Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 27 November 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 64....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu



Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Msife moyo wala msiwe na hofu, kwa sababu ya uvumi mnaosikia nchini. Mwaka huu kuna uvumi huu, mwaka mwingine uvumi mwingine; uvumi wa ukatili katika nchi, mtawala mmoja dhidi ya mtawala mwingine. Kweli siku zaja, nitakapoadhibu sanamu za Babuloni; nchi yake yote itatiwa aibu, watu wake wote watauawa humohumo.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....


Kisha mbingu, dunia na vyote vilivyomo vitaimba kwa furaha kuhusu kuanguka kwa Babuloni, waangamizi watakapofika kutoka kaskazini kuushambulia. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.” Babuloni umesababisha vifo duniani kote; sasa wenyewe utaangamizwa kwa mauaji ya Israeli. “Nyinyi mlinusurika kifo, ondokeni sasa, wala msisitesite! Ingawa mko nchi ya mbali mkumbukeni Mwenyezi-Mungu, ukumbukeni pia mji wa Yerusalemu.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Mnasema: ‘Tumeaibishwa na kufadhaishwa; aibu imezifunika nyuso zetu, kwa sababu wageni wameingia katika sehemu takatifu za nyumba ya Mwenyezi-Mungu.’ “Kwa hiyo, wakati unakuja, nasema mimi Mwenyezi-Mungu, ambapo nitaviadhibu vinyago vya Babuloni, na majeruhi watapiga kite katika nchi yake yote. Ingawa Babuloni atapanda mpaka mbinguni, na kuziimarisha ngome zake ndefu, waangamizi watakuja kutoka kwangu kumvamia. 2Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.



1Laiti ungalizipasua mbingu ukashuka chini,
milima ikakuona na kutetemeka kwa hofu! 64:1 Katika Kiebrania ni 64:11.
2Ingeteketea kama moto uchomavyo kichaka,
kama vile moto uchemshavyo maji.
Njoo upate kuwajulisha maadui zako jina lako
nayo mataifa yatetemeke kwa kuwako kwako!
3Wakati ulipotenda maajabu ambayo hatukutazamia,
ulishuka chini nayo milima ikatetemeka ilipokuona.
4 64:4 Taz 1Kor 2:9 Tangu kale hakuna aliyepata kuona
wala kusikia kwa masikio yake;
hakuna aliyepata kumwona Mungu aliye kama wewe
atendaye mambo kwa ajili ya wale wanaomtegemea!
5Wewe waja kuwasaidia watendao haki kwa furaha,
wanaokukumbuka na kuzingatia njia zako.
Ulitukasirikia tulipokuwa wenye dhambi;
sisi tumeasi kwa muda mrefu.64:5 aya ya 5 Kiebrania si dhahiri. Tafsiri ya hapa kufuatana na tafsiri ya Kigiriki.
6Sote tumekuwa kama watu walio najisi;
matendo yetu yote mema ni kama nguo chafu.
Sote tunanyauka kama majani,
uovu wetu watupeperusha kama upepo.
7Hakuna hata mmoja anayekuja kukuomba;
hakuna anayejishughulisha kukutafuta.
Wewe unauficha uso wako mbali nasi,
umetuacha tukumbwe na maovu yetu.
8Hata hivyo, ee Mwenyezi-Mungu, wewe ni Baba yetu.
Sisi ni kama udongo, wewe ni mfinyanzi.
Sisi sote ni kazi ya mikono yako.
9Usitukasirikie mno, ee Mwenyezi-Mungu,
usiukumbuke uovu wetu daima!
Ukumbuke kwamba sisi sote ni watu wako!
10Miji yako mitakatifu imekuwa nyika;
Siyoni umekuwa mahame,
Yerusalemu umekuwa uharibifu.
11Nyumba yetu takatifu na nzuri,
ambamo wazee wetu walikusifu,
imeteketezwa kwa moto.
Mahali petu pote pazuri pamekuwa magofu.
12Je, kwa hayo yote utajizuia usifanye kitu?
Je, utaendelea kunyamaza tu, ee Mwenyezi-Mungu,
na kututesa kupita kiasi?

Isaya64;1-12

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

2 comments:

Benjamin said...

Huduma yako ni njema sana Mtumishi,
Ubarikiwe sana!

Rachel Siwa said...

Benjami...

Amina!!
Asante kwa baraka.