Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 12 November 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 53....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Basi, mkuu wa jeshi aliwaita askari wawili akawaambia, “Wekeni tayari askari 200, wapandafarasi sabini na askari 200 wa mikuki, waende Kaisarea; muwe tayari kuondoka kabla ya saa tatu leo usiku. Wekeni farasi kadhaa kwa ajili ya Paulo; mfikisheni salama kwa Felisi, mkuu wa mkoa.” Halafu mkuu huyo wa jeshi akaandika barua hivi:
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

“Mimi Klaudio Lusia ninakuandikia wewe Mheshimiwa Felisi, mkuu wa mkoa. Salamu! “Wayahudi walimkamata mtu huyu na karibu wangemuua kama nisingalifahamishwa kwamba yeye ni raia wa Roma na hivyo nikaenda pamoja na askari nikamwokoa.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Nilimpeleka mbele ya Baraza lao kuu nikitaka kujua kisa cha mashtaka yao. Niligundua kwamba mashtaka yenyewe yalihusu ubishi juu ya sehemu kadha wa kadha za sheria yao na hivyo sikuona kwamba amefanya chochote kinachostahili auawe au afungwe gerezani.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

1Nani aliyeamini mambo tuliyosikia?
Nani aliyetambua kuwa mkono wa Mwenyezi-Mungu ulihusika?
2Maana, mbele yake Mwenyezi-Mungu,
mtumishi wake alikua kama mti mchanga,
kama mzizi katika nchi kavu.
Hakuwa na umbo wala sura ya kutupendeza,
wala hakuwa na uzuri wowote wa kutuvutia.
3Alidharauliwa na kukataliwa na watu,
alikuwa mtu wa uchungu na huzuni.
Alikuwa kama mtu kinyaa kwa watu;
alidharauliwa na tukamwona si kitu.
4 53:4 Taz Mat 8:17 Hata hivyo alivumilia majonzi yetu,
na kubeba huzuni zetu.
Sisi tulifikiri amepata adhabu,
amepigwa na Mungu na kuteswa.
5 53:5 Taz 1Pet 2:24 Lakini alijeruhiwa kwa sababu ya dhambi zetu,
aliumizwa kwa sababu ya maovu yetu.
Kwa kuadhibiwa kwake sisi tumepata uhai;
kwa kupigwa kwake sisi tumepona.
6 53:6 Taz 1Pet 2:25 Sisi sote tumepotea kama kondoo,
kila mmoja wetu ameelekea njia yake.
Lakini Mwenyezi-Mungu alimtwika adhabu,
ambayo sisi wenyewe tuliistahili.
7 53:7 Taz Ufu 5:6 Alidhulumiwa na kuteswa,
lakini alivumilia kwa unyenyekevu,
bila kutoa sauti hata kidogo.
Alikuwa kama mwanakondoo apelekwaye machinjoni,
kama kondoo akaavyo kimya anapokatwa manyoya.
Hakutoa sauti hata kidogo. 53:7-8 Taz Mate 8:32-33
8Alidhulumiwa, akahukumiwa na kupelekwa kuuawa;
na hakuna mtu aliyejali yanayompata.
Alifukuzwa kutoka nchi ya walio hai,
kwa sababu ya makosa ya watu wangu.
9 53:9 Taz 1Pet 2:22 Walimzika pamoja na wahalifu;
katika kifo aliwekwa pamoja na matajiri,
ingawa hakutenda ukatili wowote,
wala hakusema neno lolote la udanganyifu.
10Mwenyezi-Mungu alipenda kumwumiza
na kumweka katika huzuni.
Alijitoa mhanga kwa ajili ya kuondoa dhambi.
Mtumishi wa Mungu atakuwa na wazawa;
ataishi maisha marefu.
Yeye ndiye atakayetimiza mpango wa Mwenyezi-Mungu.
11Mungu asema:
“Baada ya kutaabika sana,
mtumishi wangu atafurahi.
Kwa kuwajibika kwake kikamilifu,
atatosheka na matokeo hayo.
Kwa maarifa yake mtumishi wangu mwadilifu
atawafanya wengi wawe waadilifu
Yeye atazibeba dhambi zao.53:11 atazibeba dhambi zao: Yaani kwa mateso yake adhabu ya dhambi ambayo watu walistahili imempata yeye nao watu wakasamehewa.
12Kwa hiyo, nitamweka katika cheo cha wakuu,
atagawa nyara pamoja na wenye nguvu;
kwa kuwa alijitolea mwenyewe kufa,
akawekwa katika kundi moja na wakosefu,
alizibeba dhambi za watu wengi,
akawaombea msamaha hao wakosefu.”



Isaya53;1-12

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: