Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 3 July 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Mika 7...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Fadhili zako zinijie, ee Mwenyezi-Mungu; uniokoe kama ulivyoahidi. Hapo nitaweza kuwajibu hao wanaonitukana, maana mimi nina imani sana na neno lako.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Unijalie kusema ukweli wako daima, maana tumaini langu liko katika maagizo yako. Nitatii sheria yako daima, nitaishika milele na milele. Nitaishi katika uhuru kamili, maana nazitilia maanani kanuni zako.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Nitawatangazia wafalme maamuzi yako, wala sitaona aibu. Furaha yangu ni kuzitii amri zako, ambazo mimi nazipenda. Naziheshimu na kuzipenda amri zako; nitayatafakari masharti yako.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Lalamiko la nabii
1Ole wangu!
Hali ilivyo ni kama baada ya mavuno;
hakuna tini za mwanzoni ninazotamani.
Ni kama wakati wa kuchuma zabibu
hakuna hata shada moja la zabibu la kula!
2Hakuna mcha Mungu aliyebaki nchini,
hakuna mtu yeyote mnyofu miongoni mwa watu.
Kila mmoja anavizia kumwaga damu;
kila mmoja anamwinda mwenzake amnase.
3Wote ni mabingwa wa kutenda maovu;
viongozi na mahakimu hutaka rushwa.
Wakubwa huonesha wazi nia zao mbaya,
na kufanya hila kuzitekeleza.
4Mwema zaidi kati yao hutaabisha kama mbigili,
aliye mnyofu zaidi ni kama ua wa miiba.
Siku iliyongojewa ya adhabu yao imefika.
Na sasa mahangaiko yamewakumba.
5Usimwamini mwenzako,
wala usimtumainie rafiki yako.
Chunga unachosema kwa mdomo wako,
hata na mke wako wewe mwenyewe.
6Maana, mtoto wa kiume anamdharau baba yake;
mtoto wa kike anashindana na mama yake,
mke wa mwana anapingana na mama mkwe wake.
Maadui wa mtu ni watu wa nyumbani mwake.
7Lakini mimi namtumainia Mwenyezi-Mungu,
namtazamia Mungu mwenye kuniokoa;
Mungu wangu atanisikiliza.
Tumaini na sala ya watu
8Usifurahie maafa yangu ewe adui yangu!7:8 hapa na aya zifuatazo yaani 9-10 nabii anaongea kwa niaba ya watu.
Nikianguka, nitainuka tena;
Nikiwa gizani, Mwenyezi-Mungu ni mwanga wangu.
9Kwa vile nimemkosea Mwenyezi-Mungu,
sina budi kuvumilia ghadhabu yake,
mpaka atakapotetea kisa changu
na kunijalia haki yangu.
Atanileta nje kwenye mwanga,
nami nitaona akithibitisha haki.
10Hapo adui yangu ataona hayo
naye atajaa aibu;
maana aliniambia: “Wapi basi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako?”
Mimi mwenyewe nitamwona adui akianguka;
atakanyagwakanyagwa chini kama tope la njiani.
11Siku yaja ambapo kuta za mji wenu zitajengwa upya.
Siku hiyo mipaka ya nchi yenu itapanuliwa.
12Siku hiyo ndugu zenu watawarudia,
kutoka Ashuru na vijiji vya Misri,
kutoka nchi ya Misri na eneo la Eufrate;
kutoka sehemu za maji na sehemu za milima.
13Lakini nchi yote nyingine itakuwa jangwa,
kwa sababu ya uovu wa wakazi wake.
Maombi
14Ee Mungu, uwachunge watu wako kwa fimbo yako,
uwachunge hao walio kundi lako mwenyewe
ambao wanaishi peke yao katika msitu
wamezungukwa na ardhi yenye rutuba.
Uwachunge kama ulivyofanya pale awali
katika malisho ya Bashani na Gileadi.
15Kama wakati ulipotutoa nchini Misri,
utuoneshe7:15 Utuoneshe: Makala ya Kiebrania: Nitawaonyesheni. Katika aya 15 mpaka 20 nabii anaongea tena kwa niaba ya watu (taz pia aya 8-10). tena maajabu yako.
16Nao watu wa mataifa watakapoona hayo,
watajaa fedheha hata kama wana nguvu.
Watashikwa na bumbuazi na kukosa cha kusema
na kuwa kama viziwi.
17Watatambaa mavumbini kama nyoka;
naam, kama viumbe watambaao.
Watatoka katika ngome zao
huku wanatetemeka na kujaa hofu.
Watakugeukia wewe Mungu wetu kwa hofu,
wataogopa kwa sababu yako.
18Ee Mungu, ni nani aliye kama wewe?
Wewe wasamehe dhambi za watu wako waliobaki,
wala huyaangalii makosa yao.
Hasira yako haidumu milele,
ila wapendelea zaidi kutuonesha fadhili zako.
19Utatuhurumia tena, ee Mwenyezi-Mungu;
utafutilia mbali dhambi zetu,
utazitupa zote katika vilindi vya bahari.
20Utaonesha uaminifu wako na rehema zako
kwa wazawa wa Abrahamu na wa Yakobo,
kama ulivyowaahidi wazee wetu tangu zamani.

Mika7;1-20

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

No comments: