Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 10 July 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Habakuki 2...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Niko hoi kwa kukungojea uniokoe; naweka tumaini langu katika neno lako. Macho yangu yanafifia nikingojea ulichoahidi. Nauliza: “Utakuja lini kunifariji?”
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako,
Tukijinyenyekeza,tukijiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunamomba utusamehe dhambi zetu
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
 ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea

Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Nimekunjamana kama kiriba katika moshi, hata hivyo sijasahau masharti yako. Mimi mtumishi wako nitasubiri mpaka lini? Utawaadhibu lini wale wanaonidhulumu? Wenye kiburi wamenichimbia mashimo, watu ambao hawafuati sheria yako.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Amri zako zote ni za kuaminika; watu wananitesa bila haki; unisaidie! Karibu wangefaulu kuniangamiza, lakini mimi sijavunja kanuni zako. Unisalimishe kadiri ya fadhili zako, nipate kuzingatia maamuzi uliyotamka.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...

Nawapenda.

1Mimi nitasimama mahali pa kuchungulia,
na kukaa juu mnarani;
nitakaa macho nione ataniambia nini,
atajibu nini kuhusu lalamiko langu.”
Mungu anamjibu Habakuki
2Kisha, Mwenyezi-Mungu akanijibu hivi:
“Yaandike maono haya;
yaandike wazi juu ya vibao,
anayepitia hapo apate kuyasoma.
3 Taz Ebr 10:37 Maono haya yanangoja wakati wa kufaa;
ni maono ya ukweli juu ya mwisho.
Kama yaonekana kuchelewa, uyasubiri;
hakika yatafika, wala hayatachelewa.
4Andika:
‘Waangalie wenye kiburi, hao wataangamia;
lakini waadilifu wataishi kwa kumwamini Mungu.’”
Waovu wataangamia
5Zaidi ya hayo, divai hupotosha;
mtu mwenye kiburi hatadumu.
Yuko tayari kuwameza wengine kama Kuzimu;
kama vile kifo, hatosheki na kitu.
Hujikusanyia mataifa yote,
na watu wote kama mali yake.
6Kila mtu atamdhihaki mtu wa namna hiyo
na kumtungia misemo ya dhihaka:
“Ole wako unayejirundikia visivyo vyako,
na kuchukua rehani mali za watu lakini hulipi!
Utaendelea kufanya hivyo hadi lini?
7Siku moja wadeni wako watainuka ghafla,
wale wanaokutetemesha wataamka.
Ndipo utakuwa mateka wao.
8Wewe umeyapora mataifa mengi,
lakini wote wanaosalimika watakupora wewe,
kwa mauaji na dhuluma uliyoitendea dunia,
naam, uliyoifanyia miji na wakazi wake wote.
9“Ole wako unayejitajirisha kwa hasara ya mwingine,
ujengaye nyumba yako juu milimani
ukidhani kuwa salama mbali na madhara.
10Lakini kwa mipango yako umeiaibisha jamaa yako.
Kwa kuyaangamiza mataifa mengi,
umeyaangamiza maisha yako mwenyewe.
11Ndiyo maana hata mawe yatalalamika ukutani,
na boriti za nyumba zitayaunga mkono.
12“Ole wako unayejenga mji kwa mauaji
unayesimika jiji kwa maovu!
13Mwenyezi-Mungu wa majeshi husababisha
juhudi za watu zipotelee motoni,
na mataifa yajishughulishe bure.
14 Taz Isa 11:9 Utukufu wa Mwenyezi-Mungu utaenea pote duniani,
kama vile maji yaeneavyo baharini.
15Ole wako unayewalewesha jirani zako,
na kutia sumu katika divai yao
ili upate kuwaona wamekaa uchi.
16Utajaa aibu badala ya heshima.
Utakunywa wewe mwenyewe na kupepesuka!
Mwenyezi-Mungu mwenyewe atakulevya,
na aibu itaifunika heshima yako!
17Maovu uliyoitenda Lebanoni yatakuvamia wewe;
uliwaua wanyama, wanyama nao watakutisha.
Yote hayo yatakupata wewe,
kwa mauaji na dhuluma uliyoitendea dunia,
naam, uliyoifanyia miji na wakazi wake wote.
18“Chafaa nini kinyago alichotengeneza mtu?
Sanamu ni madini yaliyoyeyushwa,
ni kitu cha kueneza udanganyifu!
Mtengeneza sanamu hutumaini alichotengeneza mwenyewe,
kinyago ambacho hakiwezi hata kusema!
19Ole wake mtu aliambiaye gogo: ‘Amka!’
Au jiwe bubu ‘Inuka!’
Je, sanamu yaweza kumfundisha mtu?
Tazama imepakwa dhahabu na fedha,
lakini haina uhai wowote.”
20Lakini Mwenyezi-Mungu yumo katika hekalu lake takatifu;
dunia yote na ikae kimya mbele yake.

Habakuki2;1-20

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

No comments: