Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 6 November 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 49....



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Paulo aliwakodolea macho wale wanabaraza, halafu akaanza kusema, “Ndugu zangu, mpaka hivi leo nimekuwa nikiishi na dhamiri njema mbele ya Mungu.” Hapo kuhani mkuu Anania akaamuru wale waliokuwa wamesimama karibu na Paulo wampige kofi mdomoni. Basi, Paulo akamwambia, “Mungu mwenyewe atakupiga kofi wewe uliye kama ukuta uliopakwa chokaa! Unawezaje kukaa hapo ili unihukumu kisheria na huku wewe mwenyewe unaivunja sheria kwa kuamuru nipigwe?”
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Watu waliokuwa wamesimama pale wakamwambia Paulo, “Unamtukana kuhani mkuu wa Mungu!” Paulo akajibu, “Ndugu zangu, sikujua kama yeye ni kuhani mkuu. Maana Maandiko yasema hivi: ‘Usiseme vibaya juu ya mtawala wa watu wako.’”
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Wakati huo Paulo alikwisha tambua kwamba sehemu moja ya wanabaraza wale ilikuwa ni Masadukayo na nyingine Mafarisayo. Basi, alipaza sauti yake mbele ya Baraza, “Ndugu zangu, mimi ni Mfarisayo, mwana wa Mfarisayo. Mimi nimeletwa mahakamani kwa kuwa ninatumaini kwamba wafu watafufuka.”
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Israeli: Mwanga wa mataifa
1Nisikilizeni, enyi nchi za mbali,
tegeni sikio, enyi watu wa mbali!
Mwenyezi-Mungu aliniita kabla sijazaliwa,
alitaja jina langu nikiwa tumboni mwa mama yangu.
2Aliyapa ukali maneno yangu kama upanga mkali,
alinificha katika kivuli cha mkono wake;
aliufanya ujumbe wangu mkali kama ncha ya mshale,
akanificha katika podo lake.
3Aliniambia, “Wewe ni mtumishi wangu;
kwako, Israeli, watu watanitukuza.”
4Lakini mimi nikafikiri,
“Nimeshughulika bure,
nimetumia nguvu zangu bure kabisa.”
Hata hivyo, Mwenyezi-Mungu atanipa haki yangu;
tuzo la kazi yangu liko kwa Mungu.
5Lakini asema sasa Mwenyezi-Mungu,
ambaye aliniita tangu tumboni mwa mama yangu
ili nipate kuwa mtumishi wake;
nilirudishe taifa la Yakobo kwake,
niwakusanye wazawa wa Israeli kwake.
Mwenyezi-Mungu amenijalia heshima mbele yake.
Mungu wangu amekuwa ndiye nguvu yangu.
6Yeye asema: “Haitoshi tu wewe kuwa mtumishi wangu,
uyainue makabila ya Yakobo,
na kurekebisha watu wa Israeli waliobaki.
Nitakufanya uwe mwanga wa mataifa,
niwaletee wokovu watu wote duniani.”49:6 sehemu hii imekaririwa katika Mate 13:47, 26:23. Luka naye anaigusia katika 2:32; Taz pia Isa 42:6.
7Mwenyezi-Mungu, Mkombozi na Mtakatifu wa Israeli,
amwambia hivi yule anayedharauliwa mno,
yule anayechukiwa na mataifa,
na ambaye ni mtumishi wa watawala:
“Wafalme watakuona nao watasimama kwa heshima,
naam, wakuu watainama na kukusujudia
kwa sababu yangu mimi Mwenyezi-Mungu
ambaye hutimiza ahadi zangu;
kwa sababu yangu mimi Mtakatifu wa Israeli
ambaye nimekuteua wewe.”
Kujengwa upya kwa Yerusalemu
8Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Wakati wa kufaa nilikujibu ombi lako;
wakati wa wokovu nilikusaidia.
Nimekuweka na kukufanya
uwe kiungo cha agano langu na mataifa yote:
Kuirekebisha nchi iliyoharibika,
na kuwarudishia wenyewe ardhi hiyo;
9kuwaambia wafungwa, ‘Tokeni humo gerezani’,
na wale walio gizani, ‘Njoni nje mwangani!’
Kila mahali watakapokwenda watapata chakula
hata kwenye vilima vitupu watapata malisho.
10Hawataona tena njaa wala kuwa na kiu.
Upepo wa hari wala jua havitawachoma,
mimi niliyewahurumia nitawaongoza
na kuwapeleka kwenye chemchemi za maji.
11Milima yote nitaifanya kuwa njia,
na barabara zangu kuu nitazitengeneza.
12Watu wangu watarudi kutoka mbali,
wengine kutoka kaskazini na magharibi,
wengine kutoka upande wa kusini.”49:12 kutoka upande wa kusini: Makala ya Kiebrania Sinimu mji uliokaliwa na Waisraeli kusini mwa Misri.
13Imbeni kwa furaha, enyi mbingu!
Shangilia ewe dunia.
Pazeni sauti mwimbe enyi milima,
maana Mwenyezi-Mungu amewafariji watu wake,
naam, atawaonea huruma watu wake wanaoteseka.
14Wewe Siyoni wasema:
“Mwenyezi-Mungu ameniacha;
hakika Bwana wangu amenisahau.”
15Lakini Mwenyezi-Mungu asema:
“Je, mama aweza kumsahau mwanawe anayenyonya,
asimwonee huruma mtoto wa tumbo lake?
Hata kama mama aweza kumsahau mwanawe,
mimi kamwe sitakusahau.
16Nimekuchora katika viganja vyangu;
kuta zako naziona daima mbele yangu.
17Watakaokujenga49:17 Watakaokujenga: Kulingana na makala ya Kiebrania iliyopatikana Kumrani na hati nyingine za kale. Tafsiri za mapokeo: Watoto wako. upya wanakuja haraka,
wale waliokuharibu wanaondoka.
18Inua macho uangalie pande zote;
watu wako wote wanakusanyika na kukujia.
Naapa kwa nafsi yangu mimi Mwenyezi-Mungu,
watu wako watakuwa kwako kama mapambo,
utawafurahia kama afanyavyo bibi arusi na utaji wake.
19“Kweli umekumbana na uharibifu,
makao yako yamekuwa matupu,
na nchi yako imeteketezwa.
Lakini sasa itakuwa ndogo mno kwa wakazi wake;
na wale waliokumaliza watakuwa mbali.
20Wanao waliozaliwa uhamishoni,
watakulalamikia wakisema:
‘Nchi hii ni ndogo mno;
tupatie nafasi zaidi ya kuishi.’
21Hapo ndipo utakapojiuliza mwenyewe:
‘Nani aliyenizalia watoto wote hawa?
Nilifiwa na wanangu bila kupata wengine.
Nilipelekwa uhamishoni na kutupwa mbali;
nani basi aliyewalea watoto hawa?
Mimi niliachwa peke yangu,
sasa, hawa wametoka wapi?’”
22Bwana Mungu asema hivi:
“Nitayapungia mkono mataifa;
naam, nitayapa ishara,
nayo yatawabeba watoto wenu wa kiume,
kadhalika na watoto wenu wa kike
na kuwarudisha kwako.
23Wafalme watakushughulikia,
na malkia watakutengenezea chakula.
Watakusujudia na kukupa heshima,
na kuramba vumbi iliyo miguuni pako.
Hapo utatambua kuwa mimi ni Mwenyezi-Mungu;
wote wanaonitegemea hawataaibika.”
24Watu wa Yerusalemu walalamika:
“Je, shujaa aweza kunyanganywa nyara zake?
Au mateka wa mtu katili waweza kuokolewa?”
25Mwenyezi-Mungu ajibu:
“Naam! Hata nyara za shujaa zitachukuliwa,
mateka wa mtu katili wataokolewa.
Mimi mwenyewe nitawakabili maadui zako,
mimi mwenyewe nitawaokoa watoto wako.
26Nitawafanya wanaokukandamiza watafunane;
watalewa damu yao wenyewe kama divai.
Hapo binadamu wote watatambua kwamba
mimi ni Mwenyezi-Mungu, Mwokozi wako,
mimi ni Mkombozi wako, Mwenye Nguvu wa Yakobo.”

Isaya49;1-26

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: