Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 26 November 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 63....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Nitawashusha chini kama kondoo wa kuchinjwa, kama vile kondoo dume na beberu. Ajabu kutekwa kwa Babuloni; mji uliosifika duniani kote umechukuliwa! Babuloni umekuwa kinyaa kati ya mataifa!
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....


Bahari imefurika juu ya Babuloni, Babuloni imefunikwa mawimbi yaliyochafuka. Miji yake imekuwa kinyaa, nchi ya ukavu na jangwa, nchi isiyokaliwa na mtu yeyote, wala kupitika na binadamu yeyote.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Nitamwadhibu mungu Beli huko Babuloni, nitamfanya akitoe alichokimeza. Mataifa hayatamiminika tena kumwendea. Ukuta wa Babuloni umebomoka. “Tokeni humo enyi watu wangu! Kila mtu na ayasalimishe maisha yake, kutoka hasira kali ya Mwenyezi-Mungu.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

Mungu awaadhibu maadui za watu wake
1Ni nani huyu ajaye kutoka Edomu,
anayefika kutoka Bosra na mavazi ya madoa mekundu?
Ni nani huyo aliyevaa mavazi ya fahari,
anatembea kwa nguvu zake kubwa?
Ni mimi Mwenyezi-Mungu
ninayetangaza ushindi wangu;
nami ni mwenye nguvu ya kuokoa.
2Lakini mbona nguo yako ni nyekundu,
nyekundu kama ya mtu anayekamua zabibu?
3Naam, nimekamua zabibu peke yangu,
wala hakuna mtu aliyekuja kunisaidia.
Nimeyakanyaga mataifa kwa hasira yangu,
niliyapondaponda kwa ghadhabu yangu.
Nguo zangu zimejaa madoa ya damu yao,
imeyachafua kabisa mavazi yangu.
4Niliamua kuwa siku ya kulipiza kisasi imefika;
wakati wa kuwakomboa watu wangu umefika.
5Nilitazama na hapakuwa na wa kunisaidia;
nilishangaa hapakuwa na wa kuniunga mkono.
Lakini nilijipatia ushindi kwa mkono wangu,
ghadhabu yangu ilinihimiza.
6Kwa hasira yangu niliwaponda watu,
niliwalewesha kwa ghadhabu yangu;
damu yao niliimwaga chini ardhini.”
Wema wa Mungu kwa Israeli
7Nitasimulia fadhili za Mwenyezi-Mungu;
nitataja matendo yake yote yastahiliyo sifa,
kwa sababu ya yote aliyotutendea,
wema wake mkuu aliowapa Waisraeli kwa huruma yake,
kadiri ya wingi wa fadhili zake.
8Maana alisema juu yao:
“Hakika, hawa ni watu wangu;
watoto wangu ambao hawatanidanganya.”
Basi yeye akawa Mwokozi wao.
9Katika taabu zao zote,
hakumtuma mjumbe63:9 … hakumtuma mjumbe … au Malaika; Yeye aliwaokoa. Yeye Mwenyewe alitaabika walipotaabika, akamtuma malaika wake awaokoe. mwingine kuwasaidia,
ila yeye mwenyewe alikuja kuwaokoa.
kwa upendo na huruma yake aliwakomboa.
Aliwabeba na kuwachukua tangu zamani.
10Lakini wao walikuwa wakaidi,
wakaihuzunisha roho yake takatifu.
Basi, Mungu akageuka, akawa adui yao;
yeye mwenyewe akapigana nao.
11Ndipo walipokumbuka63:11 walipokumbuka: Kiebrania: Alipozikumbuka. siku za zamani,
wakati wa Mose mtumishi wa Mwenyezi-Mungu.
Wakauliza, “Yuko wapi sasa Mwenyezi-Mungu,
aliyewaokoa wachungaji wa kundi lake baharini?
Yuko wapi yule aliyeiweka roho yake takatifu kati yao,
12ambaye kwa mkono wake wenye nguvu
alifanya maajabu kwa njia ya Mose,
akapasua bahari na kuwaongoza watu wake,
na kujipatia jina la milele?
13Aliwaongoza katikati ya vilindi vya bahari,
wakapita humo kama farasi bila kujikwaa.
14Kama ng'ombe wapelekwavyo malishoni bondeni,
ndivyo roho ya Mungu ilivyowapumzisha watu wake.
Ndivyo ee Mungu ulivyowaongoza watu wako,
nawe ukajipatia jina tukufu.”
Sala ya kuomba msaada
15Ututazame kutoka mbinguni ee Mungu, uone,
utuangalie kutoka makao yako matakatifu na matukufu.
Iko wapi bidii yako kwa ajili yetu na nguvu yako?
Usiache kutuonesha upendo wako.63:15 Usiache … upendo wako: Tafsiri ya neno kwa neno: Upendo na huruma yako vimezuiwa visionekane kwetu.
16Maana wewe ndiwe Baba yetu;
Abrahamu, mzee wetu, hatujali,
naye Israeli hatutambui;
lakini wewe, ee Mwenyezi-Mungu, ni Baba yetu.
Wewe umeitwa tangu kale: “Mkombozi wetu.”
17Ee Mwenyezi-Mungu, mbona unatukosesha njia zako?
Mbona unatufanya kuwa wakaidi hata tusikuogope?
Rudi ee Mungu kwa ajili ya watumishi wako,
makabila ambayo daima yalikuwa mali yako.
18Kwa kitambo tu sisi watakatifu wako tulimiliki nchi,
lakini maadui zetu wakaja wakaharibu maskani yako.63:18 aya 18 makala ya Kiebrania si dhahiri.
19Tumekuwa kama watu ambao hujawatawala kamwe,
kama watu ambao hawakujulikana kwa jina lako.

Isaya63;1-19

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: