Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 25 November 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 62....



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki
Nyingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu

Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!


Mfalme Nebukadneza wa Babuloni aliuharibu na kuuponda mji wa Yerusalemu aliuacha kama chungu kitupu; aliumeza kama joka. Alijaza tumbo lake vitu vyake vizurivizuri, akautupilia mbali kama matapishi. Watu wa Yerusalemu na waseme: “Babuloni na ulipizwe ukatili uleule, tuliotendwa sisi pamoja na jamaa zetu! Babuloni ipatilizwe kwa umwagaji wa damu yetu.”
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona....

Kwa hiyo asema hivi Mwenyezi-Mungu: “Nitawatetea kuhusu kisa chenu, na kulipiza kisasi kwa ajili yenu. Nitaikausha bahari ya Babuloni na kuvifanya visima vyake vikauke. Babuloni itakuwa rundo la magofu, itakuwa makao ya mbweha, itakuwa kinyaa na kitu cha kuzomewa; hakuna mtu atakayekaa huko.
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Wababuloni watanguruma pamoja kama simba; watakoroma kama wanasimba. Wakiwa na uchu mkubwa nitawaandalia karamu: Nitawalewesha mpaka wapepesuke; nao watalala usingizi wa daima na hawataamka tena. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimamie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.




1Kwa ajili ya Siyoni sitakaa kimya,

kwa ajili ya Yerusalemu sitatulia,
mpaka kuokolewa kwake kuchomoze kama umeme,
wokovu wake utokeze kama mwenge.
2Mataifa watauona wokovu wako,
wafalme wote watauona utukufu wako.
Nawe utaitwa kwa jina jipya,
jina atakalokupa Mwenyezi-Mungu mwenyewe.
3Utakuwa taji zuri mkononi mwa Mwenyezi-Mungu;
kilemba cha kifalme mkononi mwa Mungu wako.
4Hutaitwa tena: “Aliyeachwa”,
wala nchi yako haitaitwa: “Ukiwa”.
Bali utaitwa: “Namfurahia,”
na nchi yako itaitwa: “Aliyeolewa.”
Maana Mwenyezi-Mungu amependezwa nawe,
naye atakuwa kama mume wa nchi yako.
5Maana kama kijana mwanamume amwoavyo msichana,
ndivyo aliyekujenga62:5 aliyekujenga: Kiebrania: Wanao. atakavyokuwa mume wako.
Kama bwana arusi afurahivyo juu ya bibi arusi,
ndivyo Mungu atakavyofurahi juu yako.
6“Juu ya kuta zako ee Yerusalemu nimeweka walinzi,
usiku na mchana kamwe hawatakaa kimya.”
Enyi mnaomkumbusha Mwenyezi-Mungu ahadi yake,
msikae kimya;
7msimpe hata nafasi ya kupumzika,
mpaka atakapousimika mji wa Yerusalemu,
na kuufanya uwe fahari ulimwenguni kote.
8Mwenyezi-Mungu ameapa kwa mkono wake wa kulia,
naam, ameapa kwa mkono wake wenye nguvu akisema:
“Sitawapa tena maadui zako nafaka yako;
wala wageni hawatakunywa tena divai yako
ambayo umeitolea jasho.
9Bali nyinyi mliyoivuna nafaka hiyo,
mtaila na kunitukuza mimi Mwenyezi-Mungu.
Nyinyi mliochuma zabibu hizo,
mtakunywa divai yake katika nyua zangu takatifu.”
10Wakazi wa Yerusalemu, tokeni, tokeni nje ya mji,
watayarishieni njia watu wenu wanaorejea!
Jengeni! Jengeni barabara na kuondoa mawe yote!
Wekeni alama kwa ajili ya watu.
11 62:11 Taz Isa 40:10; Ufu 22:12 Mwenyezi-Mungu ametangaza duniani kote,
waambie watu wa Siyoni:
“Mkombozi wenu anakuja,
zawadi yake iko pamoja naye
na tuzo lake liko mbele yake.”
12Nyinyi mtaitwa: “Watu Watakatifu”,
“Watu waliokombolewa na Mwenyezi-Mungu.”
Na Yerusalemu utaitwa: “Mji aupendao Mungu”,
“Mji ambao Mungu hakuuacha.”


Isaya62;1-12

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Friday 22 November 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 61....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!


Tweka bendera ya vita duniani, piga tarumbeta kati ya mataifa; yatayarishe mataifa kupigana naye; ziite falme kuishambulia; falme za Ararati, Mini na Ashkenazi. Weka majemadari dhidi yake; walete farasi kama makundi ya nzige. Yatayarishe mataifa kupigana naye vita; watayarishe wafalme wa Medi, watawala na mawakili wao, tayarisheni nchi zote katika himaya yake.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Nchi inatetemeka na kugaagaa kwa maumivu, maana nia ya Mwenyezi-Mungu kuhusu Babuloni ni thabiti: Ataifanya nchi ya Babuloni kuwa jangwa, ataifanya iwe bila watu. Askari wa Babuloni wameshindwa kupigana, wamebaki katika ngome zao; nguvu zao zimewaishia, wamekuwa kama wanawake. Nyumba za Babuloni zimechomwa moto, malango yake ya chuma yamevunjwa.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Tarishi baada ya tarishi wanapiga mbio, mjumbe mmoja anamfuata mjumbe mwingine, kumpasha habari mfalme wa Babuloni kwamba mji wake umevamiwa kila upande. Vivuko vya mto vimetekwa, ngome zimechomwa moto, askari wamekumbwa na hofu. Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli asema hivi: “Babuloni ni kama uwanja wa kupuria nafaka wakati unapotayarishwa. Lakini bado kidogo tu, wakati wa mavuno utaufikia.”
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Habari njema ya wokovu
1Bwana Mwenyezi-Mungu amenijaza roho yake,
maana Mwenyezi-Mungu ameniweka wakfu,61:1 ameniweka wakfu: Neno kwa neno Kiebrania: Amenipaka mafuta; Taz Orodha ya Maneno chini ya Paka mafuta.
akanituma niwaletee wanaokandamizwa habari njema,
niwatibu waliovunjika moyo,
niwatangazie mateka kwamba watapata uhuru,
na wafungwa kwamba watafunguliwa.
2Amenituma niutangaze mwaka wake wa neema,
na siku ya Mungu wetu ya kulipiza kisasi;
niwafariji wote wanaoomboleza;
3niwape wale wanaoomboleza katika Siyoni
taji la maua badala ya majivu,
mafuta ya furaha badala ya maombolezo,
vazi la sifa badala ya moyo mzito.
Nao wataitwa mialoni madhubuti,
aliyopanda Mwenyezi-Mungu kuonesha utukufu wake.
4Watayajenga upya magofu ya zamani,
wataisimika miji iliyoharibiwa hapo kwanza;
wataitengeneza miji iliyobomolewa,
uharibifu wa vizazi vingi vilivyopita.
5Wageni watakuwa hapo kuwachungia mifugo yenu;
watawalimia na kuwatunzia mizabibu yenu.
6Nanyi mtaitwa: “Makuhani wa Mwenyezi-Mungu”,
Mtaitwa: “Watumishi wake Mungu wetu”.
Mtafaidika kwa utajiri wa mataifa,
mtatukuka kwa mali zao.
7Kwa vile mlipata aibu maradufu,
watu wakaona kuwa fedheha ni majaliwa yenu,
sasa mtapata eneo maradufu kuwa mali yenu,
na furaha yenu itadumu milele.
8“Mimi Mwenyezi-Mungu napenda haki;
nachukia unyanganyi na uhalifu.
Nitawatuza watu wangu kwa uaminifu,
nitafanya nao agano la milele.
9Wazawa wao watakuwa maarufu kati ya mataifa;
watajulikana kuwa maarufu kati ya watu wengine.
Kila atakayewaona atakiri kwamba
wao ni watu aliowabariki Mwenyezi-Mungu.”
10Nitafurahi sana kwa sababu ya Mwenyezi-Mungu,
nafsi yangu itashangilia kwa sababu ya Mungu wangu.
Maana amenivika vazi la wokovu,
amenivalisha vazi la uadilifu,
kama bwana arusi ajipambavyo kwa shada la maua,
kama bibi arusi ajipambavyo kwa johari zake.
11Hivyo, kama vile ardhi ioteshavyo mimea,
na shamba lichipushavyo mbegu zilizopandwa humo,
Mwenyezi-Mungu atasababisha uadilifu na sifa
kuchomoza mbele ya mataifa yote.


Isaya61;1-11

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 21 November 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 60....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!


Mwenyezi-Mungu asema hivi: “Wewe Babuloni ni rungu na silaha yangu ya vita; nakutumia kuyavunjavunja mataifa, nakutumia kuangamiza falme. Nakutumia kuponda farasi na wapandafarasi, magari ya kukokotwa na waendeshaji wake. Ninakutumia kuwaponda wanaume na wanawake, wazee na vijana, wavulana na wasichana. Ninakutumia kuponda wachungaji na makundi yao, wakulima na wanyama wao wa kulimia, wakuu wa mikoa na madiwani.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....


“Nitaiadhibu Babuloni na wakazi wote wa Kaldayo mkiona kwa macho yenu wenyewe, kwa sababu ya uovu wote walioufanya katika Siyoni. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....


Mimi ninapingana nawe ewe mlima mharibifu, mlima unaoharibu dunia nzima! Nasema mimi Mwenyezi-Mungu. Nitanyosha mkono wangu dhidi yako, nitakuangusha kutoka miambani juu na kukufanya kuwa mlima uliochomwa moto; hata hamna jiwe lako litakalochukuliwa kujengea, hakuna jiwe litakalochukuliwa kuwekea msingi! Utakuwa kama jangwa milele. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

Yerusalemu mpya
1Inuka ee Siyoni uangaze;
maana mwanga unachomoza kwa ajili yako,
utukufu wa Mwenyezi-Mungu unakuangaza.
2Tazama, giza litaifunika dunia,
giza nene litayafunika mataifa;
lakini wewe, Mwenyezi-Mungu atakuangazia,
utukufu wake utaonekana kwako.
3Mataifa yataujia mwanga wako,
wafalme waujia mwanga wa pambazuko lako.
4Inua macho utazame pande zote;
wote wanakusanyika waje kwako.
Wanao wa kiume watafika toka mbali,
wanao wa kike watabebwa mikononi.
5Utaona na uso wako utangara,
moyo wako utasisimka na kushangilia.
Maana utajiri wa bahari utakutiririkia,
mali za mataifa zitaletwa kwako.
6Makundi ya ngamia yataifunika nchi yako,
naam, ndama wa ngamia kutoka Midiani na Efa;
wote kutoka Sheba watakuja.
Watakuletea dhahabu na ubani,
wakitangaza sifa za Mwenyezi-Mungu.
7Makundi ya kondoo wa Kedari yatakusanywa kwako,
utaweza kuwatumia kondoo madume wa Nebayothi kuwa kafara;
utawatoa kuwa tambiko inayokubalika madhabahuni pa Mungu,
naye ataitukuza nyumba yake tukufu.
8Nani hao wanaopepea kama mawingu,
kama njiwa wanaoruka kwenda viotani mwao?
9Ni meli zitokazo nchi za mbali,
zikitanguliwa na meli za Tarshishi.
Zinawaleta watoto wako,
pamoja na fedha na dhahabu yao,
kwa sifa ya Mwenyezi-Mungu, Mungu wako,
kwa sifa ya Mungu, Mtukufu wa Israeli,
maana amewafanya mtukuke.
10Mwenyezi-Mungu asema:
“Wageni watazijenga upya kuta zako,
wafalme wao watakutumikia.
Maana kwa hasira yangu nilikupiga,
lakini kwa fadhili yangu nimekuhurumia.
11 60:11 Taz Ufu 21:25-26 Malango yako yatakuwa wazi daima;
usiku na mchana hayatafungwa,
ili watu wakuletee utajiri wa mataifa,
pamoja na wafalme wao katika maandamano.
12Kila ufalme au taifa lisilokutumikia litaangamia;
mataifa hayo yatatokomezwa kabisa.
13“Utaletewa fahari ya msitu wa Lebanoni:
Mbao za miberoshi, mivinje na misonobari,
zitumike kupamba mahali pa maskani yangu;
nami nitaparembesha hapo ninapokaa.
14 60:14 Taz Ufu 3:9 Wazawa wa wale waliokudhulumu,
watakuja na kukuinamia kwa heshima.
Wote wale waliokudharau,
watasujudu mbele ya miguu yako.
Watakuita: ‘Mji wa Mwenyezi-Mungu’,
‘Siyoni, Mji wa Mtakatifu wa Israeli’.
15“Wewe ulikuwa umeachwa na kuchukiwa,
hakuna aliyependa hata kupitia kwako.
Lakini sasa nitakufanya uwe na fahari milele,
utakuwa mji wa furaha kizazi hata kizazi.
16Utaletewa chakula na watu wa mataifa,
naam, wafalme watakupatia chakula bora.
Hapo utatambua kuwa mimi Mwenyezi-Mungu ni Mwokozi wako;
mimi Mwenye Nguvu wa Yakobo ni Mkombozi wako.
17“Badala ya shaba nitakuletea dhahabu,
badala ya chuma nitakuletea fedha,
badala ya miti, nitakuletea shaba,
na badala ya mawe nitakuletea chuma.
Amani itatawala juu yako,
uadilifu utakuongoza.
18Ukatili hautasikika tena nchini mwako;
wala uharibifu na maangamizi ndani ya mipaka yako.
Utaweza kuziita kuta zako: ‘Wokovu’,
na malango yako: ‘Sifa’.60:18 Wokovu, Sifa: Majina mapya yanamaanisha hali mpya.
19Hutahitaji tena jua kukuangazia mchana,
wala mwezi kukumulikia usiku;
maana mimi Mwenyezi-Mungu ni mwanga wako milele;
mimi Mungu wako nitakuwa fahari yako.
20Mwanga wako mchana hautatua kama jua,
wala mwangaza wako usiku kufifia kama mbalamwezi;
maana Mwenyezi-Mungu ni mwanga wako milele,
nazo siku zako za kuomboleza zitakoma.
21Watu wako wote watakuwa waadilifu,
nao wataimiliki nchi milele.
Hao ni chipukizi nililopanda mimi,
kazi ya mikono yangu kwa ajili ya utukufu wangu.
22Aliye mdogo kati yenu atakuwa ukoo,
aliye mdogo kuliko wote atakuwa taifa kubwa.
Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu;
wakati ufikapo nitayatekeleza hayo haraka.”


Isaya60;1-22

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Wednesday 20 November 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 59....



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu



Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!




Mwenyezi-Mungu ndiye aliyeumba dunia kwa nguvu yake, aliyeuimarisha ulimwengu kwa hekima yake, na kwa maarifa yake akazitandaza mbingu. Anapotoa sauti yake maji hutitima mbinguni, hufanya ukungu upande kutoka mipaka ya dunia. Hufanya umeme umulike wakati wa mvua huvumisha upepo kutoka ghala zake.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Kila mtu ni mpumbavu bila maarifa, kila mhunzi anaaibishwa na vinyago vyake; maana sanamu zake ni udanganyifu mtupu, wala hazina pumzi ndani yake. Hazina thamani, ni udanganyifu mtupu; wakati watakapoadhibiwa, nazo zitaangamia.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Mungu aliye hazina ya Yakobo si kama hizo, maana yeye ndiye aliyeviumba vitu vyote, na Israeli ni kabila lililo mali yake; Mwenyezi-Mungu wa Majeshi, ndilo jina lake.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Nabii azilaani dhambi za watu
1Msifikiri mkono wa Mungu ni mfupi,
hata asiweze kuwaokoeni;
au masikio yake yamezibika,
hata asiweze kuwasikieni.
2Dhambi zenu ndizo zinazowatenga na Mungu wenu,
dhambi zenu zimemfanya ajifiche mbali nanyi
hata asiweze kuwasikieni.
3Maana mikono yenu imetiwa najisi kwa mauaji,
na vidole vyenu kwa matendo maovu.
Midomo yenu imesema uongo,
na ndimi zenu husema uovu.
4Hakuna atoaye madai yake kwa haki,
wala anayeshtaki kwa uaminifu.
Mnategemea hoja batili;
mnasema uongo.
Mnatunga hila na kuzaa uovu.
5Mnaangua mayai ya joka lenye sumu,
mnafuma utando wa buibui.
Anayekula mayai yenu hufa,
na yakipasuliwa nyoka hutokea.
6Utando wenu haufai kwa mavazi,
watu hawawezi kujifunikia mnachofuma.
Kazi zenu ni kazi za uovu,
matendo yenu yote ni ukatili mtupu.
7Mko mbioni kutenda maovu,
mnaharakisha kumwaga damu isiyo na hatia.
Mawazo yenu ni mawazo ya uovu,
popote mwendapo mnaacha ukiwa na uharibifu.
8Njia ya amani hamwijui kamwe;
njia zenu zote ni za dhuluma.
Mmejifanyia njia potovu,
yeyote anayepitia humo hapati amani.
Watu wanakiri dhambi yao
9Ndio maana haki iko mbali nasi,
maongozi ya uadilifu hayapo kwetu.
Tunatazamia kupata mwanga kumbe ni giza tupu,
twatazamia mwangaza, lakini twatembea gizani.
10Kama vipofu twapapasapapasa ukuta;
tunasitasita kama watu wasio na macho.
Tunajikwaa mchana kana kwamba ni usiku,
miongoni mwa wenye nguvu sisi ni kama wafu.
11Twanguruma kama dubu,
twaomboleza tena na tena kama hua.
Twatazamia hukumu ya haki, lakini haipo,
twatazamia wokovu, lakini uko mbali nasi.
12Makosa yetu mbele yako ni mengi mno,
dhambi zetu zashuhudia dhidi yetu.
Naam, makosa yetu tunaandamana nayo,
tunayajua maovu yetu.
13Tumekuasi na kukukana ee Mwenyezi-Mungu,
tumekataa kukufuata ewe Mungu wetu.
Udhalimu na uasi ndivyo tunavyopania,
mioyoni mwetu twatunga na kutoa maneno ya uongo.
14Haki imewekwa kando,
uadilifu uko mbali;
ukweli unakanyagwa mahakamani,
uaminifu haudiriki kuingia humo.
15Ukweli umekosekana,
naye anayeacha uovu hunyanyaswa.
Mungu ajiandaa kuwakomboa watu wake
Mungu aliona mambo hayo, akachukizwa,
alichukizwa kwamba hakuna haki.
16Aliona kwamba hakuna mtu aliyejali,
akashangaa kwamba hakuna aliyeingilia kati.
Basi akaamua kunyosha mkono wake mwenyewe,
uadilifu wake ukamhimiza.
17Alivaa uadilifu kama vazi la kujikinga kifuani,
na wokovu kama kofia ya chuma kichwani.
Atajivika kisasi kama vazi,
na kujifunika wivu kama joho.
18Atawaadhibu maadui kadiri ya matendo yao,
naam, ghadhabu yake na kisasi vitawapata maadui zake;
atawaadhibu hata wakazi wa nchi za mbali.
19Toka magharibi hadi mashariki,
kila mtu atamcha Mwenyezi-Mungu
na kutambua utukufu wake.
Maana atakuja kama mto uendao kasi,
mto unaosukumwa kwa upepo wa Mwenyezi-Mungu.
20Naye atakuja Siyoni kama Mkombozi,
Mkombozi wa wazawa wa Yakobo
ambao wataachana na makosa yao.
Asema Mwenyezi-Mungu.
21Mwenyezi-Mungu asema:
“Mimi nafanya nanyi agano hili:
Roho yangu niliyowajazeni,
maneno niliyoyaweka mdomoni mwenu,
hayataondoka kwenu kamwe,
wala kwa watoto na wajukuu zenu,
tangu sasa na hata milele.”


Isaya59;1-21

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.