Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 6 July 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Tunamshukuru Mungu kwa kumaliza Kitabu cha Mika,Leo Tunaanza Kitabu cha Nahumu....1


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?
Haleluyah ni siku/wiki/mwezi mwingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....
Tunamshukuru Mungu kwa kutupa kibali cha
 kupitia kitabu cha "MIKA
"
Ni matumaini yangu kuna mengi tumejifunza/kufaidika
na kutupa mwanga/kuelewa kwenye kitabu hiki...

Leo tunapokwenda anza kupitia Kitabu cha"NAHUMU"tunamuomba Mungu wetu akatupe kibali,macho ya rohoni
 na akili ya kuelewa katika kujifunza NENO lake...
Ee Mungu  tunaomba ukatuongoze...!!
Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Ukumbuke ahadi yako kwangu mimi mtumishi wako, ahadi ambayo imenipa matumaini. Hata niwapo taabuni napata kitulizo, maana ahadi yako yanipa uhai.
Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...


Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Wasiomjali Mungu hunidharau daima, lakini mimi sikiuki sheria yako. Ninapoyakumbuka maagizo yako ya tangu kale, nafarijika, ee Mwenyezi-Mungu.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Nashikwa na hasira kali, nionapo waovu wakivunja sheria yako. Masharti yako yamekuwa wimbo wangu, nikiwa huku ugenini. Usiku ninakukumbuka, ee Mwenyezi-Mungu, na kushika sheria yako. Hii ni baraka kubwa kwangu, kwamba nazishika kanuni zako.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

1Kauli ya Mungu juu ya Ninewi. Kitabu cha maono ya Nahumu wa Elkoshi.
Ghadhabu ya Mungu dhidi ya Ninewi
2Mwenyezi-Mungu ni Mungu mwenye wivu, mlipiza kisasi;
Mwenyezi-Mungu hulipiza kisasi na ni mwenye ghadhabu;
Mwenyezi-Mungu hulipiza kisasi kwa adui zake,
huwaka ghadhabu juu ya adui zake.
3Mwenyezi-Mungu hakasiriki upesi, lakini amejaa nguvu,
Mwenyezi-Mungu kamwe hatawaachilia wenye hatia.
Apitapo Mwenyezi-Mungu, huzuka kimbunga na dhoruba;
mawingu ni vumbi litimuliwalo na nyayo zake.
4Huikaripia bahari na kuikausha,
yeye huikausha mito yote.
Mbuga za Bashani na mlima Karmeli hunyauka,
maua ya Lebanoni hudhoofika.
5Milima hutetemeka mbele yake,
navyo vilima huyeyuka;
dunia hutetemeka mbele yake,
ulimwengu na vyote vilivyomo.
6Nani awezaye kuikabili ghadhabu ya Mwenyezi-Mungu?
Nani awezaye kustahimili ukali wa hasira yake?
Yeye huimwaga hasira yake iwakayo kama moto,
hata miamba huipasua vipandevipande.
7Mwenyezi-Mungu ni mwema,
yeye ni ngome ya usalama wakati wa taabu.
Yeye huwalinda wote wanaokimbilia usalama kwake.
8Adui wakiivamia nchi kama mafuriko, yeye huwaangamiza;
huwafuatia na kuwafukuza mpaka gizani.
9Mbona mnafanya mipango dhidi ya Mwenyezi-Mungu?
Yeye atawakomesha na kuwaangamiza,
wala mpinzani wake hataweza kuinuka tena.
10 1:10 maana ya aya hii katika Kiebrania si dhahiri.Watateketezwa kama kichaka cha miiba,
kama vile nyasi zilizokauka.
11Kwako kumetoka aliyepanga maovu dhidi ya Mwenyezi-Mungu
aliyefanya njama za ulaghai.
12Mwenyezi-Mungu awaambia hivi watu wake:
“Ingawa Waashuru ni wengi na wenye nguvu,
wao wataangushwa na kuangamizwa.
Ingawa nimewatesa nyinyi watu wangu,
sitawateseni tena zaidi.
13Sasa nitaivunja nira ya Ashuru shingoni mwenu,
na minyororo waliyowafungia nitaikatakata.”
14Mwenyezi-Mungu ameamuru hivi kuhusu Ninewi:
“Hutapata wazawa kulidumisha jina lako.
Sanamu zako za kuchonga na za kusubu,
nitazivunjavunja nyumbani mwa miungu yako.
Mimi nitakuchimbia kaburi lako,
maana wewe hufai kitu chochote.”
15Enyi watu wa Yuda tazameni:
Anakuja kutoka mlimani mtu anayeleta habari njema,
mjumbe ambaye anatangaza amani.
Adhimisheni sikukuu zenu, enyi watu wa Yuda,
timizeni nadhiri zenu,
maana waovu hawatawavamia tena,
kwani wameangamizwa kabisa.

Nahumu1;1-15

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

Friday 3 July 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Mika 7...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Fadhili zako zinijie, ee Mwenyezi-Mungu; uniokoe kama ulivyoahidi. Hapo nitaweza kuwajibu hao wanaonitukana, maana mimi nina imani sana na neno lako.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Unijalie kusema ukweli wako daima, maana tumaini langu liko katika maagizo yako. Nitatii sheria yako daima, nitaishika milele na milele. Nitaishi katika uhuru kamili, maana nazitilia maanani kanuni zako.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Nitawatangazia wafalme maamuzi yako, wala sitaona aibu. Furaha yangu ni kuzitii amri zako, ambazo mimi nazipenda. Naziheshimu na kuzipenda amri zako; nitayatafakari masharti yako.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Lalamiko la nabii
1Ole wangu!
Hali ilivyo ni kama baada ya mavuno;
hakuna tini za mwanzoni ninazotamani.
Ni kama wakati wa kuchuma zabibu
hakuna hata shada moja la zabibu la kula!
2Hakuna mcha Mungu aliyebaki nchini,
hakuna mtu yeyote mnyofu miongoni mwa watu.
Kila mmoja anavizia kumwaga damu;
kila mmoja anamwinda mwenzake amnase.
3Wote ni mabingwa wa kutenda maovu;
viongozi na mahakimu hutaka rushwa.
Wakubwa huonesha wazi nia zao mbaya,
na kufanya hila kuzitekeleza.
4Mwema zaidi kati yao hutaabisha kama mbigili,
aliye mnyofu zaidi ni kama ua wa miiba.
Siku iliyongojewa ya adhabu yao imefika.
Na sasa mahangaiko yamewakumba.
5Usimwamini mwenzako,
wala usimtumainie rafiki yako.
Chunga unachosema kwa mdomo wako,
hata na mke wako wewe mwenyewe.
6Maana, mtoto wa kiume anamdharau baba yake;
mtoto wa kike anashindana na mama yake,
mke wa mwana anapingana na mama mkwe wake.
Maadui wa mtu ni watu wa nyumbani mwake.
7Lakini mimi namtumainia Mwenyezi-Mungu,
namtazamia Mungu mwenye kuniokoa;
Mungu wangu atanisikiliza.
Tumaini na sala ya watu
8Usifurahie maafa yangu ewe adui yangu!7:8 hapa na aya zifuatazo yaani 9-10 nabii anaongea kwa niaba ya watu.
Nikianguka, nitainuka tena;
Nikiwa gizani, Mwenyezi-Mungu ni mwanga wangu.
9Kwa vile nimemkosea Mwenyezi-Mungu,
sina budi kuvumilia ghadhabu yake,
mpaka atakapotetea kisa changu
na kunijalia haki yangu.
Atanileta nje kwenye mwanga,
nami nitaona akithibitisha haki.
10Hapo adui yangu ataona hayo
naye atajaa aibu;
maana aliniambia: “Wapi basi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako?”
Mimi mwenyewe nitamwona adui akianguka;
atakanyagwakanyagwa chini kama tope la njiani.
11Siku yaja ambapo kuta za mji wenu zitajengwa upya.
Siku hiyo mipaka ya nchi yenu itapanuliwa.
12Siku hiyo ndugu zenu watawarudia,
kutoka Ashuru na vijiji vya Misri,
kutoka nchi ya Misri na eneo la Eufrate;
kutoka sehemu za maji na sehemu za milima.
13Lakini nchi yote nyingine itakuwa jangwa,
kwa sababu ya uovu wa wakazi wake.
Maombi
14Ee Mungu, uwachunge watu wako kwa fimbo yako,
uwachunge hao walio kundi lako mwenyewe
ambao wanaishi peke yao katika msitu
wamezungukwa na ardhi yenye rutuba.
Uwachunge kama ulivyofanya pale awali
katika malisho ya Bashani na Gileadi.
15Kama wakati ulipotutoa nchini Misri,
utuoneshe7:15 Utuoneshe: Makala ya Kiebrania: Nitawaonyesheni. Katika aya 15 mpaka 20 nabii anaongea tena kwa niaba ya watu (taz pia aya 8-10). tena maajabu yako.
16Nao watu wa mataifa watakapoona hayo,
watajaa fedheha hata kama wana nguvu.
Watashikwa na bumbuazi na kukosa cha kusema
na kuwa kama viziwi.
17Watatambaa mavumbini kama nyoka;
naam, kama viumbe watambaao.
Watatoka katika ngome zao
huku wanatetemeka na kujaa hofu.
Watakugeukia wewe Mungu wetu kwa hofu,
wataogopa kwa sababu yako.
18Ee Mungu, ni nani aliye kama wewe?
Wewe wasamehe dhambi za watu wako waliobaki,
wala huyaangalii makosa yao.
Hasira yako haidumu milele,
ila wapendelea zaidi kutuonesha fadhili zako.
19Utatuhurumia tena, ee Mwenyezi-Mungu;
utafutilia mbali dhambi zetu,
utazitupa zote katika vilindi vya bahari.
20Utaonesha uaminifu wako na rehema zako
kwa wazawa wa Abrahamu na wa Yakobo,
kama ulivyowaahidi wazee wetu tangu zamani.

Mika7;1-20

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

Thursday 2 July 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Mika 6...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Ee Mwenyezi-Mungu, unifundishe kutii masharti yako; nami nitayashika mpaka mwisho. Unieleweshe nipate kuishika sheria yako, niifuate kwa moyo wangu wote. Uniongoze katika njia ya amri zako, maana humo napata furaha yangu.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako,
Tukijinyenyekeza,tukijiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunamomba utusamehe dhambi zetu
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
 ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea

Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Unipe ari ya kuzingatia maamuzi yako, na si kwa ajili ya kupata faida isiyofaa. Uniepushe, nisifuate mambo ya upuuzi; unioneshe njia yako, unipe uhai.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Unitimizie mimi mtumishi wako ahadi yako; ahadi unayowapa wale wanaokuheshimu. Uniokoe na lawama ninazoogopa; maana maagizo yako ni mema. Natamani sana kuzitii kanuni zako; unijalie uhai maana wewe ni mwadilifu.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...

Nawapenda.

Lalamiko la nabii
1Sikilizeni anachosema Mwenyezi-Mungu:
“Wewe nabii, nenda ukailalamikie milima,
navyo vilima visikie sauti yako.”
2Sikilizeni kesi ya Mwenyezi-Mungu enyi milima,
sikilizeni enyi misingi ya kudumu ya dunia!
Mwenyezi-Mungu anayo kesi dhidi ya watu wake.
Yeye atatoa mashtaka dhidi ya Waisraeli.
3Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Enyi watu wangu, nimewatendea nini?
Nimewachosha kwa kitu gani?
Nijibuni!
4Mimi niliwatoa nchini Misri;
niliwakomboa kutoka utumwani;
niliwapeni Mose, Aroni na Miriamu kuwaongoza.
5Enyi watu wangu,
kumbukeni njama za Balaki mfalme wa Moabu,
na jinsi Balaamu mwana wa Beori alivyomjibu.
Kumbukeni yaliyotukia njiani kati ya Shitimu na Gilgali.
Kumbukeni mtambue matendo yangu ya kuwaokoa!”
Swali la watu
6Nimwendee Mwenyezi-Mungu na kitu gani,
nipate kumwabudu Mungu aliye juu?
Je, nimwendee na sadaka za kuteketezwa,
nimtolee ndama wa mwaka mmoja?
7Je, Mwenyezi-Mungu atapendezwa
nikimtolea maelfu ya kondoo madume,
au mito elfu na elfu ya mafuta?
Je, nimtolee mzaliwa wangu wa kwanza
kwa ajili ya kosa langu,
naam, mtoto wangu
kwa ajili ya dhambi yangu?
Jibu la nabii
8Mungu amekuonesha yaliyo mema, ewe mtu;
anachotaka Mwenyezi-Mungu kwako ni hiki:
Kutenda mambo ya haki,
kupenda kuwa na huruma,
na kuishi kwa unyenyekevu na Mungu wako.
9Mwenyezi-Mungu anawaita wakazi wa mji,
na ni jambo la busara sana kumcha yeye:
“Sikilizeni, enyi watu wa Yuda;
sikilizeni enyi mliokusanyika mjini.6:9 maana ya aya hii katika Kiebrania si dhahiri.
10“Je, nitavumilia maovu
yaliyorundikwa nyumbani mwao,
mali zilizopatikana kwa udanganyifu,
na matumizi ya mizani danganyifu,
jambo ambalo ni chukizo?
11Je, naweza kusema hawana hatia
watu wanaotumia mizani ya danganyifu
na mawe ya kupimia yasiyo halali?
12Matajiri wa miji wamejaa dhuluma,
wakazi wake husema uongo,
kila wasemacho ni udanganyifu.
13Kwa hiyo nami, nimeanza kuwaangusha chini,
na kuwaangamiza kwa sababu ya dhambi zenu.
14Mtakula lakini hamtashiba;
ndani mwenu njaa itazidi kuwauma.
Mkiweka akiba haitahifadhiwa,
na mkihifadhi kitu nitakiharibu kwa vita.
15Mtapanda mbegu, lakini hamtavuna.
Mtasindika zeituni, lakini hamtatumia hayo mafuta.
Mtasindika zabibu, lakini hamtakunywa hiyo divai.
16Nyinyi mnafuata mfano mbaya wa mfalme Omri
na mfano wa jamaa ya mfalme Ahabu
na mfano mbaya wa jamaa ya mwanawe, Ahabu,
na mmefuata mashauri yao.
Kwa hiyo nitawaleteeni maangamizi,
na kila mtu atawadharau.
Watu watawadhihaki kila mahali.”

Mika6;1-16

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

Wednesday 1 July 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Mika 5...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Nagaagaa chini mavumbini; unipe tena uhai kama ulivyoahidi. Nimeungama niliyotenda, nawe ukanijibu; unifundishe masharti yako. Unifundishe namna ya kushika kanuni zako, nami nitayatafakari matendo yako ya ajabu.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Niko hoi kwa uchungu; unirudishie nguvu kama ulivyoahidi. Uniepushe na njia za upotovu; unifundishe kwa wema sheria yako.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Nimechagua njia ya uaminifu; nimezingatia maagizo yako. Nazingatia maamuzi yako, ee Mwenyezi-Mungu; usikubali niaibishwe! Nitafuata maelekezo ya amri zako, maana unanipa maarifa zaidi.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Kiongozi mpya kutoka Bethlehemu
1Jumuikeni mkajikusanye enyi watu wa Yerusalemu;
mkisema: “Tumezingirwa, tumesongwa;
naye kiongozi wa Israeli wanampiga shavuni kwa fimbo.”
2Mwenyezi-Mungu asema,
“Lakini wewe Bethlehemu katika Efratha,
wewe ni mdogo tu kati ya jamii za Yuda,
lakini kwako kutatoka mtawala
atakayetawala juu ya Israeli kwa niaba yangu.
Asili yake ni ya zama za kale.”
3Hivyo Mungu atawaacha watu wake kwa maadui,
mpaka yule mama mjamzito atakapojifungua.
Kisha ndugu zake waliobakia,
watarudi na kuungana na Waisraeli wenzao.
4Huyo mtawala atawachunga watu wake kwa nguvu ya Mwenyezi-Mungu,
kwa fahari yake Mwenyezi-Mungu, Mungu wake.
Watu wake wataishi kwa usalama,
maana atakuwa mkuu mpaka miisho ya dunia.
5Yeye ndiye atakayeleta amani.
Ukombozi na adhabu
Waashuru wakivamia nchi yetu,
na kuupenya ulinzi wetu,
tutapeleka walinzi wawakabili,
naam, tutawapeleka viongozi wetu kwa wingi.
6Kwa silaha zao wataitawala nchi ya Ashuru,
na kuimiliki nchi ya Nimrodi.5:5 kadiri ya Mwanzo 10:8-11 Nimrodi alikuwa babu wa watu walioishi huko Mesopotamia.
Watatuokoa mikononi mwa Waashuru,
watakapowasili mipakani mwa nchi yetu
na kuanza kuivamia nchi yetu.
7Wazawa wa Yakobo watakaobaki hai
wameenea miongoni mwa mataifa mengi,
watakuwa kama umande wa Mwenyezi-Mungu uburudishao,
kama manyunyu yaangukayo penye nyasi
ambayo hayasababishwi na mtu
wala kumtegemea binadamu.
8Wazawa wa Yakobo watakaobaki hai,
wameenea miongoni mwa mataifa na watu wengi
watakuwa na nguvu kubwa
kama simba kati ya wanyama wa porini,
kama mwanasimba miongoni mwa makundi ya kondoo,
ambaye kila mahali apitapo,
huyarukia na kuyararua mawindo yake,
asiwepo mtu yeyote wa kuyaokoa.
9Waisraeli watawashinda adui zao
na kuwaangamiza kabisa.
10Mwenyezi-Mungu asema,
“Wakati huo nitawaondoa farasi wenu,
na kuyaharibu magari yenu ya farasi.
11Nitaiharibu miji ya nchi yenu,
na kuzibomolea mbali ngome zenu.
12Nitatokomeza matendo yenu ya uchawi,
nanyi hamtakuwa tena na wapiga ramli.
13Nitaziharibu sanamu zenu,
na nguzo zenu za ibada;
nanyi mtakoma kuabudu vitu mlivyotengeneza wenyewe.
14Nitazing'oa sanamu za Ashera kutoka kwenu,
na kuiangamiza miji yenu.
15Kwa hasira na ghadhabu yangu,
nitalipiza kisasi mataifa yote yasiyonitii.”

Mika5;1-15

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe