Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 17 October 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 35....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Kwako ee Mwenyezi-Mungu, nakimbilia usalama; kamwe usiniache niaibike! Kwa uadilifu wako uniokoe na kunisalimisha; unitegee sikio lako na kuniokoa! Uwe mwamba wangu wa kukimbilia usalama, ngome imara ya kuniokoa, kwani wewe ni mwamba na ngome yangu.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Niokoe, ee Mungu wangu, mikononi mwa waovu, kutoka makuchani mwa wabaya na wakatili. Maana wewe Bwana u tumaini langu; tegemeo langu ee Mwenyezi-Mungu, tangu ujana wangu; nimekutegemea tangu kuzaliwa kwangu, ndiwe uliyenitoa tumboni mwa mama yangu. Mimi nitakusifu wewe daima.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Kwa wengi nimekuwa kioja, lakini wewe u kimbilio langu imara. Kinywa changu kimejaa sifa zako, na utukufu wako mchana kutwa. Wakati wa uzee usinitupe; niishiwapo na nguvu usiniache.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

Furaha ijayo ya Yerusalemu
1Nyika na nchi kavu vitachangamka,
jangwa litafurahi na kuchanua maua.
2Litachanua maua kwa wingi kama waridi,
litashangilia na kuimba kwa furaha.
Mungu atalijalia fahari ya milima ya Lebanoni,
uzuri wa mlima Karmeli na wa bonde la Sharoni.
Watu watauona utukufu wa Mwenyezi-Mungu,
watauona ukuu wa Mungu wetu.
3 35:3 Taz Ebr 12:12 Imarisheni mikono yenu dhaifu,
kazeni magoti yenu manyonge.
4Waambieni waliokufa moyo:
“Jipeni moyo, msiogope!
Tazameni Mungu wenu atakuja kulipiza kisasi,
atakuja kuwaadhibu maadui zenu;
atakuja yeye mwenyewe kuwaokoeni.”
5 35:5-6 Taz Mat 11:5; Luka 7:22 Hapo vipofu wataona tena,
na viziwi watasikia tena.
6Walemavu watarukaruka kama paa,
na bubu wataimba kwa furaha.
Maji yatabubujika nyikani
na vijito vya maji jangwani.
7Mchanga wa moto jangwani utakuwa bwawa la maji,
ardhi kavu itabubujika vijito vya maji.
Makao ya mbwamwitu yatajaa maji;
nyasi zitamea na kukua kama mianzi.
8Humo kutakuwa na barabara kuu,
nayo itaitwa “Njia Takatifu.”
Watu najisi hawatapitia humo,
ila tu watu wake Mungu;
wapumbavu hawatadiriki kuikanyaga,
9humo hakutakuwa na simba,
mnyama yeyote mkali hatapitia humo,
hao hawatapatikana humo.
Lakini waliokombolewa ndio watakaopita humo.
10Waliokombolewa na Mwenyezi-Mungu watarudi,
watakuja Siyoni wakipiga vigelegele.
Watakuwa wenye furaha ya milele,
watajaliwa furaha na shangwe;
huzuni na kilio vitatoweka kabisa.

Isaya35;1-10

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: