Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 25 June 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Tunamshukuru Mungu kwa kumaliza Kitabu cha Yona,Leo Tunaanza Kitabu cha Mika....1

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tunamshukuru Mungu kwa kutupa kibali cha
 kupitia kitabu cha "YONA
"
Ni matumaini yangu kuna mengi tumejifunza/kufaidika
na kutupa mwanga/kuelewa kwenye kitabu hiki...

Leo tunapokwenda anza kupitia Kitabu cha"MIKA"tunamuomba Mungu wetu akatupe kibali,macho ya rohoni
 na akili ya kuelewa katika kujifunza NENO lake...
Ee Mungu  tunaomba ukatuongoze...!!
Tumshukuru Mungu wetu katika yote...Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...


Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Kisha Elifazi, Mtemani, akajibu: “Je, mtu wa hekima hujibu kwa maneno ya upuuzi? Je, mtu huyo amejaa maneno matupu? Je, mwenye hekima hujitetea kwa maneno yasiyofaa, au kwa maneno yasiyo na maana?
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....


Lakini wewe unapuuza uchaji wa Mungu; na kuzuia kutafakari mbele ya Mungu. Uovu wako ndio unaokifundisha kinywa chako, nawe wachagua kusema kama wadanganyifu.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Maneno yako mwenyewe yanakuhukumu, sio mimi; matamshi yako yashuhudia dhidi yako. Je, wewe ni mtu wa kwanza kuzaliwa? Je, wewe ulizaliwa kabla ya kuweko vilima? Je, ulipata kuweko katika halmashauri ya Mungu? au, wewe ndiwe peke yako mwenye hekima?
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

1Neno la Mwenyezi-Mungu lilimjia Mika, mwenyeji wa Moreshethi, wakati Yothamu, Ahazi na Hezekia walipokuwa wafalme wa Yuda. Mika aliona mambo yote haya kuhusu Samaria na Yerusalemu.
Mwenyezi-Mungu aja kuhukumu
2Sikilizeni enyi watu wote;
sikiliza ewe dunia na vyote vilivyomo.
Mwenyezi-Mungu anakuja kuwashtaki,
Bwana anena kutoka hekalu lake takatifu.
3Naam! Mwenyezi-Mungu yuaja kutoka makao yake;
atashuka na kutembea juu ya vilele vya dunia.
4Milima itayeyuka chini ya nyayo zake,
kama nta karibu na moto;
mabonde yatapasuka,
kama maji yaporomokayo kwenye mteremko.
5Haya yote yatatukia
kwa sababu ya makosa ya wazawa wa Yakobo,
kwa sababu ya dhambi za wazawa wa Israeli.
Je, uhalifu wa Yakobo waonekana wapi?
Katika mji wake mkuu Samaria!
Je, uhalifu wa Yuda waonekana wapi?
Katika Yerusalemu kwenyewe!
6Kwa hiyo, Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Mji wa Samaria nitaufanya magofu nyikani,
shamba ambalo watu watapanda mizabibu.
Mawe yaliyoujenga nitayatupa bondeni,
na misingi yake nitaichimbuachimbua.
7Sanamu zake zote zitavunjwavunjwa,
kila kilichochumwa kitateketezwa kwa moto.
Vinyago vyake vyote nitaviharibu.
Vilirundikwa kutokana na ujira wa malaya,
navyo vitatumiwa tena kulipia umalaya.”
Nabii anaomboleza juu ya Yerusalemu na Yuda
8Kwa sababu hiyo, mimi nitalia na kuomboleza;
nitatembea uchi na bila viatu.
Nitaomboleza na kulia kama mbweha,
nitasikitika na kulia kama mbuni.
9Majeraha ya Samaria hayaponyeki,
nayo yameipata pia Yuda;
yamefikia lango la Yerusalemu,
mahali wanapokaa watu wangu.
10Msiitangaze habari hii huko Gathi,
wala msilie machozi!
Huko Beth-leafra mgaegae mavumbini kwa huzuni.
11Nendeni enyi wakazi wa Shafiri,
mkiwa uchi na wenye haya.
Wakazi wa Zaanani msitoke nje ya mji wenu.
Watu wa Beth-ezeli wanalia;
msaada wao kwenu umeondolewa.
12Wakazi wa Marothi wanangojea msaada kwa hamu kubwa,
lakini maangamizi yaja kutoka kwa Mwenyezi-Mungu
karibu kabisa na lango la Yerusalemu.
13Enyi wakazi wa Lakishi,
fungeni farasi wepesi na magari ya vita.
Nyinyi mlikuwa mmeiga dhambi ya watu wa Siyoni,
makosa ya Waisraeli yalikuwa kwenu.
14Hivyo, mnapaswa kuagana na kuwaacha wakazi wa Morasheth-gathi.
Nao mji wa Akzibu hautawasaidia wafalme wa Israeli,
15Enyi wakazi wa Maresha,
Mungu atawaleteeni tena adui atakayewateka.
Viongozi waheshimiwa wa Israeli
watakimbilia pangoni huko Adulamu.
16Enyi watu wa Yuda, nyoeni upara
kuwaombolezea watoto wenu wapenzi;
panueni upara wenu uwe mpana kama wa tai,
maana watoto wenu watawaacha kwenda uhamishoni.

Mika1;1-16

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

No comments: