Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 25 February 2019

Kikombe Cha Asubuhi ;Zaburi 68...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?
Haleluyah ni siku/wiki  nyingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!

Mimi Paulo, niliyeitwa kuwa mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na ndugu Sosthene, tunawaandikia nyinyi mlio kanisa la Mungu huko Korintho. Nyinyi mmefanywa watakatifu katika kuungana na Kristo Yesu, mkaitwa muwe watu wa Mungu, pamoja na watu wote popote wanaomwomba Bwana wetu Yesu Kristo aliye Bwana wao na wetu pia. Nawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana wetu Yesu Kristo.
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona...

Ninamshukuru Mungu wangu daima kwa ajili yenu kwa sababu amewatunukia nyinyi neema yake kwa njia ya Kristo Yesu. Maana, kwa kuungana na Kristo mmetajirishwa katika kila kitu. Mmejaliwa elimu yote na uwezo wote wa kuhubiri. Maana ujumbe juu ya Kristo umethibitishwa ndani yenu,
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

hata hampungukiwi kipaji chochote cha kiroho mkiwa mnangojea kufunuliwa kwake Bwana wetu Yesu Kristo. Yeye atawaimarisheni nyinyi mpaka mwisho mpate kuonekana bila hatia siku ile ya Bwana wetu Yesu Kristo. Mungu ni mwaminifu; yeye aliwaita nyinyi muwe na umoja na Mwanae Yesu Kristo Bwana wetu.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopotia magumu/majaribu mbalimbali
watoto wako wanaokuomba kwa bidii na imani
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Yahweh tunaomba ukaonekane katika maisha yao
Jehovah tunaomba ukawaokoe,ukawavushe salama na  kuwalinda
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimaie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Baba wa Mbinguni ukapokee sala/maombi yetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.

Wimbo wa ushindi
(Kwa Mwimbishaji. Zaburi ya Daudi)
1Mungu ainuka, na maadui zake watawanyika;
wanaomchukia wakimbia mbali naye!
2Kama moshi unavyopeperushwa na upepo,
ndivyo anavyowapeperusha;
kama nta inavyoyeyuka karibu na moto,
ndivyo waovu wanavyoangamia mbele ya Mungu!
3Lakini waadilifu hufurahi ajapo Mungu,
hushangilia na kuimba kwa furaha.
4Mwimbieni Mungu, lisifuni jina lake;
mtengenezeeni njia yake apandaye mawinguni.68:4 apandaye mawinguni: Au apitaye jangwani.
Jina lake ni Mwenyezi-Mungu; furahini mbele yake.
5Mungu akaaye mahali pake patakatifu,
ni Baba wa yatima na mlinzi wa wajane.
6Mungu huwapa fukara makao ya kudumu,
huwafungua wafungwa na kuwapa fanaka.
Lakini waasi wataishi katika nchi kame.
7Ee Mungu, ulipowaongoza watu wako,
uliposafiri kule jangwani,
8dunia ilitetemeka, mbingu zilitiririsha mvua;
kwa kuweko kwako, Mungu wa Sinai,
naam, kwa kuweko kwako, Mungu wa Israeli!
9Ee Mungu, uliinyeshea nchi mvua nyingi,
uliiburudisha nchi yako ilipokuwa imechakaa.
10Watu wako wakapata humo makao;
ukawaruzuku maskini kwa wema wako.
11Bwana alitoa amri,
nao wanawake wengi wakatangaza habari:
12“Wafalme na majeshi yao wanakimbia ovyo!”
Kina mama majumbani waligawana nyara,
13ingawa walibaki mazizini:
Sanamu za njiwa wa madini ya fedha,
na mabawa yao yanangaa kwa dhahabu.
14Mungu Mwenye Nguvu alipowatawanya wafalme huko,
theluji ilianguka juu ya mlima Salmoni.
15Ewe mlima mrefu, mlima wa Bashani,
ewe mlima wa vilele vingi, mlima wa Bashani!
16Mbona unauonea kijicho
mlima aliochagua Mungu akae juu yake?
Mwenyezi-Mungu atakaa huko milele!
17Akiwa na msafara mkubwa,
maelfu na maelfu ya magari ya kukokotwa,
Bwana anakuja patakatifuni pake kutoka Sinai.
18Anapanda juu akichukua mateka;
anapokea zawadi kutoka kwa watu,
hata kutoka kwa watu walioasi;
Mwenyezi-Mungu apate kukaa huko.68:18 Taz Efe 4:8. Mstari wa mwisho wa aya hii si dhahiri katika makala ya Kiebrania.
19Mwenyezi-Mungu asifiwe siku kwa siku!
Yeye hutubebea mizigo yetu;
yeye ndiye Mungu wa wokovu wetu.
20Mungu wetu ni Mungu mwenye kutuokoa;
Bwana Mungu pekee ndiye aokoaye katika kifo.
21Mungu ataviponda vichwa vya maadui zake,
naam, vichwa vya wanaoshikilia njia mbaya.
22Bwana alisema: “Nitawarudisha maadui kutoka Bashani;
nitawarudisha kutoka vilindi vya bahari,
23uoshe miguu katika damu ya maadui zako,
nao mbwa wako wale shibe yao.”
24Ee Mungu, misafara yako ya ushindi yaonekana;
misafara ya Mungu wangu, mfalme wangu, hadi patakatifu pake!
25Mbele waimbaji, nyuma wanamuziki,
katikati wasichana wanavumisha vigoma.
26“Msifuni Mungu katika jumuiya kubwa ya watu.
Msifuni Mwenyezi-Mungu, enyi wazawa wa Israeli!”
27Kwanza ni Benyamini, mdogo wa wote;
kisha viongozi wa Yuda na kundi lao,
halafu wakuu wa Zebuluni na Naftali.
28Onesha, ee Mungu, nguvu yako kuu;
enzi yako uliyotumia kwa ajili yetu,
29kutoka hekaluni mwako, Yerusalemu,
ambapo wafalme watakujia na zawadi zao.
30Uwakemee wale wanyama wakaao bwawani,
kundi la mabeberu na fahali,
mpaka mataifa hayo yakupe heshima na kodi.
Uwatawanye hao watu wenye kupenda vita!68:30 aya ya 30 Kiebrania si dhahiri.
31Mabalozi68:31 Mabalozi: Au Madini ya fedha yataletwa; maana katika Kiebrania si dhahiri. watakuja kutoka Misri,
Waethiopia watamletea Mungu mali zao.68:31 watamletea … zao: Au watamnyoshea Mungu mikono yao.
32Enyi falme za dunia, mwimbieni Mungu,
mwimbieni Bwana nyimbo za sifa;
33mwimbieni yeye apitaye katika mbingu,
mbingu za kale na kale.
Msikilizeni akinguruma kwa kishindo.
34Itambueni nguvu kuu ya Mungu;
yeye atawala juu ya Israeli,
enzi yake yafika katika mbingu.
35Mungu ni wa kutisha patakatifuni pake,
naam, yeye ni Mungu wa Israeli!
Huwapa watu wake nguvu na enzi.
Asifiwe Mungu!


Zaburi68;1-35

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: