Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!
Showing posts with label jikoni leo/Watoto na Malezi. Show all posts
Showing posts with label jikoni leo/Watoto na Malezi. Show all posts

Thursday 26 March 2020

Watoto na Malezi;Shule ya Nyumbani-Jikoni Leo;Ratiba Ya Chakula Na Rachel-siwa...







Ratiba ya chakula ya watoto Waswahili wakati huu Wa Shule Ya Nyumbani

 :8:30-Uji;wa-Mchele,wa-Dona,wa-urezi,wa-Muhogo n.k.

 :10:30-CHai/juisi; na-Mihogo,Viazi,Chapati,maandazi,                             Vitumbua n.k.

 :1:00-Ugali/wali,Ndizi/viazi,Makande n.k
         Mboga;Nyama/kuku/samaki,Maharage/kunde/mbaazi,
        Mboga za majani,bamia/mrenda n.k

 :4:00-Chai/juisi/maji;na kachori,visheti,katlesi,                                        Keki,Bagia/badia/bajia ๐Ÿคท๐Ÿฝ‍♀️za dengu/kunde n.k

 :6:00-Wali,Tambi,chipsi(zege)n.k

       : Chakula cha mchana kama kimebaki kinaweza kuliwa ..
       :Matunda wakati wowote ๐ŸŽ(Desert)upendavyo ๐Ÿฎ๐Ÿง
    :Jumamosi/jumapili,wajiachie tuu wanavyopenda -๐Ÿ”๐ŸŒญ๐ŸŒฎ
    :Kutupa chakula ni mwiko ..

   :Ratiba ya chakula kipindi hiki watoto wapo nyumbani 
   :Tujaribu kuwalisha kama waswahili ๐Ÿคฃkama itawezekana ๐Ÿค”
     :
     :
  :Nimatumaini yangu wakirudi shule watakuwa wenye nguvu na        Afya Njema ๐Ÿ’ช๐Ÿฝ๐Ÿ’ƒ๐Ÿพ...

  :Mzazi/Mlezi;unaweza kuongeza/kupunguza na kusahihisha                              nilipokosea.
 :Pia unaweza kuandaa ya kwako ili tupate kujifunza zaidi
 :Unaweza kunitumia kwa :E-mail;rasca@hotmail.co.uk

  :
  :
 : Angalizo;mimi si mtaalamu wa Chakula na Lishe..
                 Unaweza kufanya utafiti zaidi
                Kulingana na afya ya mtoto wako ๐Ÿ™๐Ÿฝ


Imeandikwa na Rachel siwa ๐Ÿ™๐Ÿฝ❤️
Asanteni.





"Swahili Na Waswahili"Pamoja Sana.

Friday 14 June 2013

Kuelekea Siku Ya Mtoto Wa Afrika;Da'Tolly Tolly Anauliza;UNALEA WATOTO AU MAYAI?KESHO YAO ITAKUAJE?




Imeandikwa na da'Tolly .....wa TOLLYZKITCHEN

Kama  Unalolote linalohusu Siku Ya Mtoto wa Afrika na unapenda kushiriki nasi usisite kututumia Email;rasca@hotmail.co.uk

kwa Habari na Mambo Meengi  ya Watoto,Wazazi/Walezi.nifuate huku;http://www.watotonajamii.blogspot.co.uk/

   Pia Usisahau kuungana nasi katika kucheza pamoja na watoto wetu..hapa UK siku hiyo tarehe 16 ni Siku  ya BABA..[FATHER'S DAY] Watoto na Wazazi watakuwa na Mambo meengi..
Basi Tukutane wiki inayofuata  J'Mosi ya tarehe 22/06/2013.


Unalea Watoto au Mayai? si Maneno yangu msome da'Tolly.



043
Katika maisha si kila unalolifanya unafanya kwasababu unapenda au unafurahia, wakati mwingine maisha yanatulazimu kufanya mambo Fulani au kujua jambo Fulani kwasababu ni muhimu kwetu au kwasababu jamii inatutaka tujue na kuweza.
Kupika ni moja ya hayo. si kila mtu anapenda kupika, lakini ualisia wa maisha unawalazimu  watu kujua kupika.Kwa maisha yetu ya kiafrika kujua kupika ni jambo la lazima kwa mwanamke,hata ivyo ualisia wa mabadiliko ya maisha karne hii ya 21 yanawalazimu hata wanaume kujua kupika.
Kupika ni jambo la kujifunza kwa wazazi na ndugu wanaokuzunguka katika kukua kwake,ni kitu unachojifunza kila siku ya maisha yako na kwakufanya mazoezi ya kupika mara kwa mara kama sehem ya ushiriki wa kazi za nyumbani.
Wazazi wa siku hizi wanawanyima watoto  nafasi ya kujifunza kupika kwa kushiriki kazi za nyumbani.Familia nyingi zina dada au kaka anaefanya kazi zote za ndani na matokeo yake watoto wengi hufanya kazi ya kuangalia Tv siku nzima na kukaa kwenye viti kama mayai  kwenye trei.
Kuwalea watoto wako kama mayai,kutowashirikisha katika kazi za nyumbani na shughuli zako za biashara na mambo mengine ni kosa kubwa sana.Ni kumnyima mtoto nafasi ya kujifunza mambo mbalimbali yampasayo kujua kwenye maisha.
Huku jikoni mtoto anatakiwa kushiki kazi ndugo ndogo tangu anapokua mdogo,aanze kwa kutoan vyombo mezani,kufuta meza,kupanga meza,kufagia jiko,kutwanga vitunguu swaumu na mambo madogo madogo kama hayo kutokana na umri wake.
Hapo nyumbani wapangie watoto zamu na taratibu za kufanya kazi za nyumbani.si kupika tu,bali kazi za nyumbani kwa ujumla.
Tulipokuwa wadogo,mama yetu alitupangia zamu na ratiba ya kazi zote,kutofanya kazi katika wakati husika kuliambatana na adhabu ya kufanya kazi hiyo kwa siku tatu  mfululizo kama kazi ya nyongeza,uku wengine wakipumzika.Ratiba ya kazi hizi ilibandikwa nyuma ya mlango wa kabati  jikoni na ilizingatia umri.Ratiba yetu likua na mambo haya:
1.Ratiba ya kuamka kuandaa chai asubuhi
2.Ratiba ya kupika  mchana na usiku
3.Ratiba ya kuosha vyombo,wadogo wanaosha vyombo vya chai asubuhi
4.Ratiba ya kupanga meza(wadogo)
5.Ratiba ya kufuta meza(wadogo)
6.Ratiba ya kusafisha Sebule na jiko
7.Ratiba ya kusafisha vyumba
8.Ratiba ya kusafisha choo na bafu
9.Ratiba ya kufagia nje
10.Ratiba ya kumwagilizia mauwa
11.Ratiba ya kumsaidia mama kwenye biashara
12.Zamu ya kusali na kuongoza ibada ya jioni
042
Zaidi ya ratiba kulikua na kanuni au sharia ambazo zilikua lazima kufuata na kila moja ilikua na adhabu yake pale unapoivunja.
1.Lazima kuoga kabla ya kwenda mezani kupata kifungua kinywa na kabla ya kwenda kupata chakula cha jioni.Usipooga basi hakuna kwenda mezani,ikimaanisha hautakula.
2.Lazima kufua nguo na kupanga kabati kila jumamosi.Usipofanya hivyo jumapili wengine wakipelekwa kutembea,wewe unabaki nyumbani .
3.Home work zote lazima zifanywe kabla ya saa moja jioni,na umpe mama,baba,mtu mkubwa yoyote akague .Usipofanya hivyo mara nyingi adhabu ilikua kufanya maswali mengine kumi kama hayo au anamwambia mwalimu wako akushugulikie shuleni.
4.Kwenda kanisani ni lazima,hili halikua na mjadala na hakukua na namna ya kulikwepa.
5.Hakuna kuangalia Tv wala sinema kabla ya saa nane mchana.Asubuhi ni walkati wa kazi,mapumziko ni Baada ya  Lunch.Adhabu ya kuvunja hili ilikua ni kupewa kazi za kufanya,kwani kukaa unaangalia Tv maana yake huna kazi.Unaambiwa kashone vifungo vilivyotoka kwenye nguo zako,au kafute na kubrashi viatu vyako.
  • Hizi ni baadhi ya ratiba na sharia au kanuni zilizonilea,na kunifanya niwe hivi nilivyo leo.ratiba hizi zilihusisha watoto wote,wakiume na wakike.Kwa ratiba kama hizi mtoto anajifunza kila kitu  na anajifunza kujitegemea kwa kila kitu.
Ifike mahala muone aibu na mjiulize watoto wenu watakua kina baba au kina mama wanamna gani wakikua.Waswahili husema  Samaki mkunje  angali mbichi.Wewe unaengoja Samaki wako aive ndipo umkunje,utatia aibu na utaumbuka.
Pia ni vyema kujua kuwa,ni katika ufanyaji wa kazi hizi unaanza kuona na kutambua uwezo na vipaji vya watoto.Mpishi mzuri utaanza kumuona mapema,wale wanaopenda kusimamia wenzao ndio vipaji vya uongozi hivyo,kuna wale wa maneno mengi ila hawafanyi kazi nao utawajua na uanze kuwasaidia kubadili tabia hizo zisizofaa.
Hapa jikoni watoto wakija lazima niwape kazi yakufanya,kama hakuna kazi basi nampa kiti akae mlangoni(kukwepa ajali) tuongee mawili matatu wakati napika.Kwani najua anapoangalia niachofanya kula jambo anajifunza,na mara nyingi wanakua na maswali mengi juuu ya lile ninalolifanya.
Yangu ni haya tu kwa leo,yaliyobaki kazi kwako.Ukiamua kulea watoto kama mayai  basi endelea ukijua unamuharibia mtoto maisha.
kwa mambo ya mapishi na malezi ingia hapa;http://tollyzkitchen.wordpress.com/



Wednesday 17 April 2013

Watoto na Vipaji;Botlahle - Winner Of South Africa's Talent!!


Waungwana ;"Watoto na Malezi"Leo tuangalie Vipaji vya watoto Wetu...
Vipi utagundua mtoto wako anakipaji gani?

 Jee Unakubaliana na Mtoto wako nini anapenda kwa Mfano;Michezo,Kushona,Kutengeneza/Ubunifu,Kucheza Ngoma/Muziki,Kusuka,Kuchora na Mingine mingi...
Pasipo kumkatisha Tamaa kwasababu wewe hupendi hicho afanyacho na Ungependa Afanye unacho Penda wewe?

Karibu kwa Maoni/Ushaurina Kuelimishana kwa Upendo.

 Mengi kuhusiana na Watoto ingia;http://watotonajamii.blogspot.co.uk/

    "Swahili Na Waswahili" Pamoja Sana.

Wednesday 30 May 2012

Jikoni Leo; ni Wasomali na Darasa la Mapishi na Utamaduni wao;Wazazi wa Marekani.na Da'Mariam!!!!!!

Waungwana "Jikoni Leo" ni Wasomali;
Wazazi/Walezi wa Marekani Wakiwafundisha Watoto wao Jinsi ya Kupika na Tamaduni za Kwao.


Pia da'Mariam naye Hayuko Nyuma kuonyesha/Kuwafunza watu wengine Jinsi "East Africa" wapikavyo.
 

Hapa nimeona Wasomali wanajitahidi kuwafundisha kupika watoto wa kike tuu,Sijui watoto wa kiume kwao Hawapiki?au bado wanamambo yaleee mtoto wakike "LAKE JIKO".

Waungwana Mmejifunza nini kwa haya ya Wenzetu Wasomali?

Karibuni sana kwa Maoni,Ushauri na Kuelimishana kwa Upendo.

Pamoja sana."Swahili na Waswahili."