Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 4 November 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 47....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki/mwezi mw
ingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu

Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!


Yoshua mwana wa Nuni na mtumishi wa Mwenyezi-Mungu, alifariki akiwa na umri wa miaka 110. Wakamzika katika sehemu aliyogawiwa iwe yake huko Timnath-heresi, katika nchi ya milima ya Efraimu kaskazini ya mlima Gaashi. Kisha watu wote wa kizazi chake walifariki, kikafuata kizazi kingine ambacho hakikumjua Mwenyezi-Mungu wala matendo aliyowatendea watu wa Israeli.
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona....

Basi, Waisraeli walitenda uovu mbele ya Mwenyezi-Mungu na kuabudu Mabaali. Walimwacha Mwenyezi-Mungu, Mungu wa wazee wao, ambaye aliwatoa katika nchi ya Misri, wakaifuata miungu mingine, miungu iliyoabudiwa na watu walioishi kandokando yao. Waliisujudia miungu hiyo, wakamkasirisha sana Mwenyezi-Mungu.
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Walimwacha Mwenyezi-Mungu, wakatumikia Mabaali na Maashtarothi. Basi, hasira ya Mwenyezi-Mungu iliwaka dhidi ya Israeli, naye akawaacha wanyanganyi wapore mali zao. Aliwakabidhi kwa adui zao waliowazunguka hata wasiweze tena kuwapinga.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimamie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.

Hukumu dhidi ya Babuloni
1“Teremka uketi mavumbini
ewe Babuloni binti mzuri!
Keti chini pasipo kiti cha enzi
ewe binti wa Wakaldayo!
Tokea sasa hutaitwa tena mwororo wala nadhifu.
2Twaa mawe ya kusagia, usage unga kama mtumwa!
Vua utaji wako, ukavue na mavazi yako!
Pandishia vazi lako miguuni, ukavuke mito.
3Watu watauona uchi wako;
naam, wataiona aibu yako.
Mimi nitalipiza kisasi,
wala sitamhurumia yeyote.”
4Mkombozi wetu ndiye Mtakatifu wa Israeli;
Mwenyezi-Mungu wa majeshi ndilo jina lake.
5Mwenyezi-Mungu asema:
“Ewe taifa la Wakaldayo
lililo kama binti mzuri,
keti kimya na kutokomea gizani.
Maana umepoteza hadhi yako
ya kuwa bimkubwa wa falme.
6Niliwakasirikia watu wangu Israeli,
nikawafanya watu wangu kuwa haramu.
Niliwatia mikononi mwako,
nawe hukuwaonea huruma;
na wazee uliwatwisha nira nzito mno.
7Ulijisemea moyoni: ‘Nitakuwa malkia milele’,
nawe hukuyatafakari mambo yanayotokea,
wala kufikiri mwisho wake.
8 47:8-9 Taz Ufu 18:7-8 “Sasa, basi, sikiliza ewe mpenda anasa,
wewe unayedhani kuwa u salama,
na kujisemea: ‘Ni mimi tu,
na hakuna mwingine isipokuwa mimi.
Kamwe sitakuwa mjane,
wala sitafiwa na wanangu.’
9Haya yote mawili yatakupata,
ghafla, katika siku moja:
Kupoteza watoto wako na kuwa mjane,
ijapokuwa una wingi wa uchawi wako,
na nguvu nyingi za uganga wako.
10“Ulijiona salama katika uovu wako;
ukajisemea, ‘Hakuna mtu anayeniona.’
Hekima na elimu yako vilikupotosha,
ukajisemea moyoni mwako, ‘Mimi ndiye;
hakuna mwingine anayenishinda.’
11Lakini maafa yatakupata
ambayo hutaweza kujiepusha nayo.
Balaa litakukumba
ambalo hutaweza kulipinga;
maangamizi yatakujia ghafla
ambayo hujapata kamwe kuyaona.
12Endelea basi na uganga wako,
tegemea wingi wa uchawi wako.
Wewe uliyapania hayo tangu ujana wako
ukitumainia kwamba utafanikiwa
au kusababisha kitisho kwa watu!
13Wewe umejichosha bure na washauri wako.
Basi, na wajitokeze hao wanajimu wakuokoe!
Wao huzigawa mbingu sehemusehemu,
huzichunguza nyota
na kubashiri kila mwezi yatakayokupata.
14“Kumbuka, wao ni kama mabua makavu:
Moto utayateketezea mbali!
Hawawezi hata kujiokoa wenyewe
mbali na ukali wa moto huo.
Moto huo si wa kujipatia joto,
huo si moto wa kuota!
15Ndivyo watakavyokuwa hao uliowategemea hivyo,
hao uliojishughulisha nao tangu ujana wako.
Watatangatanga kila mmoja njia yake;
hakuna hata mmoja atakayeweza kukuokoa.”


Isaya47;1-15

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: