Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 14 November 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 55....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Wastahili sifa, ee Mungu, huko Siyoni, watu watakutimizia wewe ahadi zao, maana wewe wajibu sala zetu. Binadamu wote watakujia wewe.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Tunapolemewa na makosa yetu, wewe mwenyewe watusamehe. Heri wale unaowachagua na kuwaleta karibu, waishi katika maskani yako. Sisi tutatoshelezwa na mema ya nyumba yako; mema ya hekalu lako takatifu.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Kwa matendo yako makuu watuitikia na kutuokoa, ewe Mungu wa wokovu wetu; wewe ndiwe tumaini la viumbe vyote, duniani kote na mbali baharini.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

Njoni hata kama hamna fedha
1Haya! Kila mwenye kiu na aje kwenye maji!
Njoni, nyote hata msio na fedha;
nunueni ngano mkale,
nunueni divai na maziwa.
Bila fedha, bila gharama!
2Mbona mnatumia fedha yenu
kwa ajili ya kitu kisicho chakula?
Ya nini kutoa jasho lenu kwa kitu kisichoshibisha?
Nisikilizeni mimi kwa makini,
nanyi mtakula vilivyo bora,
na kufurahia vinono.
3Tegeni sikio enyi watu wangu, mje kwangu;
nisikilizeni, ili mpate kuishi.
Nami nitafanya nanyi agano la milele;
nitawapeni fadhili nilizomwahidi Daudi.
4Mimi nilimfanya kiongozi na kamanda wa mataifa
ili yeye anishuhudie kwa watu wa mataifa.
5Sasa utayaita mataifa usiyoyajua,
watu wa mataifa yasiyokutambua watakujia mbio,
kwa sababu yangu mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako;
kwa sababu yangu mimi Mtakatifu wa Israeli
niliyekufanya wewe utukuke.”
6Mtafuteni Mwenyezi-Mungu wakati bado anapatikana,
mwombeni msaada wakati yupo bado karibu.
7Waovu na waache njia zao mbaya,
watu wabaya waachane na mawazo yao mabaya;
wamrudie Mwenyezi-Mungu apate kuwahurumia,
wamwendee Mungu wetu maana atawasamehe.
8Maana, Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Mawazo yangu si kama mawazo yenu,
wala njia zangu si kama njia zenu.
9Kama vile mbingu zilivyo mbali na dunia,
ndivyo njia zangu zilivyo mbali na zenu,
na mawazo yangu mbali na mawazo yenu.
10Kama vile mvua na theluji ishukavyo toka mbinguni,
wala hairudi huko bali huinywesha ardhi,
ikaifanya ichipue mimea ikakua,
ikampatia mpanzi mbegu na kuwapa watu chakula,
11vivyo hivyo na neno langu mimi:
Halitanirudia bila mafanikio,
bali litatekeleza matakwa yangu,
litafanikiwa lengo nililoliwekea.
12“Mtatoka Babuloni kwa furaha;
mtaongozwa mwende kwa amani.
Milima na vilima mbele yenu vitapaza sauti na kuimba,
na miti yote mashambani itawapigia makofi.
13Badala ya michongoma kutamea misonobari,
na badala ya mbigili kutamea mihadasi.
Hilo litakuwa jambo litakalowakumbusha watu
juu ya mambo niliyotenda mimi Mwenyezi-Mungu;
ishara ya milele ambayo haitafutwa.”


Isaya55;1-13

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: