Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 10 July 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Habakuki 2...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Niko hoi kwa kukungojea uniokoe; naweka tumaini langu katika neno lako. Macho yangu yanafifia nikingojea ulichoahidi. Nauliza: “Utakuja lini kunifariji?”
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako,
Tukijinyenyekeza,tukijiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunamomba utusamehe dhambi zetu
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
 ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea

Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Nimekunjamana kama kiriba katika moshi, hata hivyo sijasahau masharti yako. Mimi mtumishi wako nitasubiri mpaka lini? Utawaadhibu lini wale wanaonidhulumu? Wenye kiburi wamenichimbia mashimo, watu ambao hawafuati sheria yako.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Amri zako zote ni za kuaminika; watu wananitesa bila haki; unisaidie! Karibu wangefaulu kuniangamiza, lakini mimi sijavunja kanuni zako. Unisalimishe kadiri ya fadhili zako, nipate kuzingatia maamuzi uliyotamka.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...

Nawapenda.

1Mimi nitasimama mahali pa kuchungulia,
na kukaa juu mnarani;
nitakaa macho nione ataniambia nini,
atajibu nini kuhusu lalamiko langu.”
Mungu anamjibu Habakuki
2Kisha, Mwenyezi-Mungu akanijibu hivi:
“Yaandike maono haya;
yaandike wazi juu ya vibao,
anayepitia hapo apate kuyasoma.
3 Taz Ebr 10:37 Maono haya yanangoja wakati wa kufaa;
ni maono ya ukweli juu ya mwisho.
Kama yaonekana kuchelewa, uyasubiri;
hakika yatafika, wala hayatachelewa.
4Andika:
‘Waangalie wenye kiburi, hao wataangamia;
lakini waadilifu wataishi kwa kumwamini Mungu.’”
Waovu wataangamia
5Zaidi ya hayo, divai hupotosha;
mtu mwenye kiburi hatadumu.
Yuko tayari kuwameza wengine kama Kuzimu;
kama vile kifo, hatosheki na kitu.
Hujikusanyia mataifa yote,
na watu wote kama mali yake.
6Kila mtu atamdhihaki mtu wa namna hiyo
na kumtungia misemo ya dhihaka:
“Ole wako unayejirundikia visivyo vyako,
na kuchukua rehani mali za watu lakini hulipi!
Utaendelea kufanya hivyo hadi lini?
7Siku moja wadeni wako watainuka ghafla,
wale wanaokutetemesha wataamka.
Ndipo utakuwa mateka wao.
8Wewe umeyapora mataifa mengi,
lakini wote wanaosalimika watakupora wewe,
kwa mauaji na dhuluma uliyoitendea dunia,
naam, uliyoifanyia miji na wakazi wake wote.
9“Ole wako unayejitajirisha kwa hasara ya mwingine,
ujengaye nyumba yako juu milimani
ukidhani kuwa salama mbali na madhara.
10Lakini kwa mipango yako umeiaibisha jamaa yako.
Kwa kuyaangamiza mataifa mengi,
umeyaangamiza maisha yako mwenyewe.
11Ndiyo maana hata mawe yatalalamika ukutani,
na boriti za nyumba zitayaunga mkono.
12“Ole wako unayejenga mji kwa mauaji
unayesimika jiji kwa maovu!
13Mwenyezi-Mungu wa majeshi husababisha
juhudi za watu zipotelee motoni,
na mataifa yajishughulishe bure.
14 Taz Isa 11:9 Utukufu wa Mwenyezi-Mungu utaenea pote duniani,
kama vile maji yaeneavyo baharini.
15Ole wako unayewalewesha jirani zako,
na kutia sumu katika divai yao
ili upate kuwaona wamekaa uchi.
16Utajaa aibu badala ya heshima.
Utakunywa wewe mwenyewe na kupepesuka!
Mwenyezi-Mungu mwenyewe atakulevya,
na aibu itaifunika heshima yako!
17Maovu uliyoitenda Lebanoni yatakuvamia wewe;
uliwaua wanyama, wanyama nao watakutisha.
Yote hayo yatakupata wewe,
kwa mauaji na dhuluma uliyoitendea dunia,
naam, uliyoifanyia miji na wakazi wake wote.
18“Chafaa nini kinyago alichotengeneza mtu?
Sanamu ni madini yaliyoyeyushwa,
ni kitu cha kueneza udanganyifu!
Mtengeneza sanamu hutumaini alichotengeneza mwenyewe,
kinyago ambacho hakiwezi hata kusema!
19Ole wake mtu aliambiaye gogo: ‘Amka!’
Au jiwe bubu ‘Inuka!’
Je, sanamu yaweza kumfundisha mtu?
Tazama imepakwa dhahabu na fedha,
lakini haina uhai wowote.”
20Lakini Mwenyezi-Mungu yumo katika hekalu lake takatifu;
dunia yote na ikae kimya mbele yake.

Habakuki2;1-20

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

Thursday 9 July 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Tunamshukuru Mungu kwa kumaliza Kitabu cha Nahumu,Leo Tunaanza Kitabu cha Habakuki....1

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tunamshukuru Mungu kwa kutupa kibali cha
 kupitia kitabu cha "Nahumu
"
Ni matumaini yangu kuna mengi tumejifunza/kufaidika
na kutupa mwanga/kuelewa kwenye kitabu hiki...

Leo tunapokwenda anza kupitia Kitabu cha"Habakuki"tunamuomba Mungu wetu akatupe kibali,macho ya rohoni
 na akili ya kuelewa katika kujifunza NENO lake...
Ee Mungu  tunaomba ukatuongoze...!!
Tumshukuru Mungu wetu katika yote...Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...


Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Mikono yako iliniumba na kuniunda; unijalie akili nijifunze amri zako. Wakuchao wataniona na kufurahi, maana tumaini langu liko katika neno lako.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Najua hukumu zako ni adili, ee Mwenyezi-Mungu, na kwamba umeniadhibu kwani wewe ni mwaminifu. Fadhili zako na zinipe faraja, kama ulivyoniahidi mimi mtumishi wako. Unionee huruma nipate kuishi, maana sheria yako ni furaha yangu.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Wenye kiburi waaibike kwa maana wamenifanyia hila, lakini mimi nitazitafakari kanuni zako. Wote wakuchao na waje kwangu, wapate kuyajua maamuzi yako. Moyo wangu na uzingatie masharti yako, nisije nikaaibishwa.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

1Kauli ya Mungu aliyoiona nabii Habakuki.
Lalamiko la nabii
2“Ee Mwenyezi-Mungu, nitakulilia mpaka lini,
nawe usinisikilize na kunisaidia?
Kwa nini nalia: ‘Dhuluma’
nawe hutuokoi?
3Kwa nini wanifanya nishuhudie mabaya na taabu?
Uharibifu na ukatili vinanizunguka,
ugomvi na mashindano yanazuka.
4Hivyo sheria haina nguvu,
wala haki haitekelezwi.
Waovu wanawazunguka waadilifu,
hivyo hukumu hutolewa ikiwa imepotoshwa.”
Jibu la Mungu
5 Taz Mate 13:41 Mungu akasema:
“Yaangalie mataifa, uone!
Utastaajabu na kushangaa.
Maana ninatenda kitu ukiwa bado unaishi,
kitu ambacho ungeambiwa hungesadiki.
6Maana ninawachochea Wakaldayo,
taifa lile kali na lenye hamaki!
Taifa lipitalo katika nchi yote,
ili kunyakua makao ya watu wengine.
7Wao ni watu wa kuchukiza na kutisha;
wao hujiamulia wenyewe nini haki na adhama.
8“Farasi wao ni wepesi kuliko chui;
wakali kuliko mbwamwitu wenye njaa.
Wapandafarasi wao wanatoka mbali,
wanaruka kasi kama tai arukiavyo mawindo.
9“Wote wanakuja kufanya ukatili;
kwa nyuso kakamavu wanasonga mbele,
wanakusanya mateka wengi kama mchanga.
10Wanawadhihaki wafalme,
na kuwadharau watawala.
Kila ngome kwao ni mzaha,
wanairundikia udongo na kuiteka.
11Kisha wanasonga mbele kama upepo,
wafanya makosa na kuwa na hatia,
maana, nguvu zao ndizo mungu wao!”
Habakuki analalamika tena
12“Je, wewe si ndiwe Mwenyezi-Mungu,
tangu kale na kale?
Wewe ndiwe Mungu wangu, Mtakatifu wangu, usiyekufa
Ee Mwenyezi-Mungu, umewateua Wakaldayo watuhukumu;
Ewe Mwamba, umewaimarisha ili watuadhibu!
13Wewe ni mtakatifu kabisa, huwezi kutazama uovu,
huwezi kustahimili kamwe kuona mabaya.
Mbona basi wawaona wafanya maovu na kunyamaza,
kwa nini unanyamaza waovu wanapowamaliza
wale watu walio waadilifu kuliko wao?
14“Umewafanya watu kama samaki baharini,
kama viumbe vitambaavyo visivyo na kiongozi!
15Wakaldayo huwavua watu kwa ndoana,
huwavutia nje kwa wavu wao,
huwakusanya wote katika jarife lao,
kisha hufurahi na kushangilia.
16Kwa hiyo, wanazitambikia nyavu zao,
na kuzifukizia ubani;
maana kwa hizo huweza kuishi kwa anasa,
na kula chakula cha fahari.
17“Je, hawataacha kamwe kuvuta upinde wao?
Je, wataendelea tu kuwanasa watu,
na kuyaangamiza mataifa bila huruma?

Habakuki1;1-17

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

Wednesday 8 July 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Nahumu 3...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Umenitendea vema mimi mtumishi wako, kama ulivyoahidi, ee Mwenyezi-Mungu. Unifundishe akili na maarifa, maana nina imani sana na amri zako.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Kabla ya kuniadhibu nilikuwa nikikosea, lakini sasa nashika neno lako. Wewe ni mwema na mfadhili; unifundishe masharti yako.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Wenye kiburi wanasema uongo juu yangu, lakini mimi nashika kanuni zako kwa moyo wote. Mioyo yao imejaa upumbavu, lakini mimi nafurahia sheria yako. Nimefaidika kutokana na taabu yangu, maana imenifanya nijifunze masharti yako. Sheria uliyoweka ni bora kwangu, kuliko mali zote za dunia.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

1Ole wako mji wa mauaji!
Umejaa udanganyifu mtupu na nyara tele,
usiokoma kamwe kuteka nyara.
2Sikia! Mlio wa mjeledi,
mrindimo wa magurudumu,
vishindo vya farasi
na ngurumo za magari!
3Wapandafarasi wanashambulia,
panga na mikuki inametameta;
waliouawa hawana idadi,
maiti wengi sana;
watu wanajikwaa juu ya maiti!
4Ninewi! Wewe umekuwa kama malaya.
Umewashawishi watu, ewe binti wa uchawi,
uliyeyafanya mataifa kuwa watumwa kwa umalaya wako,
na watu wa mataifa kwa uchawi wako.
5Mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi nasema nitapambana nawe;
nitalipandisha vazi lako hadi kichwani,
niyaache mataifa yauone uchi wako,
tawala ziikodolee macho aibu yako.
6Nitakutupia uchafu,
na kukutendea kwa dharau,
na kukufanya uwe kioja kwa watu.
7Kisha wote watakaokuona watakukimbia wakisema,
“Ninewi umeangamizwa,
ni nani atakayeuombolezea?
Nani atakayekufariji?”
8Je, wewe Ninewi, ni bora kuliko Thebesi,
mji uliojengwa kando ya mto Nili?
Thebesi ulizungukwa na maji,
bahari ilikuwa boma lake,
maji yalikuwa ukuta wake!
9Kushi ilikuwa nguvu yake;
nayo Misri pia, tena bila kikomo;
watu wa Puti na Libia waliusaidia!
10Hata hivyo, ulichukuliwa mateka,
watu wake wakapelekwa uhamishoni.
Hata watoto wake walipondwapondwa
katika pembe ya kila barabara;
watu wake mashuhuri walinadiwa,
wakuu wake wote walifungwa minyororo.
11Ninewi, nawe pia utalewa;
utamkimbia adui na kujaribu kujificha.
12Ngome zako zote ni za tini za mwanzo;
zikitikiswa zinamwangukia mlaji kinywani.
13Tazama askari wako:
Wao ni waoga kama wanawake.
Milango ya nchi yako ni wazi mbele ya adui zako;
moto umeyateketeza kabisa makomeo yake.
14Tekeni maji muwe tayari kuzingirwa;
imarisheni ngome zenu.
Pondeni udongo kwa kuukanyagakanyaga,
tayarisheni tanuri ya kuchomea matofali!
15Lakini huko pia moto utawateketezeni,
upanga utawakatilia mbali;
utawamaliza kama nzige walavyo.
Ongezekeni kama nzige,
naam, ongezekeni kama panzi!
16Wafanyabiashara wako waliongezeka kuliko nyota;
lakini sasa wametoweka kama panzi warukavyo.
17Wakuu wako ni kama panzi,
maofisa wako kama kundi la nzige;
wakati wa baridi wanakaa kwenye kuta,
lakini jua lichomozapo, huruka,
wala hakuna ajuaye walikokwenda.
18Ewe mfalme wa Ashuru, wachungaji wako wamelala,
waheshimiwa wako wamesinzia.
Watu wako wametawanyika milimani,
wala hakuna yeyote wa kuwakusanya.
19Hakuna wa kuyapa nafuu majeraha yako,
vidonda vyako ni vya kifo.
Wote wanaosikia habari zako wanashangilia.
Maana ni nani aliyeuepa ukatili wako usio na kikomo?

Nahumu3;1-19

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe

Tuesday 7 July 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Nahumu 2...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Wewe, ee Mwenyezi-Mungu, ndiwe riziki yangu kuu; naahidi kushika maneno yako. Naomba radhi yako kwa moyo wangu wote; unionee huruma kama ulivyoahidi!
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako,
Tukijinyenyekeza,tukijiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunamomba utusamehe dhambi zetu
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
 ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea

Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....


Nimeufikiria mwenendo wangu, na nimerudi nifuate maamuzi yako. Bila kukawia nafanya haraka kuzishika amri zako. Waovu wametega mitego waninase, lakini mimi sisahau sheria yako.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Usiku wa manane naamka kukusifu, kwa sababu ya maagizo yako maadilifu. Mimi ni rafiki ya wote wakuchao, rafiki yao wanaozitii kanuni zako. Dunia imejaa fadhili zako, ee Mwenyezi-Mungu, unifundishe masharti yako.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...

Nawapenda.

Kuanguka kwa Ninewi
1Mwangamizi amekuja kukushambulia ee Ninewi.
Chunga ngome zako!
Weka ulinzi barabarani!
Jiweke tayari!
Kusanya nguvu zako zote!
2Mwenyezi-Mungu anamrudishia Yakobo fahari yake,
naam, anawapa tena Waisraeli fahari yao,
ingawa wavamizi hawakuwaachia kitu,
hata matawi yao ya mizabibu waliyakata.
3Ngao za mashujaa wake ni nyekundu,
askari wake wamevaa mavazi mekundu sana.
Magari yao ya farasi2:3 farasi: Kiebrania: Miberoshi. yanamulika kama miali ya moto,
yamepangwa tayari kushambulia;
farasi hawatulii kwa uchu wa kushambulia.
4Magari ya farasi yanatimua mbio barabarani,
yanakwenda huko na huko uwanjani.
Yanamulika kama miali ya moto!
Yanakwenda kasi kama umeme.
5Sasa anawaita maofisa wake,
nao wanajikwaa wanapomwendea;
wanakwenda ukutani himahima
kutayarisha kizuizi.
6Vizuizi vya mito vimefunguliwa,
ikulu imejaa hofu.
7Mji uko wazi kabisa,
watu wamechukuliwa mateka.
Wanawake wake wanaomboleza,
wanalia kama njiwa,
na kujipigapiga vifuani.
8Ninewi ni kama bwawa lililobomoka,
watu wake wanaukimbia ovyo.
“Simameni! Simameni!” Sauti inaita,
lakini hakuna anayerudi nyuma.
9“Chukueni nyara za fedha,
chukueni nyara za dhahabu!
Hazina yake haina mwisho!
Kuna wingi wa kila kitu cha thamani!”
10Mji wa Ninewi ni maangamizi matupu na uharibifu!
Watu wamekufa moyo, magoti yanagongana,
nguvu zimewaishia, nyuso zimewaiva!
11Limekuwaje basi hilo pango la simba,
hilo lililokuwa maficho ya wanasimba?
Pamekuwaje hapo mahali pa simba,
mahali pa wanasimba ambapo hakuna aliyeweza kuwashtua?
12Simba dume amewararulia watoto wake nyama ya kutosha,
akawakamatia simba majike mawindo yao;
ameyajaza mapango yake mawindo,
na makao yake mapande ya nyama.
13Tazama, mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi nitapambana nawe: Nitayateketeza kwa moto magari yako ya farasi, nitawamaliza kwa upanga hao simba wako vijana, nyara ulizoteka nitazitokomeza kutoka nchini, na sauti ya wajumbe wako haitasikika tena.

Nahumu2;1-13

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe