Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 2 July 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Mika 6...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Ee Mwenyezi-Mungu, unifundishe kutii masharti yako; nami nitayashika mpaka mwisho. Unieleweshe nipate kuishika sheria yako, niifuate kwa moyo wangu wote. Uniongoze katika njia ya amri zako, maana humo napata furaha yangu.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako,
Tukijinyenyekeza,tukijiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunamomba utusamehe dhambi zetu
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
 ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea

Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Unipe ari ya kuzingatia maamuzi yako, na si kwa ajili ya kupata faida isiyofaa. Uniepushe, nisifuate mambo ya upuuzi; unioneshe njia yako, unipe uhai.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Unitimizie mimi mtumishi wako ahadi yako; ahadi unayowapa wale wanaokuheshimu. Uniokoe na lawama ninazoogopa; maana maagizo yako ni mema. Natamani sana kuzitii kanuni zako; unijalie uhai maana wewe ni mwadilifu.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...

Nawapenda.

Lalamiko la nabii
1Sikilizeni anachosema Mwenyezi-Mungu:
“Wewe nabii, nenda ukailalamikie milima,
navyo vilima visikie sauti yako.”
2Sikilizeni kesi ya Mwenyezi-Mungu enyi milima,
sikilizeni enyi misingi ya kudumu ya dunia!
Mwenyezi-Mungu anayo kesi dhidi ya watu wake.
Yeye atatoa mashtaka dhidi ya Waisraeli.
3Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Enyi watu wangu, nimewatendea nini?
Nimewachosha kwa kitu gani?
Nijibuni!
4Mimi niliwatoa nchini Misri;
niliwakomboa kutoka utumwani;
niliwapeni Mose, Aroni na Miriamu kuwaongoza.
5Enyi watu wangu,
kumbukeni njama za Balaki mfalme wa Moabu,
na jinsi Balaamu mwana wa Beori alivyomjibu.
Kumbukeni yaliyotukia njiani kati ya Shitimu na Gilgali.
Kumbukeni mtambue matendo yangu ya kuwaokoa!”
Swali la watu
6Nimwendee Mwenyezi-Mungu na kitu gani,
nipate kumwabudu Mungu aliye juu?
Je, nimwendee na sadaka za kuteketezwa,
nimtolee ndama wa mwaka mmoja?
7Je, Mwenyezi-Mungu atapendezwa
nikimtolea maelfu ya kondoo madume,
au mito elfu na elfu ya mafuta?
Je, nimtolee mzaliwa wangu wa kwanza
kwa ajili ya kosa langu,
naam, mtoto wangu
kwa ajili ya dhambi yangu?
Jibu la nabii
8Mungu amekuonesha yaliyo mema, ewe mtu;
anachotaka Mwenyezi-Mungu kwako ni hiki:
Kutenda mambo ya haki,
kupenda kuwa na huruma,
na kuishi kwa unyenyekevu na Mungu wako.
9Mwenyezi-Mungu anawaita wakazi wa mji,
na ni jambo la busara sana kumcha yeye:
“Sikilizeni, enyi watu wa Yuda;
sikilizeni enyi mliokusanyika mjini.6:9 maana ya aya hii katika Kiebrania si dhahiri.
10“Je, nitavumilia maovu
yaliyorundikwa nyumbani mwao,
mali zilizopatikana kwa udanganyifu,
na matumizi ya mizani danganyifu,
jambo ambalo ni chukizo?
11Je, naweza kusema hawana hatia
watu wanaotumia mizani ya danganyifu
na mawe ya kupimia yasiyo halali?
12Matajiri wa miji wamejaa dhuluma,
wakazi wake husema uongo,
kila wasemacho ni udanganyifu.
13Kwa hiyo nami, nimeanza kuwaangusha chini,
na kuwaangamiza kwa sababu ya dhambi zenu.
14Mtakula lakini hamtashiba;
ndani mwenu njaa itazidi kuwauma.
Mkiweka akiba haitahifadhiwa,
na mkihifadhi kitu nitakiharibu kwa vita.
15Mtapanda mbegu, lakini hamtavuna.
Mtasindika zeituni, lakini hamtatumia hayo mafuta.
Mtasindika zabibu, lakini hamtakunywa hiyo divai.
16Nyinyi mnafuata mfano mbaya wa mfalme Omri
na mfano wa jamaa ya mfalme Ahabu
na mfano mbaya wa jamaa ya mwanawe, Ahabu,
na mmefuata mashauri yao.
Kwa hiyo nitawaleteeni maangamizi,
na kila mtu atawadharau.
Watu watawadhihaki kila mahali.”

Mika6;1-16

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

No comments: