali sana hata ikawafanya watu wote katika nchi ya Misri na ya Kanaani kudhoofika. 14Yosefu akakusanya fedha yote ya nchi ya Misri na Kanaani kutokana na nafaka waliyonunua, akaipeleka fedha hiyo ikulu kwa Farao. 15Baada ya watu wote wa nchi ya Misri na Kanaani kutumia fedha yao yote Wamisri wote walimjia Yosefu na kumwambia, “Tupe chakula! Kwa nini tufe mbele ya macho yako? Tazama, sasa fedha yetu imekwisha!” 16Yosefu akawaambia, “Kama fedha yenu imekwisha, basi nipeni mifugo yenu, nami nitawapa nafaka.” 17Ndipo wakamletea Yosefu mifugo yao: Farasi, ng'ombe, kondoo, mbuzi na punda, naye akawapa chakula. Mwaka huo Yosefu akawa anawapa chakula kwa kubadilishana na mifugo yao yote.
18Mwaka uliofuata wakamjia tena na kumwambia, “Bwana, ukweli ni kwamba fedha yetu yote imekwisha, na wanyama wetu wamekuwa mali yako. Sasa, bwana, sisi watumishi wako hatuna chochote tunachoweza kukupa isipokuwa miili yetu na mashamba yetu. 19Ya nini sisi tufe mbele ya macho yako na mashamba yetu yaharibike? Utununue sisi pamoja na mashamba yetu, tuwe watumwa wa Farao, mradi tu utupe chakula. Tupe nafaka, tusije tukafa; utupe na mbegu kwa ajili ya mashamba yetu.”
20Hivyo Yosefu akainunua nchi yote ya Misri iwe mali ya Farao. Kila Mmisri alilazimika kuuza shamba lake, kwa jinsi njaa ilivyokuwa kali. Nchi yote ikawa mali ya Farao, 21na Yosefu akawafanya watu kuwa watumwa,47:21 akawafanya … watumwa: Kiebrania na Septuaginta “akawahamishia mijini”. kutoka pembe moja hadi pembe nyingine ya nchi ya Misri. 22Ardhi ambayo Yosefu hakuinunua ni ile iliyomilikiwa na makuhani. Hao hawakulazimika kuiuza ardhi yao kwani waliishi kwa posho maalumu waliyopewa na Farao. 23Kisha Yosefu akawaambia watu, “Tazameni, nimekwisha wanunua nyinyi nyote na mashamba yenu kuwa mali ya Farao. Mtapewa mbegu nanyi mtapanda mashamba yenu. 24Wakati wa mavuno, sehemu moja ya tano mtampa Farao. Sehemu nne zitakazobaki zitakuwa mbegu na chakula kwa ajili yenu na jamaa zenu na watoto wenu.” 25Wakamjibu, “Bwana, umeyaokoa maisha yetu! Kwa vile umetuonesha wema wako, sisi tutakuwa watumwa wa Farao.” 26Ndivyo Yosefu alivyotangaza sheria moja ambayo iko mpaka leo nchini Misri: Kila raia lazima atoe sehemu moja ya tano ya mavuno yake kwa Farao. Ardhi ya makuhani tu ndiyo haikununuliwa na kufanywa mali ya Farao.

Wosia wa Yakobo

27Basi, watu wa Israeli wakakaa katika eneo la Gosheni nchini Misri. Wakiwa huko, wakachuma mali nyingi, wakazaana na kuongezeka sana. 28Yakobo alikaa katika nchi ya Misri kwa muda wa miaka kumi na saba, hadi alipofikia umri wa miaka 147.
29Wakati wa kufa kwake ulipokaribia, Yakobo akamwita mwanawe Yosefu, akamwambia, “Sasa, kama kweli unanipenda, weka mkono wako mapajani mwangu, uniahidi kwamba utanitendea kwa heshima na haki. Usinizike huku Misri, 30ila unilaze pamoja na babu zangu. Nichukue kutoka Misri, ukanizike katika makaburi yao.” Yosefu akamjibu, “Nitafanya kama ulivyosema.” 31Yakobo akamwambia, “Niapie!” Yosefu akamwapia. Kisha Israeli akainamia upande wa kichwa cha kitanda chake.Mwanzo47;1-31

Bible Society of Tanzania

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.