Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 15 October 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 33....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Mfalme Ahasuero alitoza kodi watu wa bara na pwani. Matendo yake yote makuu na ya ajabu, pamoja na simulizi kamili kuhusu jinsi alivyompandisha cheo Mordekai na kumtunukia heshima kuu, yote yameandikwa katika Kitabu cha Kumbukumbu za wafalme wa Media na Persia.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Mordekai, Myahudi, alikuwa wa kwanza chini ya mfalme Ahasuero katika madaraka. Alipendwa na kuheshimiwa na Wayahudi, maana aliwafanyia mema watu wake na kuwatakia amani wazawa wao wote.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.


Maafa kwa mwangamizi
1Ole wako ewe mwangamizi,
unayeangamiza bila wewe kuangamizwa!
Ole wako wewe mtenda hila,
ambaye hakuna aliyekutendea hila!
Utakapokwisha kuangamiza
wewe utaangamizwa!
Utakapomaliza kuwatendea watu hila
wewe utatendewa hila.
2Ee Mwenyezi-Mungu, utuonee huruma,
kwako tumeliweka tumaini letu.
Uwe kinga yetu kila siku,
wokovu wetu wakati wa taabu.
3Kwa kishindo cha sauti yako watu hukimbia;
unapoinuka tu, mataifa hutawanyika.
4Maadui zao wanakusanya mateka,
wanayarukia kama panzi.
5Mwenyezi-Mungu ametukuka,
yeye anaishi juu mbinguni.
Ameujaza Siyoni haki na uadilifu.
6Enyi watu wa Yerusalemu,
Mwenyezi-Mungu atawajalieni usalama,
atawaokoa na kuwapa hekima na maarifa.
Hazina yenu kuu ni kumcha Mwenyezi-Mungu.
7Haya, mashujaa wao wanalia,
wajumbe wa amani wanaomboleza.
8Barabara kuu zimebaki tupu;
hamna anayesafiri kupitia humo.
Mikataba inavunjwa ovyo,
mashahidi wanadharauliwa.
Hamna anayejali tena maisha ya binadamu.
9Nchi inaomboleza na kunyauka;
misitu ya Lebanoni imekauka,
bonde zuri la Sharoni limekuwa jangwa,
huko Bashani na mlimani Karmeli
miti imepukutika majani yake.
Mwenyezi-Mungu awaonya maadui zake
10Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Sasa mimi nitainuka;
sasa nitajiweka tayari;
sasa mimi nitatukuzwa.
11Mipango yenu yote ni kama makapi,
na matokeo yake ni takataka tupu.
Pumzi yangu33:11 Pumzi yangu: Kadiri ya hati kadhaa za kale; makala ya Kiebrania ina pumzi yenu. itawaangamiza kama moto.
12Watu watakuwa kama wamechomwa kuwa majivu,
kama miiba iliyokatwa na kuteketezwa motoni.
13Sikilizeni mambo mliyofanya enyi mlio mbali,
nanyi mlio karibu kirini uwezo wangu.”
14Wenye dhambi katika Siyoni wanaogopa,
wasiomcha Mungu wanatetemeka na kusema:
“Nani awezaye kuukaribia moto huu mkali?
Nani awezaye kustahimili miali ya moto wa milele?”
15Ni mtu aishiye kwa uadilifu na asemaye ukweli;
mtu anayedharau kabisa utajiri wa dhuluma,
anayekataa hongo kata kata,
asiyekubali kamwe kusikia mipango ya mauaji,
wala hakubali macho yake yaone maovu.
16Mtu wa namna hiyo anaishi juu,
mahali salama penye ngome na miamba;
chakula chake atapewa daima,
na maji yake ya kunywa hayatakosekana.
Wakati mzuri ujao
17Mtaweza kumwona mfalme katika fahari yake,
mtaiona nchi anayotawala, kubwa na pana.
18Mtafikiria tisho lililopita na kujiuliza,
“Wako wapi wale waliokadiria na kukisia kodi?
Wako wapi wale waliopeleleza ulinzi wetu?”
19Hamtawaona tena watu wale wenye kiburi,
wanaozungumza lugha isiyoeleweka.
20Tazameni Siyoni tunamofanya sikukuu zetu;
tazameni mji Yerusalemu, makao matulivu, hema imara;
vigingi vyake havitangolewa kamwe,
kamba zake hazitakatwa hata moja.
21Humo Mwenyezi-Mungu atatuonesha ukuu wake.
Kutakuwa na mito mikubwa na vijito,
ambamo meli za vita hazitapita,
wala meli kubwa kuingia.
22Maana Mwenyezi-Mungu ni hakimu wetu,
yeye ni mtawala wetu;
Mwenyezi-Mungu ni mfalme wetu,
yeye ndiye anayetuokoa.
23Ewe Siyoni, kamba zako zimelegea,
haziwezi kushikilia matanga yake,
wala kuyatandaza.
Lakini nyara nyingi zitagawanywa;
hata vilema wataweza kuchukua sehemu yao.
24Hakuna atakayesema tena ni mgonjwa;
watu watasamehewa uovu wao wote.

Isaya33;1-24

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

No comments: