Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 1 July 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Mika 5...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Nagaagaa chini mavumbini; unipe tena uhai kama ulivyoahidi. Nimeungama niliyotenda, nawe ukanijibu; unifundishe masharti yako. Unifundishe namna ya kushika kanuni zako, nami nitayatafakari matendo yako ya ajabu.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Niko hoi kwa uchungu; unirudishie nguvu kama ulivyoahidi. Uniepushe na njia za upotovu; unifundishe kwa wema sheria yako.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Nimechagua njia ya uaminifu; nimezingatia maagizo yako. Nazingatia maamuzi yako, ee Mwenyezi-Mungu; usikubali niaibishwe! Nitafuata maelekezo ya amri zako, maana unanipa maarifa zaidi.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Kiongozi mpya kutoka Bethlehemu
1Jumuikeni mkajikusanye enyi watu wa Yerusalemu;
mkisema: “Tumezingirwa, tumesongwa;
naye kiongozi wa Israeli wanampiga shavuni kwa fimbo.”
2Mwenyezi-Mungu asema,
“Lakini wewe Bethlehemu katika Efratha,
wewe ni mdogo tu kati ya jamii za Yuda,
lakini kwako kutatoka mtawala
atakayetawala juu ya Israeli kwa niaba yangu.
Asili yake ni ya zama za kale.”
3Hivyo Mungu atawaacha watu wake kwa maadui,
mpaka yule mama mjamzito atakapojifungua.
Kisha ndugu zake waliobakia,
watarudi na kuungana na Waisraeli wenzao.
4Huyo mtawala atawachunga watu wake kwa nguvu ya Mwenyezi-Mungu,
kwa fahari yake Mwenyezi-Mungu, Mungu wake.
Watu wake wataishi kwa usalama,
maana atakuwa mkuu mpaka miisho ya dunia.
5Yeye ndiye atakayeleta amani.
Ukombozi na adhabu
Waashuru wakivamia nchi yetu,
na kuupenya ulinzi wetu,
tutapeleka walinzi wawakabili,
naam, tutawapeleka viongozi wetu kwa wingi.
6Kwa silaha zao wataitawala nchi ya Ashuru,
na kuimiliki nchi ya Nimrodi.5:5 kadiri ya Mwanzo 10:8-11 Nimrodi alikuwa babu wa watu walioishi huko Mesopotamia.
Watatuokoa mikononi mwa Waashuru,
watakapowasili mipakani mwa nchi yetu
na kuanza kuivamia nchi yetu.
7Wazawa wa Yakobo watakaobaki hai
wameenea miongoni mwa mataifa mengi,
watakuwa kama umande wa Mwenyezi-Mungu uburudishao,
kama manyunyu yaangukayo penye nyasi
ambayo hayasababishwi na mtu
wala kumtegemea binadamu.
8Wazawa wa Yakobo watakaobaki hai,
wameenea miongoni mwa mataifa na watu wengi
watakuwa na nguvu kubwa
kama simba kati ya wanyama wa porini,
kama mwanasimba miongoni mwa makundi ya kondoo,
ambaye kila mahali apitapo,
huyarukia na kuyararua mawindo yake,
asiwepo mtu yeyote wa kuyaokoa.
9Waisraeli watawashinda adui zao
na kuwaangamiza kabisa.
10Mwenyezi-Mungu asema,
“Wakati huo nitawaondoa farasi wenu,
na kuyaharibu magari yenu ya farasi.
11Nitaiharibu miji ya nchi yenu,
na kuzibomolea mbali ngome zenu.
12Nitatokomeza matendo yenu ya uchawi,
nanyi hamtakuwa tena na wapiga ramli.
13Nitaziharibu sanamu zenu,
na nguzo zenu za ibada;
nanyi mtakoma kuabudu vitu mlivyotengeneza wenyewe.
14Nitazing'oa sanamu za Ashera kutoka kwenu,
na kuiangamiza miji yenu.
15Kwa hasira na ghadhabu yangu,
nitalipiza kisasi mataifa yote yasiyonitii.”

Mika5;1-15

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

No comments: