Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 4 June 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Yoel 3...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Mwenyezi-Mungu asema, “Kwa hiyo, mimi nitawalaumu nyinyi, na nitawalaumu wazawa wenu. Haya, vukeni bahari hadi Kupro mkaone, au tumeni watu huko Kedari wakachunguze, kama jambo kama hili limewahi kutokea:
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako,
Tukijinyenyekeza,tukijiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunamomba utusamehe dhambi zetu
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
 ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea

Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Kwamba kuna taifa lililowahi kubadilisha miungu yake ingawa miungu hiyo si miungu! Lakini watu wangu wameniacha mimi, utukufu wao, wakafuata miungu isiyofaa kitu.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Shangaeni enyi mbingu, juu ya jambo hili, mkastaajabu na kufadhaika kabisa. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema. Maana, watu wangu wametenda maovu mawili; wameniacha mimi niliye chemchemi ya maji ya uhai, wakajichimbia visima vyao wenyewe, visima vyenye nyufa, visivyoweza kuhifadhi maji.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...

Nawapenda.

Mungu atayahukumu mataifa
1“Wakati huo na siku hizo
nitakapoirekebisha hali ya Yuda na Yerusalemu,
2nitayakusanya mataifa yote,
niyapeleke katika bonde liitwalo,
‘Mwenyezi-Mungu Ahukumu.
Huko nitayahukumu mataifa hayo,
kwa mambo yaliyowatendea watu wangu Israeli,
hao walio mali yangu mimi mwenyewe.
Maana waliwatawanya miongoni mwa mataifa,
waligawa nchi yangu
3na kugawana watu wangu kwa kura.
Waliwauza wavulana ili kulipia malaya,
na wasichana ili kulipia divai.
4“Mnataka kunifanya nini enyi Tiro na Sidoni na maeneo yote ya Filistia? Je, mna kisasi nami mnachotaka kulipiza? Kama mnalipiza kisasi, mimi nitawalipizeni mara moja! 5Mmechukua fedha na dhahabu yangu, na kuvibeba vitu vyangu vya thamani hadi kwenye mahekalu yenu. 6Mmewapeleka watu wa Yuda na Yerusalemu mbali na nchi yao, mkawauza kwa Wagiriki. 7Sasa, nitawarudisha watu wangu kutoka huko mlikowauza. Nitawalipizeni kisasi kwa yote mliyowatendea. 8Watoto wenu wa kiume na wa kike nitawafanya wauzwe kwa watu wa Yuda, nao watawauzia Washeba, watu wa taifa la mbali kabisa. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
9“Watangazieni watu wa mataifa jambo hili:
Jitayarisheni kwa vita,
waiteni mashujaa wenu;
askari wote na wakusanyike,
waende mbele.
10 Taz Isa 2:4; Mika 4:3 Majembe yenu yafueni yawe mapanga,
miundu yenu ya kupogolea iwe mikuki.
Hata aliye dhaifu na aseme:
‘Mimi pia ni shujaa’.
11Njoni haraka, enyi mataifa yote jirani,
kusanyikeni huko bondeni.”
Ee Mwenyezi-Mungu!
Teremsha askari wako dhidi yao!
12“Haya mataifa na yajiweke tayari;
yaje kwenye bonde liitwalo:
‘Mwenyezi-Mungu Ahukumu’.
Huko, mimi Mwenyezi-Mungu,
nitaketi kuyahukumu mataifa yote ya jirani.
13 Taz Ufu. 14:14-16, 19-20 Haya! Chukueni mundu wa kuvuna,
kwani sasa ni wakati wa mavuno.
Ingieni! Wapondeni kama zabibu
ambazo zimejaza shinikizo.
Uovu wao umepita kiasi
kama mapipa yanayofurika.”
14Wanafika makundi kwa makundi
kwenye bonde la Hukumu,
maana siku ya Mwenyezi-Mungu imekaribia.
15Jua na mwezi vinatiwa giza,
na nyota zimeacha kuangaza.
Mungu atawabariki watu wake
16Mwenyezi-Mungu ananguruma huko Siyoni;
sauti yake inavuma kutoka Yerusalemu;
mbingu na dunia vinatetemeka.
Lakini Mwenyezi-Mungu ni kimbilio la watu wake,
ni ngome ya usalama kwa Waisraeli.
17“Hapo, ewe Israeli,
utajua kwamba mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako,
nakaa Siyoni, mlima wangu mtakatifu,
Yerusalemu utakuwa mji mtakatifu;
na wageni hawatapita tena humo.
18“Wakati huo, milima itatiririka divai mpya,
na vilima vitatiririka maziwa.
Vijito vyote vya Yuda vitajaa maji;
chemchemi itatokea nyumbani mwa Mwenyezi-Mungu,
na kulinywesha bonde la Shitimu.3:18 Shitimu: Kiebrania; au Mgunga.
19“Misri itakuwa mahame,
Edomu itakuwa jangwa tupu,
kwa sababu waliwashambulia watu wa Yuda
wakawaua watu wasio na hatia.
20Bali Yuda itakaliwa milele,
na Yerusalemu kizazi hata kizazi.
21Nitawaadhibu waliomwaga damu ya watu wa Yuda
wala sitawaachia wenye hatia.
Mimi, Mwenyezi-Mungu nakaa Siyoni.”

Yoeli3;1-21

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

No comments: