Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 5 December 2019

Kikombe Cha Asubuhi; Yeremia 4....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!



Huyo mama akamwambia, “Najua kwamba Masiha, aitwaye Kristo, anakuja. Atakapokuja atatujulisha kila kitu.” Yesu akamwambia, “Mimi ninayeongea nawe, ndiye.” Hapo wanafunzi wake wakarudi, wakastaajabu sana kuona anaongea na mwanamke. Lakini hakuna mtu aliyesema: “Unataka nini?” au, “Kwa nini unaongea na mwanamke?”
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....



Huyo mama akauacha mtungi wake pale, akaenda mjini na kuwaambia watu, “Njoni mkamwone mtu aliyeniambia mambo yote niliyotenda! Je, yawezekana kuwa yeye ndiye Kristo?” Watu wakatoka mjini, wakamwendea Yesu.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....



Wakati huohuo wanafunzi wake walikuwa wanamsihi Yesu: “Mwalimu, kula chakula.” Lakini Yesu akawaambia, “Mimi ninacho chakula msichokijua nyinyi.” Wanafunzi wake wakaulizana, “Je, kuna mtu aliyemletea chakula?” Yesu akawaambia, “Chakula changu ni kufanya anachotaka yule aliyenituma na kuitimiza kazi yake.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

Wito wa toba
1Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Ukitaka kurudi ee Israeli, nirudie mimi.
Ukiviondoa vitu vya kuchukiza mbele yangu,
usipotangatanga huko na huko,
2ukiapa kwa ukweli, unyofu na uadilifu,
kwa kusema, ‘Kama Mwenyezi-Mungu aishivyo’,
ndipo mataifa yatakapopata baraka kwangu,
na kutukuka kwa sababu yangu.”
3Mwenyezi-Mungu awaambia hivi watu wa Yuda na wakazi wa Yerusalemu:
“Limeni mashamba yenu mapya;
msipande mbegu zenu penye miiba.
4Enyi watu wa Yuda na wakazi wa Yerusalemu,
jitakaseni kwa ajili yangu mimi Mwenyezi-Mungu,
wekeni mioyo yenu wazi mbele yangu.4:4 wekeni … yangu: Kiebrania: Ondoeni govi za mioyo yenu.
La sivyo, ghadhabu yangu itachomoza kama moto,
iwake hata pasiwe na mtu wa kuizima,
kwa sababu ya uovu wa matendo yenu.
Yuda hatarini
5“Tangazeni huko Yuda,
pazeni sauti huko Yerusalemu!
Pigeni tarumbeta kila mahali nchini!
Pazeni sauti na kusema:
Kusanyikeni pamoja!
Kimbilieni miji yenye ngome!
6Twekeni bendera ya vita kuelekea Siyoni,
kimbilieni usalama wenu, msisitesite!
Mwenyezi-Mungu analeta maafa
na maangamizi makubwa kutoka kaskazini.
7Kama simba atokavyo mafichoni mwake,
mwangamizi wa mataifa ameanza kuja,
anakuja kutoka mahali pake,
ili kuiharibu nchi yako.
Miji yako itakuwa magofu matupu,
bila kukaliwa na mtu yeyote.
8Kwa hiyo, vaa vazi la gunia,
omboleza na kulia;
maana, hasira kali ya Mwenyezi-Mungu,
bado haijaondoka kwetu.
9Mwenyezi-Mungu asema hivi: “Siku hiyo, mfalme na wakuu watakufa moyo; makuhani watapigwa na bumbuazi, na manabii watashangaa.” 10Kisha nikasema: “Aa, Mwenyezi-Mungu, hakika umewadanganya kabisa watu hawa na mji wa Yerusalemu! Uliwaambia mambo yatawaendea vema, kumbe maisha yao yamo hatarini kabisa!”
11Wakati huo, wataambiwa hivi watu hawa pamoja na mji wa Yerusalemu, “Upepo wa hari kutoka vilele vikavu vya jangwani utawavumia watu wangu. Huo si upepo wa kupepeta au kusafisha, 12bali ni upepo mkali sana utokao kwangu. Ni mimi Mwenyezi-Mungu nitakayetoa hukumu juu yao.”
Yuda imezingirwa na maadui
13Tazama! Adui anakuja kama mawingu.
Magari yake ya vita ni kama kimbunga,
na farasi wake waenda kasi kuliko tai.
Ole wetu! Tumeangamia!
14Yerusalemu, yasafishe maovu moyoni mwako,
ili upate kuokolewa.
Mpaka lini utaendelea kuwaza maovu?
15Sauti kutoka Dani inatoa taarifa;
inatangaza maafa kutoka vilima vya Efraimu.
16Inayaonya mataifa,
inaitangazia Yerusalemu:
“Wavamizi waja kutoka nchi ya mbali,
wanaitisha miji ya Yuda,
17wanauzingira Yerusalemu kama walinda mashamba,
kwa sababu watu wake wameniasi mimi Mwenyezi-Mungu.
18Yuda, mwenendo wako na matendo yako yamekuletea hayo.
Hayo ndiyo maafa yaliyokupata, tena ni machungu;
yamepenya mpaka ndani moyoni mwako.”
Yeremia awasikitikia watu wake
19Uchungu, uchungu!
Nagaagaa kwa uchungu!
Moyo wangu unanigonga vibaya.
Wala siwezi kukaa kimya.
Maana naogopa mlio wa tarumbeta,
nasikia kingora cha vita.
20Maafa baada ya maafa,
nchi yote imeharibiwa.
Ghafla makazi yangu yameharibiwa,
na hata mapazia yake kwa dakika moja.
21Hadi lini nitaona bendera ya vita
na kuisikia sauti ya tarumbeta?
22Mwenyezi-Mungu asema:
“Watu wangu ni wapumbavu,
hawanijui mimi.
Wao ni watoto wajinga;
hawaelewi kitu chochote.
Ni mabingwa sana wa kutenda maovu,
wala hawajui kutenda mema.”
Ono la Yeremia kuhusu maangamizi
23Niliiangalia nchi, lo! Imekuwa mahame na tupu;
nilizitazama mbingu, nazo hazikuwa na mwanga.
24Niliiangalia milima, lo, ilikuwa inatetemeka,
na vilima vyote vilikuwa vinayumbayumba.
25Nilikodoa macho wala sikuona mtu;
hata ndege angani walikuwa wametoweka.
26Niliona nchi yenye rutuba imekuwa jangwa,
na miji yake yote imekuwa magofu matupu,
kwa sababu ya hasira kali ya Mwenyezi-Mungu.
27Maana Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Nchi nzima itakuwa jangwa tupu;
lakini sitaiharibu kabisa.
28Kwa hiyo, nchi itaomboleza,
na mbingu zitakuwa nyeusi.
Maana, nimetamka na sitabadili nia yangu;
nimeamua, wala sitarudi nyuma.
29Watakaposikika wapandafarasi na wapiga mishale,
kila mmoja atatimua mbio.
Baadhi yao watakimbilia msituni,
wengine watapanda majabali.
Kila mji utaachwa tupu;
hakuna mtu atakayekaa ndani.
30Nawe Yerusalemu uliyeachwa tupu,
unavalia nini mavazi mekundu?
Ya nini kujipamba kwa dhahabu,
na kujipaka wanja machoni?
Unajirembesha bure!
Wapenzi wako wanakudharau sana;
wanachotafuta ni kukuua.
31Nilisikia sauti kama ya mwanamke anayejifungua,
yowe kama anayejifungua mtoto wa kwanza.
Ilikuwa sauti ya Yerusalemu akitweta,
na kuinyosha mikono yake akisema,
‘Ole wangu!
Wanakuja kuniua!’”


Yeremia4;1-31

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Wednesday 4 December 2019

Kikombe Cha Asubuhi; Yeremia 3....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu



Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Huyo mwanamke akamwambia, “Mimi sina mume.” Yesu akamwambia, “Umesema kweli, kwamba huna mume. Maana umekuwa na waume watano, na huyo unayeishi naye sasa si mume wako. Hapo umesema kweli.”
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Huyo Mwanamke akamwambia, “Bwana, naona ya kuwa wewe u nabii. Babu zetu waliabudu juu ya mlima huu, lakini nyinyi mwasema kwamba mahali pa kumwabudia Mungu ni kule Yerusalemu.”
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Yesu akamwambia, “Niamini; wakati unakuja ambapo hamtamwabudu Baba juu ya mlima huu, wala kule Yerusalemu. Nyinyi Wasamaria mnamwabudu yule msiyemjua, lakini sisi tunamjua huyo tunayemwabudu, kwa maana wokovu unatoka kwa Wayahudi. Lakini wakati waja, tena umekwisha wasili, ambapo wenye kuabudu wa kweli watamwabudu Baba katika roho na ukweli. Maana Baba anawataka watu wanaomwabudu namna hiyo. Mungu ni roho, na watu wanaomwabudu lazima wamwabudu kwa Roho na ukweli.”
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Mwisraeli asiye mwaminifu
1“Mume akimpa talaka mkewe,
naye akaondoka kwake,
na kuwa mke wa mwanamume mwingine,
je mume yule aweza kumrudia mwanamke huyo?
Je, kufanya hivyo hakutaitia nchi unajisi mkubwa?
Wewe Israeli, umefanya ukahaba na wapenzi wengi,
je, sasa unataka kunirudia mimi?
2Inua macho uvitazame vilele vya vilima!
Pako wapi mahali ambapo hawajalala nawe?
Uliwangoja wapenzi wako kando ya njia,
kama bedui aviziavyo watu jangwani.
Umeifanya nchi kuwa najisi,
kwa ukahaba wako mbaya kupindukia.
3Ndiyo maana manyunyu yamezuiliwa,
na wala mvua za vuli hazijanyesha.
Hata hivyo uko macho makavu kama kahaba,
huna haya hata kidogo.
4“Hivi punde tu si ulinililia ukisema:
‘Wewe u baba yangu,
ulinipenda tangu utoto wangu?
5Je, utanikasirikia daima?
Utachukizwa nami milele?’
Israeli, hivyo ndivyo unavyosema;
na kumbe umetenda uovu wote ulioweza.”
Israeli na Yuda sharti watubu
6Wakati wa utawala wa mfalme Yosia, Mwenyezi-Mungu aliniambia hivi: “Je, umeona jinsi Israeli asiye mwaminifu alivyofanya? Aliniacha, akapanda juu ya kila kilima kirefu na kwenda chini ya kila mti wenye majani mabichi, akafanya ukahaba wake humo! 7Mimi nilidhani kuwa baada ya kufanya yote hayo, atanirudia. Lakini wapi; hakunirudia. Yuda, dada yake mdanganyifu, alishuhudia yote hayo. 8Zaidi ya hayo, Yuda alishuhudia kuwa nilimpa Israeli talaka kwa sababu ya ukahaba wake na kwa kukosa uaminifu kwangu. Lakini hata hivyo, Yuda, dada yake mdanganyifu, hakuogopa; naye pia alikwenda na kufanya ukahaba! 9Na, kwa kuwa yeye aliona kuwa ukahaba ni jambo dogo sana kwake, aliitia nchi unajisi, na kufanya ukahaba kwa kuabudu mawe na miti. 10Pamoja na hayo yote, Yuda, dada mdanganyifu wa Israeli, hakunirudia kwa moyo wote, bali kwa unafiki tu. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”
11Mwenyezi-Mungu akaniambia, “Mwasi Israeli amedhihirisha kuwa yeye ni afadhali kuliko Yuda mdanganyifu. 12Basi, nenda ukamtangazie Israeli maneno yafuatayo:
Rudi, ewe Israeli, usiye mwaminifu.
Nami sitakutazama kwa hasira
kwa kuwa mimi ni mwenye huruma.
Naam, sitakukasirikia milele.
13Wewe, kiri tu kosa lako:
Kwamba umeniasi mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako;
kwamba chini ya kila mti wenye majani,
umewapa miungu wengine mapenzi yako
wala hukuitii sauti yangu.
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
14“Rudini, enyi watoto msio na uaminifu,
maana, mimi ndimi Bwana wenu.
Nitawachukua mmoja kutoka kila mji,
na wawili kutoka katika kila ukoo,
niwapeleke hadi mlimani Siyoni.
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
15“Nitawapeni wachungaji wanipendao moyoni, watakaowalisha kwa maarifa na busara. 16Siku hizo, wakati mtakapokuwa mmeongezeka na kuwa wengi nchini, watu hawatalitajataja tena sanduku langu la agano. Hawatalifikiria kabisa, wala hawatalikumbuka tena; hawatalihitaji, wala hawataunda jingine. 17Wakati huo, mji wa Yerusalemu utaitwa ‘Kiti cha Enzi cha Mwenyezi-Mungu’, na mataifa yote yatakusanyika humo mbele yangu. Hawatafuata tena ukaidi wa matendo yao. 18Siku hizo, watu wa Yuda wataungana na watu wa Israeli, na wote kwa pamoja watatoka katika nchi ya kaskazini na kurudi katika nchi niliyowapa wazee wenu iwe mali yao.”
Watu wa Mungu waabudu sanamu
19Mwenyezi-Mungu asema,
“Israeli, mimi niliwaza,
laiti ningekuweka miongoni mwa wanangu,
na kukupa nchi nzuri ajabu,
urithi usio na kifani kati ya mataifa yote.
Nilidhani ungeniita, ‘Baba Yangu’,
na kamwe usingeacha kunifuata.
20Lakini kama mke asiye mwaminifu amwachavyo mumewe,
ndivyo ulivyokosa uaminifu kwangu.
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
21“Kelele zasikika juu ya vilima:
Waisraeli wanalia na kuomboleza,
kwa kuwa wamepotoka katika njia zao,
wamenisahau mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wao.
22Rudini, enyi watoto msio na uaminifu,
mimi nitaponya utovu wenu wa uaminifu.
“Nanyi mwasema: ‘Tazama, sisi tunarudi kwako,
maana, wewe ndiwe Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu.
23Kweli tumedanganyika mno kuabudu huko vilimani,
hakika wokovu wa Israeli
watoka kwake Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu.
24“ ‘Tangu ujana wetu, tendo hili la aibu limeangamiza kila kitu walichotolea jasho wazee wetu: Makundi yao ya kondoo na ng'ombe, wana wao na binti zao. 25Hatuna budi kujilaza chini kwa aibu, na kuiacha fedheha yetu itufunike. Tangu ujana wetu hadi leo hii, wazee wetu na sisi wenyewe tumetenda dhambi mbele ya Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, wala hatukumtii Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu.’”

Yeremia3;1-25

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Tuesday 3 December 2019

Kikombe Cha Asubuhi; Yeremia 2....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Yesu akamjibu, “Kama tu ungalijua zawadi ya Mungu na ni nani anayekuambia: ‘Nipatie maji ninywe,’ ungalikwisha mwomba, naye angekupa maji yenye uhai.” Huyo mama akasema, “Bwana, wewe huna chombo cha kutekea maji, nacho kisima ni kirefu; utapata wapi maji yenye uhai? Au, labda wewe wajifanya mkuu zaidi kuliko baba yetu Yakobo? Yeye alitupa sisi kisima hiki; na yeye mwenyewe, watoto wake na mifugo wake walikunywa maji ya kisima hiki.”
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Yesu akamjibu, “Kila anayekunywa maji haya ataona kiu tena. Lakini atakayekunywa maji nitakayompa mimi, hataona kiu milele. Maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji ya uhai na kumpatia uhai wa milele.”
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....


Huyo mwanamke akamwambia, “Bwana, nipe maji hayo ili nisione kiu tena; na, nisije tena mpaka hapa kuteka maji.” Yesu akamwambia, “Nenda ukamwite mumeo, uje naye hapa.”
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.


Mungu awalinda Waisraeli
1Neno la Mwenyezi-Mungu likanijia: 2“Nenda ukawatangazie waziwazi wakazi wote wa Yerusalemu kuwa mimi Mwenyezi-Mungu nasema hivi:
Naukumbuka uaminifu wako ulipokuwa kijana,
jinsi ulivyonipenda kama mchumba wako,
ulivyonifuata jangwani
kwenye nchi ambayo haikupandwa kitu.
3Israeli, wewe ulikuwa mtakatifu kwangu,
ulikuwa matunda ya kwanza ya mavuno yangu.
Wote waliokudhuru walikuwa na hatia,
wakapatwa na maafa.
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”
Dhambi ya wazee wa Israeli
4Sikilizeni neno la Mwenyezi-Mungu, enyi wazawa wa Yakobo. Sikilizeni enyi jamaa zote za wazawa wa Israeli.
5Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Wazee wenu waliona kosa gani kwangu
hata wakanigeuka na kuniacha,
wakakimbilia miungu duni,
hata nao wakawa watu duni?
6Hawakujiuliza:
‘Yuko wapi Mwenyezi-Mungu aliyetutoa nchini Misri,
aliyetuongoza nyikani
katika nchi ya jangwa na makorongo,
nchi kame na yenye giza nene,
nchi isiyopitiwa na mtu yeyote,
wala kukaliwa na binadamu?’
7Niliwaleta katika nchi yenye rutuba,
muyafurahie mazao yake na mema yake mengine.
Lakini mlipofika tu mliichafua nchi yangu,
mkaifanya chukizo nchi niliyowapa iwe yenu.
8Nao makuhani hawakujiuliza: ‘Yuko wapi Mwenyezi-Mungu?’
Wataalamu wa sheria hawakunijua,
viongozi2:8 viongozi: Kiebrania: Wachungaji. wa watu waliniasi;
manabii nao walitabiri kwa jina la Baali
na kuabudu sanamu zisizo na faida yoyote.”
Mashtaka ya Mwenyezi-Mungu dhidi ya watu wake
9Mwenyezi-Mungu asema,
“Kwa hiyo, mimi nitawalaumu nyinyi,
na nitawalaumu wazawa wenu.
10Haya, vukeni bahari hadi Kupro2:10 Kupro: Au Mwambao wa nchi za Ugiriki na Italia. mkaone,
au tumeni watu huko Kedari2:10 Kedari: Makazi ya Mabedui katika jangwa la Suria na Arabia. wakachunguze,
kama jambo kama hili limewahi kutokea:
11Kwamba kuna taifa lililowahi kubadilisha miungu yake
ingawa miungu hiyo si miungu!
Lakini watu wangu wameniacha mimi, utukufu wao,
wakafuata miungu isiyofaa kitu.
12Shangaeni enyi mbingu, juu ya jambo hili,
mkastaajabu na kufadhaika kabisa.
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
13Maana, watu wangu wametenda maovu mawili;
wameniacha mimi niliye chemchemi ya maji ya uhai,
wakajichimbia visima vyao wenyewe,
visima vyenye nyufa, visivyoweza kuhifadhi maji.
Matokeo ya utovu wa imani ya Israeli
14“Je, Israeli ni mtumwa,
ama amezaliwa utumwani?
Mbona basi amekuwa kama mawindo?
15Simba wanamngurumia,
wananguruma kwa sauti kubwa.
Nchi yake wameifanya jangwa,
miji yake imekuwa magofu, haina watu.
16Isitoshe, watu wa Memfisi na Tahpanesi,
wameuvunja utosi wake.2:16 wameuvunja … wake: Kitendo kinachomaanisha angamizo kubwa.
17Israeli, je, hayo yote si umejiletea mwenyewe,
kwa kuniacha mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako,
niliyekuwa ninakuongoza njiani?
18Na sasa itakufaa nini kwenda Misri,
kunywa maji ya mto Nili?
Au itakufaa nini kwenda Ashuru,
kunywa maji ya mto Eufrate?
19Uovu wako utakuadhibu;
na uasi wako utakuhukumu.
Ujue na kutambua kuwa ni vibaya mno
kuniacha mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako,
na kuondoa uchaji wangu ndani yako.
Mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi nimesema.
Israeli yakataa kumwabudu Mwenyezi-Mungu
20“Tangu zamani wewe ulivunja nira yako,
ukaikatilia mbali minyororo yako,
ukasema, ‘Sitakutumikia’.
Juu ya kila kilima kirefu
na chini ya kila mti wa majani mabichi,
uliinamia miungu ya rutuba kama kahaba.2:20 Katika Israeli kuabudu miungu mingine kulifananishwa na ukahaba.
21Lakini mimi nilikupanda kama mzabibu mteule,
mzabibu wenye afya na wa mbegu safi;
mbona basi umeharibika,
ukageuka kuwa mzabibu mwitu?
22Hata ukijiosha kwa magadi,
na kutumia sabuni nyingi,
madoa ya uovu wako bado yatabaki mbele yangu.
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
23“Unawezaje kusema, ‘Mimi si najisi;
sijawafuata Mabaali?’
Tazama ulivyotenda dhambi kule bondeni;
angalia ulivyofanya huko!
Wewe ni kama mtamba wa ngamia,
akimbiaye huko na huko;
24kama pundamwitu aliyezoea jangwani.
Katika tamaa yake hunusanusa upepo;
nani awezaye kuizuia hamu yake?
Amtakaye hana haja ya kujisumbua;
wakati wake ufikapo watampata tu.
25Israeli, usiichakaze miguu yako
wala usilikaushe koo lako.
Lakini wewe wasema: ‘Hakuna tumaini lolote.
Nimeipenda miungu ya kigeni,
hiyo ndiyo nitakayoifuata.’
Israeli astahili kuadhibiwa
26“Kama vile mwizi aonavyo aibu akishikwa,
ndivyo Waisraeli watakavyoona aibu;
wao wenyewe, wafalme wao, wakuu wao,
makuhani wao na manabii wao.
27Hao huuambia mti: ‘Wewe u baba yangu,’
na jiwe: ‘Wewe ndiwe uliyenizaa;’
kwa maana wamenipa kisogo,
wala hawakunielekezea nyuso zao.
Lakini wakati wa shida husema: ‘Inuka utuokoe!’
28“Lakini iko wapi miungu yako uliyojifanyia?
Iinuke basi, kama inaweza kukusaidia,
wakati unapokuwa katika shida.
Ee Yuda, idadi ya miungu yako
ni sawa na idadi ya miji yako!
29Mbona mnanilalamikia?
Nyinyi nyote mmeniasi.
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
30Niliwaadhibu watu wako bila kufanikiwa,
wao wenyewe walikataa kukosolewa.
Upanga wako uliwamaliza manabii wako
kama simba mwenye uchu.
31Enyi watu! Sikilizeni ninachosema mimi Mwenyezi-Mungu:
Je, nimekuwa jangwa kwa Israeli
au nchi yenye giza nene?
Kwa nini basi watu wangu waseme:
‘Sisi tu watu huru;
hatutakuja kwako tena!’
32Kijana msichana aweza kusahau mapambo yake
au bibi arusi mavazi yake?
Lakini watu wangu wamenisahau
kwa muda wa siku zisizohesabika.
33Kweli wewe ni bingwa wa kutafuta wapenzi!
Hata wanawake wabaya huwafundisha njia zako.
34Nguo zako zina damu ya maskini wasio na hatia,
japo hukuwakuta wakivunja nyumba yako.
“Lakini licha ya hayo yote,
35wewe wasema: ‘Mimi sina hatia;
hakika hasira yake imegeuka mbali nami.’
Lakini mimi nitakuhukumu kwa sababu unasema:
‘Sikutenda dhambi.’
36Kwa nini unajirahisisha hivi,
ukibadilibadili mwenendo wako?
Utaaibishwa na Misri,
kama ulivyoaibishwa na Ashuru.
37Na huko pia utatoka,
mikono kichwani kwa aibu.
Mimi Mwenyezi-Mungu nimewakataa wale uliowategemea,
wala hutafanikiwa kwa msaada wao.


Yeremia2;1-37

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 2 December 2019

Kikombe Cha Asubuhi; Tunamshukuru Mungu kwa kumaliza Kitabu cha Isaya,Leo Tunaanza Kitabu cha Yeremia 1....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki/Mwezi
Mwingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....


Tunamshukuru Mungu kwa kutupa kibali cha

 kupitia kitabu cha "ISAYA
"
Ni matumaini yangu kuna mengi tumejifunza/kufaidika
na kutupa mwanga/kuelewa kwenye kitabu hiki...


Leo tunapokwenda anza kupitia Kitabu cha"YEREMIA"tunamuomba Mungu wetu akatupe kibali,macho ya rohoni
 na akili ya kuelewa katika kujifunza NENO lake...
Ee Mungu  tunaomba ukatuongoze...!!

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni
Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!


Mafarisayo walisikia kwamba Yesu alikuwa anabatiza na kuwapata wanafunzi wengi kuliko Yohane. (Lakini ukweli ni kwamba Yesu hakuwa anabatiza ila wanafunzi wake.) Basi, Yesu aliposikia hayo, alitoka Yudea akarudi Galilaya; na katika safari hiyo ilimbidi apitie Samaria.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza
kuwasamehe wale wote waliotukosea,
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,

Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Basi, akafika Sukari, mji mmoja wa Samaria, karibu na shamba ambalo Yakobo alikuwa amempa mwanawe, Yosefu. Mahali hapo palikuwa na kisima cha Yakobo, naye Yesu, kutokana na uchovu wa safari, akaketi kando ya kisima. Ilikuwa yapata saa sita mchana.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Basi, mwanamke mmoja Msamaria akafika kuteka maji. Yesu akamwambia, “Nipatie maji ninywe.” (Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wamekwenda mjini kununua chakula.) Lakini huyo mwanamke akamwambia, “Wewe ni Myahudi; mimi ni mwanamke Msamaria! Unawezaje kuniomba maji?” (Wayahudi hawakuwa na ushirikiano na Wasamaria katika matumizi ya vitu).
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....
Nawapenda.

1Yafuatayo ni maneno ya Yeremia mwana wa Hilkia, mmoja wa makuhani wa mji wa Anathothi, katika nchi ya Benyamini. 2Neno la Mwenyezi-Mungu lilimjia Yeremia mnamo mwaka wa kumi na tatu wa utawala wa Yosia mwana wa Amoni, mfalme wa Yuda. 3Lilimjia tena wakati Yehoyakimu mwana wa Yosia, alipokuwa mfalme wa Yuda. Yeremia aliendelea kupata neno la Mwenyezi-Mungu hadi mwishoni mwa mwaka wa kumi na moja wa utawala wa Sedekia mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda. Mnamo mwezi wa tano wa mwaka huo, watu wa Yerusalemu walipelekwa uhamishoni.
Yeremia anaitwa kuwa nabii
4Mwenyezi-Mungu aliniambia neno lake:
5“Kabla hujachukuliwa mimba, mimi nilikujua,
kabla hujazaliwa, mimi nilikuweka wakfu;
nilikuteua uwe nabii kwa mataifa.”
6Nami nikajibu, Aa! Bwana Mwenyezi-Mungu,
mimi sijui kusema, kwa kuwa bado ningali kijana.
7Lakini Mwenyezi-Mungu akaniambia,
“Usiseme kwamba wewe ni kijana bado.
Utakwenda kwa watu wote nitakaokutuma kwao,
na yote nitakayokuamuru utayasema.
8Wewe usiwaogope watu hao,
kwa maana niko pamoja nawe kukulinda.
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”
9Kisha Mwenyezi-Mungu akaunyosha mkono wake, akagusa kinywa changu, akaniambia,
“Tazama nimeyatia maneno yangu kinywani mwako.
10Leo nimekupa mamlaka juu ya mataifa na falme,
uwe na mamlaka ya kungoa na kubomoa,
mamlaka ya kuharibu na kuangamiza,
mamlaka ya kujenga na ya kupanda.”
Maono mawili
11Neno la Mwenyezi-Mungu lilinijia: “Yeremia, unaona nini?” Nami nikasema, “Ninaona tawi la mlozi1:11 mlozi: Mti wa kwanza kuchanua baada ya mvua nchini Palestina; aidha hapa tunapewa picha ya mti ambao ulikuwa “macho” tayari kuchanua mara baada ya mvua. unaochanua.” 12Mwenyezi-Mungu akaniambia, “Umeona vizuri, maana niko macho kulitekeleza neno langu.”
13Neno la Mwenyezi-Mungu likanijia mara ya pili: “Unaona nini?” Nami nikasema, “Ninaona chungu kinatokota kimeinama upande wangu kutoka kaskazini.”
14Mwenyezi-Mungu akaniambia, “Maangamizi yataanzia kutoka kaskazini na kuwapata wakazi wote wa nchi hii. 15Maana naziita falme zote za kaskazini na makabila yote. Wafalme wake wote watakuja na kila mmoja wao ataweka kiti chake cha enzi mbele ya malango ya Yerusalemu na kandokando ya kuta zake zote, na kuizunguka miji yote ya Yuda. 16Nami nitawahukumu Waisraeli kwa ajili ya uovu wao wote wa kuniacha mimi, wakafukizia ubani miungu mingine na kuabudu sanamu walizojitengenezea wenyewe. 17Sasa basi, wewe Yeremia jiweke tayari. Haya! Nenda ukawaambie mambo yote ninayokuamuru. Usiwaogope, nisije nikakufanya mwoga mbele yao. 18Leo hii nakufanya kuwa imara kama mji uliozungukwa na ngome, kama mnara wa chuma na kama ukuta wa shaba nyeusi, dhidi ya nchi yote, dhidi ya wafalme wa Yuda, wakuu wake, makuhani wake na watu wake wote. 19Watapigana nawe, lakini hawatashinda kwa sababu mimi niko pamoja nawe kukuokoa. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”


Yeremia1;1-19

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.