Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 15 July 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Sefania 2...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Neno lako ni taa ya kuniongoza, na mwanga katika njia yangu. Nimeapa na kuthibitisha kiapo changu, kwamba nitashika maagizo yako adili.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Ee Mwenyezi-Mungu, ninateseka mno; unijalie uhai kama ulivyoahidi. Ee Mwenyezi-Mungu, upokee sala yangu ya shukrani; na kunifundisha maagizo yako. Maisha yangu yamo hatarini daima, lakini siisahau sheria yako.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Waovu wamenitegea mitego, lakini sikiuki kanuni zako. Maamuzi yako ni riziki kubwa kwangu milele; hayo ni furaha ya moyo wangu. Nimekusudia kwa moyo wote kufuata masharti yako milele.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Mwito wa toba
1Kusanyikeni, kusanyikeni enyi taifa la watu wasio na aibu,
2kabla hamjapeperushwa mbali kama makapi,2:2 kabla … makapi: Makala ya Kiebrania si dhahiri.
kabla haijawajia siku ya hasira kali ya Mwenyezi-Mungu,
kabla haijawajia siku ya ghadhabu ya Mwenyezi-Mungu.
3Mtafuteni Mwenyezi-Mungu enyi wanyenyekevu wote nchini,
enyi mnaozitii amri zake.
Tafuteni uadilifu, tafuteni unyenyekevu;
labda mtaiepa siku ya ghadhabu ya Mwenyezi-Mungu.
Maangamizi kwa mataifa ya jirani
4Mji wa Gaza utahamwa,
Ashkeloni utakuwa tupu.
Wakazi wa Ashdodi watatimuliwa mchana,
na wale wa Ekroni watang'olewa.
5Ole wenu wakazi wa nchi za pwani,
watu mnaoishi huko Krete!
Mwenyezi-Mungu ametamka dhidi yenu
enyi wakazi wa Kanaani, nchi ya Filistia:
Mimi nitawaangamiza asibaki hata mkazi mmoja!
6Nanyi nchi za pwani mtafanywa kuwa malisho;
mtakuwa vibanda vya wachungaji
na mazizi ya kondoo.
7Nchi ya pwani itamilikiwa na mabaki ya ukoo wa Yuda.
Watachunga mifugo yao huko.
Nyumba za mji wa Ashkeloni
zitakuwa mahali pao pa kulala.
Maana Mwenyezi-Mungu, Mungu wao atawakumbuka
na kuwarudishia hali yao njema.
8“Nimeyasikia masuto ya Moabu
na dhihaka za Waamoni;
jinsi walivyowasuta watu wangu,
na kujigamba kuiteka nchi yao.
9Kwa hiyo, niishivyo mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi,
mimi Mungu wa Israeli,
Moabu itakuwa kama Sodoma
na Amoni itakuwa kama Gomora.
Nchi zake zitakuwa za viwavi na mashimo ya chumvi,
zitakuwa ukiwa milele.
Watu wangu watakaobaki wataziteka nyara,
watu wa taifa langu waliosalia watazimiliki.”
10Hayo yatakuwa malipo ya kiburi chao,
kwa sababu waliwadhihaki na kujigamba
dhidi ya watu wa Mwenyezi-Mungu wa majeshi.
11Mwenyezi-Mungu atakuwa wa kutisha dhidi yao;
miungu yote ya dunia ataikondesha.
Mataifa yote duniani yatamsujudia;
kila taifa katika mahali pake.
12Nanyi watu wa Kushi pia
mtauawa kwa upanga wake.
13Mwenyezi-Mungu atanyosha mkono wake kaskazini,
na kuiangamiza nchi ya Ashuru.
Ataufanya mji wa Ninewi kuwa ukiwa,
kuwa mahali pakavu kama jangwa.
14Makundi ya mifugo yatalala humo,
kadhalika kila mnyama wa porini.
Tai na yangeyange na korongo wataishi juu ya nguzo zake,
bundi watalia kwenye madirisha yake,
kunguru watalia kwenye vizingiti,
maana nyumba zake za mierezi zitakuwa tupu.
15Je, huu ndio mji uliojivuna na kuishi kwa usalama,
mji uliojisemea, “Ni mimi tu, hakuna mwingine!”
Jinsi gani umekuwa mtupu
na makao ya wanyama wa mwituni!
Kila apitaye karibu atauzomea na kuudharau.

Sefania2;1-15

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

No comments: