Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 19 November 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 58....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Tulijaribu kuuponya Babuloni, lakini hauwezi kuponywa. Uacheni, twendeni zetu, kila mmoja katika nchi yake, maana hukumu yake ni kuu mno imeinuka mpaka mawinguni. Mwenyezi-Mungu amethibitisha kuwa hatuna hatia. Twendeni Siyoni tukatangaze matendo ya Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....


Mwenyezi-Mungu amezichochea roho za wafalme wa Media, kwa maana amenuia kuiangamiza Babuloni. Naam, hicho ndicho kisasi cha Mwenyezi-Mungu; analipiza kisasi kwa ajili ya hekalu lake. Noeni mishale yenu! Chukueni ngao! Twekeni bendera ya vita kushambulia kuta za Babuloni. Imarisheni ulinzi; wekeni walinzi; tayarisheni mashambulizi. Mwenyezi-Mungu amepanga na kutekeleza mambo aliyosema juu ya wakazi wa Babuloni.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....


Nchi hiyo imejaa mito na hazina tele, lakini mwisho wake umefika, uzi wa uhai wake umekatwa. Mwenyezi-Mungu wa majeshi ameapa kwa nafsi yake: “Hakika nitakujaza majeshi mengi kama nzige, nayo yatapiga vigelegele vya ushindi juu yako”
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

Mfungo wa kweli
1Mwenyezi-Mungu asema:
“Piga kelele, wala usijizuie;
paza sauti yako kama tarumbeta.
Watangazie watu wangu makosa yao,
waambie wazawa wa Yakobo dhambi zao.
2Siku hata siku wananijia kuniabudu,
wanatamani kujua mwongozo wangu,
kana kwamba wao ni taifa litendalo haki,
taifa lisilosahau sheria za Mungu wao.
Wananitaka niamue kwa haki,
na kutamani kukaa karibu na Mungu.
3“Nyinyi mnaniuliza:
‘Mbona tunafunga lakini wewe huoni?
Mbona tunajinyenyekesha, lakini wewe hujali?’
“Ukweli ni kwamba wakati mnapofunga,
mnatafuta tu furaha yenu wenyewe,
na kuwakandamiza wafanyakazi wenu!
4Mnafunga, na kugombana na kupigana ngumi.
Mkifunga namna hiyo
maombi yenu hayatafika kwangu juu.
5Mfungapo, nyinyi mnajitaabisha;
mnaviinamisha vichwa vyenu kama unyasi,
na kulalia nguo za magunia na majivu.
Je, huo ndio mnaouita mfungo?
Je, hiyo ni siku inayokubaliwa nami?
6“La! Mfungo ninaotaka mimi ni huu:
Kuwafungulia waliofungwa bila haki,
kuziondoa kamba za utumwa,
kuwaachia huru wanaokandamizwa,
na kuvunjilia mbali udhalimu wote!
7 58:7 Taz Mat 25:35 Mfungo wa kweli ni kuwagawia wenye njaa chakula chako,
kuwakaribisha nyumbani kwako maskini wasio na makao,
kuwavalisha wasio na nguo,
bila kusahau kuwasaidia jamaa zenu.
8“Mkifanya hivyo mtangara kama pambazuko,
mkiwa wagonjwa mtapona haraka.
Matendo yenu mema yatawatangulia,
nami nitawalindeni kutoka nyuma kwa utukufu wangu.
9Ndipo mtakapoomba,
nami Mwenyezi-Mungu nitawaitikia;
mtalia kwa sauti kuomba msaada,
nami nitajibu, ‘Niko hapa!’
“Kama mkiiondoa dhuluma kati yenu,
mkiacha kudharau wengine na kusema maovu,
10mkiwapa chakula kwa ukarimu wenye njaa,
mkitosheleza mahitaji ya wenye dhiki,
mwanga utawaangazia nyakati za giza,
giza lenu litakuwa kama mchana.
11Mimi Mwenyezi-Mungu nitawaongozeni daima,
nitatosheleza mahitaji yenu wakati wa shida.58:11 maana ya neno hili Kiebrania si dhahiri.
Nitawaimarisha mwilini,
nanyi mtakuwa kama bustani iliyomwagiliwa maji,
kama chemchemi ya maji
ambayo maji yake hayakauki kamwe.
12Magofu yenu ya kale yatajengwa;
mtajenga upya juu ya misingi iliyoachwa zamani.
Nanyi mtaitwa watu waliotengeneza upya kuta,
watu waliozifanya barabara za mji zipitike tena.
Tuzo kwa kuiadhimisha Sabato
13“Kama ukiacha kufanya kazi siku ya Sabato,
ukaacha shughuli zako siku yangu hiyo takatifu;
kama ukiifanya siku yangu kuwa ya furaha,
ukaiheshimu siku hiyo takatifu ya Mwenyezi-Mungu,
ukaacha na shughuli58:13 shughuli: Au anasa. zako na kupiga domo,
14utapata furaha yako kwangu mimi Mwenyezi-Mungu,
nitakupatia ushindi katika kila pingamizi nchini,
nitakulisha mali ya Yakobo, babu yako.
Mimi, Mwenyezi-Mungu, nimesema.”


Isaya58;1-14

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: