Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 25 October 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 41....



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Baada ya mambo hayo, Paulo aliamua kwenda Yerusalemu kwa kupitia Makedonia na Akaya. Alisema, “Baada ya kufika huko, itanilazimu kuona Roma pia.” Hivyo, aliwatuma wawili wa wasaidizi wake, Timotheo na Erasto, wamtangulie kwenda Makedonia, naye akabaki kwa muda huko Asia.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Wakati huo ndipo kulipotokea ghasia kubwa huko Efeso kwa sababu ya hiyo njia ya Bwana. Kulikuwa na mfua fedha mmoja aitwaye Demetrio, ambaye alikuwa na kazi ya kutengeneza sanamu za nyumba ya mungu wa kike aitwaye Artemi. Shughuli hiyo iliwapatia mafundi wake faida kubwa.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Demetrio aliwakusanya hao wafanyakazi pamoja na wengine waliokuwa na kazi kama hiyo, akawaambia, “Wananchi, mnafahamu kwamba kipato chetu kinatokana na biashara hii. Sasa, mnaweza kusikia na kujionea wenyewe mambo Paulo anayofanya, si hapa Efeso tu, ila pia kote katika Asia. Yeye amewashawishi na kuwageuza watu wakakubali kwamba miungu ile iliyotengenezwa na watu si miungu hata kidogo. Hivyo iko hatari kwamba biashara yetu itakuwa na jina baya. Si hivyo tu, bali pia jambo hilo linaweza kuifanya nyumba ya mungu Artemi kuwa si kitu cha maana. Hatimaye sifa zake huyo ambaye Asia na dunia yote inamwabudu, zitakwisha.”
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Mungu anaahidi kuisaidia Israeli
1Mungu asema hivi:
“Enyi wakazi wa mbali nyamazeni mnisikilize!
Enyi mataifa jipeni nguvu;
jitokezeni mkatoe hoja zenu,
na tuje pamoja kwa hukumu.
2“Nani, ila mimi, aliyemwita shujaa toka mashariki,
mtu ambaye hupata ushindi popote aendako?
Mimi huyatia mataifa makuchani mwake,
naye huwaponda wafalme chini ya miguu yake!
Upanga wake huwafanya kuwa kama vumbi,
kwa upinde wake huwapeperusha kama makapi.
3Yeye huwafuatia na kupita salama;
huenda kasi kana kwamba hagusi chini.
4Nani aliyefanya yote haya yatendeke?
Ni nani aliyepanga wakati wa kila tukio?
Mimi Mwenyezi-Mungu nipo tangu mwanzo,
mimi nitakuwapo hata milele.
5“Wakazi wa mbali wameona niliyotenda, wakaogopa;
dunia yote inatetemeka kwa hofu.
Watu wote wamekusanyika, wakaja.
6Kila mmoja anamhimiza mwenzake akisema,
‘Haya! Jipe moyo!’
7Fundi anamhimiza mfua dhahabu,
naye alainishaye sanamu kwa nyundo,
anamhimiza anayeiunga kwa misumari.
Wote wanasema, ‘Imeungika vizuri sana!’
Kisha wanaifunga kwa misumari isitikisike.
8Sikiliza ewe Israeli, mtumishi wangu,
wewe, Yakobo ambaye nimekuchagua,
wewe mzawa wa Abrahamu, rafiki yangu;
9wewe niliyekuleta toka miisho ya dunia,
wewe niliyekuambia: ‘Wewe u mtumishi wangu;
mimi sikukutupa, bali nilikuchagua.’
10Basi, usiogope, mimi nipo pamoja nawe.
Usifadhaike, mimi ni Mungu wako.
Nitakuimarisha na kukusaidia;
nitakulinda kwa mkono wangu wa ushindi.
11“Naam! Wote waliokuwakia hasira,
wataaibishwa na kupata fedheha.
Wote wanaopingana nawe,
watakuwa si kitu na kuangamia.
12Utawatafuta hao wanaopingana nawe,
lakini watakuwa wameangamia.
13Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako,
ndimi ninayetegemeza mkono wako.
Mimi ndimi ninayekuambia:
‘Usiogope, nitakusaidia.’”
14Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Enyi watu wa Yakobo dhaifu kama mdudu,
enyi Waisraeli, msiogope!
Mimi Mwenyezi-Mungu nasema nitawasaidia.
Mimi ni Mkombozi wenu,
Mtakatifu wa Israeli.
15Nitawafanya muwe kama chombo cha kupuria,
chenye meno mapya na makali.
Mtaipura milima na kuipondaponda;
vilima mtavisagasaga kama makapi.
16Mtaipepeta milima hiyo,
nao upepo utaipeperushia mbali,
naam, dhoruba itaitawanya huko na huko.
Nanyi mtafurahi kwa sababu yangu Mwenyezi-Mungu;
mtaona fahari kwa sababu yangu
Mungu Mtakatifu wa Israeli.
17“Maskini na fukara wakitafuta maji wasipate,
wakiwa wamekauka koo kwa kiu,
mimi Mwenyezi-Mungu nitawajibu;
mimi Mungu wa Israeli, sitawaacha.
18Nitabubujisha mito kwenye milima mikavu,
na chemchemi katika mabonde.
Nitaigeuza nyika kuwa bwawa la maji,
na nchi kame kuwa chemchemi za maji.
19Nitapanda miti huko nyikani:
Mierezi, mikakaya, mijohoro, na mizeituni;
nitaweka huko jangwani:
Miberoshi, mivinje na misonobari.
20Watu wataona jambo hilo,
nao watatambua na kuelewa kwamba
mimi Mwenyezi-Mungu nimetenda hayo,
mimi Mtakatifu wa Israeli nimefanya jambo hilo.”
Mwenyezi-Mungu aipuuza miungu ya uongo
21Mwenyezi-Mungu, Mfalme wa Yakobo, asema:
“Enyi miungu ya mataifa,
njoni mtoe hoja zenu!
22Leteni hoja zenu, mtuambie yatakayotukia.
Tuambieni matukio ya kwanza yalikuwa yapi
nasi tutayatafakari moyoni.
Au tutangazieni yajayo,
tujue yatakayokuja.
23Tuambieni yatakayotokea baadaye,
nasi tujue basi kama nyinyi ni miungu.
Fanyeni kitu chochote, chema au kibaya,
ili tutishike na kuogopa.
24Hakika, nyinyi si kitu kabisa.
hamwezi kufanya chochote kile.
Anayechagua kuwaabudu nyinyi ni chukizo.
25“Nimechochea mtu toka kaskazini,
naye amekuja;
naam, nimemchagua mtu toka mashariki,
naye atalitamka jina langu.
Yeye atawakanyaga wafalme kama tope,
kama vile mfinyanzi apondavyo udongo wake.
26Nani aliyebashiri haya tangu mwanzo,
hata sisi tupate kuyatambua?
Nani aliyetangulia kuyatangaza,
ili sasa tuseme, alisema ukweli?
Hakuna hata mmoja wenu aliyeyataja,
wala hakuna aliyesikia maneno yenu.
27Mimi ni yule wa kwanza, niliyetangaza kwa Siyoni,
nikapeleka Yerusalemu mjumbe wa habari njema.
28Nimeangalia kwa makini sana,
lakini simwoni yeyote yule;
hamna yeyote kati ya hao miungu awezaye kushauri;
nikiuliza hakuna awezaye kunijibu.
29La! Miungu hiyo yote ni udanganyifu,
haiwezi kufanya chochote;
sanamu zao za kusubu ni upuuzi.


Isaya41;1-29

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: