Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 30 June 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Mika 4...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Unitendee mimi mtumishi wako kwa ukarimu, nipate kuishi na kushika neno lako. Uyafumbue macho yangu, niyaone maajabu ya sheria yako. Mimi ni mkimbizi tu hapa duniani; usinifiche amri zako.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako,
Tukijinyenyekeza,tukijiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunamomba utusamehe dhambi zetu
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
 ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea

Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Roho yangu yaugua kwa hamu kubwa ya kutaka kujua daima maagizo yako. Wewe wawakemea wenye kiburi, walaanifu, ambao wanakiuka amri zako.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Uniepushe na matusi na madharau yao, maana nimeyazingatia maamuzi yako. Hata kama wakuu wanakula njama dhidi yangu; mimi mtumishi wako nitayatafakari maamuzi yako. Masharti yako ni furaha yangu; hayo ni washauri wangu.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...

Nawapenda.

Mungu atatawala watu wote kwa amani
(Isa 2:1-4)
1Utakuja wakati ambapo
mlima wa nyumba ya Mwenyezi-Mungu
utakuwa mkubwa kuliko milima yote.
Naam, utakwezwa juu ya vilima vyote.
Watu wengi watamiminika huko,
2mataifa mengi yataujia na kusema:
“Twendeni juu kwenye mlima wa Mwenyezi-Mungu,
twende katika nyumba ya Mungu wa Yakobo,
ili atufundishe njia zake,
nasi tufuate nyayo zake.
Maana mwongozo utatoka huko Siyoni;
neno la Mwenyezi-Mungu huko Yerusalemu.”
3Mungu atasuluhisha mizozo ya mataifa mengi,
atakata mashauri ya mataifa makubwa ya mbali.
Nayo yatafua mapanga yao kuwa majembe,
na mikuki yao kuwa miundu ya kupogolea.
Taifa halitapigana na taifa lingine,
wala hayatafanya tena mazoezi ya vita.
4Kila mtu atakaa kwa amani
chini ya mitini na mizabibu yake,
bila kutishwa na mtu yeyote.
Mwenyezi-Mungu wa majeshi, ametamka yeye mwenyewe.
5Mataifa mengine hufuata njia zao,
kwa kuitegemea miungu yao,
lakini sisi twafuata njia zetu kwa kumtegemea Mwenyezi-Mungu,
Mungu wetu, milele na milele.
Waisraeli watarudi kutoka utumwani
6Mwenyezi-Mungu asema,
“Siku ile nitawakusanya walemavu,
naam, nitawakusanya waliochukuliwa uhamishoni,
watu wale ambao niliwaadhibu.
7Hao walemavu ndio watakaobaki hai;
hao waliochukuliwa uhamishoni watakuwa taifa lenye nguvu.
Nami Mwenyezi-Mungu nitawatawala mlimani Siyoni,
tangu wakati huo na hata milele.”
8Nawe kilima cha Yerusalemu,
wewe ngome ya Siyoni,
ambamo Mungu anafanya ulinzi juu ya watu wake,
kama mchungaji juu ya kondoo wake;
wewe utakuwa tena mji maarufu kama hapo awali,
Yerusalemu utakuwa tena mji mkuu wa mfalme.
9Sasa kwa nini mnalia kwa sauti?
Je, hamna mfalme tena?
Mshauri wenu ametoweka?
Mnapaza sauti ya uchungu,
kama mama anayejifungua!
10Enyi watu wa Siyoni,
lieni na kugaagaa kama mama anayejifungua!
Maana sasa mtaondoka katika mji huu
mwende kukaa nyikani,
mtakwenda mpaka Babuloni.
Lakini huko, mtaokolewa.
Huko Mwenyezi-Mungu atawakomboa makuchani mwa adui zenu.
11Mataifa mengi yamekusanyika kuwashambulia.
Yanasema: “Acheni mji wao utiwe najisi,
nasi tuyaone magofu ya Siyoni!”
12Lakini wao
hawafahamu mawazo ya Mwenyezi-Mungu
wala hawaelewi mpango wake:
Kwamba amewakusanya pamoja,
kama miganda mahali pa kupuria.
13Mwenyezi-Mungu asema,
“Enyi watu wa Siyoni,
inukeni mkawaadhibu adui zenu!
Nitawapeni nguvu kama fahali
mwenye pembe za chuma na kwato za shaba.
Mtawasaga watu wa mataifa mengi;
mapato yao mtaniwekea wakfu mimi,
mali zao mtanitolea mimi Bwana wa dunia yote.”


Mika4;1-13

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

No comments: