Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 5 November 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 48....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Kila walipokwenda kupigana, mkono wa Mwenyezi-Mungu uliwakabili kuwaletea balaa, kama alivyokuwa amewaonya na kuapa. Nao wakawa katika huzuni kubwa. Ndipo Mwenyezi-Mungu akawapa waamuzi ambao waliwaokoa mikononi mwa watu waliopora mali zao.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Hata hivyo, Waisraeli hawakuwasikiliza waamuzi wao, maana walifanya kama wazinzi kwa kufuata miungu mingine na kuisujudia. Waliacha upesi nyayo walizofuata babu zao ambao walitii amri za Mwenyezi-Mungu; bali wao hawakufanya hivyo. Kila mara Mwenyezi-Mungu alipowapelekea mwamuzi, yeye mwenyewe alikuwa pamoja na mwamuzi huyo, akawaokoa mikononi mwa adui zao muda wote wa uhai wa mwamuzi huyo. Aghalabu, Mwenyezi-Mungu aliwaonea huruma aliposikia kilio chao kutokana na mateso na dhuluma walizofanyiwa.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Lakini kila mara mwamuzi alipofariki walirudia mienendo yao ya zamani, wakaishi vibaya kuliko babu zao. Waliifuata miungu mingine, wakaitumikia na kuisujudia, wala hawakuyaacha matendo yao wala ukaidi wao. Kwa hiyo Mwenyezi-Mungu akawaka hasira dhidi ya Waisraeli, akasema, “Kwa kuwa watu hawa wamevunja agano nililofanya na babu zao, wakakataa kutii sauti yangu, sitayafukuza tena mataifa ambayo Yoshua aliyabakiza, wakati alipofariki. Nitayatumia mataifa hayo kuwajaribu Waisraeli nione kama watairudia njia yangu kama babu zao au sivyo.” Basi, Mwenyezi-Mungu akayaacha mataifa hayo, wala hakuyafukuza mara moja, wala hakumpa Yoshua ushindi juu ya mataifa hayo!
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

Mungu atangaza matukio mapya
1Sikilizeni, enyi watu wa Yakobo,
enyi mnaojulikana kwa jina la Israeli,
nyinyi mlio wa ukoo wa Yuda.
Nyinyi huapa kwa jina la Mwenyezi-Mungu,
na kudai mnamwabudu Mungu wa Israeli;
lakini hayo si ukweli wala sawa.
2Nyinyi mnaona fahari kujiita watu wa mji mtakatifu,
na kujidai kumtegemea Mungu wa Israeli,
ambaye jina lake ni Mwenyezi-Mungu wa majeshi.
3“Nilitangaza zamani matukio ya awali,
niliyatamka mimi mwenyewe
na kuyafanya yajulikane kwenu.
Mara nikaanza kuyatekeleza,
nayo yakapata kutukia.
4Lakini nilikujua wewe kuwa mkaidi;
kichwa kigumu kama chuma,
uso wako mkavu kama shaba.
5Kwa hiyo nilikutangazia tangu zamani,
kabla hayajatukia mimi nilikutangazia,
usije ukasema, ‘Kinyago changu kiliyatenda hayo,
sanamu zangu za kuchonga na kusubu ziliyafanya.’
6“Wewe uliyasikia na sasa unayaona yote.
Kwa nini huwezi kuyakiri?
Tangu sasa nitakujulisha mambo mapya;
mambo yaliyofichika ambayo hukuyajua.
7Mambo hayo yanatukia sasa;
hukupata kuyasikia kabla ya leo,
hivyo huwezi kusema, ‘Aa! Nilikwisha yajua.’
8Hujapata kamwe kuyasikia wala kuyajua;
tangu zamani masikio yako hayakuyasikia.
Nilijua kuwa wewe ni mwenye hila,
na kwamba wewe ni mwasi tangu kuzaliwa.
9“Kwa heshima ya jina langu,
ninaiahirisha hasira yangu;
kwa ajili ya heshima yangu,
ninaizuia nisije nikakuangamiza.
10Mimi nitawajaribu lakini si kama fedha katika tanuri.
Nitawajaribu katika tanuri ya taabu.
11Ninafanya hivyo kwa ajili yangu mwenyewe.
Kwa nini jina langu lidharauliwe?
Utukufu wangu siwezi kumpa mwingine!
Koreshi, mteule wa Mwenyezi-Mungu
12“Nisikilize ee taifa la Yakobo,
nisikilize ee Israeli niliyekuita.
Mimi ndiye Mungu;
mimi ni wa kwanza na wa mwisho.
13Kwa mkono wangu niliuweka msingi wa dunia,
mimi mwenyewe nilizitandaza mbingu.
Nikiziita mbingu na dunia,
zinasimama haraka mbele yangu.
14“Kusanyikeni nyote msikilize!
Nani kati ya miungu yenu aliyetabiri vitu hivi?
Mimi Mwenyezi-Mungu nampenda Koreshi;
yeye atatekeleza lengo langu kuhusu Babuloni,
naam, yeye atawashambulia Wakaldayo.
15Mimi, naam, mimi nimeyasema na kumwita;
nimemleta, naye atafaulu katika mpango wake.
16Njoni karibu nami msikie jambo hili:
Tangu mwanzo mimi sikusema kwa siri,
tangu mambo hayo yaanze kutendeka, nimekuwapo.”
Sasa, Bwana Mungu amenituma,
na kunipa nguvu ya roho yake.48:16 Sasa … roho wake: Maneno haya hayaonyeshi dhahiri ni nani anayesema; Pengine ni rafiki (Koreshi) aliyetajwa katika aya ya 14.
Mpango wa Mungu kwa watu wake
17Mwenyezi-Mungu, Mtakatifu wa Israeli,
Mkombozi wako, asema hivi:
“Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako,
ninayekufundisha kwa faida yako,
ninayekuongoza katika njia unayotakiwa kwenda.
18Laiti ungalizitii amri zangu!
Hapo baraka zingekutiririkia kama mto,
ungepata fanaka kwa wingi kama mawimbi ya bahari.
19Wazawa wako wangekuwa wengi kama mchanga,
naam, wangekuwa wengi kama chembe za mchanga.
Jina lao kamwe lisingaliondolewa,
kumbukumbu lao halingalitoweka mbele yangu.”
20 48:20 Taz Ufu 18:4 Sasa, ondokeni Babuloni!
Kimbieni kutoka Kaldayo!
Tangazeni jambo hili kwa sauti za shangwe,
enezeni habari zake kila mahali duniani.
Semeni: “Mwenyezi-Mungu amelikomboa
taifa la mtumishi wake Yakobo.”
21Alipowaongoza jangwani hawakuona kiu,
aliwatiririshia maji kutoka mwambani,
aliupasua mwamba maji yakabubujika.
22Lakini Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Watu waovu sitawapa amani.”

Isaya48;1-22

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: