Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 26 March 2019

Kikombe Cha Asubuhi ;Zaburi 89...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Neno la Mwenyezi-Mungu lililomjia Yeremia mnamo mwaka wa kumi wa utawala wa Sedekia, mfalme wa Yuda, ambao ulikuwa mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Nebukadneza. Wakati huo, majeshi ya mfalme wa Babuloni yalikuwa yakiuzingira mji wa Yerusalemu, naye nabii Yeremia alikuwa amezuiliwa katika ukumbi wa walinzi uliokuwa ndani ya ikulu ya mfalme wa Yuda.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizo zifanya
Kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Maana Sedekia, mfalme wa Yuda, alikuwa amemfunga Yeremia akisema, “Kwa nini unatabiri na kusema: ‘Mwenyezi-Mungu asema hivi: Tazama, mimi nautia mji huu mikononi mwa mfalme wa Babuloni, naye atauteka. Sedekia, mfalme wa Yuda, hataepa kutiwa mikononi mwa Wakaldayo; hakika atatekwa na mfalme wa Babuloni, ataonana naye uso kwa uso na kuongea naye ana kwa ana.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji

Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu Baba wa Mbinguni
tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe....


Yahweh  tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni

Yahweh ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe

Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Sedekia atachukuliwa hadi Babuloni, naye atakaa huko mpaka nitakapomchukulia hatua. Hata kama Sedekia atapigana na Wakaldayo, hatashinda.’”
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,
wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake

Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe Yahweh tunaomba ukawape neema ya kujiombea
Kufuata njia zako nazo zikawaweke huru
Ukawaokoe na kuwalinda,ukawaponye kimwili na kiroho
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao,Amani ikatawale katika maisha yao,Upendo ukadumu kati yao Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako,kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina..!



Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,
Mungu Baba aendelee kuwatendea sawasawa na mapezni yake...

Nawapenda.

Wakati wa taabu ya kitaifa

(Utenzi wa Ethani Mwezrahi)
1Ee Mwenyezi-Mungu, nitaimba fadhili zako milele;
nitavitangazia vizazi vyote uaminifu wako.
2Natamka kuwa fadhili zako zadumu milele;
uaminifu wako ni thabiti kama mbingu.
3Umesema: “Nimefanya agano na mteule wangu,
nimemwapia mtumishi wangu Daudi:
4 Taz Zab 132:11; Mate 2:30 ‘Daima nitamweka mzawa wako kuwa mfalme,
tena nitaudumisha ufalme wako milele.’”
5Mbingu na zisifu maajabu yako, ee Mwenyezi-Mungu;
uaminifu wako usifiwe katika kusanyiko la watakatifu.
6Nani mbinguni awezaye kulinganishwa nawe ee Mwenyezi-Mungu?
Nani aliye sawa nawe kati ya viumbe vya mbinguni?
7Wewe waogopwa katika baraza la watakatifu;
wote wanaokuzunguka wanatiwa hofu kuu.
8Ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wa majeshi,
ni nani mwenye nguvu kama wewe, ee Mwenyezi-Mungu?
Uaminifu umekuzunguka pande zote.
9Wewe watawala machafuko ya bahari;
mawimbi yake yakiinuka, wayatuliza.
10Uliliponda joka Rahabu na kuliua;
uliwatawanya adui zako kwa nguvu yako.
11Mbingu ni zako na dunia ni yako pia;
ulimwengu na vitu vyote vilivyomo wewe uliviumba.
12Wewe uliumba kaskazini na kusini;
milima Tabori na Hermoni inakusifu kwa furaha.
13Mkono wako una nguvu,
mkono wako una nguvu na umeshinda!
14Uadilifu na haki ni msingi wa utawala wako;
fadhili na uaminifu vyakutangulia!
15Heri watu wanaojua kukushangilia,
wanaoishi katika mwanga wa wema wako, ee Mwenyezi-Mungu.
16Wanafurahi mchana kutwa kwa sababu yako,
na kukusifu kwa ajili ya uadilifu wako.
17Wewe ndiwe fahari na nguvu yao;
kwa wema wako twapata ushindi.
18Ee Mwenyezi-Mungu, mlinzi wetu ni wako,
mfalme wetu ametoka kwako ewe Mtakatifu wa Israeli.
Ahadi ya Mungu kwa Daudi
19Zamani ulinena katika maono,
ukawaambia watumishi wako waaminifu:
“Nimempa nguvu shujaa mmoja,
nimemkuza huyo niliyemteua kati ya watu.
20 Taz Mate 13:22 Nimempata Daudi, mtumishi wangu;
nimemweka wakfu kwa mafuta yangu matakatifu.
21Mkono wangu wa nguvu utakuwa naye daima;
mkono wangu mimi mwenyewe utamwimarisha.
22Maadui hawataweza kumshinda,
wala waovu hawatamnyanyasa.
23Mimi nitawaponda wapinzani wake;
nitawaangamiza wote wanaomchukia.
24Nitakuwa mwaminifu kwake na kumfadhili,
kwa jina langu atapata ushindi mkubwa.
25Nitaimarisha nguvu na utawala wake,
toka bahari hata mito.
26Yeye ataniita: ‘Wewe ni Baba yangu,
Mungu wangu, mwamba wa wokovu wangu.’
27 Taz Ufu 1:5 Nami nitamfanya kuwa mzaliwa wangu wa kwanza,
mkuu kuliko wafalme wote duniani.
28Fadhili zangu nitamwekea milele,
na agano langu kwake litadumu daima.
29Nitaudumisha daima ukoo wake wa kifalme,
na ufalme wake kama mbingu.
30“Lakini wazawa wake wakiiacha sheria yangu,
wasipoishi kadiri ya maagizo yangu,
31kama wakizivunja kanuni zangu,
na kuacha kutii amri zangu,
32hapo nitawaadhibu makosa yao;
nitawapiga kwa sababu ya uovu wao.
33Lakini sitaacha kumfadhili Daudi,
wala kuwa mwongo kuhusu uaminifu wangu.
34Sitavunja agano langu naye,
wala kubatili neno nililotamka kwa mdomo wangu.
35“Nimeapa mara moja tu kwa utakatifu wangu;
nami sitamwambia Daudi uongo.
36Ukoo wake utadumu milele;
na ufalme wake kama jua.
37Utadumu milele
kama mwezi utokezavyo angani.”
Majonzi ya sasa
38Lakini sasa ee Mungu, umemtupa na kumkataa,
umejaa ghadhabu dhidi ya huyo uliyemweka wakfu.
39Umefuta agano ulilofanya na mtumishi wako;
umeitupa taji yake mavumbini.
40Kuta zote za mji wake umezibomoa;
ngome zake umezivunjavunja.
41Wote wapitao wanampokonya mali zake;
amekuwa dharau kwa jirani zake.
42Maadui zake umewapa ushindi;
umewafurahisha maadui zake wote.
43Silaha zake umezifanya butu;
ukamwacha ashindwe vitani.
44Umemvua madaraka yake ya kifalme89:44 Umemvua … kifalme: Kiebrania: Umemvua usafi wake wa kifalme.
ukauangusha chini utawala wake.
45Umezipunguza siku za ujana wake,
ukamfunika fedheha tele.
Kuomba usalama
46Ee Mwenyezi-Mungu, utajificha hata milele?
Hata lini hasira yako itawaka kama moto?
47Ukumbuke, ee Bwana, ufupi wa maisha yangu;
kwamba binadamu uliyemuumba anaishi muda mfupi!
48Ni mtu gani aishiye asipate kufa?
Nani awezaye kujiepusha na kifo?
49Ee Bwana, ziko wapi basi fadhili zako,
ulizomwapia Daudi kwa uaminifu wako?
50Ee Bwana, ukumbuke anavyotukanwa mtumishi wako,
jinsi nivumiliavyo matusi ya wasiokujua.
51Ona wanavyomzomea, ee Mwenyezi-Mungu;
jinsi wanavyomdhihaki mteule wako kila aendako.
52Asifiwe Mwenyezi-Mungu milele!
Amina! Amina!


Zaburi89;1-52

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: