Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 28 February 2019

Kikombe Cha Asubuhi ;Zaburi 71...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo..
Yahweh..!Jehovah..! Adonai..!Elohim..!El Olam..!El Qanna..!
El Elyon..!El shaddai..!Emanueli...!-Mungu pamoja nasi...
Unastahili sifa Mungu wetu,Unastahili kuabudiwa Jehovah,
Unastahili kuhimidiwa Yahweh,Unastahili Kutukuzwa Baba wa Mbinguni....!


Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Kutatokea chipukizi katika kisiki cha Yese, tawi litachipua mizizini mwake. Roho ya Mwenyezi-Mungu itakaa kwake, roho ya hekima na maarifa, roho ya shauri jema na nguvu, roho ya ujuzi na ya kumcha Mwenyezi-Mungu. Atafurahia kumcha Mwenyezi-Mungu. Hatahukumu kadiri ya mambo ya njenje, wala kuamua kufuatana na yale anayosikia.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizo zifanya
Kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Atawapatia haki watu maskini, atawaamulia sawasawa wanyonge nchini. Kwa neno lake ataiadhibu dunia, kwa tamko lake atawaua waovu. Haki itakuwa kama mkanda wa kujifunga, uaminifu utakaa naye kama mkanda kiunoni.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji

Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu Baba wa Mbinguni
tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe....


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,

watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka...
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahweh ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu...
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahwe tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu Baba wa Mbinguni tukanene yaliyo yako
ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho 
akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Mbwamwitu ataishi pamoja na mwanakondoo, chui watapumzika pamoja na mwanambuzi. Ndama na wanasimba watakula pamoja, na mtoto mdogo atawaongoza. Ngombe na dubu watakula pamoja, ndama wao watapumzika pamoja; na simba atakula majani kama ng'ombe. Mtoto mchanga atacheza kwenye shimo la nyoka mtoto ataweza kutia mkono shimoni mwa nyoka wa sumu. Katika mlima mtakatifu wa Mungu hakutakuwa na madhara wala uharibifu. Maana kumjua Mwenyezi-Mungu kutaenea pote nchini, kama vile maji yajaavyo baharini.
Tazama watoto wako wanaokutafuta/kukuomba kwa bidii na imani, Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,
wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukaonekane katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe Yahweh tunaomba ukawape neema ya kujiombea
Kufuata njia zako nazo zikawaweke huru
Ukawape macho ya rohoni ee Mungu wetu na masikio ya kusikia
sauti yako,Ukawaokoe na kuwalinda,ukawaponye kimwili na kiroho
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao,Amani ikatawale katika maisha yao,Upendo ukadumu kati yao...

Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako tukiamini Mungu wetu utawatendea sawasawa na mapenzi yako 
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
 Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwanami/kunisoma Mungu Baba aendelee
kuwabariki na kuwatendea kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na Upendo wa Mungu wa Mungu Baba ukae nanyi daima
Nawapenda.


Mungu tumaini la wazee
1Kwako ee Mwenyezi-Mungu, nakimbilia usalama;
kamwe usiniache niaibike!
2Kwa uadilifu wako uniokoe na kunisalimisha;
unitegee sikio lako na kuniokoa!
3Uwe mwamba wangu wa kukimbilia usalama,
ngome imara ya kuniokoa,
kwani wewe ni mwamba na ngome yangu.
4Niokoe, ee Mungu wangu, mikononi mwa waovu,
kutoka makuchani mwa wabaya na wakatili.
5Maana wewe Bwana u tumaini langu;
tegemeo langu ee Mwenyezi-Mungu, tangu ujana wangu;
6nimekutegemea tangu kuzaliwa kwangu,
ndiwe uliyenitoa tumboni mwa mama yangu.
Mimi nitakusifu wewe daima.
7Kwa wengi nimekuwa kioja,
lakini wewe u kimbilio langu imara.
8Kinywa changu kimejaa sifa zako,
na utukufu wako mchana kutwa.
9Wakati wa uzee usinitupe;
niishiwapo na nguvu usiniache.
10Maana maadui zangu wanasema vibaya juu yangu;
wanaovizia uhai wangu wanafanya mipango,
11na kusema: “Mungu amemwacha;
mfuateni na kumkamata,
kwani hakuna wa kumwokoa!”
12Usikae mbali nami, ee Mungu;
uje haraka kunisaidia, ee Mungu wangu.
13Wapinzani wangu wote waaibishwe na kuangamizwa;
wenye kutaka kuniumiza wapate aibu na fedheha.
14Lakini mimi nitakuwa na matumaini daima;
tena nitakusifu zaidi na zaidi.
15Kinywa changu kitatamka matendo yako ya haki,
nitatangaza mchana kutwa matendo yako ya wokovu
ijapokuwa hayo yanapita akili zangu.
16Nitataja matendo yako makuu, ee Bwana Mwenyezi-Mungu;
nitatangaza kuwa ndiwe mwadilifu peke yako.
17Ee Mungu, wewe umenifunza tangu ujana wangu;
tena na tena, natangaza matendo yako ya ajabu.
18Usiniache, ee Mungu, niwapo mzee mwenye mvi,
hata nivitangazie vizazi vijavyo nguvu yako.
19Nguvu na uadilifu wako, ee Mungu,
vyafika mpaka mbingu za juu.
Wewe umefanya mambo makuu mno.
Ee Mungu, ni nani aliye kama wewe?
20Umenifanya nione taabu nyingi ngumu,
lakini utanirudishia tena uhai,
wewe utaniinua tena kutoka huko chini.
21Utaniongezea heshima yangu,
na kunifariji tena.
22Nitakusifu pia kwa kinubi,
kwa sababu ya uaminifu wako, ee Mungu wangu;
nitakuimbia sifa kwa zeze, ewe Mtakatifu wa Israeli.
23Nitapaza sauti kwa furaha,
ninapokuimbia wewe sifa zako,
na roho yangu itakusifu maana umeniokoa.
24Nitatamka uadilifu wako mchana kutwa,
maana waliotaka kuniumiza wameaibishwa na kufedheheshwa.



Zaburi71;1-24

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Wednesday 27 February 2019

Kikombe Cha Asubuhi ;Zaburi 70...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Maana ujumbe kuhusu kifo cha Kristo msalabani ni jambo la kipumbavu kwa wale walio katika mkumbo wa kupotea, lakini kwetu sisi tulio katika njia ya wokovu, ujumbe huo ni nguvu ya Mungu. Maana Maandiko Matakatifu yasema: “Nitaiharibu hekima yao wenye hekima, na elimu ya wataalamu nitaitupilia mbali.” Yu wapi basi, mwenye hekima? Yu wapi basi, mwalimu wa sheria? Naye bingwa wa mabishano wa nyakati hizi yuko wapi? Mungu ameifanya hekima ya ulimwengu kuwa upumbavu.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizo zifanya
Kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Maana, kadiri ya hekima ya Mungu, watu hawawezi kumjua Mungu kwa njia ya hekima yao wenyewe. Badala yake, Mungu amependa kuwaokoa wale wanaoamini kwa njia ya kile ambacho wenye hekima wanakiona kuwa ni upumbavu, yaani ujumbe tunaohubiri. Wayahudi wanataka ishara, na Wagiriki wanatafuta hekima; lakini sisi tunamhubiri Kristo aliyesulubiwa. Kwa Wayahudi jambo hili ni kikwazo, na kwa watu wa mataifa ni upumbavu; lakini kwa wale walioitwa, Wayahudi kwa Wagiriki, Kristo ni nguvu ya Mungu na hekima ya Mungu. Maana kinachoonekana kuwa ni upumbavu wa Mungu, kina busara kuliko hekima ya binadamu; na kinachoonekana kuwa ni udhaifu wa Mungu, kina nguvu kuliko nguvu za binadamu.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji

Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu Baba wa Mbinguni
tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe....


Yahweh  tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni

Yahweh ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetuBaba wa Mbinguni tukanene yaliyo yako
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....


Ndugu, kumbukeni wakati mlipoitwa: Wengi wenu hawakuwa wenye hekima hata kwa fikira za binadamu; wengi hawakuwa wenye nguvu au watu wa tabaka la juu. Ndiyo kusema, Mungu aliyachagua yale ambayo ulimwengu huyaona ni upumbavu, ili awaaibishe wenye hekima; na aliyachagua yale ambayo ulimwengu huyaona ni dhaifu, ili awaaibishe wenye nguvu. Mungu ameyachagua yale ambayo kwa fikira za dunia ni mambo yaliyo duni na yanayodharauliwa, mambo ambayo hata hayakuwako, ili kwa hayo ayafutilie mbali yale ambayo kwa fikira za binadamu ni mambo ya maana. Basi, hakuna mtu awezaye kujivunia chochote mbele ya Mungu. Mungu mwenyewe ndiye aliyewaunganisha nyinyi na Kristo Yesu. Mungu amemfanya Kristo awe hekima yetu; kwa njia yake sisi tunapatanishwa na Mungu, tunakuwa watu wake Mungu na kukombolewa. Basi, kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Mwenye kutaka kujivuna, na ajivunie kazi ya Bwana.”
Tazama watoto wako wanaokutafuta/kukuomba kwa bidii na imani, Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,
wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukaonekane katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe Yahweh tunaomba ukawape neema ya kujiombea
Kufuata njia zako nazo zikawaweke huru
Ukawape macho ya rohoni ee Mungu wetu na masikio ya kusikia
sauti yako,Ukawaokoe na kuwalinda,ukawaponye kimwili na kiroho
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao,Amani ikatawale katika maisha yao,Upendo ukadumu kati yao Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako,kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina..!



Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,
Mungu Baba aendelee kuwatendea sawasawa na mapezni yake...

Nawapenda.

Kuomba msaada
(Kwa Mwimbishaji. Zaburi ya Daudi ya matoleo ya ukumbusho)
1Upende kuniokoa ee Mungu!
Ee Mwenyezi-Mungu, uje haraka kunisaidia.
2Wanaonuia kuniangamiza,
na waaibike na kufedheheka!
Hao wanaotamani niumie,
na warudi nyuma na kuaibika.
3Hao wanaonisimanga,
na wapumbazike kwa kushindwa kwao.
4Lakini wote wale wanaokutafuta,
wafurahi na kushangilia kwa sababu yako.
Wapendao wokovu wako,
waseme daima: “Mungu ni mkuu!”
5Nami niliye maskini na fukara,
unijie haraka, ee Mungu!
Ndiwe msaada wangu na mkombozi wangu;
ee Mwenyezi-Mungu, usikawie!


Zaburi70;1-5

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Tuesday 26 February 2019

Kikombe Cha Asubuhi ;Zaburi 69...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante

 kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Jehovah  Jireh..!Jehovah Nissi..!Jehovah Raah..!
Jehovah Rapha..!Jehovah Shammah..!Jehovah Shamlom..!
Emanuel-Mungu pamohja nasi..!!
Neema yako yatutosha Baba wa Mbinguni..!

Ndugu, nawasihini kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo: Pataneni nyote katika kila jambo msemalo; yasiweko mafarakano kati yenu; muwe na fikira moja na nia moja. Ndugu zangu, habari nilizopata kutoka kwa watu kadhaa wa jamaa ya Kloe, zaonesha wazi kwamba kuna kutoelewana kati yenu.

Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona.....

Nataka kusema hivi: Kila mmoja anasema chake: Mmoja husema, “Mimi ni wa Paulo”, mwingine: “Mimi ni wa Apolo”, mwingine: “Mimi ni wa Kefa,” na mwingine: “Mimi ni wa Kristo.” Je, Kristo amegawanyika? Je, Paulo ndiye aliyesulubiwa kwa ajili yenu? Au je, mlibatizwa kwa jina la Paulo? Namshukuru Mungu kwamba sikumbatiza mtu yeyote miongoni mwenu isipokuwa tu Krispo na Gayo.

Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu wetu tunaomba ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya Baba wa Mbinguni ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo Mungu wetu

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Kwa hiyo hakuna awezaye kusema amebatizwa kwa jina langu. ( Samahani, nilibatiza pia jamaa ya Stefana; lakini zaidi ya hawa, sidhani kama nilimbatiza mtu mwingine yeyote). Kristo hakunituma kubatiza, bali kuhubiri Habari Njema; tena, niihubiri bila kutegemea maarifa ya hotuba za watu, kusudi nguvu ya kifo cha Kristo msalabani isibatilishwe.
Tazama wenye shida/tabu,watoto wako wanaokutafuta kwa bidii na imani
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
Yahweh tunaomba  ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu  unajua haja za mioyo ya kila mmoja
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Jehovah ukaonekane katika maisha yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....
Nawapenda.

Maombolezo
(Kwa Mwimbishaji: Mtindo wa Yungiyungi. Zaburi ya Daudi)
1Uniokoe, ee Mungu;
maji yamenifika shingoni.
2Ninazama ndani ya matope makuu,
hamna hata mahali pa kuweka miguu.
Nimetumbukia kwenye kilindi cha maji,
nachukuliwa na mawimbi.
3Niko hoi kwa kupiga yowe,
na koo langu limekauka.
Macho yangu yamefifia,
nikikungojea ewe Mungu wangu.
4 Taz Zab 35:19; Yoh 15:25 Watu wengi kuliko nywele zangu ndio wanichukiao bure.
Wana nguvu sana hao wanaotaka kuniua,
hao wanaonishambulia kwa mambo ya uongo.
Je, nirudishe kitu ambacho sikuiba?
5Ee Mungu, waujua upumbavu wangu;
makosa yangu hayakufichika kwako.
6Wanaokutumainia wasiaibishwe kwa sababu yangu,
ee Bwana Mwenyezi-Mungu wa majeshi;
wanaokutafuta, wasione fedheha kwa sababu yangu
ee Mungu wa Israeli.
7Kwa ajili yako nimefedheheshwa,
aibu imefunika uso wangu.
8Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu,
kaka na dada zangu hawanitambui.
9 Taz Yoh 2:17; Rom 15:3 Upendo wangu kwa nyumba yako unanimaliza.
Kashfa zote wanazokutolea wewe zimenipata mimi.
10Nilipojinyenyekesha kwa kufunga,
watu walinilaumu.
11Nilipovaa vazi la gunia kuomboleza,
wao walinidharau.
12Watu wananisengenya mabarabarani;
walevi wanatunga nyimbo juu yangu.
13Lakini mimi nakuomba wewe, ee Mwenyezi-Mungu;
nikubalie ombi langu wakati unaopenda, ee Mungu.
Kwa wingi wa fadhili zako unijibu.
Wewe ni mkombozi wa kuaminika.
14Kwa msaada wako amini uniokoe
nisizame katika matope;
uniokoe na hao wanaonichukia,
unisalimishe kutoka vilindi vya maji.
15Usiniache nikumbwe na mkondo wa maji,
au nizame kwenye kilindi
au nimezwe na kifo.
16Unijibu, ee Mwenyezi-Mungu,
kwa wema na fadhili zako;
unielekee kwa wingi wa huruma yako.
17Usimfiche mtumishi wako uso wako;
unijibu haraka, maana niko hatarini.
18Unijie karibu na kunikomboa,
uniokoe na maadui zangu wengi.
19Wewe wajua ninavyotukanwa,
wajua aibu na kashfa ninazopata;
na maadui zangu wote wewe wawajua.
20Kashfa zimeuvunja moyo wangu,
nami nimekata tamaa.
Nimetafuta kitulizo lakini sikupata,
wa kunifariji lakini sikumpata.
21 Taz Mat 27:48; Marko 15:36; Luka 23:36; Yoh 19:28-29 Walinipa sumu kuwa chakula,
na nilipokuwa na kiu wakanipa siki.
22 Taz Rom 11:9-10 Karamu zao na ziwe mtego kwao,
na sikukuu zao za sadaka ziwanase.
23Macho yao yatiwe giza wasiweze kuona,
uitetemeshe daima migongo yao.
24Uwamwagie hasira yako,
ghadhabu yako iwakumbe.
25 Taz Mate 1:20 Kambi zao ziachwe mahame,
asiishi yeyote katika mahema yao.
26Maana wanawatesa wale uliowaadhibu,
wanawaongezea majeraha wale uliowajeruhi.
27Uwaadhibu kwa kila uovu wao;
uwakatalie kabisa msamaha wako.
28 Taz Ufu 3:5; 13:8; 17:8 Uwafute katika kitabu cha walio hai,
wasiwemo katika orodha ya waadilifu.
29Lakini mimi mnyonge na mgonjwa;
uniinue juu, ee Mungu, uniokoe.
30Kwa wimbo nitalisifu jina la Mungu,
nitamtukuza kwa shukrani.
31Jambo hili litampendeza Mwenyezi-Mungu zaidi,
kuliko kumtolea tambiko ya ng'ombe,
kuliko kumtolea fahali mzimamzima.
32Wanyonge wataona hayo na kufurahi;
wanaomheshimu Mungu watapata moyo.
33Mwenyezi-Mungu huwasikiliza fukara;
hatawasahau kamwe watu wake wafungwa.
34Enyi mbingu na dunia msifuni Mungu;
bahari na vyote vilivyomo, msifuni.
35Maana Mungu atauokoa mji Siyoni,
na kuijenga tena miji ya Yuda.
Watu wake wataishi humo na kuimiliki;
36wazawa wa watumishi wake watairithi,
wale wanaopenda jina lake wataishi humo.

Zaburi69;1-36

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 25 February 2019

Kikombe Cha Asubuhi ;Zaburi 68...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?
Haleluyah ni siku/wiki  nyingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!

Mimi Paulo, niliyeitwa kuwa mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na ndugu Sosthene, tunawaandikia nyinyi mlio kanisa la Mungu huko Korintho. Nyinyi mmefanywa watakatifu katika kuungana na Kristo Yesu, mkaitwa muwe watu wa Mungu, pamoja na watu wote popote wanaomwomba Bwana wetu Yesu Kristo aliye Bwana wao na wetu pia. Nawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana wetu Yesu Kristo.
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona...

Ninamshukuru Mungu wangu daima kwa ajili yenu kwa sababu amewatunukia nyinyi neema yake kwa njia ya Kristo Yesu. Maana, kwa kuungana na Kristo mmetajirishwa katika kila kitu. Mmejaliwa elimu yote na uwezo wote wa kuhubiri. Maana ujumbe juu ya Kristo umethibitishwa ndani yenu,
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

hata hampungukiwi kipaji chochote cha kiroho mkiwa mnangojea kufunuliwa kwake Bwana wetu Yesu Kristo. Yeye atawaimarisheni nyinyi mpaka mwisho mpate kuonekana bila hatia siku ile ya Bwana wetu Yesu Kristo. Mungu ni mwaminifu; yeye aliwaita nyinyi muwe na umoja na Mwanae Yesu Kristo Bwana wetu.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopotia magumu/majaribu mbalimbali
watoto wako wanaokuomba kwa bidii na imani
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Yahweh tunaomba ukaonekane katika maisha yao
Jehovah tunaomba ukawaokoe,ukawavushe salama na  kuwalinda
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimaie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Baba wa Mbinguni ukapokee sala/maombi yetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.

Wimbo wa ushindi
(Kwa Mwimbishaji. Zaburi ya Daudi)
1Mungu ainuka, na maadui zake watawanyika;
wanaomchukia wakimbia mbali naye!
2Kama moshi unavyopeperushwa na upepo,
ndivyo anavyowapeperusha;
kama nta inavyoyeyuka karibu na moto,
ndivyo waovu wanavyoangamia mbele ya Mungu!
3Lakini waadilifu hufurahi ajapo Mungu,
hushangilia na kuimba kwa furaha.
4Mwimbieni Mungu, lisifuni jina lake;
mtengenezeeni njia yake apandaye mawinguni.68:4 apandaye mawinguni: Au apitaye jangwani.
Jina lake ni Mwenyezi-Mungu; furahini mbele yake.
5Mungu akaaye mahali pake patakatifu,
ni Baba wa yatima na mlinzi wa wajane.
6Mungu huwapa fukara makao ya kudumu,
huwafungua wafungwa na kuwapa fanaka.
Lakini waasi wataishi katika nchi kame.
7Ee Mungu, ulipowaongoza watu wako,
uliposafiri kule jangwani,
8dunia ilitetemeka, mbingu zilitiririsha mvua;
kwa kuweko kwako, Mungu wa Sinai,
naam, kwa kuweko kwako, Mungu wa Israeli!
9Ee Mungu, uliinyeshea nchi mvua nyingi,
uliiburudisha nchi yako ilipokuwa imechakaa.
10Watu wako wakapata humo makao;
ukawaruzuku maskini kwa wema wako.
11Bwana alitoa amri,
nao wanawake wengi wakatangaza habari:
12“Wafalme na majeshi yao wanakimbia ovyo!”
Kina mama majumbani waligawana nyara,
13ingawa walibaki mazizini:
Sanamu za njiwa wa madini ya fedha,
na mabawa yao yanangaa kwa dhahabu.
14Mungu Mwenye Nguvu alipowatawanya wafalme huko,
theluji ilianguka juu ya mlima Salmoni.
15Ewe mlima mrefu, mlima wa Bashani,
ewe mlima wa vilele vingi, mlima wa Bashani!
16Mbona unauonea kijicho
mlima aliochagua Mungu akae juu yake?
Mwenyezi-Mungu atakaa huko milele!
17Akiwa na msafara mkubwa,
maelfu na maelfu ya magari ya kukokotwa,
Bwana anakuja patakatifuni pake kutoka Sinai.
18Anapanda juu akichukua mateka;
anapokea zawadi kutoka kwa watu,
hata kutoka kwa watu walioasi;
Mwenyezi-Mungu apate kukaa huko.68:18 Taz Efe 4:8. Mstari wa mwisho wa aya hii si dhahiri katika makala ya Kiebrania.
19Mwenyezi-Mungu asifiwe siku kwa siku!
Yeye hutubebea mizigo yetu;
yeye ndiye Mungu wa wokovu wetu.
20Mungu wetu ni Mungu mwenye kutuokoa;
Bwana Mungu pekee ndiye aokoaye katika kifo.
21Mungu ataviponda vichwa vya maadui zake,
naam, vichwa vya wanaoshikilia njia mbaya.
22Bwana alisema: “Nitawarudisha maadui kutoka Bashani;
nitawarudisha kutoka vilindi vya bahari,
23uoshe miguu katika damu ya maadui zako,
nao mbwa wako wale shibe yao.”
24Ee Mungu, misafara yako ya ushindi yaonekana;
misafara ya Mungu wangu, mfalme wangu, hadi patakatifu pake!
25Mbele waimbaji, nyuma wanamuziki,
katikati wasichana wanavumisha vigoma.
26“Msifuni Mungu katika jumuiya kubwa ya watu.
Msifuni Mwenyezi-Mungu, enyi wazawa wa Israeli!”
27Kwanza ni Benyamini, mdogo wa wote;
kisha viongozi wa Yuda na kundi lao,
halafu wakuu wa Zebuluni na Naftali.
28Onesha, ee Mungu, nguvu yako kuu;
enzi yako uliyotumia kwa ajili yetu,
29kutoka hekaluni mwako, Yerusalemu,
ambapo wafalme watakujia na zawadi zao.
30Uwakemee wale wanyama wakaao bwawani,
kundi la mabeberu na fahali,
mpaka mataifa hayo yakupe heshima na kodi.
Uwatawanye hao watu wenye kupenda vita!68:30 aya ya 30 Kiebrania si dhahiri.
31Mabalozi68:31 Mabalozi: Au Madini ya fedha yataletwa; maana katika Kiebrania si dhahiri. watakuja kutoka Misri,
Waethiopia watamletea Mungu mali zao.68:31 watamletea … zao: Au watamnyoshea Mungu mikono yao.
32Enyi falme za dunia, mwimbieni Mungu,
mwimbieni Bwana nyimbo za sifa;
33mwimbieni yeye apitaye katika mbingu,
mbingu za kale na kale.
Msikilizeni akinguruma kwa kishindo.
34Itambueni nguvu kuu ya Mungu;
yeye atawala juu ya Israeli,
enzi yake yafika katika mbingu.
35Mungu ni wa kutisha patakatifuni pake,
naam, yeye ni Mungu wa Israeli!
Huwapa watu wake nguvu na enzi.
Asifiwe Mungu!


Zaburi68;1-35

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.