Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 31 March 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 2...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru Mungu kwa  kutuchagua tena na kutupa kibali cha kuiona leo hii,si kwa ujuzi wetu, wala si kwa uwezo wetu,si kwamba sisi ni wema sana,  si kwamba ni wazuri mno zaidi ya wengine ambao Leo hii wapo hoi kitandani, wengine hawana hata kauli ya kusema au kuita Mungu wangu niokoe..na wengine wameaga Dunia..


Nini tumempa Mungu zaidi  ilituendelee kuishi na tukiwa na uwezo wa kumtukuza, kumsifu, kuomba toba,kujifunza na kumtafuta yeye?
Mungu ametupa nafasi hii ya  kuiona siku hii kwa Neema/Rehema yake..
Nimapenzi yake basi nasi tusisite wala kuchelewa kutumia nafasi hii tuliyo ipata kutoka kwa Muumba wetu,Baba yetu,Muumba Mbingu na Nchi,Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo..Yahweh...!!! Jehovah..!!
Tunakuja mbele zako na kujinyenyekeza Baba Mungu,Tunaomba utubariki katika maisha yetu, Baba ubariki Kazi zetu,Biashara,Masomo, Tuingiapo/Tutokapo,Vyombo vya usafiri, tutembeapo na hatua zetu ziwe nawe Yahweh..!!!!


Baba tunakwenda kinyume na adui, Mwovu, Nguvu za Giza,Nguvu za mapepo,Nguvu za mizimu,Nguvu za Mpinga Kristo zishindwe katika Jina lililo kuu la Yesu Kristo wa Nazareti...


1“Nimewaambieni hayo kusudi msiiache imani yenu. 2Watu watawafukuza nyinyi katika masunagogi yao. Tena, wakati unakuja ambapo kila atakayewaua nyinyi atadhani anamhudumia Mungu. 3Watawatendeeni mambo hayo kwa sababu hawamjui Baba, wala hawanijui mimi. 
4Basi, nimewaambieni mambo haya ili saa yake itakapofika mkumbuke kwamba niliwaambieni.[Yohane 16:1-4]



Tunakuja mbele zako Baba tunaomba utusamehe dhambi zetu zote

tulizowaza,tulizo nena,tulizo tenda kwakujua/kutojua Mfalme wa Amani
tunaomba utupe Neema ya kuweza kuwasamehe wale waliotukosea..
Baba ukawaponye/kuwagusa wenye Shida/Tabu, Wagonjwa,wafiwa ukawe mfariji wao..waliovifungoni Baba ukawafungue na kuwaponya kimwili na kiroho..
Roho mtakatifu akatuongoze kwenye kunena/kutenda,kutambua/kujitambua..



Basi, nimewaambieni mambo haya ili saa yake itakapofika mkumbuke kwamba niliwaambieni. “Sikuwaambieni mambo haya tangu mwanzo kwa sababu nilikuwa pamoja nanyi. Lakini sasa namwendea yule aliyenituma; na hakuna hata mmoja wenu anayeniuliza: ‘Unakwenda wapi?’ Kwa kuwa nimewaambieni mambo hayo mmejaa huzuni mioyoni mwenu. Lakini, nawaambieni ukweli: Afadhali kwenu mimi niende zangu, maana nisipokwenda Msaidizi hatakuja kwenu. Lakini nikienda, basi, nitamtuma kwenu. Naye atakapokuja atawathibitishia walimwengu kwamba wamekosea kuhusu dhambi, uadilifu na hukumu ya Mungu. Wamekosea kuhusu dhambi kwa sababu hawaniamini; kuhusu uadilifu, kwa sababu nakwenda zangu kwa Baba, nanyi hamtaniona tena; kuhusu hukumu, kwa sababu mkuu wa ulimwengu huu amekwisha hukumiwa. “Ninayo bado mengi ya kuwaambieni, ila kwa sasa hamwezi kuyastahimili. Lakini atakapokuja huyo Roho wa ukweli atawaongoza kwenye ukweli wote; maana hatasema kwa mamlaka yake mwenyewe, bali atasema atakayoyasikia na kuwajulisheni yatakayokuja. Yeye atanitukuza mimi kwa kuwa atawajulisheni yale atakayopata kutoka kwangu. Vyote alivyo navyo Baba ni vyangu; ndiyo maana nimesema kwamba huyo Roho atawajulisheni yale atakayopata kutoka kwangu.

Baba ukabariki Ridhiki zetu ziingiapo/zitokapo..
Mfalme wa Amani tunaiweke nchi hii tunayoshi mikononi mwako na ukaibariki na kuwabariki watu wake...Baba tunaiweka mikononi mwako na  Tanzania uibariki na kubariki watu wake,Bariki Afrika Baba na Dunia yote wewe ukatawale..Bariki wanaotuongoza nawo wakatuongoze katika haki na kweli..
Baba tunayaweka haya mikononi mwako, Sifa na Utukufu ni wako Daima..
Tukishukuru na kuamini wewe ni Bwana na Mwokozi wetu..
Amina..!!!!

Amani ya Bwana iwe Nanyi.



Mtoto Mose anaokotwa mtoni Nili

1Kulikuwa na mtu mmoja wa ukoo wa Walawi aliyemwoa mwanamke mmoja ambaye pia alikuwa wa ukoo wa Walawi. 2Taz Mate 7:20; Ebr 11:23 Basi, mama huyu akapata mimba, akajifungua mtoto wa kiume. Alipoona kwamba mtoto huyo mchanga alikuwa mzuri, akamficha kwa muda wa miezi mitatu. 3Lakini kwa vile hakuweza kumficha zaidi ya muda huo, alitengeneza namna ya kikapu cha mafunjo,2:3 mafunjo: Aina ya majani yaotayo mtoni au ziwani na mabua yake yalitumika hapo kale kutengenezea karatasi (papiro). akakipaka namna ya lami, akamtia huyo mtoto ndani. Kisha akakiweka kikapu kando ya mto Nili kwenye majani. 4Dada yake huyo mtoto akajificha karibu na mahali hapo ili aone yatakayompata nduguye.
5Basi, binti Farao akashuka mtoni kuoga, na watumishi wake wakawa wanatembeatembea kandokando ya mto. Binti Farao akakiona kile kikapu katika majani, akamtuma mjakazi wake akichukue. 6Alipokifungua, alimwona yule mtoto mchanga, analia. Basi, akamwonea huruma, akasema, “Huyu ni mmojawapo wa watoto wa Waebrania.”
7Papo hapo dada yake yule mtoto akajitokeza, akamwambia binti Farao, “Je, niende nikakutafutie yaya miongoni mwa wanawake wa Kiebrania akulelee mtoto huyu?” 8Binti Farao akamwambia, “Naam; nenda.” Basi, huyo msichana akaenda, akamwita mama yake huyo mtoto. 9Binti Farao akamwambia huyo mama, “Mtunze mtoto huyu, umlee kwa niaba yangu, nami nitakulipa mshahara wako.” Basi, huyo mama akamchukua mtoto, akamlea.
10Mtoto alipokuwa mkubwa kiasi, mama yake akampeleka kwa binti Farao, naye akamchukua na kumfanya mwanawe. Binti Farao akasema, “Nimemtoa majini,” kwa hiyo akampa mtoto huyo jina Mose.2:10 Mose: Jina “Mose” katika Kiebrania lafanana na neno “mashah” maana yake “kutoa” lakini jina hilo ni la Kimisri maana yake “Kupata mtoto.” (Linganisha aya hii na Mate 7:21.)

Mose anakimbilia Midiani
11Siku moja, Mose alipokuwa mtu mzima, aliwaendea Waebrania wenzake ili kujionea taabu zao. Basi, akamwona Mmisri mmoja anampiga Mwebrania, mmoja wa ndugu zake Mose. 12Mose akatazama huku na huko, na alipoona kwamba hakuna mtu karibu, alimuua yule Mmisri na kumficha mchangani. 13Kesho yake, Mose alitoka tena, akaona Waebrania wawili wanapigana. Basi, akamwuliza yule aliyekosea, “Kwa nini unampiga mwenzako?” 14Naye akamjibu, “Nani aliyekuweka wewe kuwa mkuu na mwamuzi wetu? Je, unataka kuniua kama ulivyomuua yule Mmisri?” Hivyo, Mose aliogopa na kufikiri, “Bila shaka jambo hilo limejulikana!” 15Naye Farao aliposikia juu ya tukio hilo akakusudia kumuua Mose. Lakini Mose alimkimbia Farao, akaenda kukaa katika nchi ya Midiani.2:15 Midiani: Jina la makabila ambayo yalihamahama kwenye eneo la kusini mwa nchi ya Palestina. Kulingana na Mwa 25:2, Midiani alikuwa mtoto wa Abrahamu.
Siku moja, Mose alikuwa ameketi kando ya kisima cha maji. 16Basi, binti saba wa kuhani mmoja wa huko Midiani walifika kuchota maji na kuwanywesha kondoo na mbuzi wa baba yao. 17Wachungaji wengine wakaja na kuwafukuza hao binti. Lakini Mose akawasaidia binti hao na kuwanywesha wanyama wao. 18Walipomrudia baba yao Reueli, yeye akawauliza, “Mbona leo mmerudi upesi hivyo?” 19Nao wakamjibu, “Mmisri mmoja alituokoa mikononi mwa wale wachungaji, naye mwenyewe akachota maji na kuwanywesha wanyama wetu.” 20Baba yao akawauliza binti zake, “Yuko wapi? Mbona mmemwacha huko? Mwiteni aje ale chakula.”
21Mose akakubali kukaa kwa huyo mtu. Basi, huyo mtu akampa Mose binti yake aitwaye Zipora awe mke wake. 22Zipora akamzalia mtoto wa kiume. Mose akasema, “Nimekimbilia katika nchi ya kigeni”, kwa hiyo akampa huyo mtoto jina Gershomu.2:22 Gershomu: Neno kwa neno maana yake ni “mkimbizi huko”.

Kilio cha Waisraeli utumwani

23Baada ya muda mrefu, mfalme wa Misri akafa. Waisraeli wakapiga kite na kulia kutokana na hali yao ya utumwa, na kilio chao kikamfikia Mungu juu. 24Mungu akasikia kilio chao, naye akakumbuka agano alilofanya na Abrahamu, na Isaka na Yakobo. 25Mungu aliwaangalia Waisraeli, akaona kuwa hali yao ni mbaya.
Kutoka2;1-25
Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: