Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 10 April 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 8...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru Mungu katika roho na kweli..
Mtakatifu , Mtakatifu, Mtakatifu...!! Baba wa mbinguni, Baba yetu Mungu wetu, Muumba wetu,Muumba Mbingu na nchi na Vyote vilivyomo ni mali yako, Hata sisi Baba ni mali yako..Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo, Muweza wa yote,wewe ni mwanzo na wewe ni mwisho...Alfa na Omega...
Yahweh..!!!!!Jehovah..!!
Tunashukuru Baba kwa kutupa Kibali hiki cha kutuchagua na kuendelea kuiona Leo..Baba si kwamba wajuzi sana, wenye nguvu sana, wema na wazuri mno.. Hapa ni kwa Neema/Rehema yako tuu Mfalme wa Amani...
Baba tunaomba ukaibariki siku hii ikawe njema na yenye Amani, Furaha, wema na Fadhili,Ukatubariki tuingiapo/tutokapo,vyombo vya usafiri, tutembeapo hatua zetu ziwe nawe Baba...
Baba ukabariki  kazi zetu,Biashara,Masomo na vyote tunavyoenda kugusa/kutumia ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti..Yeye aliteseka pale Msalabani ili sisi tupate kupona..Ukatutakase Akili na miili yetu..Roho Mtakatifu akatuongoze kwenye kunena/kutenda, kutambua/kujitambua..
Baba utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe kwa kuwaza,kutenda, kwakujua/kutojua..Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe Neema ya kuweza kuwasamehe waliotukosea..
Mfalme wa Amani ukawaguse na kuwaponya wote wanaopitia magumu/majaribu,shida/tabu,wagonjwa,wafiwa ukawe mfariji wao,waliovivfungoni baba ukawafungue na kuwaponya kimwili na kiroho pia..
Baba ukatamalaki katika nchi hii tunayoishi.. Ukaibariki na kutubariki wote tunaoishi hapa..ukatulinde na adui yeyote anayepanga kwenda kinyume nawe..Ukatuatamie Jehovah..!!

Mfalme wa Amani Tanzania tunaiweka mikononi mwako na watanzania wote popote walipo,Ukaibariki na kutubariki katika kila lililojema na ukatulinde na uovu wowote unaondelea na kunaopangwa kufanyika..mikononi mwako yote yanawezekena..
Afrika ikawe nawe Baba wa mbinguni ..Dunia yote ukawe mtawala na Amani iliyo juu yako ikatawale..
Ukawabariki na kuwaongoza wote wanaotuongoza wakatuongoze katika haki na kweli..


2“Hakuna aliye mtakatifu kama Mwenyezi-Mungu;
hakuna yeyote aliye kama yeye;

hakuna aliye mwamba kama Mungu wetu.[1 Samueli 2:2]
 20Hakuna mwingine kama wewe, ee Mwenyezi-Mungu, na yote tunayoyasikia yanathibitisha kwamba hakuna Mungu mwingine ila wewe.[1 Mambo ya Nyakati 17:20]
Tunayaweka haya yote mikononi mwako, Tukijinyeyekeza, kukusifu,Tunashukuru na kuamini wewe ni Mungu wetu na hakuna mwingine kama wewe na hatokuwepo..Milele na Milele..
Amina..!!!!! 





Pigo la pili: Vyura

1Kisha Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Nenda kwa Farao ukamwambie Mwenyezi-Mungu asema hivi: Waache watu wangu waondoke ili wanitumikie. 2Lakini ukikataa kuwaacha waondoke, basi, nitaipiga nchi yako yote kwa kuiletea vyura. 3Mto Nili utafurika vyura, nao wataingia mpaka ndani ya nyumba yako, chumba chako cha kulala, kitandani mwako, na katika nyumba za watumishi wako na watu wako. Vyura hao wataingia katika majiko yenu na vyombo vyenu vya kukandia unga. 4Vyura watapanda juu ya mwili wako, miili ya watu wako na watumishi wenu!”
5Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Mwambie Aroni anyoshe mkono wake na fimbo yake juu ya mito, juu ya mifereji na madimbwi, nao vyura watatokea na kuenea kila mahali nchini Misri.”8:5 katika makala ya Kiebrania ni 8:1. 6Basi, Aroni akanyosha fimbo yake juu ya maji yote, vyura wakatokea na kuifunika nchi nzima ya Misri. 7Lakini wachawi wa Misri kwa uchawi wao pia wakaleta vyura nchini Misri.
8Kisha Farao akamwita Mose na Aroni, akamwambia, “Msihi Mwenyezi-Mungu, ili aniondolee mimi na watu wangu vyura hawa, nami nitawaacha Waisraeli waende zao na kumtambikia Mwenyezi-Mungu.” 9Mose akamjibu Farao, “Haya! Waweza kutaja wakati unaotaka nikuombee kwa Mungu, niwaombee maofisa wako na watu wako; nitamwomba awaangamize vyura hawa waliomo katika nyumba zenu; watabaki tu mtoni Nili!”
10Farao akamwambia, “Kesho.” Mose akasema, “Nitafanya kama unavyosema, ili ujue kwamba hakuna yeyote anayelingana na Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu. 11Vyura wataondoka kwako, na kwenye nyumba zenu, kwa maofisa wako na kwa watu wako; watabaki tu katika mto Nili.”
12Basi, Mose na Aroni wakaondoka nyumbani kwa Farao, na Mose akamlilia Mwenyezi-Mungu amwondolee Farao uvamizi wa vyura hao aliomletea. 13Mwenyezi-Mungu akafanya kama Mose alivyomwomba: Vyura wakafa majumbani, viwanjani na kwenye kumbi za nyumba na katika mashamba. 14Watu wakawakusanya vyura hao marundo marundo; nchi nzima ikanuka. 15Lakini Farao alipoona kwamba nchi imepata nafuu, akawa mkaidi tena, wala hakuwasikiliza Mose na Aroni, kama Mwenyezi-Mungu alivyokuwa amesema.

Pigo la tatu: Viroboto

16Kisha, Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Mwambie Aroni anyoshe fimbo yake na kuyapiga mavumbi, nayo yatageuka kuwa viroboto kote nchini Misri.” 17Mose na Aroni wakafanya hivyo. Aroni alinyosha fimbo yake na kuyapiga mavumbi, nayo yakageuka kuwa viroboto na kuwaparamia watu na wanyama. Mavumbi yote nchini kote Misri yakageuka kuwa viroboto. 18Wachawi wa Misri, kwa uchawi wao, wakajaribu kuyageuza mavumbi yawe viroboto, lakini hawakufaulu. Viroboto hao wakaenea juu ya watu na wanyama. 19Taz Luka 11:20 Wale wachawi wakamwambia Farao, “Hii ni kazi ya mkono wa Mungu.”8:19 au Hii ni nguvu ya kimungu Kiebrania, neno kwa neno: “Ni kidole cha Mungu”. Lakini moyo wa Farao ukaendelea kuwa mgumu; wala hakuwasikiliza Mose na Aroni. Ikawa kama Mwenyezi-Mungu alivyokuwa amesema.

Pigo la nne: Nzi

20Kisha Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Kesho amka asubuhi mapema umwendee Farao wakati anapokwenda mtoni umwambie, ‘Mwenyezi-Mungu asema hivi: Waache watu wangu waondoke ili wanitumikie. 21Kama ukikataa kuwaacha waondoke, basi, nitakuletea makundi ya nzi, wewe, maofisa wako na watu wako wote. Wataingia kwenye nyumba zenu na nyumba zote za Wamisri zitajaa makundi ya nzi, kadhalika na ardhi yote ya Misri. 22Lakini siku hiyo sehemu ya Gosheni wanakoishi watu wangu nitaikinga: Humo nzi hao hawatakuwamo. Hapo ndipo utakapotambua kwamba mimi Mwenyezi-Mungu natenda mambo nchini mwako. 23Nitawakinga watu wangu na mambo yatakayowapata watu wako. Mambo hayo yatafanyika kesho.’” 24Mwenyezi-Mungu akafanya kama alivyosema: Makundi makubwa ya nzi yakaivamia nyumba ya Farao, nyumba za maofisa wake na nchi nzima ya Misri. Nchi nzima ya Misri ikaharibiwa na nzi hao.
25Ndipo Farao akawaita Mose na Aroni, akasema, “Mnaweza kwenda kumtambikia Mungu wenu, lakini iwe humuhumu nchini Misri.” 26Lakini Mose akamjibu, “La! Haifai kufanya hivyo, maana tambiko tutakazomtolea Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, zitawachukiza Wamisri. Je, Wamisri wakituona tukitoa tambiko ambazo ni chukizo kwao, si watatupiga mawe? 27Ni lazima tusafiri mwendo wa siku tatu jangwani tukamtambikie Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, kama atakavyotuamuru.”
28Basi, Farao akasema, “Nitawaacha mwende zenu kumtambikia Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, jangwani. Walakini msiende mbali mno. Niombeeni na mimi.” 29Mose akamjibu, “Mara tu nitakapokuacha, nitamwomba Mwenyezi-Mungu makundi haya ya nzi yatoweke kwako wewe Farao, maofisa wako na watu wako, kesho. Lakini wewe usitudanganye tena kwa kukataa kuwaacha watu kwenda kumtambikia Mwenyezi-Mungu.”
30Basi, Mose akaondoka nyumbani kwa Farao, akamwomba Mwenyezi-Mungu. 31Mwenyezi-Mungu akafanya kama Mose alivyomwomba, wale nzi wakatoweka kutoka kwa Farao, maofisa wake na watu wake, wala hakusalia hata mmoja. 32Lakini hata safari hii Farao alikuwa mkaidi, wala hakuwaruhusu Waisraeli kuondoka.Kutoka8;1-32

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)
"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Sunday 9 April 2017

Nimatumaini Yangu Jumapili ilikuwa/inaendelea nyema;Burudani-UPENDO CHOIR. AZANIA FRONT KKKT CATHEDRAL CHURCH (TUKITEMBEA NURUNI ALBUM)

Wapendwa/Waungwana nimatumaini yangu mmekuwa na mnaendelea na Jumapili hii vizuri..hapa kwetu ni salama kabisa na leo kijua kimeonekana..
Mungu yu mwema na aendelee kuwabariki katika yote..Mkawe na wakati mwema..
Watoto hapa kwetu wapo likizo pia baadhi ya wazazi waliowahi kuomba likizo muwe na wakati mwema natumai mtakuwa na wakati mwema na watoto/familia..
Wanaondelea na kazi Mungu aendelee kuwaongoza katika kazi zenu...
Basi tukatumie Ulimi wetu vyema..Roho mtakatifu akatuongoze katika yote na tuwe na kiasi..

Nawapenda...
 Neno La Leo;Yakobo3:1-18

Ulimi
1Ndugu zangu, wengi wenu msiwe waalimu. Kama mjuavyo, sisi waalimu tutapata hukumu kubwa zaidi kuliko wengine. 2Lakini kama mtu hakosi katika usemi wake, basi, huyo ni mkamilifu, na anaweza kutawala nafsi yake yote. 3Sisi huwatia farasi lijamu kinywani mwao ili watutii; na kwa njia hiyo twaweza kuwaongoza kokote tunakotaka. 4Meli nazo pia, ingawa ni kubwa sana, na husukumwa na upepo mkali, huweza kugeuzwa kwa usukani mdogo sana, zikaelekea kokote nahodha anakotaka. 5Vivyo hivyo, ulimi, ingawa ni kiungo kidogo cha mwili, hujisifia makuu sana.
Moto mdogo waweza kuteketeza msitu mkubwa. 6Hali kadhalika ulimi ni kama moto. Umejaa maovu chungu nzima, unayo nafasi yake katika miili yetu na hueneza ubaya katika nafsi zetu zote. Huteketeza maisha yetu yote kwa moto utokao Jehanamu kwenyewe

7Binadamu anaweza kuwafuga wanyama, na amefaulu kufuga viumbe vyote – wanyama wa mwituni, ndege, nyoka na viumbe vya baharini. 8Lakini hakuna mtu aliyefaulu kuufuga ulimi. Ulimi ni kitu kiovu, hakitawaliki, na kimejaa sumu inayoua. 9Kwa ulimi sisi twamshukuru Bwana na Baba yetu. Kwa ulimi huhuo twawalaani watu, watu ambao wameumbwa kwa mfano wa Mungu. 10Maneno ya kubariki na ya kulaani hutoka katika kinywa kimoja. Ndugu zangu, mambo haya hayapaswi kuwa hivyo. 11Je, chemchemi moja yaweza kutoa maji matamu na maji machungu pamoja? 12Ndugu zangu, je, mtini waweza kuzaa zeituni? Au, mzabibu waweza kuzaa tini? Chemchemi ya maji ya chumvi haiwezi kutoa maji matamu.

Hekima itokayo juu mbinguni
13Je, ni nani mwenye hekima na akili miongoni mwenu? Basi, aoneshe jambo hilo kwa mwenendo wake mzuri na kwa matendo yake mema yanayofanyika kwa unyenyekevu na hekima. 14Lakini ikiwa mioyo yenu imejaa wivu, chuki na ubinafsi, basi, msijisifu na kusema uongo dhidi ya ukweli. 15Hekima ya namna hiyo haitoki juu mbinguni; hekima hiyo ni ya ulimwengu, na ya kidunia, tena ni ya kishetani. 16Maana popote palipo na wivu na ubinafsi, hapo pana fujo na kila aina ya uovu. 17Lakini hekima itokayo juu mbinguni, kwanza ni safi; inapenda amani, upole na huwajali watu; imejaa huruma na huzaa matunda ya matendo mema; haina ubaguzi wala unafiki. 18Uadilifu ni mazao ya mbegu ambazo wapenda amani hupanda katika amani.




Shukrani;Daniel Christopher

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Friday 7 April 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 7...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru Mungu..
Asante Baba wa Mbinguni kwakutuamsha tena na Kutupa Kibali cha  kuendelea kuiona Leo hii..Baba ikawe yenye Amani,Furaha,Upendo na Baraka..Baba wa Mbinguni utubariki tuingiapo/tutokapo,Vilaji/vinywaji,vyombo vya usafiri na tutembeapo hatua zetu ziwe nawe Baba..Ukabariki Ridhiki zetu ziingiazo /zitokazo,Mfalme wa Amani ukabariki Kazi zetu,Biashara,Masomo na ukatakase vyote tunavyoenda kugusa/kutumia..Baba ukatutakase Miili yetu na Akili zetu kwa Damu ya Bwana wetu na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti..Roho Mtakatifu akatuongoze katika Kunena/kutenda, kuamua,kutambua/kujitambua..

Jehovah..! Tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza na kujiachilia mikononi mwako,utamalaki na kutuatamia,Utuokoe na kutuponya, Utupe Amani ya rohoni na kukujua wewe na tuwe na kiu ya kukutafuta zaidi..
Tunakwenda kinyume na kazi zote za Mwovu na kuvunja maagano na utawala wake katika Jina lililokuu kupita majina yote..Yesu Kristo yeye aliteseka ili sisi tupate kupona..

Mungu Baba tunaomba ukawaguse/kuwaponya wote wanaopitia Magumu/Majaribu,Shida/Tabu,Wagonjwa,wafiwa ukawe mfariji wao Baba..
Yahweh..!!!!Tamalaki na uatamie  watoto wetu,Uwalinde na kuwaongoza vyema katika makuzi yao..Shuleni wapate kukumbuka na kuelewa yote wanayofundishwa..wawe na kiu ya kukujua wewe zaidi, wakawe Baraka kwa wazazi/walezi na jamii pia..
Jehovah..Tamalaki na kuibariki Nchi hii tunatoishi na wote tunaoshi hapa Baba..Tanzania tunaiweka mikononi mwako Baba na wa Tanzania wote..ukatuongezee Imani,Amani na wewe ukawe Mtawala mkuu..
Afrika yote iwe mikononi mwako Baba wa Mbinguni Dunia nzima Ukatawale na kuongoza.. Ukawaongoze wanaotuongoza wakatuongoze katika haki na kweli..
Chochote kinachokwenda kinyume nawe Baba kikashindwe na ukuu wako ukashinde..!!!

22Maana Mwenyezi-Mungu ni hakimu wetu,
yeye ni mtawala wetu;
Mwenyezi-Mungu ni mfalme wetu,
yeye ndiye anayetuokoa.[Isaya 33:22]

Tunayaweka haya mikononi mwako Baba wa Mbinguni,Tunashukuru na kukusifu na Tukiamini wewe ni Mungu wetu Leo na hata milele..
Amina..!!!!

12Salimianeni kwa ishara ya upendo. 13Watu wote wa Mungu huku wanawasalimuni.
14Neema ya Bwana Yesu Kristo na upendo wa Mungu na umoja wa Roho Mtakatifu, viwe nanyi nyote.[2Wakorintho13;12-14]





1Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Tazama, mimi nakufanya kuwa kama mungu kwa Farao, naye ndugu yako Aroni atakuwa nabii wako. 2Utamwambia ndugu yako Aroni mambo yote nitakayokujulisha, naye Aroni nduguyo, atamwambia Farao awaache Waisraeli watoke nchini mwake. 3Taz Mate 7:36 Lakini nitaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu. Na hata kama nitazidisha miujiza na maajabu yangu katika nchi ya Misri, 4Farao hatakusikiliza, na hapo nitaunyosha mkono wangu wenye nguvu na kuiadhibu vikali nchi ya Misri, na kuwatoa watu wangu, makabila ya Israeli, kutoka Misri. Nitafanya hivyo kwa matendo makuu ya hukumu dhidi ya Misri. 5Wakati nitakapounyosha mkono wangu dhidi ya nchi ya Misri na kuwatoa Waisraeli miongoni mwao. Ndipo Wamisri watakapotambua kwamba mimi ndimi Mwenyezi-Mungu.” 6Basi, Mose na Aroni wakafanya hivyo; naam, walifanya kama Mwenyezi-Mungu alivyowaamuru. 7Mose alikuwa na umri wa miaka themanini, na Aroni alikuwa na umri wa miaka themanini na mitatu wakati huo walipoongea na Farao.

Fimbo ya Aroni

8Mwenyezi-Mungu aliwaambia Mose na Aroni, 9“Farao atakapowaambieni mthibitishe jambo hilo kwa kutenda miujiza, wewe utamwambia Aroni aichukue fimbo yake, aitupe mbele ya Farao, nayo itakuwa nyoka.” 10Basi, Mose na Aroni wakamwendea Farao na kufanya kama walivyoamriwa na Mwenyezi-Mungu. Aroni aliitupa fimbo yake chini mbele ya Farao na maofisa wake, nayo ikawa nyoka. 11Lakini, Farao akawaita wenye hekima wake na wachawi; hao wachawi wa Misri wakafanya vivyo hivyo kwa uchawi wao. 12Kila mmoja akaitupa fimbo yake chini, ikawa nyoka. Lakini fimbo ya Aroni ikazimeza fimbo zao. 13Hata hivyo, moyo wa Farao bado ulibaki kuwa mgumu, wala hakuwasikiliza; ikawa kama alivyosema Mwenyezi-Mungu.

MAPIGO KUMI
(Kut 7:14–12:36)
Pigo la kwanza: Damu

14 Taz Hek 11:6-8 Kisha Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Moyo wa Farao umekuwa mgumu. Anakataa kuwaacha Waisraeli waondoke. 15Basi, nenda ukakutane naye kesho asubuhi, wakati anapokwenda mtoni Nili. Mngojee kando ya mto. Chukua mkononi mwako ile fimbo iliyogeuka kuwa nyoka. 16Kisha mwambie hivi, Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Waebrania, amenituma kwako, naye asema hivi, ‘Waache watu wangu waende zao ili wanitumikie jangwani, lakini mpaka sasa wewe hupendi kutii. 17Taz Ufu 16:4 Basi, Mwenyezi-Mungu asema kwamba sasa utamtambua yeye ni nani. Nitayapiga maji ya mto Nili kwa fimbo hii, na maji yote yatageuka kuwa damu. 18Samaki waliomo mtoni Nili watakufa, mto wote utanuka vibaya, na Wamisri watachukia kabisa kunywa maji yake.’”
19Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Mwambie Aroni aichukue fimbo yake na kuinyosha juu ya maji ya Misri, juu ya mito yote, mifereji, madimbwi na mabwawa yao yote, nayo yatakuwa damu. Kutakuwa na damu nchini kote, na hata katika vyombo vyote vya mbao na vya mawe.”
20Mose na Aroni wakafanya kama Mwenyezi-Mungu alivyowaamuru. Aroni aliinua fimbo yake juu mbele ya Farao na maofisa wake, akayapiga maji ya mto Nili, na maji yote mtoni yakageuka kuwa damu. 21Samaki wakafa, mto ukanuka vibaya sana hata Wamisri wasiweze kunywa maji yake. Nchi nzima ikajaa damu. 22Lakini wachawi wa Misri kwa kutumia uchawi wao wakafanya vivyo hivyo. Kwa hiyo moyo wa Farao ukabaki kuwa mgumu, naye hakuwasikiliza Mose na Aroni; ikawa kama Mwenyezi-Mungu alivyokuwa amesema. 23Basi, Farao akarudi nyumbani kwake, na hata haya yaliyotokea hakuyajali. 24Wamisri wote wakachimbachimba kandokando ya mto Nili ili wapate maji ya kunywa, kwani hawakuweza kunywa maji ya mto huo.
25Pigo hilo la mto Nili lilidumu siku saba.

Kutoka7;1-22

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)
"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 6 April 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 6...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru Mungu kwa maana Fadhili zake ni za milele..
Asante Mungu Baba kwa kutuchagua sisi na kutupa kibali cha kuendelea kuiona siku hii..si kwamba sisi ni wema sana,kwamba ni wenyenguvu/utashi,si kwamba sisi ni bora mno, si kwamba wengine ni wakosaji sana hapana Baba wa Mbinguni ni kwa Neema/Rehema yako tuu..

Tazama Jana imepita Baba Leo ni siku mpya Kesho ni siku nyingine Yahweh...!!Tunakuja mbelezako tukijinyenyekeza na Tunaomba ukabariki maisha yetu Baba..Maisha yetu yapo mikononi mwako Jehovah..!!Wewe unatujua kuliko tunavyojijua Baba wewe ni Mungu wetu,Muumba wetu,wewe ni Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo..Wewe ni mwanzo na wewe ni mwisho,Wewe Ndimi Mwenyezi-Mungu ujapokuwa nasi hakuna linaloshindikana,Wewe ni kila kitu hakuna kama wewe na hatokuwepo..Wewe ni Alfa na Omega..!!!
Tunaomba utubariki Tuingiapo/tutokapo,vilaji/vinywaji,vyombo vya usafiri,tutembeapo hatua zetu ziwe nawe Yahweh..!!
Ukabariki kazi zetu,Biashara,Masomo na ukaguse na kutakasa vyote tunavyo enda kutumia,Ukatutakase Miili yetu na Akili zetu Baba wa Mbinguni na Damu ya mwanao mpendwa Bwana wetu na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti..Aliteseka na kumwaga damu ili sisi tupate kupona..
Tunakwenda kinyume na Mwovu, Nguvu za Giza,Nguvu za Mizimu,Nguvu za mapepo,Nguvu za Mpinga Kristo Zishindwe katika Jina la Bwana wetu Yesu  Kristo wa Nazareti...

“Sikiliza!” Asema Yesu, “Naja upesi pamoja na tuzo nitakalompa kila mmoja kufuatana na matendo yake. Mimi ni Alfa na Omega, wa kwanza na wa mwisho, mwanzo na mwisho.” Heri yao wale wanaoosha mavazi yao, wapate kuwa na haki ya kula tunda la mti wa uhai, na haki ya kuingia mjini kwa kupitia milango yake. Lakini mbwa, wachawi, wazinzi, wauaji, waabudu sanamu na wote wanaopenda kusema uongo, watakaa nje ya mji. “Mimi, Yesu, nimemtuma malaika wangu awathibitishieni mambo haya katika makanisa. Mimi ni mzawa wa ukoo wa Daudi. Mimi ni nyota angavu ya asubuhi!” Roho na Bibi arusi waseme, “Njoo!” Kila mtu asikiaye hili, na aseme, “Njoo!” Aliye na kiu na aje; anayependa, na achukue maji ya uhai bila malipo.
Tunakuja mbelezako Baba tukiomba na utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe..kwakujua/kutojua,kwakunena/kwakutenda na kwakuwaza..
Baba ukatupe Neema ya sisi kuweza kuwasamehe wote waliotukosea.

Mfalme wa Amani tunaomba ukawaponye na ukawaguse wenzetu walio wagonjwa,wasiojiweza,wafiwa ukawe mfariji wao,wenye shida/tabu,waliokatika vifungo mbalimbali baba ukawaponye kimwili na kiroho..wanaopitia Magumu/majaribu..Baba Yatima na wajane na walidhurumiwa haki zao zikapatikane..
Jehovah..Yahweh..!!Mfalme wa Amani..Tunayaweka haya yote mikononi mwako..Sifa na Utukufu ni wako,Tukishukuru na kuamini wewe ni Mungu wetu..Jana Leo na hata milele na ilele..

Amina..!!

Mimi Yohane nayaandikia makanisa saba yaliyoko Asia. Nawatakieni neema na amani kutoka kwake yeye aliyeko, aliyekuwako na anayekuja; na kutoka kwa roho saba walio mbele ya kiti chake cha enzi, na kutoka kwa Yesu Kristo, shahidi mwaminifu, wa kwanza kufufuliwa kutoka kwa wafu, na ambaye ni mtawala wa wafalme wa dunia. Yeye anatupenda, na kwa damu yake ametufungua kutoka vifungo vya dhambi zetu, akatufanya sisi kuwa ufalme wa makuhani, tumtumikie Mungu, Baba yake. Kwake Yesu Kristo uwe utukufu na nguvu, milele na milele! Amina. Tazama! Anakuja na mawingu! Kila mtu atamwona, na hata wale waliomtoboa. Makabila yote duniani yataomboleza juu yake. Naam! Amina. “Mimi ni Alfa na Omega,” asema Bwana Mungu Mwenye Nguvu , aliyeko, aliyekuwako na anayekuja.
Mungu aendelee kuwabariki.


1Lakini Mwenyezi-Mungu akamjibu Mose, “Sasa utaona jinsi nitakavyomtenda Farao; maana kwa nguvu atalazimika kuwaacha watu wangu watoke. Naam, kwa nguvu atawafukuza waondoke nchini mwake.”

Mungu anamwita Mose

2 Taz Mwa 17:1; 28:3; 35:11; Kut 3:13-15 Mungu akamwambia Mose, “Mimi ni Mwenyezi-Mungu. 3Nilimtokea Abrahamu, Isaka na Yakobo nikijulikana kama Mungu Mwenye Nguvu,6:3 Mungu mwenye nguvu: Kiebrania: El Shadai. ingawa kwa jina langu, Mwenyezi-Mungu, sikuwajulisha. 4Tena nilifanya agano nao kwamba nitawapa nchi ya Kanaani ambako waliishi kama wageni. 5Zaidi ya hayo, nimesikia kilio cha Waisraeli ambao wamelazimishwa kufanya kazi za kitumwa na Wamisri, nikalikumbuka agano langu. 6Kwa hiyo, waambie Waisraeli hivi, ‘Mimi ni Mwenyezi-Mungu! Mimi nitawatoa katika nira mlizowekewa na Wamisri. Nitawaokoeni utumwani mwenu. Nitaunyosha mkono wangu wenye nguvu na kuwaadhibu vikali Wamisri na kuwakomboa nyinyi. 7Nitawafanyeni kuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu. Nyinyi mtatambua kuwa mimi ndimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, niliyewatoa katika nira za Wamisri. 8Nami nitawapeleka katika nchi ile niliyoapa kumpa Abrahamu, Isaka na Yakobo. Nitawapeni nchi hiyo iwe yenu. Mimi ni Mwenyezi-Mungu.’” 9Mose akawaeleza Waisraeli maneno hayo. Lakini wao hawakumsikiliza kwa sababu walikuwa wamekufa moyo kutokana na utumwa mkali.
10Kisha Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, 11“Nenda kwa Farao, mfalme wa Misri, umwambie awaache Waisraeli waondoke nchini mwake.” 12Lakini Mose akamwambia Mwenyezi-Mungu, “Tazama, Waisraeli hawanisikilizi mimi, sembuse Farao! Tena mimi ni mtu asiye na ufasaha wa kuongea!” 13Lakini Mwenyezi-Mungu akaongea na Mose na Aroni, akawaagiza waende kwa Farao, mfalme wa Misri, na kuwatoa Waisraeli nchini Misri.

Ukoo wa Mose na Aroni

14Hii ndiyo orodha ya wakuu wa jamaa za Waisraeli, Wana wa Reubeni, mzaliwa wa kwanza wa Israeli: Henoki, Palu, Hesroni na Karmi. Hao walikuwa mababu wa jamaa za Reubeni. 15Wana wa Simeoni walikuwa: Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Sohari na Shauli; huyu wa mwisho alikuwa mtoto wa mwanamke wa Kikanaani. Hao walikuwa mababu wa jamaa za Simeoni. 16Taz Hes 3:17-20; 26:57-58; 1Nya 6:16-19 Sasa yafuata majina ya wana wa Lawi na wazawa wao: Gershoni, Kohathi na Merari. Lawi aliishi miaka 137. 17Wana wa Gershoni walikuwa: Libni na Shimei; jamaa zao zilitajwa kwa majina yao. 18Wana wa Kohathi walikuwa: Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli. Kohathi aliishi miaka 133. 19Wana wa Merari walikuwa: Mahli na Mushi. Hao ndio mababu wa jamaa za Walawi.
20Amramu alimwoa Yokebedi, shangazi yake, naye akamzalia Aroni na Mose. Amramu aliishi miaka 137. 21Na watoto wa kiume wa Ishari walikuwa: Kora, Nefegi na Zikri. 22Watoto wa kiume wa Uzieli walikuwa: Mishaeli, Elsafani na Sithri.
23Aroni alimwoa Elisheba, binti yake Aminadabu, dada yake Nashoni; naye akamzalia Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari. 24Nao watoto wa kiume wa Kora walikuwa: Asiri, Elkana na Abiasafu, ambao walikuwa mababu wa jamaa za Kora. 25Eleazari, mwana wa Aroni, alimwoa mmoja wa binti za Putieli, naye akamzalia Finehasi. Hawa ndio waliokuwa wakuu wa jamaa za Lawi.
26Aroni na Mose ndio walioambiwa na Mwenyezi-Mungu, “Watoeni watu wa Israeli kutoka nchi ya Misri, vikundi kwa vikundi.” 27Ndio haohao Mose na Aroni walioongea na Farao, mfalme wa Misri, juu ya kuwatoa Waisraeli nchini Misri.

Mungu amwamuru Mose na Aroni

28Siku ile Mwenyezi-Mungu alipoongea na Mose nchini Misri, 29alimwambia, “Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu. Mwambie Farao, mfalme wa Misri, maneno yote ninayokuambia.” 30Lakini Mose akamwambia Mwenyezi-Mungu, “Mimi sina ufasaha wa kuongea; Farao atanisikilizaje?”

Kutoka6;1-30

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)
"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Wednesday 5 April 2017

Kikombe Cha Asubuhi; Kutoka 5...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru Mungu kwa yote...
Mtakatifu Mtakatifu Mtakatifu...!!!!!!! Baba wa Mbinguni, Mungu wetu na Mwokozi wetu,Muumba wetu na Muumba mbingu,Nchi na vyote vilivyomo ni mali yake.Hata sisi Baba ni mali yako..Tunashukuru na kukusifu Daima..Asante Baba kwa wema,Fadhili,Ridhiki na yote..Asante kwakutuchagua tena na kutupa kibali cha kuendelea kuona leo hii..
Ikawe siku njema na yenye Baraka..Utubariki tuingiapo/tutokapo,vyombo vya usafiri,tutembeapo Baba hatua zetu ziwe nawe.. Baba wa Mbinguni Ukabariki Kazi zetu,Biashara,Masomo na vyote tunavyoenda kugusa/kutumia Baba ukavitakase na ukatutakase kwa Damu ya mwanao Bwana wetu na Mwokozi wetu aliteseka pale msalabani ili sisi tupate kupona Yesu Kristo wa Nazareti..
Baba ukatamalaki  kwenye maisha yetu,Baba na  Uatamie watoto wetu na familia zetu..ukawalinde watoto wetu na kuwaongoza katika ujana wao,Masomo yao na wapate kuelewa na kukumbuka yote wanayofundishwa..wawe na kiu ya kutaka kukujua Mungu zaidi..
Mfalme wa Amani tunaomba utusamehe pale tulipoenda kinyume nawe..Tunajinyenyekeza mbele zako Baba wa Mbinguni..nasi utupe Neema ya kuweza kuwasamehe waliotukosea..
Yahweh..!!Tunaomba ukawaguse/kuwaponya wote wanaopitia Magumu/Majaribu, Wenye Shida/Tabu,Wagonjwa,Wafiwa wakawemfariji wao..Ukawafungue waliokuwa katika vifungo mbalimbali na wapate kupona kimwili na kiroho..

Baba utajaalie Hekima,Busara na Roho Mtakatifu akatuongoze kwenye kunena/kutenda,kuamua,kutambua/kujitambua..tukawe barua njema na tusomeke..ukatufanye chombo chako na tukatumike sawasawa na mapenzi yako..


Asante kwa yote Jehovah...!!Tunayaweka maisha yetu mikononi mwako..Tunashukuru na kukusifu,Tukiamini wewe ni Mungu wetu na Mlinzi wetu..Leo na hata milele..
Amina.



Mungu wa amani awakamilishe katika kila tendo jema ili mtekeleze matakwa yake; yeye na afanye ndani yetu kwa njia ya Kristo yale yanayompendeza mwenyewe. Utukufu uwe kwake, milele na milele! Amina.[Waebrania 13:21]

Mose na Aroni mbele ya Farao

1Baadaye, Mose na Aroni walimwendea Farao, wakamwambia, “Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli anasema hivi, ‘Waache watu wangu waondoke, wakanifanyie sikukuu jangwani.’” 2Lakini Farao akawauliza, “Ni nani huyo Mwenyezi-Mungu, hata nimsikilize na kuwaacha Waisraeli waondoke? Mimi simtambui huyo Mwenyezi-Mungu, wala sitawaruhusu Waisraeli waondoke.” 3Mose na Aroni wakamwambia, “Mungu wa Waebrania amekutana nasi. Tunakusihi utuache twende zetu jangwani mwendo wa siku tatu tukamtambikie Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu. La sivyo, yeye atatuua kwa maradhi mabaya au vita.” 4Lakini mfalme wa Misri akawajibu, “Enyi Mose na Aroni, kwa nini mnajaribu kuwatoa watu kazini mwao? Rudini kazini mwenu.” 5Tena Farao akasema, “Hawa watu wenu ni wengi kuliko wananchi; mnataka waache kufanya kazi!”
6Siku hiyohiyo Farao aliwaamuru wanyapara pamoja na wasimamizi, akasema, 7“Tangu leo msiwape watu hawa nyasi za kutengenezea matofali kama ilivyo kawaida. Wao wenyewe watakwenda kujitafutia. 8Lakini idadi ya matofali yanayotengenezwa kila siku iwe ileile, wala lisipungue hata tofali moja, kwa kuwa watu hawa ni wavivu ndio maana wanapiga kelele: ‘Tuache twende tukamtambikie Mungu wetu.’ 9Wazidishieni watu hawa kazi ngumu ili waitolee jasho na kuacha kusema maneno ya uongo.”
10Basi, wanyapara na wasimamizi wa watu wakatoka na kuwaambia watu, “Farao anasema hivi, ‘Sitawapeni nyasi. 11Nendeni nyinyi wenyewe mkatafute popote mtakapoweza kuzipata, na wala kazi yenu haitapunguzwa hata kidogo.’” 12Basi, watu wote wakatawanyika kila mahali nchini Misri wakitafuta nyasi za kutengenezea matofali. 13Nao Wanyapara wakakazana wakisema, “Timizeni kazi yenu ya kila siku kama hapo awali mlipoletewa nyasi.” 14Wanyapara Wamisri wakawapiga wasimamizi wa Waisraeli waliochaguliwa kusimamia kazi wakisema, “Kwa nini hamtimizi kazi yenu na kufikisha idadi ileile ya matofali kama awali?”
15Ndipo wasimamizi wa Waisraeli walipomwendea Farao, wakamlilia wakisema, “Kwa nini unatutenda hivi sisi watumishi wako? 16Hatupewi tena nyasi zozote na huku tunalazimishwa kufyatua matofali. Tena sisi watumishi wako tunapigwa, hali kosa ni la watu wako.” 17Lakini Farao akasema, “Wavivu nyinyi; nyinyi ni wavivu, ndio maana mnasema, ‘Tuache twende tukamtambikie Mwenyezi-Mungu’. 18Nendeni sasa mkafanye kazi; maana hamtapewa nyasi zozote na mtafyatua idadi ileile ya matofali.” 19Basi, hao wasimamizi wa Waisraeli sasa walijiona kuwa wako taabuni, kwani waliambiwa, “Hamtaipunguza kamwe idadi ya matofali ya kila siku.”
20Walipoondoka kwa Farao, walikutana na Mose na Aroni ambao walikuwa wanawangojea. 21Basi, wakawaambia Mose na Aroni, “Mwenyezi-Mungu na aone jambo hili na kuwahukumu nyinyi kwa sababu mmetufanya sisi kuwa chukizo kwa Farao na maofisa wake; nyinyi mmewapa sababu ya kutuua.”

Mose anamlalamikia Mwenyezi-Mungu

22Kisha Mose akamgeukia tena Mwenyezi-Mungu, akasema, “Ee Mwenyezi-Mungu, kwa nini unawatendea watu hawa uovu? Kwa nini hata ulinituma? 23Tangu nilipokwenda na kuongea na Farao kwa jina lako, yeye amewatendea uovu watu hawa. Wewe hujafanya lolote kuwakomboa watu wako.”

Kutoka5;1-23

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)
"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Tuesday 4 April 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 4...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Ni siku nyingine tena Mungu wetu,Muumba wetu,Muumba Mbingu na Nchi,Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo..Muweza wa yote,Yahweh...!!

Jehovah...!!!!Mungu asiye lala wala kusinzia,Mungu anayejibu,Mungu anayetenda,Anaye sikia,Yeye akisema ndiyo nani aseme habana?
Tumtegemee yeye daima kamwe hatotuacha.. Yeye ni mwanzo nayeye ni mwisho..Hakuna linaloshindikana kwakwe,ukimtumainia yeye,Ukifuata njia zake.. Atakutendea na kukujibu...Yeye atosha..!



Mungu si mtu, aseme uongo, wala si binadamu, abadili nia yake! Je, ataahidi kitu na asikifanye, au kusema kitu asikitimize?[Hesabu 23:19]


Asante Baba wa Mbinguni kwa Neema/Rehema hii.. Umetuchakugua na kutupa kibali cha kuendelea kuiona siku hii..Tazama Jana imepita Baba Leo ni siku mpya Kesho ni siku nyingine...!!!! Tunaomba utubariki katika maisha yetu..Mfalme wa Amani Ubariki Tuingiapo/Tutokapo,Vyombo vya usafiri,tutembeapo hatua zetu ziwe nawe Yahweh..!!
Ukabariki kazi zetu,Biashara,Masomo na vyote tunavyoenda Kugusa/kutumia Baba ukavitakase na Damu ya mwanao Bwana na mwokozi wetu Yesu Kristo..
Baba ukatutakase miili yetu na Akili zetu..Roho Mtakatifu akatuongoze katika Kunena/kutenda,kuamua,kutambua/kujitambua..
Baba tukawe chombo chema na tukatumike sawasawa na mapenzi yako..

Tunakwenda kinyume na Mwovu,Nguvu za giza,nguvu za mapepo,Nguvu za mizimu,Nguvu za mpinga Kristo..Tunajifunika na Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo wa Nazareti..yeye aliteseka ili sisi tupate kupona..


Baba utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe,Nasi tunaomba utupe Neema ya kuweza kuwasamehe waliotukosea..
Mfalme wa Amani tunaomba ukawaguse na kuwaponya wote wanaopitia magumu/majaribu,shida/tabu,wagonjwa,wafiwa wakawe mfariji wao,wenye vifungo mbalimbali Baba ukawafungue wapate kupona kimwili na kiroho pia..

Mfalme wa Amani tunaiweka Nchi hii tunayoishi mikononi mwako... Ukaibariki na kutubariki wote tunaoshi hapa..Ukailinde na ukatulinde wote tunaoishi hapa..
Baba wa mbinguni tunaiweka Tanzania na watanzania wote  mikononi mwako, ukawe mlinzi mkuu Yahweh.. Baba Afrika iwe mikononi mwako..Baba Dunia yote wewe ukawe Mtawala mkuu..
Baba ukawape ufahamu na kuwaongoza wanaotuongoza wakatuongoze katika haki na kweli..

Mwenyezi-Mungu asipoijenga nyumba, waijengao wanajisumbua bure. Mwenyezi-Mungu asipoulinda mji, waulindao wanakesha bure.[Zaburi 127:1]

Tunashukuru na kulisifu Jina Lako Daima..Tunajinyenyekeza na kujiachilia mikononi mwako Mungu wetu..Tunarudisha Shukrani na tukiamini wewe ni Mungu wetu na maisha yetu yapo mikononi mwako..
Sifa na utukufu ni kwako..Leo kesho na hata milele..
Amina..!!!
Mungu awabariki.


Mose apewa uwezo wa kufanya miujiza

1Mose akamwambia Mungu, “Lakini Waisraeli hawataniamini wala kunisikiliza, bali watasema kuwa wewe Mwenyezi-Mungu hukunitokea.” 2Hapo Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Unashika nini mkononi mwako?” Mose akamwambia, “Fimbo.” 3Mwenyezi-Mungu akamwambia, “Itupe chini.” Mose akaitupa fimbo chini, nayo ikageuka kuwa nyoka! Mose akaikimbia. 4Lakini Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Nyosha mkono wako, umkamate mkia!” Mose akanyosha mkono wake, akamkamata; nyoka akageuka tena kuwa fimbo mkononi mwake. 5Mwenyezi-Mungu akamwambia, “Hivyo Waisraeli watapata kuamini kuwa mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wa baba zao, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo, nimekutokea.”
6Tena, Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Ingiza mkono wako kifuani mwako.” Mose akafanya hivyo, lakini alipoutoa nje, kumbe ukawa na ukoma; mweupe kama theluji. 7Kisha Mungu akamwambia, “Ingiza tena mkono wako kifuani mwako!” Mose akauingiza mkono wake kifuani. Na alipoutoa nje, kumbe ukarudia hali yake ya kawaida kama ulivyo mwili wake. 8Mungu akamwambia Mose, “Wasipokuamini au kusadiki ishara ya kwanza, yawezekana wakaamini ishara ya pili. 9Lakini wasipoamini hata ishara hizi mbili, au kuamini maneno yako, utachota maji ya mto Nili na kuyamwaga juu ya nchi kavu. Maji hayo yatakuwa damu juu ya nchi kavu.”
10Lakini Mose akamwambia Mwenyezi-Mungu, “Ewe Bwana wangu, mimi sina ufasaha wa kuongea tangu zamani; hata baada ya wewe kusema nami mtumishi wako. Ulimi wangu ni mzito.” 11Hapo Mwenyezi-Mungu akamwuliza, “Ni nani aliyeumba kinywa cha mtu? Ni nani amfanyaye mtu kuwa bubu au kiziwi? Aone au awe kipofu? Je, si mimi Mwenyezi-Mungu? 12Basi, nenda! Mimi nitakiongoza kinywa chako na kukufundisha cha kusema.”
13Lakini Mose akasema, “Ee Bwana wangu, tafadhali nakusihi, umtume mtu mwingine.” 14Ndipo hasira ya Mungu ilipowaka dhidi ya Mose, akamwambia, “Je, si yuko ndugu yako Aroni ambaye ni Mlawi? Najua yeye ana ufasaha wa kuongea. Tena anakuja kukutana nawe, na mara tu atakapokuona atafurahi moyoni. 15Wewe utaongea naye na kumwambia yote atakayosema. Mimi nitawasaidieni na kuwafundisha mambo mtakayofanya. 16Aroni ataongea na Waisraeli kwa niaba yako. Yeye atakuwa msemaji wako, nawe utakuwa kama Mungu kwake. 17Utaichukua mkononi mwako fimbo hii ambayo utaitumia kufanya zile ishara.”
Mose anarudi Misri

18Mose alirudi kwa Yethro, baba mkwe wake, akamwambia, “Tafadhali niruhusu nirudi Misri kwa ndugu zangu, nikaone kama bado wako hai.” Yethro akamwambia, “Nenda kwa amani.”
19Mose akiwa bado nchini Midiani, Mwenyezi-Mungu akamwambia, “Rudi Misri kwa sababu wale wote waliotaka kukuua wamekwisha kufa.” 20Basi, Mose akamchukua mkewe na watoto wake, akawapandisha juu ya punda, akaanza safari ya kurudi Misri. Mkononi mwake alichukua ile fimbo aliyoamriwa na Mungu aichukue.
21Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Utakapofika Misri, hakikisha kwamba umetenda mbele ya Farao miujiza yote niliyokupa uwezo kuifanya. Lakini mimi nitaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu, naye hatawaachia Waisraeli waondoke. 22Nawe utamwambia Farao kuwa Mwenyezi-Mungu asema hivi, ‘Israeli ni mzaliwa wangu wa kwanza wa kiume! 23Taz Kut 12:29 Nami nakuambia: Mwache mwanangu aondoke, ili anitumikie! Kama ukikataa kumwachia aondoke, tazama nitamuua mzaliwa wako wa kwanza wa kiume.’”
24Akiwa bado njiani kurudi Misri, Mose alikuwa mahali pa kulala wageni; basi, Mungu alikutana naye na kutaka kumuua. 25Hapo Zipora akakimbia haraka, akachukua jiwe kali, akalikata govi la mwanawe na kumgusa nalo Mose miguuni akisema, “Wewe ni bwana harusi wa damu”. 26Hapo Mwenyezi-Mungu akamwacha Mose. Zipora alikuwa amesema, “Bwana harusi wa damu,” kwa sababu ya kutahiri.
27Mwenyezi-Mungu akamwambia Aroni, “Nenda jangwani ukakutane na Mose.” Basi, Aroni akaenda, akakutana na Mose kwenye mlima wa Mungu, akambusu. 28Naye Mose akamwambia Aroni maneno yote aliyoambiwa na Mwenyezi-Mungu ayaseme, na miujiza yote aliyoagizwa atende. 29Kisha Mose na Aroni wakaenda, wakawakusanya wazee wote wa Waisraeli. 30Aroni akawaambia maneno yote Mwenyezi-Mungu aliyokuwa amemwagiza Mose, na kuifanya ile miujiza mbele ya watu wote. 31Watu wakaamini. Na waliposikia kwamba Mwenyezi-Mungu amewajia kuwasaidia Waisraeli, na kwamba ameyaona mateso yao, wote wakainamisha vichwa vyao na kumwabudu.

Kutoka4;1-31

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)
"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 3 April 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 3...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tuanze na Mungu katika siku/wiki hii,Tumshukuru kwa yote mema aliyotutendea/anayotundea...Yeye ndiye aliyetupa kibali cha kuiona leo hii..Yeye alituchagua sisi kuendelea kuiona siku hii..Yeye ni Muumba wetu na Muumba mbingu na Nchi,Yeye awezaye yote akisema ndiyo nani aseme hapana,Yeye ni Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo..Yeye atupeae ridhiki zetu na yeye tunaomba azibariki ziingiapo/zitokapo..
Upendo,Furaha,Amani, wema na Fadhili zipo kwake..




Namngojea Mungu peke yake kwa utulivu; kwake naliweka tumaini langu. Yeye peke yake ndiye mwamba na wokovu wangu, yeye ni ngome yangu, sitatikisika. Wokovu na fahari yangu vyatoka kwa Mungu; mwamba wangu mkuu na kimbilio langu ni Mungu. Enyi watu, mtumainieni Mungu daima; mfungulieni Bwana yaliyo moyoni mwenu. Mungu ndiye kimbilio la usalama wetu. Binadamu wote ni kama pumzi tu; wote, wakubwa kwa wadogo, hawafai kitu. Tena ukiwapima uzito hawafikii kilo, wote pamoja ni wepesi kuliko pumzi. Msitegemee dhuluma, msijisifie mali ya wizi; kama mali zikiongezeka, msizitegemee. Mungu ametamka mara moja, nami nimesikia tena na tena: Kwamba enzi ni mali yake Mungu; naam, nazo fadhili ni zake Bwana; humlipa kila mtu kadiri ya matendo yake.


Asante Mungu Baba wa Mbinguni kwa nafasi hii..Tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza na kujiachilia mikononi mwako..Tukiomba na kulisifu jina lako lilo kuu..Mungu Baba tunaomba utubariki Tuingiapo/Tutokapo,Vyombo vya usafiri,tutembeapo hatua zetu ziwe nawe Yahweh..Baba ukabariki kazi zetu,Biashara,Masomo na vyote tunavyoenda kugusa/kutumia ukavitakase kwa Damu ya mwanao Bwana wetu na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti aliteseka ili sisi tupate kupona..Roho Mtakatifu akatuongoze kwenye kunena/kutenda, tupate kujitambua/kutambua..
Baba tunaomba utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe..
nasi utupe Neema ya kuweza kusameheana..
Jehovah...! uwaponye wote wanaopitia Magumu,Majaribu, Shida/Tabu,Wagonjwa,Wafiwa ukawe mfariji wao,Baba tazama walio magerezani pasipo na hatia,pia waliofungwa na mwovu..tunaomba ukawaguse na kuwaponya kimwili na kiroho..
Sema nasi Baba..!!Sema na mioyo yetu Baba..!!Sema nasi tupate kupona..!!



Ilikuwa jioni ya siku hiyo ya Jumapili. Wanafunzi walikuwa wamekutana pamoja ndani ya nyumba, na milango ilikuwa imefungwa kwa sababu waliwaogopa viongozi wa Wayahudi. Basi, Yesu akaja, akasimama kati yao, akawaambia, “Amani kwenu!” Alipokwisha sema hayo, akawaonesha mikono yake na ubavu wake. Basi, hao wanafunzi wakafurahi mno kumwona Bwana. Yesu akawaambia tena, “Amani kwenu! Kama vile Baba alivyonituma mimi, nami nawatuma nyinyi.” Alipokwisha sema hayo, akawapulizia na kuwaambia, “Pokeeni Roho Mtakatifu. Mkiwasamehe watu dhambi zao, wamesamehewa; msipowasamehe, hawasamehewi.” Thoma, mmoja wa wale kumi na wawili (aitwaye Pacha), hakuwa pamoja nao wakati Yesu alipokuja. Basi, wale wanafunzi wengine wakamwambia, “Tumemwona Bwana.” Thoma akawaambia, “Nisipoona mikononi mwake alama za misumari na kutia kidole changu katika kovu hizo, na kutia mkono wangu ubavuni mwake, sitasadiki.” Basi, baada ya siku nane hao wanafunzi walikuwa tena pamoja mle ndani, na Thoma alikuwa pamoja nao. Milango ilikuwa imefungwa, lakini Yesu akaja, akasimama kati yao, akasema, “Amani kwenu!” Kisha akamwambia Thoma, “Lete kidole chako hapa uitazame mikono yangu; lete mkono wako ukautie ubavuni mwangu. Usiwe na mashaka, ila amini!” Thoma akamjibu, “Bwana wangu na Mungu wangu!” Yesu akamwambia, “Je, unaamini kwa kuwa umeniona? Heri yao wale ambao hawajaona, lakini wameamini.” Yesu alifanya mbele ya wanafunzi wake ishara nyingine nyingi ambazo hazikuandikwa katika kitabu hiki. Lakini hizi zimeandikwa ili mpate kuamini kwamba Yesu ni Kristo, Mwana wa Mungu; na kwa kuamini mpate kuwa na uhai kwa nguvu ya jina lake.
Tunarudisha Shukrani na Utukufu ni kwao..Tunayaweka haya yote mikononi mwako Baba yetu..Tukiamini wewe ni Bwana na Mwokozi wetu,Leo na Hata milele..!!
Amina.
Mungu ni Pendo.

Mungu anamwita Mose

1Siku moja, Mose alikuwa anachunga kundi la kondoo la baba mkwe wake, Yethro, kuhani wa Midiani. Mose alilipeleka kundi hilo upande wa magharibi wa jangwa, akaufikia mlima Horebu,3:1 Horebu: Jina lingine la mlima Sinai. Hapa waitwa mlima wa Mungu, kwani Mungu atajidhihirisha hapa; Taz sura 19. mlima wa Mungu. 2Basi, malaika wa Mwenyezi-Mungu akamtokea katika mwali wa moto katikati ya kichaka. Mose akaangalia, akashangaa kuona kichaka kinawaka moto na wala hakiungui. 3Basi, akajisemea, “Hiki ni kioja! Kichaka kuwaka moto na kisiungue? Hebu nitazame vizuri.”
4Mwenyezi-Mungu alipoona kwamba Mose amegeuka kukiangalia kichaka, akamwita pale kichakani, “Mose! Mose!” Mose akaitika, “Naam! Nasikiliza!” 5Mwenyezi-Mungu akamwambia, “Usije karibu! Vua viatu vyako kwa sababu mahali unaposimama ni mahali patakatifu.” 6Kisha Mungu akamwambia, “Mimi ndimi Mungu wa baba yako; Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, Mungu wa Yakobo.” Mose akaufunika uso wake kwa kuwa aliogopa kumwangalia Mungu.
7Kisha Mwenyezi-Mungu akamwambia, “Nimeyaona mateso ya watu wangu walioko nchini Misri na nimekisikia kilio chao kinachosababishwa na wanyapara wao. Najua mateso yao, 8na hivyo, nimeshuka ili niwaokoe mikononi mwa Wamisri. Nitawatoa humo nchini na kuwapeleka katika nchi nzuri na kubwa; nchi inayotiririka maziwa na asali,3:8 nchi inayotiririka maziwa na asali: Ni nchi yenye rutuba na wingi wa mifugo (maziwa) na mavuno (asali). nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi. 9Naam, kilio cha Waisraeli kimenifikia; nimeona jinsi Wamisri wanavyowatesa. 10Sasa, nitakutuma kwa Farao ili uwatoe watu wangu, watu hao wa Israeli, kutoka nchini Misri.”
11Lakini Mose akamwambia Mungu, “Mimi ni nani hata nimwendee Farao na kuwatoa Waisraeli nchini Misri?” 12Mungu akamwambia, “Mimi nitakuwa pamoja nawe. Utawatoa watu wa Israeli na kuja kuniabudu mimi Mungu juu ya mlima huu. Hiyo itakuwa ishara kwamba ni mimi Mungu niliyekutuma wewe.”
13 Taz Kut 6:2-3 Hapo, Mose akamwambia Mungu, “Sasa, nikiwaendea Waisraeli na kuwaambia, ‘Mungu wa babu zenu amenituma kwenu,’ nao wakiniuliza, ‘Jina lake ni nani,’ nitawaambia nini?” 14Taz Ufu 1:4,8 Mungu akamjibu, “MIMI NDIMI NILIYE.3:14 MIMI NDIMI NILIYE: Au, NIKO KAMA NILIVYO au NITAKUWA KAMA NITAKAVYOKUWA. Waambie hivi watu wa Israeli: Yule anayeitwa, NDIMI NILIYE, amenituma kwenu. 15Waambie hivi Waisraeli: Mwenyezi-Mungu,3:15 Tafsiri hii mpya ya Kiswahili kila mara jina la Kiebrania Yahweh linapotumika limewekwa katika Kiswahili jina la kawaida la Mungu kama anavyotajwa katika lugha yetu, yaani, Mwenyezi-Mungu. Mungu wa babu zenu, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, Mungu wa Yakobo, amenituma kwenu. Hili ndilo jina langu milele, na hivyo ndivyo nitakavyokumbukwa katika vizazi vyote. 16Nenda ukawakusanye wazee wa Israeli na kuwaambia: Mwenyezi-Mungu, Mungu wa babu zenu: Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, Mungu wa Yakobo, amenitokea na kusema, ‘Nimewachunguzeni na kuyaona mambo mnayotendewa nchini Misri! 17Naahidi kuwa nitawatoa katika mateso yenu huko Misri na kuwapeleka katika nchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi; nitawapeleka katika nchi inayotiririka maziwa na asali.’
18“Wao watakusikiliza, nawe pamoja na wazee wa Waisraeli mtamwendea mfalme wa Misri na kumwambia, ‘Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Waebrania, ametutokea. Sasa, uturuhusu tuende safari ya mwendo wa siku tatu jangwani, tukamtambikie Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu.’ 19Najua kuwa mfalme wa Misri hatawaacha mwende asipolazimishwa kwa mkono wenye nguvu. 20Kwa hiyo nitaunyosha mkono wangu na kuipiga nchi ya Misri kwa maajabu ambayo nitayafanya huko. Baadaye mfalme atawaacha mwondoke. 21Taz Hek 10:17 Tena nitahakikisha Wamisri wanawapendelea Waisraeli, na mtakapoondoka Misri, hamtatoka mikono mitupu. 3:21 Taz Kut 12:35-36 22Kila mwanamke Mwebrania atamwomba jirani yake Mmisri, au mgeni wake aliye nyumbani kwake, ampe vito vya fedha na dhahabu pamoja na nguo. Hivyo mtawavisha watoto wenu wa kiume na wa kike. Ndivyo mtakavyowapokonya Wamisri mali yao.”

Kutoka3;1-21

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)
"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.