Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!
Showing posts with label Sherehe. Show all posts
Showing posts with label Sherehe. Show all posts

Saturday 2 January 2016

MKESHA WA MWAKA MPYA DMV WAFANA


 Mama wa mitindo Asya Idarous Khamsini akihesabu sekunde zilizoslia kuelekea mwaka mpya kwenye sherehe ya mkesha wa mwaka mpya 2016 iliyofanyika Lanham, Maryland siku ya Alhamisi Desemba 31, 2015 iliyoandaliwa na Jumuiya ya Watanzania DMV na kuwakutanisha wana DMV na familia zao wakiwemo marafiki kutoka majimbo mengine huku wengine wakiokea Tanzania. PICHA NA KILIMANJARO STUDIO
Wafuangaji champagne wakiwa tayari kama kikosi cha mizinga wakisubilia sekunde zilizobaki kuingia mwaka 2016 kuachia mizinga yao ikiwa ni sehemu yakusherehekea mwaka mpya wa 2016.
 Mama wa mitindo Asya Idarous Khamsini akifuahia kuuona mwaka mpaya, wapili toka kulia ni Rais wa Jumuiya ya Watanzania DMV Bwn. Iddi Sandaly pamoja na Asha Hariz (kulia) wakifurahia kuuona mwaka 2016.
WanaDMV wakikumbatiana kama familia moja na kupongezana "tumeuona mwaka 2016"
 Wanafamilia wakipongezana.
 Ni furaha ya mwaka mpya
Wanafamilia wakiwa katika picha ya pamoja kusherehekea kuuona mwaka,


Ni 2016 hiyo ni furaha kwa kwenda mbele.
Kwa picha zaidi bofya HAPA

Wednesday 27 June 2012

SHEREHE YA SENDOFF YA DORIS KASAKA (KAPINGA) ILIVYOFANA USIKU WA JANA NDANI YA DELUXE HALL SINZA!!!!!!!!!!


Doris Kasaka (Kushoto) akiwa na mpambe wake jana ndani ya Deluxe Hall Sinza wakati wa sherehe ya kumuaga (Sendoff) na kumpongeza kwa kufanya maamuzi mazuri.

Mama Mkubwa wa Doris Mama Angelina Mwami akiwakaribisha wageni wakati wa sherehe ya Binti yake ndani ya ukumbi wa Deluxe Sinza.

Baba Mkubwa wa Doris Mzee Njelu Kasaka akiwakaribisha wageni katika sherehe ya kumuaga Binti yake ndani ya Ukumbi wa Deluxe Sinza jana usiku.

Meza kuu ya wazazi wa Doris kutoka kulia ni Mama Njelu Kasaka, Mzee Njelu Kasaka, Dr Mwami na mwisho kushoto ni Mama Mwami.
Doris akipiga picha ya kumbukumbu na wafanyakazi wenzake kutoka Zantel.


"Swahili na Waswahili" Tunakutakia Safari njema na kila lililo jema na Maandalizi mema ya Ndoa.


Pamoja sana KapingaZ!!!!!!!



Thursday 7 June 2012

"Sing" for HM Queen Elizabeth II (Diamond Jubilee)!!!!!!!

Mmmmhhh Umoja ni Nguvu na Penye Wengi Pana Mengi!!!"Sauti tamuuu Twende Sote Waungwana,Lalalalalaaaaaaaaaaa.....Swahili na Waswahili" Pamoja sana!!!!

Thursday 24 November 2011

Miaka 50 ya Uhuru - Kijitonyama Evangelical Choir!!!!!

Wanakwambia Tujibweteke aaa,Turudi Nyuma mmm,Tusonge Mbele namnamnam,
Haya wapendwa mmejiaandaje na miaka 50 ya Uhuru? Mablogger nao sijui watatoka vipi/wameandaa nini?
kwani  nimeona Vyama, Vikundi vya ngoma,Muziki,Kwaya na mengine mengi kuhusu Miaka 50 ya UHURU. Uwe Huru na mwenye Amani na kila lililo jema!!!Usisite kutujuza Nasi Umejiaandaje au Unalipi kuhusu MIAKA 50 YA UHURU WA TANZANIA BARA. NA VISIWANI TUUNGANE PAMOJA!!