Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 12 June 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Amosi 6...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Walipokwisha amua tusafiri mpaka Italia, walimweka Paulo pamoja na wafungwa wengine chini ya ulinzi wa Yulio aliyekuwa ofisa wa jeshi katika kikosi kiitwacho “Kikosi cha Augusto.”
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako,
Tukijinyenyekeza,tukijiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunamomba utusamehe dhambi zetu
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
 ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea

Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Tulipanda meli ya Adiramito iliyokuwa inasafiri na kupitia bandari kadhaa za mkoa wa Asia, tukaanza safari. Aristarko, mwenyeji wa Makedonia kutoka Thesalonike, alikuwa pamoja nasi.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Kesho yake tulitia nanga katika bandari ya Sidoni. Yulio alimtendea Paulo vizuri kwa kumruhusu awaone rafiki zake na kupata mahitaji yake.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...

Nawapenda.

Adhabu kwa sababu ya kujiamini
1Ole wenu nyinyi mnaostarehe huko Siyoni,
nanyi mnaojiona salama mlimani Samaria!
Nyinyi mwaonekana kuwa viongozi wa taifa maarufu
ambao Waisraeli wote huwategemea.
2Haya! Nendeni Kalne mkaangalie kila mahali,
tokeni huko mwende hadi mji ule mkubwa wa Hamathi,
kisha teremkeni hadi Gathi kwa Wafilisti.
Je, falme zao si bora kuliko zenu
na eneo lao si bora kuliko lenu?”
3Nyinyi mnajaribu kuifukuza siku mbaya.
Lakini mnauleta karibu utawala dhalimu.
4Ole wenu mnaolala juu ya vitanda vya pembe za ndovu
na kujinyosha juu ya masofa,
mkila nyama za wanakondoo na ndama!
5Nyinyi mnapenda kuimba ovyo na sauti ya vinubi
na kubuni ala mpya za muziki mkimwiga mfalme Daudi.
6Mnakunywa divai kwa mabakuli,
na kujipaka marashi mazuri mno.
Lakini hamhuzuniki hata kidogo
juu ya kuangamia kwa wazawa wa Yosefu.
7Kwa hiyo mtakuwa wa kwanza kwenda uhamishoni,
na karamu za wenye kustarehe zitatoweka.
8Bwana Mwenyezi-Mungu ameapa kwa nafsi yake;
Mwenyezi-Mungu, Mungu wa majeshi asema:
“Nachukizwa mno na kiburi cha wazawa wa Yakobo;
tena nayachukia majumba yao ya fahari.
Mji wao na vyote vilivyomo nitawapa adui zao.”
9Kama wakibaki watu kumi katika nyumba moja, wote watakufa. 10Na atakapokuja mjomba wa aliyekufa kuitoa maiti nje aichome, akamwuliza yeyote atakayekuwako ndani pembeni mwa nyumba, “Je kuna mtu mwingine pamoja nawe?” Naye atamjibu, “La! Hamna!” Naye atamwambia, “Nyamaza kimya! Tusilitaje hata jina la Mwenyezi-Mungu.”6:10 maana ya aya hii katika Kiebrania si dhahiri.
11Tazama! Mwenyezi-Mungu anatoa amri,
nalo jumba kubwa labomoka vipandevipande,
na nyumba ndogo kusagikasagika.
12Je, farasi waweza kupiga mbio miambani?
Je, watu huilima bahari kwa ng'ombe?
Lakini nyinyi mmeigeuza haki kuwa sumu,
na tunda la uadilifu kuwa uchungu.
13Nyinyi mnashangilia juu ya Lodebari,6:13 Lodebari: Matumizi ya jina hili katika Kiebrania ni kama neno lenye maana “kitu batili” au “upuuzi.”
na kusema mmeuteka Karnaimu6:13 Karnaimu: Maana ya jina la mji huu mdogo ni “pembe” nazo ni alama ya nguvu. kwa nguvu zenu wenyewe.
14Mwenyezi-Mungu wa majeshi asema hivi:
“Enyi Waisraeli,
kweli nitaleta taifa moja lije kuwashambulia,
nalo litawatesa nyinyi kuanzia Lebo-hamathi kaskazini,
hadi kijito cha Araba, upande wa kusini.”

Amosi6;1-14

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

No comments: