Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 21 November 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 60....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!


Mwenyezi-Mungu asema hivi: “Wewe Babuloni ni rungu na silaha yangu ya vita; nakutumia kuyavunjavunja mataifa, nakutumia kuangamiza falme. Nakutumia kuponda farasi na wapandafarasi, magari ya kukokotwa na waendeshaji wake. Ninakutumia kuwaponda wanaume na wanawake, wazee na vijana, wavulana na wasichana. Ninakutumia kuponda wachungaji na makundi yao, wakulima na wanyama wao wa kulimia, wakuu wa mikoa na madiwani.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....


“Nitaiadhibu Babuloni na wakazi wote wa Kaldayo mkiona kwa macho yenu wenyewe, kwa sababu ya uovu wote walioufanya katika Siyoni. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....


Mimi ninapingana nawe ewe mlima mharibifu, mlima unaoharibu dunia nzima! Nasema mimi Mwenyezi-Mungu. Nitanyosha mkono wangu dhidi yako, nitakuangusha kutoka miambani juu na kukufanya kuwa mlima uliochomwa moto; hata hamna jiwe lako litakalochukuliwa kujengea, hakuna jiwe litakalochukuliwa kuwekea msingi! Utakuwa kama jangwa milele. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

Yerusalemu mpya
1Inuka ee Siyoni uangaze;
maana mwanga unachomoza kwa ajili yako,
utukufu wa Mwenyezi-Mungu unakuangaza.
2Tazama, giza litaifunika dunia,
giza nene litayafunika mataifa;
lakini wewe, Mwenyezi-Mungu atakuangazia,
utukufu wake utaonekana kwako.
3Mataifa yataujia mwanga wako,
wafalme waujia mwanga wa pambazuko lako.
4Inua macho utazame pande zote;
wote wanakusanyika waje kwako.
Wanao wa kiume watafika toka mbali,
wanao wa kike watabebwa mikononi.
5Utaona na uso wako utangara,
moyo wako utasisimka na kushangilia.
Maana utajiri wa bahari utakutiririkia,
mali za mataifa zitaletwa kwako.
6Makundi ya ngamia yataifunika nchi yako,
naam, ndama wa ngamia kutoka Midiani na Efa;
wote kutoka Sheba watakuja.
Watakuletea dhahabu na ubani,
wakitangaza sifa za Mwenyezi-Mungu.
7Makundi ya kondoo wa Kedari yatakusanywa kwako,
utaweza kuwatumia kondoo madume wa Nebayothi kuwa kafara;
utawatoa kuwa tambiko inayokubalika madhabahuni pa Mungu,
naye ataitukuza nyumba yake tukufu.
8Nani hao wanaopepea kama mawingu,
kama njiwa wanaoruka kwenda viotani mwao?
9Ni meli zitokazo nchi za mbali,
zikitanguliwa na meli za Tarshishi.
Zinawaleta watoto wako,
pamoja na fedha na dhahabu yao,
kwa sifa ya Mwenyezi-Mungu, Mungu wako,
kwa sifa ya Mungu, Mtukufu wa Israeli,
maana amewafanya mtukuke.
10Mwenyezi-Mungu asema:
“Wageni watazijenga upya kuta zako,
wafalme wao watakutumikia.
Maana kwa hasira yangu nilikupiga,
lakini kwa fadhili yangu nimekuhurumia.
11 60:11 Taz Ufu 21:25-26 Malango yako yatakuwa wazi daima;
usiku na mchana hayatafungwa,
ili watu wakuletee utajiri wa mataifa,
pamoja na wafalme wao katika maandamano.
12Kila ufalme au taifa lisilokutumikia litaangamia;
mataifa hayo yatatokomezwa kabisa.
13“Utaletewa fahari ya msitu wa Lebanoni:
Mbao za miberoshi, mivinje na misonobari,
zitumike kupamba mahali pa maskani yangu;
nami nitaparembesha hapo ninapokaa.
14 60:14 Taz Ufu 3:9 Wazawa wa wale waliokudhulumu,
watakuja na kukuinamia kwa heshima.
Wote wale waliokudharau,
watasujudu mbele ya miguu yako.
Watakuita: ‘Mji wa Mwenyezi-Mungu’,
‘Siyoni, Mji wa Mtakatifu wa Israeli’.
15“Wewe ulikuwa umeachwa na kuchukiwa,
hakuna aliyependa hata kupitia kwako.
Lakini sasa nitakufanya uwe na fahari milele,
utakuwa mji wa furaha kizazi hata kizazi.
16Utaletewa chakula na watu wa mataifa,
naam, wafalme watakupatia chakula bora.
Hapo utatambua kuwa mimi Mwenyezi-Mungu ni Mwokozi wako;
mimi Mwenye Nguvu wa Yakobo ni Mkombozi wako.
17“Badala ya shaba nitakuletea dhahabu,
badala ya chuma nitakuletea fedha,
badala ya miti, nitakuletea shaba,
na badala ya mawe nitakuletea chuma.
Amani itatawala juu yako,
uadilifu utakuongoza.
18Ukatili hautasikika tena nchini mwako;
wala uharibifu na maangamizi ndani ya mipaka yako.
Utaweza kuziita kuta zako: ‘Wokovu’,
na malango yako: ‘Sifa’.60:18 Wokovu, Sifa: Majina mapya yanamaanisha hali mpya.
19Hutahitaji tena jua kukuangazia mchana,
wala mwezi kukumulikia usiku;
maana mimi Mwenyezi-Mungu ni mwanga wako milele;
mimi Mungu wako nitakuwa fahari yako.
20Mwanga wako mchana hautatua kama jua,
wala mwangaza wako usiku kufifia kama mbalamwezi;
maana Mwenyezi-Mungu ni mwanga wako milele,
nazo siku zako za kuomboleza zitakoma.
21Watu wako wote watakuwa waadilifu,
nao wataimiliki nchi milele.
Hao ni chipukizi nililopanda mimi,
kazi ya mikono yangu kwa ajili ya utukufu wangu.
22Aliye mdogo kati yenu atakuwa ukoo,
aliye mdogo kuliko wote atakuwa taifa kubwa.
Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu;
wakati ufikapo nitayatekeleza hayo haraka.”


Isaya60;1-22

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: