Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 13 November 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 54....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu



Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Nilipofahamishwa kwamba Wayahudi walikuwa wamefanya njama za kumwua, niliamua kumleta kwako, nikawaambia washtaki wake walete mashtaka yao mbele yako.”
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....


Basi, hao askari walimchukua Paulo kama walivyoamriwa; wakampeleka usiku uleule mpaka Antipatri. Kesho yake askari wa miguu walirudi ngomeni, wakawaacha wale askari wapandafarasi waendelee na safari pamoja na Paulo.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Walipofika Kaisarea walimpa mkuu wa mkoa ile barua na kumweka Paulo chini ya mamlaka yake. Felisi alipoisoma hiyo barua aliwauliza Paulo ametoka mkoa gani. Alipofahamishwa kwamba alikuwa ametoka mkoa wa Kilikia, akasema, “Nitasikiliza kesi yako baada ya washtaki wako kufika.” Kisha akaamuru Paulo awekwe chini ya ulinzi ndani ya ukumbi wa Herode.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Upendo wa Mungu kwa Israeli
1Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Imba kwa shangwe ewe uliye tasa,
wewe ambaye hujapata kuzaa!
Paza sauti na kuimba kwa nguvu,
wewe usiyepata kujifungua mtoto.
Maana watoto wako wewe uliyeachwa
watakuwa wengi kuliko wa aliye na mume.54:1 aya iliyokaririwa katika Gal 4:27.
2Panua nafasi hemani mwako,
tandaza mapazia hapo unapoishi,
usijali gharama zake.
Zirefushe kamba zake,
na kuimarisha vigingi vyake;
3maana utapanuka kila upande;
wazawa wako watamiliki mataifa,
miji iliyokuwa mahame itajaa watu.
4Usiogope maana hutaaibishwa tena;
usifadhaike maana hutadharauliwa tena.
Utaisahau aibu ya ujana wako,
wala hutaikumbuka tena fedheha ya ujane wako.
5Muumba wako atakuwa mume wako;
Mwenyezi-Mungu wa majeshi, ndilo jina lake,
Mtakatifu wa Israeli ndiye Mkombozi wako;
yeye aitwa ‘Mungu wa ulimwengu wote’.
6“Yerusalemu, Mwenyezi-Mungu amekuita tena wewe
kama vile mke aliyeachwa na kuhuzunika,
mke aliyeolewa akiwa kijana akaachwa.
Mungu wako anasema:
7Nilikuacha kwa muda mfupi tu;
kwa huruma nyingi, nitakurudisha.
8Kwa hasira nyingi nilikuficha uso wangu kwa kitambo,
lakini kwa fadhili za milele nitakuonea huruma.
Mimi Mwenyezi-Mungu Mkombozi wako, nimesema.
9Nitafanya kama nilivyofanya wakati wa Noa:
Wakati ule niliapa kwamba
sitaifunika tena ardhi kwa gharika.
Basi sasa naapa kwamba sitakukasirikia tena
wala sitakukemea tena.
10Milima yaweza kutoweka,
vilima vyaweza kuondolewa,
lakini fadhili zangu hazitakuondoka,
agano langu la amani halitaondolewa.
Mimi Mwenyezi-Mungu nikuhurumiaye nimesema.
Yerusalemu mpya
11Ewe Yerusalemu uliyeteseka,
uliyetaabishwa na kukosa wa kukufariji!
Nitakujenga upya kwa mawe ya thamani,
misingi yako itakuwa ya johari ya rangi ya samawati.
12Minara yako nitaijenga kwa mawe ya akiki,
malango yako kwa almasi,
na ukuta wako kwa mawe ya thamani.
13Watu wako watafunzwa nami Mwenyezi-Mungu,
wanao watapata ustawi mwingi.
14Utaimarika katika uadilifu,
utakuwa mbali na dhuluma,
nawe hutaogopa kitu;
utakuwa mbali na hofu,
maana haitakukaribia.
15Mtu yeyote akija kukushambulia,
hatakuwa ametumwa nami.
Yeyote atakayekushambulia,
ataangamia mbele yako.
16“Tazama, mimi ndiye niliyemuumba mhunzi,
afukutaye moto wa makaa na kufua silaha.
Ni mimi pia niliyemuumba mwangamizi anayeangamiza.
17Silaha zote zilizoundwa kukudhuru wewe
hazitafaa chochote kile.
Mtu akikushtaki mahakamani, utamshinda.
Hilo ndilo fungu nililowapangia watumishi wangu.
Hizo ndizo haki nilizowathibitishia.
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.


Isaya54;1-17

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: