Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 27 June 2012

SHEREHE YA SENDOFF YA DORIS KASAKA (KAPINGA) ILIVYOFANA USIKU WA JANA NDANI YA DELUXE HALL SINZA!!!!!!!!!!


Doris Kasaka (Kushoto) akiwa na mpambe wake jana ndani ya Deluxe Hall Sinza wakati wa sherehe ya kumuaga (Sendoff) na kumpongeza kwa kufanya maamuzi mazuri.

Mama Mkubwa wa Doris Mama Angelina Mwami akiwakaribisha wageni wakati wa sherehe ya Binti yake ndani ya ukumbi wa Deluxe Sinza.

Baba Mkubwa wa Doris Mzee Njelu Kasaka akiwakaribisha wageni katika sherehe ya kumuaga Binti yake ndani ya Ukumbi wa Deluxe Sinza jana usiku.

Meza kuu ya wazazi wa Doris kutoka kulia ni Mama Njelu Kasaka, Mzee Njelu Kasaka, Dr Mwami na mwisho kushoto ni Mama Mwami.
Doris akipiga picha ya kumbukumbu na wafanyakazi wenzake kutoka Zantel.


"Swahili na Waswahili" Tunakutakia Safari njema na kila lililo jema na Maandalizi mema ya Ndoa.


Pamoja sana KapingaZ!!!!!!!



Watoto na Malezi-Tatizo la Ndoa za Watoto;Pata Video!!!!!!!

Waungwana "WATOTO NA MALEZI".
Wazazi/Walezi leo Tuangalie NDOA ZA UTOTONI.


Kwanza nikuulize swali;Jee wewe ulilazimishwa kuolewa/Kuoa?jee Mume/Mke uliyenaye ni chaguo lako? .Jee wewe Umekeketwa?.


Sasa turudi kwa Watoto wetu ndugu zetu,wadogo zetu,Jee unafikiri kukeketwa kunawafaa?
Jee Unaushauri,Maoni,Ujumbe gani kwa Wazazi/Walezi na Jamii kwa ujumla kuhusina na Ndoa hizi za Watoto?.


Karibuni sana Tuelimishane kwa Upendo.
"SWAHILI na WASWAHILI" Pamoja sana.

Tuesday 26 June 2012

DORIS KASAKA (KAPINGA) AMEREMETA KWENYE KITCHEN PARTY YAKE ILIYOFANYIKA KWENYE UKUMBI WA TBS - UBUNGO !!!!!!


Doris akiwa katika pozi mwanana huku akiwaangalia wageni waalikwa waliokuja kumpongeza katika KITCHEN PARTY yake 
Doris akiwa mbele ya wageni waalikwa ukumbini kabla ya kuanza sherehe yake ya KITCHEN PARTY yake .

Mama Mkubwa wa Doris, Angelina Mwami (Kapinga) akiwakaribisha wageni waalikwa na kuwashukuru kwa kufika kwao kwenye sherehe ya KITCHEN PARTY ya Binti yake mpendwa.

Mama Mkubwa wa Doris kwa upande wa Baba, Mama Njelu Kasaka naye hakuwa nyuma kumpongeza binti yake na kuwakaribisha wageni waalikwa wote waliokuja kwenye sherehe ya KITCHEN PARTY.
Mama Mchungaji naye alifungua sherehe ya KITCHEN PARTY ya Doris kwa Sala nzuri na kukemea mapepo yote yenye nia mbaya "YASHINDWE NA YALEGEE"
KEKI YA AINA YAKE ILIYOANDALIWA KIUSTADI NA UTAALAM ALIYOANDALIWA DORIS.

Doris akikata Keki yake ya KITCHEN PARTY ikiwa ni ishara ya upendo kwa wageni wote walioshiriki katika sherehe hiyo na kula nao pamoja


Swahili NA Waswahili tunakutakia kila lililojema,Tunasubiri mnuso wa kuagwa na Ndoa.

Monday 25 June 2012

Da'Rahifah Jamaldin Atimiza Mwaka Mmoja!!!!!!!!!

Mwenyewe  da'Rahifah!!
Akitafakari aanzie wapi kuikata keki!!!
Dada na Kakazz, Wapambe muhimu
Hehehheeh!!! kweli kulea kazi, kaka mtu Bob Malikh yupo bithe kumtengeneza dada yake
Baharia Malikh ..Leo lazima kitakaa hiki, kinanichezea mie ?Dada naye katulia mpaka macho kafumba,utafanyaje na kaka kasema?Hahahahah watu wa Ilala mbona mtakatwa mitama mkimsogelea huyu binti,Chezeya wewe Mchezaji wa kulipwa wa BOMU..............

Baba na mwana,Pole da'Sulhiya[mama mtoto] yeye alikuwa mpiga picha siku hiyo,hatukupata picha yake.
Wakisikiliza Nasaha kutoka  kwa Wazazi  hahahaha
                                                         Dada Rahifah, Akiwashukuru Wazazi,Ndugu, Jamaa na Marafiki.


Da'Rahifah Tunakutakia kila lililojema,Baraka, Amani,Upendo na Makuzi mema.Uwe Baraka kwa Wazazi na Watu wote.
Hongereni sana Bibi na Bwana Jamal.M.Jamaldin[Minanasi].Kwakukuza, Mungu awape Hekima na Maarifa katika Malezi Yenu.


Swali la kizushi;Waungwana kuna aliye na picha za kutimiza mwaka  1-5?.
Au wewe Wazazi wako Hawakuweka Kumbukumbu,Hawakuwa na Tamaduni hizi za mambo ya siku kuu yako ya kuzaliwa?


"Swahili NA Waswahili" Karibuni Wooote!!!!!!

Sunday 24 June 2012

Nawatakia J'Pili Njema,Burudani-Rose Muhando: Pasipo Maono,Ndivyo Ulivyo na Woga wako....!!!!!!

Nawatakia J'Pili yenye Amani,Upendo na Baraka.
Maana ninyi,ndugu,mliitwa mpate uhuru;Kakini uhuru wenu usiwe sababu ya kuufuata mwili,bali tumikianeni kwa Upendo.Neno la Leo;Wagalatia:5:13-26.

Mungu atubariki sote!!!!!!

Saturday 23 June 2012

Chaguo la Mswahili Leo;DDC Mlimani Park na Tancut Almasi!!!!!!!!!

Waungwana "CHAGUO LA MSWAHILI LEO"
Turudi Nyuma kidogo Tuangalie/Tusikilize Nyimbo hizi kutoka kwenye Bendi zetu..
Jee unauonaje Mziki wa Bendi za sasa na Zamani?
Karibuni sana katika Yote!!!!!
"Swahili NA Waswahili" Twende Soteeeeeee.

Jikoni Leo;Tupike Pamoja, Video Mpya-How to cook Donuts [in Swahili]!!!!!!!

Waungwana "JIKONI LEO"
Ni "TUPIKE PAMOJA" Wametoa Video mpya Jinsi ya Kupika Donuts.kama una Swali,Ushauri Usisite kuwasiliana nao kupitia.www.tupikepamoja.com.

"SWAHILI na WASWAHILI"
Pamoja Sana!!!!!

Thursday 21 June 2012

Watoto na Malezi;Violence Against Children [Ukatili Kwa Watoto]!!!!!!!


Makala hii inaonyesha ukatili dhidi ya watoto na jitihada zinazofanywa na serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto pamoja na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii wakishirikiana na wadau mbalimbali kutokomeza ukatili dhidi ya watoto.

Makala hii imetengenezwa ikiwa ni mwitikio wa hali ya unyanyasaji na ukatili ambayo watoto wanakabiliana nayo. Makala hii imeandaliwa sambamba na uzinduzi wa ripoti ya ukatili kwa watoto ambalo ni agizo la Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kutokomeza ukatili kwa watoto. Ripoti hii ilizinduliwa na Dr. Asha Rose Migiro, Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.

Waungwana;Wazazi/Walezi Mnamaoni,Ushaurigani katika haya?


Shime Wazazi/Walezi;"Tutokomeze Ukatili  kwa watoto" Tuungane Pamoja katika kuwapenda,kuwatunza,kuwapa Malezi bora,kuwapatia Elimu na Kuwasikiliza.
"Mtoto wa mwenzio ni wako".
"SWAHILI na WASWAHILI" Pamoja sana!!!!

Wednesday 20 June 2012

RATIBA YA KUUAGA MWILI WA MAREHEMU WILLIAM FOFO MAPUNDA!!!!!





WILLIAM FOFO MAPUNDA (FOFO)

MWILI WA MAREHEMU WILLIAM FOFO MAPUNDA UTAAGWA RASMI LEO TAREHE 20/06/2012 NYUMBANI KWAKE TABATA KISUKULU TAYARI KWA KUPELEKWA NYUMBANI KWAO MANDA LUDEWA KWA MAZISHI, AMBAYO YATAFANYIKA KESHO TAREHE 21/06/2012 SIKU YA ALHAMISI.

RATIBA:

SAA 5.00 ASUBUHI: - MWILI KUWASILI NYUMBANI KWAKE TABATA KISUKULU

SAA 6.00 - 7.00 MCHANA: - CHAKULA KWA WOTE

SAA 7.00 - 8.30 MCHANA: - SALAMU ZA MWISHO (LAST RESPECT)

SAA 8.30 - 9.00 ALASIRI: - MWILI KUFIKA KANISANI (KANISA LA ANGLIKANA TABATA KISUKULU KARIBU NA BAR YA MAZDA)

SAA 9.00 - 10.30 JIONI: - IBADA NA KUAGA KWA WALE AMBAO WATAKUWA WAMECHELEWA NYUMBANI

SAA 10.30 JIONI: - KUANZA SAFARI YA KWENDA MANDA LUDEWA

WILLIAM FOFO MAPUNDA ALIFARIKI GAFLA USIKU WA KUAMKIA JANA NYUMBANI KWAKE TABATA KISUKULU, KWA TAARIFA TULIZOZIPATA KUTOKA KWA MADAKTARI WA HOSPITALI YA AMANA ILALA, KIFO CHAKE KIMESABABISHWA NA KUPATWA NA BLOOD PRESSURE GAFLA.

KWA TAARIFA YOYOTE PIGA NAMBA: 0713-254553

Tuesday 19 June 2012

TAARIFA YA MSIBA: WILLIAM FOFO MAPUNDA HATUNAYE TENA!!!!!!


Marehemu William Fofo enzi za uhai wake.

Taarifa ambazo zimetufikia hivi punde Ndugu yetu, Rafiki yetu William Fofo maarufu kwa jina la FOFO amefariki dunia usiku huu akiwa nyumbani kwake Tabata.

Taarifa kamili za sababu ya kifo chake bado hatujazipata, pindi tutakapozipata tutawajulisha, kwa sasa taratibu zote inaendelea nyumbani kwake Tabata na mwili wake umehifadhiwa katika Hospitali ya Amana Ilala Dar es salaam.

Monday 18 June 2012

Wa Afrika na Sherehe zao,LeoTupo Malawi ni-Kachitsa na Farayi;Tradditional Wedding!!!!


Mwenyewe bi Arusi Mtarajiwa,da'Farayi
Bwana Arusi Mtarajiwa kaka Willy Kachitsa,Huingii hapo mmpaka utoe pesa!!!
MmePendeza sana Wapendwa!!!!!
Mmmmhh Mapenzi Motomoto!!!!
Waungwana Leo Tupo Malawi, kaka KACHITSA na da'FARAYI wanatarajia kuwa mwili mmoja hivi karibuni.
Nasi tunawatakia kila lililojema katika maandalizi yao.Mungu asimamie kila hatua na Twasubiri kwa Hamu siku yenyewe!!!!!.

Waungwana; Sherehe hizi za WaAfrika zinafanana eehh? vipi kuhusu mambo ya kutoa pesa/Kufichua kabla ujaingia kwa wakwe na Mengine Meengi, Mila/Tamaduni za ndoa. zipi ninyi mnatumia/mlitumia?
 jee bado zina nguvu/Kufaa/Kufuatwa au mmezitupa?.

Jee wewe una Maoni ,Ushauri,gani kuhusu Tamaduni/Mila hizo nivyema kuzitunza na kuzifuata au Zimepitwa na Wakati?.

[To; Willy&farayi;May Good bless you!!!
We are still waiting for the big day!!
With Love From Isaac's Family.]


"SWAHILI na WASWAHLI"Pamoja sana!!!

Sunday 17 June 2012

Tumalize J'Pili vyema,Burudani-Anita John (Jehovah Jireh) swahili !!!!!!!!!

Waswahili wakisifu na Kuabudu,Da'Anita mwenye blauzi ya maua yenye pink
Natumaini mlikuwa na J'pili njema, Mungu azidi kuwabariki wooote!!!
Tumalizie siku na Zaburi ya 23:1-6;Bwana ndiye Mchungaji wangu,Sitapungukiwa na kitu!.!!!!!
Nawapenda Wooote.!
"SWAHILI na WASWAHILI"   Pamoja sana....

EXTRA BONGO WAZEE WA KIZIGO WAZIDI KULITIKISA JIJI NDANI YA MEEDA SINZA.




Ally Choki akiwaburudisha washabiki na wapenzi wa Extra Bongo ndani ya Meeda usiku wa kuamkia leo
Choki akichea show na wanenguaji wake wa Extra bongo ndani ya Meeda Sinza.
Banza Stone Mwana wa Masanja - AKA Jenerale akiimba nyimbo yake ndani ya Meeda Sinza.

Mmiliki wa KAPINGAZ Blog Henry Kapinga alikuwepo ndani ya Meeda Sinza, hapa akishoo luv na kuwapa Big Up Ally Choki na Banza Stone wakati Extra Bongo walipokuwa wanapamofu usiku wa kuamkia leo ndani ya ukumbi huo.
Rapa maarufu namba moja Afrika mashariki wa Extra Bongo Kaba Tano akirap ndani ya Meeda Sinza usiku wa kuamkia leo

Saturday 16 June 2012

Watoto na Kujifunza Lugha-Pata video ya Mtoto wetu Wa Burundi!!!!

Wazazi/Walezi hapo vipi?Leo sina Mengi nasubiri kutoka kwenu,Mjumbe Hauawiii!!!!"
SWAHILI na WASWAHILI "Pamoja sana!!!!!!!!!!

Friday 15 June 2012

Jikoni Leo;Tupike Pamoja-How to cook Russian salad (In Swahili)!!!!!!!

Waungwana; "JIKONI LEO;"Ni Tupike Pamoja wametoa Mapishi mapya ya Russian Salad,kwa njia ya Video.Lugha ni Kiswahili.
 Usikose kujifunza kupitia "TUPIKE PAMOJA" Mmmmmhh Tamu Saaaana.
Kuona mengi zaidi ingia;www.tupikepamoja.com au hapo pembeni kuna nembo yao bonyeza tuu.

 Pamoja sana Waungwana. "SWAHILI na WASWAHILI"

Thursday 14 June 2012

Siku Kama Ya Leo da'Rehema [RayK] Alizaliwa,Burudani-Hakunaga by Suma Lee!!!!

Mwenyewe RayK
Bibi na Bwana Kiwinga!!!!!
Uzuri tangu Utotoni,ya Kale ni Dhahabu
Siku kama ya Leo miaka kadhaa iliyopita da'Rehema Alizaliwa.Tunakutakia kila lililo jema katika Maisha yako,Mungu azidi kukulinda wewe na Familia yako.Uwe Baraka kwa watu woote.Tunakupenda na kukuthamini.
Asante kwa yooote,Hakunaga Wifi wa mimi Pamoja Daima.

Swali kwa Waungwana; Hivi nini kinasababisha Mtu na Wifi zake wasielewane?Wivu,Chuki,Tamaa au.......


Karibuni sana kwa Maoni,Mawazo,Ushauri na Kuelimishana kwa Upendo.

Angalizo; Wifi zangu Sitaki kujifunza Kuharibu Nyumba zenu Akuuu hahahhahhaahahah!!!!!!!

Hakunaga hakunaga hakunaaaaa hakunaaa"Swahili na Waswahili" Pamoja sana.

Wednesday 13 June 2012

TuMpigie Kura Christina SHUSHO;Viva Shusho Viva Tanzania!!!!!!!!

Waungwana;Tumpigieni Kura Christina Shusho aweze kupata tuzo ya Africa Gospel Music Award 2012
Jinsi ya kupiga kura nenda,
www.africagospelawards.com/nominate.html

VIVA SHUSHO, VIVA TANZANIA   "pamoja Tunaweza"

Waswahili Wetu Leo;Twiga Stars: Tanzania's Soccer Sisters,Wanawake Wanaweza!!!!

Waungwana "Waswahili Wetu Leo";
Leo tuwaangalie Wanawake Waswahili Wanaocheza Mpira wa Miguu.
Wanawake hawa Wanavipaji au Wanalazimisha kwasababu ya  Maisha Magumu?
Jee Umeona Wanayopitia mpaka kufikia hapo?Unafikiri Wazazi sasa ni Wakati wa Kuamka na Kutambua hakuna Michezo ya Wanawake au Wanaume?
Jee Wewe Unaushauri,Maoni Gani kwa Wachezaji wetu wa Kike?.

Wewe unapenda Mpira? au Michezo/Ni Mchezo gani unapendelea kuangalia au kuucheza/ulicheza?jee Unaumudu?

Karibuni sana Waungwana katika Yote.Kujua zaidi kuhusu timu hii ya Twiga Stars ingia;www.twigastars.com
 "Swahili na Waswahili" Pamoja sana!!!!!!!

Tuesday 12 June 2012

Habari kuhusu kaka Med-Mod[Mbuko]Hajafa Yupo Hospitalini,Tuzidi Kuombea!!

Waungwana Habari nilizozipata sasa hivi, kwamba kaka Mbuko hajafa,Yupo Hospitalini, Tuungane pamoja katika KuMuombea apate kupona haraka.Nitawajulisha kinachoendelea.Mungu azidi kukupigania kaka Mbuko.

Sunday 10 June 2012

Nawatakia J'Pili Yenye Furaha,Burudani;Kijitonyama Evangelical Choir !!!!!


Mshukuruni BWANA kwa kuwa ni mwema;kwa maana Fadhili zake niza Milele.

Mshukuruni Mungu wa Miungu;kwa maana Fadhili zake ni za milele.

Waungwana  muwe na J'pili yenye Baraka,Amani,Shukrani na Fadhili.
Neno la Leo;Zaburi136:1-26. "Swahili na Waswahili".Pamoja sana!!!!!

Mswahili wetu Leo;kaka Mod-Med[Mbuko]Raha Jipe mwenyewe!!!!!!

Mswahili Kaka Mbuko akijipa Raha mtaani Huko Holland[Uholanzi],Raha tele Tabu ya nini?

"Swahili na Waswahili" Pamoja sana!!!!


Saturday 9 June 2012

MASHUJAA MUSICA BENDI WAZIDI KUPAA NDANI YA BUSINESS CENTRE CHINI YA UONGOZI WA CHAZ BABA.




Kiongozi na mwimbaji wa Bendi maarufu wa Mashujaa Chaz Baba jana akizikonga nyoyo za mashabiki wake kwa nyimbo zake mpya ndani ya ukumbi wa Business Centre Maeneo ya makumbusho.
Mpiga tumba maarufu Afrika Mashariki wa Bendi ya Mashujaa MCD akipafomu ndani ya Business Centre jana Usiku.


Maua ya Mashujaa Band yakiwachengua mamia ya washabiki wao ndani ya Business centre jana usiku.

Bendi ya Mashujaa ni moja ya Bendi maarufu Nchini ambazo zinakuja juu katika medani ya muziki wa bendi na kuthamini thamani ya mwanamuziki.
habari zaidi utazipata.KapingaZBlog.

Asanteni.