Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Monday 28 October 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 42....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki nyingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu

Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!

Waliposikia hayo, waliwaka hasira, wakaanza kupiga kelele: “Mkuu ni Artemi wa Efeso!” Mji wote ukajaa ghasia. Wakawavamia Gayo na Aristarko, wenyeji wa Makedonia, ambao walikuwa wasafiri wenzake Paulo, wakakimbia nao mpaka kwenye ukumbi wa michezo.
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona....

Paulo mwenyewe alitaka kuukabili huo umati wa watu, lakini wale waumini walimzuia. Maofisa wengine wa huo mkoa wa Asia, waliokuwa rafiki zake, walimpelekea Paulo ujumbe wakimsihi asijihatarishe kwa kwenda kwenye ukumbi wa michezo.
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Wakati huo, kila mtu alikuwa anapayuka; wengine hili na wengine lile, mpaka hata ule mkutano ukavurugika. Wengi hawakujua hata sababu ya kukutana kwao. Kwa vile Wayahudi walimfanya Aleksanda ajitokeze mbele, baadhi ya watu katika ule umati walidhani kuwa ndiye. Basi, Aleksanda aliwaashiria watu kwa mkono akitaka kujitetea mbele ya ule umati wa watu.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimamie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.


Mtumishi wa Mungu
1“Tazameni mtumishi wangu ninayemtegemeza;
mteule wangu ambaye moyo wangu umependezwa naye.
Nimeiweka roho yangu juu yake,
naye atayaletea mataifa haki.
2Hatalia wala hatapiga kelele,
wala hatapaza sauti yake barabarani.
3Mwanzi uliochubuka hatauvunja,
utambi ufukao moshi hatauzima;
ataleta haki kwa uaminifu.
4Yeye hatafifia wala kufa moyo,
hata atakapoimarisha haki duniani.
Watu wa mbali wanangojea mwongozo wake.”
Mwanga wa mataifa
5Hivi ndivyo asemavyo Mwenyezi-Mungu
aliyeziumba mbingu, akazitandaza kama hema,
yeye aliyeiunda nchi na vyote vilivyomo,
yeye awapaye watu waliomo pumzi,
na kuwajalia uhai wote waishio humo:
6“Mimi Mwenyezi-Mungu nimekuita kutenda haki,
nimekushika mkono na kukulinda.
Kwa njia yako nitaweka ahadi na watu wote,
wewe utakuwa mwanga wa mataifa.
7Utayafumbua macho ya vipofu,
utawatoa wafungwa gerezani,
waliokaa gizani utawaletea uhuru.
8Jina langu mimi ni Mwenyezi-Mungu;
utukufu wangu sitampa mwingine,
wala sifa zangu sanamu za miungu.
9Tazama, mambo niliyotabiri yametukia;
na sasa natangaza mambo mapya,
nakueleza hayo kabla hayajatukia.”
Wimbo wa sifa
10Mwimbieni Mwenyezi-Mungu wimbo mpya!
Dunia yote iimbe sifa zake:
Bahari na vyote vilivyomo,
nchi za mbali na wakazi wake;
11jangwa na miji yake yote ipaaze sauti,
vijiji vya wakazi wa Kedari vimsifu,
wakazi wa Sela waimbe kwa shangwe;
wapaaze sauti kutoka mlimani juu.
12Wote wakaao nchi za mbali,
na wamtukuze na kumsifu Mwenyezi-Mungu.
13Mwenyezi-Mungu ajitokeza kama shujaa;
kama askari vitani ajikakamua kupigana.
Anapaza sauti kubwa ya vita,
na kujionesha mwenye nguvu dhidi ya maadui zake.
Mungu aahidi kuwasaidia watu wake
14Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Kwa muda mrefu sasa nimenyamaza,
nimekaa kimya na kujizuia;
lakini sasa nitalia kama mama anayejifungua,
anayetweta pamoja na kuhema.
15Nitaharibu milima na vilima,
na majani yote nitayakausha.
Mito ya maji nitaigeuza kuwa nchi kavu,
na mabwawa ya maji nitayakausha.
16“Nitawaongoza vipofu katika njia wasiyoifahamu,
nitawaongoza katika njia ambazo hawazijui.
Mbele yao giza nitaligeuza kuwa mwanga,
na mahali pa kuparuza patakuwa laini.
Huo ndio mpango wangu wa kufanya,
nami nitautekeleza.
17Wote wanaotegemea sanamu za miungu,
wote wanaoziambia: Nyinyi ni miungu yetu;
watakomeshwa na kuaibishwa.
Waisraeli ni viziwi na vipofu
18“Sikilizeni enyi viziwi!
Tazameni enyi vipofu, mpate kuona!
19Nani aliye kipofu ila mtumishi wangu?
Nani aliye kiziwi kama mjumbe ninayemtuma?
Ni nani aliye kipofu kama huyu niliyemweka wakfu,
au kipofu kama mtumishi wa Mwenyezi-Mungu?
20Nyinyi mmeona mambo mengi,
lakini hamwelewi kitu.
Masikio yenu yako wazi,
lakini hamsikii kitu!”
21Mwenyezi-Mungu, kwa ajili ya uaminifu wake,
alipenda kukuza mwongozo wake na kuutukuza.
22Lakini hawa ni watu walioibiwa mali na kuporwa!
Wote wamenaswa mashimoni,
wamefungwa gerezani.
Wamekuwa kama mawindo bila mtu wa kuwaokoa,
wamekuwa nyara na hakuna asemaye, “Waokolewe!”
23Je, mtatega sikio kusikia kitu hiki?
Nani kati yenu atakayesikiliza vizuri yatakayotukia?
24Ni nani aliyewatia Waisraeli mikononi mwa adui zao?
Nani aliyewaacha wanyanganywe mali zao?
Ni Mwenyezi-Mungu ambaye tumemkosea!
Wazee wetu walikataa kuzifuata njia zake,
wala hawakuzitii amri zake.
25Kwa hiyo aliwamwagia hasira yake kali,
akawaacha wakumbane na vita vikali.
Hasira yake iliwawakia kila upande,
lakini wao hawakuelewa chochote;
iliwachoma, lakini hawakutilia jambo hilo maanani.

Isaya42;1-25

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: